Mlale JKT, nawamiss sana afande undunduundundu, huyu alikuwa RSM, alikuwa akipenda kutoa adhabu ya kibatabata, kuna pia afande mmoja akiitwa Mange K, huyu alikuwa bingwa wa kwata ya Singe, sauti yake ilikuwa kali utadhani chiriku.
Kuna matukio kama ya kuzima moto, hakika haya yalikuwa yanaudhi kweli kweli, mnaamshwa saa tisa usiku, mnazima moto upande huu, mkirudi wakati usingizi ndo unaanza kushika kasi, mnaamshwa kwenda kuzima moto upande mwingine, sometimes umbali wa zaidi ya km 2.
Kuna jamaa alianzisha wimbo wenye utata akapigwa dosodoso ile mbaya, wimbo wenyewe ulikuwa kama hivi, 'TUNAPENDA KUMAKUMA, KUMALIZA JESHI x2'halafu wengine mnatitikia hivyo hivyo, mwanzoni afande alikuwa hakuelewa lakini ilipokuja beti ya pili ndiyo akashtuka.
Beti ya pili, 'TUNAPENDA MBOOMBOO MBOGA ZA MAJANI x2' hapo kila mtu akaangua kicheko, afande akamwambia jamaa hebu rudia mbona wenzako wanacheka, ile kurudia wimbo ilikuwa balaa
Du vituko vilikuwa vingi unaweza maliza mwezi kwa kuviandika.
Enzi hizo CO alikuwa Kanali Mtono (Marehemu), huyu bwana alikuwa mjeshi kweli kweli, sio hawa wa siku hizi na kuku wa kisasa.