Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Je, unakumbuka nini enzi zako za JKT? Ni mambo gani yalikufurahisha au kukukwaza?

Mafinga JKT Operation Miaka 25 (1988/89) i realy miss you. Danger coy mko wapi wakuu? Kayange, Double P, Chalamila, Nyaulingo where are guys? Namkumbuka Sir Major Mulembo akimfokea Kayange:
Afande Mulembo: We Kuruta unajifanya mjanja sana eeh?
Kayange : Kimya
Afande : mimi ninakuuliza wewe unanyamaza Kimya?Afande akikuuliza "unajibu ndiyo afande"
Kayange: ndiyo afande
Afande : unajifanya mjanja sana?
Kayange : Ndiyo Afande
Afande: pumbafu zako
Kayange: ndiyo afande
Afande: Unatuona sisi ni wajinga sana?
Kayange: Ndiyo afande
Afande: ( akiwa amekasirika) Unatuona sisi wapumbavu sana?
Kayange: Ndiyo afande

kombania tukashindwa kuvumilia tuaanza kucheka tukala push ups wote kwa kucheka huku bado akiwa hajui kuwa amem-limit Kayange kujibu 'Ndiyo afande' hata kwa negative statements.

mmeshindikana uraiani ndio mmekuja hapa kushindanana ! ................. hapa hafukuzwi mtu !
 
Wakuu, kizazi kipya ambacho hakikupita JKT wanatulaumu kwamba tuliopita JKT wengi wetu ndiyo tumeshiriki kuifisadi nchi! Je hayo maneno yana ukweli wowote?
 
nakumbuka nikiwa Mafinga wakati BT akiwa Major Chacha(mrefu sana) na Co akiwa T Mlay. Kwa sabasu ya ile nyahenge(baridi) waliamua lijengwe bench na kwa bahati mbaya lile bench walipima urefu wa Chacha ambaye alikuwa mrefu mara 2 ya Mlay na hivyo akikaa miguu inaning'inia. Basi wale Macoplo walipigwa Kadebra ya kufa Mtu na maneno makali juu kwamba nani Co mimi au Chacha. Wako wapi ma RP Songolo, Maneno Mahenge
 
Wazalendo;

Moja ya shemu ya maisha yangu ambayo kamwe sitasahu ni kupitia JKT.

Nilijiunga na JKT Ruvu na baadaye nikaenda Service Buhemba Lwamkoma.

Sitosahau kamwe mafunzo ya ukakamavu, kwata, mchaka mchaka, disko na vitimbi mbalimbali kati ya Makuruta na Maafande. Nilikuwa Combania E.

Moja ya vituko vya kukumbuka ni simulizi kutoka- Operation OKOA, kulikuwa na huyu jamaa alikuwa ni mweusi sana anaitwa afande Lucas, badala ya kuwaaamsha kuruta kwa filimbi, alikuwa anaingia na kuvuta Sigara. Kuruta inatakiwa ukisikia harufu ya Sigara uamke na kufoleni nje. Usipotoka in time unakula mijeledi.

Basi siku moja Kuruta wakapanga wamfanyizie na wakatoka mapema nje na kujificha huku ndani kwenye Bweni wakiyaviringisha mablanketi mithili ya mtu amelala. Afande alipomaliza sigara hakuna aliyetoka akajua siku hiyo kuruta wamegoma kuamka na kuanza kuchapa viboko yale mablanketi yaliyovingirishwa. Alishtukia kaanza kushambuliwa yeye na kuruta toka nje ambao walikuwa na fimbo kibao mpaka akakoma. Kisha kuruta wakafoleni nje. Nakumbuka Mkuu wa Kombania alipata habari na kulikuwa na drill si kawaida na mpaka push ups za kunusa mkojo katika nyasi walizokuwa wanakojoa kuruta usiku. Hata hivyo yule afande naye alikoma kwani hakurudia mchezo wa kuwaamsha watu kwa sigara.

Kwa waliokuwa Ruvu Operation Okoa:

Na miss - Ugali na korosho mnapojongo kambini
Namiss Mihogo ya Vibwende kwa Babu
Wali na Maembe
Uji wa Mestin ya Jeshi
Bukta na Green Vest
Kuokota kuni
Bustani
Michezo
Disco . . . Ama Johnnnnn ambaaaa ambaaa John, amba Johnnn wa Tanzania . .

. . . . Arusha Mbali, Arusha Mbali, tukumbukane kwa Barua nk.

Nakumbuka pia siku moja sikuimbisha disco vizuri na kipindi kile 1985 bado kulikuwa kuna ubaguzi wa rangi Africa Kusini, basi afande akanipiga mkwala na kuniambia . . . .

"Kuruta nitakutemea mate yenye sumu usoni upofuke macho, na sijui utatibiwa wapi kwani mipaka yote Afrika Kusini imefungwa . . . (Kana kwamba hakukuwa na hospitali ya kutibu mate ya sumu hapa bongo"

Jamani mliokosa JKT, mlikosa mengi, japo tulipata tabu lakini tulijifunza mengi katika maisha.

Je, wewe unakumbuka nini?

nilikuwa kambi ya mafinga JKT, kombania c (chale koy) chini ya afande Kweka AKISAIDIWA na RSM by that time Danda.sitasahau siku msitu wa mafinga ulipowaka moto na kuamuliwa kwenda kuzima mida ya saa tatu asubuhi ambapo zoezi hilo lilienda mpaka kesho yake saa 11 jioni na afande co aliagiza tuletewe shea zetu zote kuanzia uji chakula cha mchana cha jana yake, jioni, uji wa asubuhi siku ya pili kwa madai shea ya mtu jeshini hailiwi. sitasahau pia siku CO Mray ametoka dodoma na azimio la kilimo kwanza ulikuwa mwezi january/february ambapo tulilazimika kupelekwa idetero karibu na msitu wa mafinga na kwa wakati huo mvua ilikuwa nyingi sana ikiwa ni pamioja na radi kwa muda wa week mbili, lakini baada ya maombi ya wapiganaji (kuruta) mvua ilisimama/radi zilikoma, kimsingi tulijengewa sana "UVUMILIVU", "UZALENDO", NA UKAKAMAVU.

 
mmeshindikana uraiani ndio mmekuja hapa kushindanana ! ................. Hapa hafukuzwi mtu !

umenikumbusha mbali sana malizia na wimbo " mimi ni pweza..... Mwenda na maji..... Wimbi likija naliepuka!!!!! Mwanzishaji ni afande then kuruta aliitikia "wewe ni pweza... Mwenda na maji .... Wimbi likija waliepuka !!! Hapakutosha
 
waoh JKT MAKUTUPORA, AFANDE ZIMWI,AFANDE LUKANGA 'kamama unachambia wembe ?' sir major Kahiriko akigawa kondomu 'mwenyewe akisema ni viwembe mwende mkanyoane,CCM inawapenda imewaweka wanawake na wanaume hivyo imeleta viwembe kwa ajili ya kunyoana' mgao ulikuwa kwa wanaume tu.
Afande George Nyeriga Nyamhanga wa acha !!! HAKIKA KUTOKWENDA JKT VIJANA WANAMISS VITU ADIMU NA ADHIMU
 
Wazalendo;

Moja ya shemu ya maisha yangu ambayo kamwe sitasahu ni kupitia JKT.

Nilijiunga na JKT Ruvu na baadaye nikaenda Service Buhemba Lwamkoma.

Sitosahau kamwe mafunzo ya ukakamavu, kwata, mchaka mchaka, disko na vitimbi mbalimbali kati ya Makuruta na Maafande. Nilikuwa Combania E.

Moja ya vituko vya kukumbuka ni simulizi kutoka- Operation OKOA, kulikuwa na huyu jamaa alikuwa ni mweusi sana anaitwa afande Lucas, badala ya kuwaaamsha kuruta kwa filimbi, alikuwa anaingia na kuvuta Sigara. Kuruta inatakiwa ukisikia harufu ya Sigara uamke na kufoleni nje. Usipotoka in time unakula mijeledi.

Basi siku moja Kuruta wakapanga wamfanyizie na wakatoka mapema nje na kujificha huku ndani kwenye Bweni wakiyaviringisha mablanketi mithili ya mtu amelala. Afande alipomaliza sigara hakuna aliyetoka akajua siku hiyo kuruta wamegoma kuamka na kuanza kuchapa viboko yale mablanketi yaliyovingirishwa. Alishtukia kaanza kushambuliwa yeye na kuruta toka nje ambao walikuwa na fimbo kibao mpaka akakoma. Kisha kuruta wakafoleni nje. Nakumbuka Mkuu wa Kombania alipata habari na kulikuwa na drill si kawaida na mpaka push ups za kunusa mkojo katika nyasi walizokuwa wanakojoa kuruta usiku. Hata hivyo yule afande naye alikoma kwani hakurudia mchezo wa kuwaamsha watu kwa sigara.

Kwa waliokuwa Ruvu Operation Okoa:

Na miss - Ugali na korosho mnapojongo kambini
Namiss Mihogo ya Vibwende kwa Babu
Wali na Maembe
Uji wa Mestin ya Jeshi
Bukta na Green Vest
Kuokota kuni
Bustani
Michezo
Disco . . . Ama Johnnnnn ambaaaa ambaaa John, amba Johnnn wa Tanzania . .

. . . . Arusha Mbali, Arusha Mbali, tukumbukane kwa Barua nk.

Nakumbuka pia siku moja sikuimbisha disco vizuri na kipindi kile 1985 bado kulikuwa kuna ubaguzi wa rangi Africa Kusini, basi afande akanipiga mkwala na kuniambia . . . .

"Kuruta nitakutemea mate yenye sumu usoni upofuke macho, na sijui utatibiwa wapi kwani mipaka yote Afrika Kusini imefungwa . . . (Kana kwamba hakukuwa na hospitali ya kutibu mate ya sumu hapa bongo"

Jamani mliokosa JKT, mlikosa mengi, japo tulipata tabu lakini tulijifunza mengi katika maisha.

Je, wewe unakumbuka nini?

1.KUNYAKUA USAWA WA GUDULIA
2.KUJIFANYA SELULE
3.KAMA NYIE NI FORM SIX BASI SISI NI MAFORM SEVEN
4.KUPOZA UJI KWA MAJI YENYE MKOJO WA NG'OMBE
5.WAKATI WA SERVICE MI NILIKUWA MPISHI.
Buhemba operation miezi 6.
 
JKT ni heri irudishwe tuu bse vijana wa leo ndo maana wanaaribika ukakamavu sifuri mara ooh mtoto si rzki.
Wale wa Mafinga mpo?
Tupo ! TN Mlay, C.O, Basi bwana kuna mshikaji kwenye grup yetu alikua anapiga mkuu wa kombani C Coy, (Captain) sasa siri ikavuja na akatafutwa mtoa huduma ! Grup likatafutiwa visa (tulikuwa 4) mie by the time nilikua 'AWOL' (nimetoroka!) washikaji wakanitaja mimi ! We acha tuu ! Nilirudi kumepoa lakini nilitolewa katika tangazo (nimesahau jina la yale matangazo ya kijeshi) siku naripoti nikakuta bogi la mlalakuwa nikaunga ! Wanashtuka niko Dar !
 
Afande Justo wa OLJORO na mkwara wake wa KWATA....Pia shamba almaarufu DUNIA...unaangalia mraba wa kupalilia huoni mwisho........Kuchonga matofali toka mwamba laini kwa Mzee Shabaan.....Hakika ulikuwa mwaka wa aina yake...Pamoja na ukakamavu nilijifunza kuwaza haraka sana hasa katika kutengeneza UONGO kujiokoa kwenye mikono ya maafande pale ukutwapo usipotakiwa kuwa🙂
unakuwa sharp, makini, muangalifu, unaishi kwa tahadhari, unapiga hesabu kila nyendo yako ! Ukika bila kufanya kazi wewe bingwa. Unaweza kudhibitiwa 24hrs!
 
Nakumbuka Mafinga Kukatangazwa master parade ya CO Mlay. Basi twatu wakakesha kufanya usafi wa kombati na kung'irisha boots na alfajiri kutandika vitanda na ndama unaikunja kama cassette. Kwenye Parade CO kaamrisha haya wote toa boots zenu, Duu acha tupate perfume za soksi.
siku ya kumaliza mazoezi ya kijeshi 'pass out' TN MLAY alileta mtihani wa mahojiano, sie havkulijua hilo, mie akaniuliuza nimuoshe sox ya kulia ni ipi kati ya sox mbili, alooooh ! Sikujuaa kama sox ina kulia na kushoto!
 
JKT ilikuwa safi sana hasa nakumbuka vituko vya wale form 7(maafande wa kwata) na mwendo wa kunyakua hasa wakati wa kwnda kula.

Ninachokumbuka zaidi ni afande mmoja alimtokea binti na wakakubaliana, walipofika faragha binti akakuta afande an "fore skin", akamwambia afande wasifanye chochote la sivyo angepiga kelele. Akamwomba afande akaondoe hiyo kitu na kidonda kitakapopona atampa bila shida. Afande akakubali akaenda kukata, akazembea kufanya dressing, akawa anatoa harufu mbaya. Akaniomba nimsaidie ili apone, maana nilikuwa pale kama tabibu, kwenye zahanati ya Kikosini. Nikamsaidia kwa dressing mpaka kidonda kikakauka vizuri. Bahati mbaya wakati afande anapona na muda wetu ukawa umekwisha na binti akaondoka,afande akawa amemkosa ila alifaidika na kutahiri akiwa na miaka 40!

Du! Hii nayo bibi kubwa!
 
Mlale JKT, nawamiss sana afande undunduundundu, huyu alikuwa RSM, alikuwa akipenda kutoa adhabu ya kibatabata, kuna pia afande mmoja akiitwa Mange K, huyu alikuwa bingwa wa kwata ya Singe, sauti yake ilikuwa kali utadhani chiriku.

Kuna matukio kama ya kuzima moto, hakika haya yalikuwa yanaudhi kweli kweli, mnaamshwa saa tisa usiku, mnazima moto upande huu, mkirudi wakati usingizi ndo unaanza kushika kasi, mnaamshwa kwenda kuzima moto upande mwingine, sometimes umbali wa zaidi ya km 2.

Kuna jamaa alianzisha wimbo wenye utata akapigwa dosodoso ile mbaya, wimbo wenyewe ulikuwa kama hivi, 'TUNAPENDA KUMAKUMA, KUMALIZA JESHI x2'halafu wengine mnatitikia hivyo hivyo, mwanzoni afande alikuwa hakuelewa lakini ilipokuja beti ya pili ndiyo akashtuka.
Beti ya pili, 'TUNAPENDA MBOOMBOO MBOGA ZA MAJANI x2' hapo kila mtu akaangua kicheko, afande akamwambia jamaa hebu rudia mbona wenzako wanacheka, ile kurudia wimbo ilikuwa balaa

Du vituko vilikuwa vingi unaweza maliza mwezi kwa kuviandika.

Enzi hizo CO alikuwa Kanali Mtono (Marehemu), huyu bwana alikuwa mjeshi kweli kweli, sio hawa wa siku hizi na kuku wa kisasa.

ha ha kwakweli jeshi zuri sana,uwezo wa kufikiria lazima uongezeke.
 
Dah! umenikumbusha mbali sana mkuu..1991/92 op. vyama vingi..Makutupora A-coy tulipangwa kumwagilia bustan.. Lakini baadae tukahamishiwa Bulombora, D-coy. Namkumbuka afande Mnzena, Mtekere, afande Sezero, coplo Ngoma, afande Mbewa na afande machachali mikwara mingii Stanslaus Makoba ''kadebra'' baiskeli yake iliandikwa ''sereuka mwana wa ndege..mnafiki hakosi sababu'' Kombania hii kulikuwa na vijana akina Robert Nyamhanga, Prudence Timanywa, Mongu Manumbu, Mpemba Francis, Safari Lucian, Redemtus Shoto, Privatus,Anterius Sostenes, Joe Kihampa (TBC1) na wengine. Akina dada kulikuwa na Kore Ally Sadick, Rose Manyama, Judith Schirima, na wengine wengi. Nakumbuka umoja, ushirikiano wa kusaidiana kuepuka visanga baina ya makuruta nk. Siku tukipokea ''kichele'' tulikuwa tunakwenda kijiji cha Kaseke kutumia. -J4 wa D-coy

Jayfour kumbe ni wewe? Wewe si ulikuwa ujenzi na akina Edward Nzigula na yule Engineer mwingine mjita mlikuwa mmetoka naye Mbeya Technical, alikuawa anaitwa Ngosi kama sikosei! Kole Sadiki yuko wapi?
Aisee mbona hujanitaja aisee babaangu? Au kwa vile niliwaacha kombania nikahamia chokaa kwa afande Mayila? Kazi inaisha saa 4 halafu tunaanza kuogelea ziwani, afande Jogoo na Makere wakija hatuelewi kitu.
Kule tulikuwa na akina Reuben Nkori, Busagala Masale, Haule, Mbuna, Chambo.
Wakati niko kombania mimi ndiye nilikuwa natangulia pale mbele ya mstari tukiwa na Karume Mbulwa ambaye baadaye alikuja kuwa ni RP, halafu wanafuatia wengine kama akina MC Nyamhanga, Commandoor Katani. Nawakumbuka sana wasichana wa Danger Coy akina Winifrida Bita, Eda (mnapata kichere mnakwenda kaseke), Esther Koroti, Yasinta John (kasheshe yake na afande Pima kwenye chenja unaikumbuka?, alirudia kutaja jina kama mara mia pale mbele ya hanga la wavulana D-coy).
Siku moja nikaokota filimbi. Niko na jamaa alikuwa anaitwa Mbogo Mnubi usiku katikati ya mahanga ya D na C, kule nyuma, nikawa napuliza filimbi "fiii" halafu Mbogo akawa anasema "ruka, ruka", halafu mimi naruka kichura na buti zangu pwaaa pwaaa, mahanga yote yakatimua mbio usiku chaga za vitanda zinadondoka chini watu wakadhani ni ma MP wako around. Baadaye na sisi tukakimbia kuogopa kibano sababu watu waligundua kuwa tumewachezea akili.
Mabigula ya usiku kwenda kuzima moto, tumeingia uchaka sana unaondoka na Blanketi mbili, kurudi majaliwa.
Mimi ndiye niliyekuwa naigiza sauti ya yule afande giant msukuma coplo alikuwa anaitwa Bujiku wa uvuvi. Akikukamata push-up una kosa anakwambia, "nipe zangu mbili, OC, Sir Major wa kombania naye tatu, OC naye nne,.... yaani we acha tu".
Halafu siku moja tunapiga kwata uwanja wa damu, mzee wa kadebula a.k.a commandoor Makoba akaingia ghafla halafu lisichana limoja la D-coy likaropoka "Cock up", mama yangu, kumbe amesikia! Akaanza, " nani amesema cock-up hapa, eeh nai,....jenga reli,... yaani ilikuwa ni issue, choka mbaya! Jeshini we acha tu, hadi nilitaka kuwa kujiunga nikasomee u-Rubani wa ndege szile ndogo za jeshi, Mungu hakujalia!

 
Dah! umenikumbusha mbali sana mkuu..1991/92 op. vyama vingi..Makutupora A-coy tulipangwa kumwagilia bustan.. Lakini baadae tukahamishiwa Bulombora, D-coy. Namkumbuka afande Mnzena, Mtekere, afande Sezero, coplo Ngoma, afande Mbewa na afande machachali mikwara mingii Stanslaus Makoba ''kadebra'' baiskeli yake iliandikwa ''sereuka mwana wa ndege..mnafiki hakosi sababu'' Kombania hii kulikuwa na vijana akina Robert Nyamhanga, Prudence Timanywa, Mongu Manumbu, Mpemba Francis, Safari Lucian, Redemtus Shoto, Privatus,Anterius Sostenes, Joe Kihampa (TBC1) na wengine. Akina dada kulikuwa na Kore Ally Sadick, Rose Manyama, Judith Schirima, na wengine wengi. Nakumbuka umoja, ushirikiano wa kusaidiana kuepuka visanga baina ya makuruta nk. Siku tukipokea ''kichele'' tulikuwa tunakwenda kijiji cha Kaseke kutumia. -J4 wa D-coy

Jayfour;
Ilikuwa 92/93.
Hivi kumbe hata Joe Kihampa tuiklikuwa naye? Simkumbuki. Possibly alianzia mgombe hivyo wakati anarudi mimi nikawa nimeshahamia HQ.
 
Dah! umenikumbusha mbali sana mkuu..1991/92 op. vyama vingi..Makutupora A-coy tulipangwa kumwagilia bustan.. Lakini baadae tukahamishiwa Bulombora, D-coy. Namkumbuka afande Mnzena, Mtekere, afande Sezero, coplo Ngoma, afande Mbewa na afande machachali mikwara mingii Stanslaus Makoba ''kadebra'' baiskeli yake iliandikwa ''sereuka mwana wa ndege..mnafiki hakosi sababu'' Kombania hii kulikuwa na vijana akina Robert Nyamhanga, Prudence Timanywa, Mongu Manumbu, Mpemba Francis, Safari Lucian, Redemtus Shoto, Privatus,Anterius Sostenes, Joe Kihampa (TBC1) na wengine. Akina dada kulikuwa na Kore Ally Sadick, Rose Manyama, Judith Schirima, na wengine wengi. Nakumbuka umoja, ushirikiano wa kusaidiana kuepuka visanga baina ya makuruta nk. Siku tukipokea ''kichele'' tulikuwa tunakwenda kijiji cha Kaseke kutumia. -J4 wa D-coy

Halafu ukimtaja Anterius lazima umtaje na Hussein nasibu, Boaz Nkoko, Muzeli Mazengo, Josephat Kataga (ukicheza naye karata akikupiku nasema "Kuleeeeee', wakati anadondosha karata yake". Aisee umenikumbusha mbali sana.
 
Hongereni mliofanikiwa kuonja utamu wa nchi yetu.
Je,mnaweza kuniambia kuwa J.K.T inaweza kupunguza migomo ya vyuo vikuu kama wabunge wetu walivyo sema mwaka juzi(2010)?
 
Back
Top Bottom