Je, unamfahamu mnyama anayeitwa Nyegere/Honey Badger? Mnyama mwenye wivu kupindukia

Je, unamfahamu mnyama anayeitwa Nyegere/Honey Badger? Mnyama mwenye wivu kupindukia

mkuu naona umedhamilia...ungekuepo enzi za tupac si ungewakataza watu wasitembee kama tupac au wasivae nguo machata ya pac..sasa kama zipo nyingi si ubadilishe kwa nini utake kuongea kwa vitu vidogo tuu ivyo avatar sijui duu wewe jamaa wa wapi..
Mimi wa Arusha
 
Uwiiiiiiiiii nimeogopa sana [emoji27] [emoji27] [emoji27] [emoji27]
Ni hatari Nifah...huyu mnyama msikie tu,yaani kana hasira sana asee,na ni kabishi hatariiiii....Babu alituambia ili kafe ni lazima upige rungu kwenye fuvu kichwani,ukipiga huko mgongoni ni kama unajisumbua tu,sbb kenyewe kana uweze wa kujitunisha rungu ukipiga linadunda kama mpira tu
Maisha ya Kijijini kuna mambo mengi ya kujifunza sana,huu u-mjini kuna mambo mengi tunakosa,kama panya tu mwanaume wa Dsm mpaka asafiri K'koo kununua sumu ya kumuua wakati bush mtu anamminya tu panya na mkono,huyo nyegere akija Sinza si wanaume wote nyeti zitakwanguliwa?Ha ha ha ha ha ha ha
Wacha kabisa habari ya nyegere...RIP my Babu...Alitufundisha mengi juu ya maisha ya wanyama wakali na jinsi ya kukabiliana nao
 
Wacha uwongo, nyegere hajambii mzinga wa nyuki hata siku moja. Ni kweli kuwa yeye anakula asali na ndiyo maana anaitwa "Honey Badger," ila ikumbukwe kuwa asali si chakula pendwa ama pekee alikacho. Nyegere ni Omnivores maana kwamba anakula kila kitu bila ubaguzi, anakula nyoka tena mambas (koboko) na aina yote ya nyoka bila tatizo kwani ana anti venom inayomfanya asife kutokana na kugongwa na nyoka. Anakula pia wanyama wadogowadogo kama paka hata vitoto vya mbwa na aina zote za ndege mwituni. Akikuta asali anaishambulia bila tatizo na nyuki wala hawamsumbui. Kule kunuka kwake anatumi ile harufu kwa ajili ya ku-mark territories tu au akiwa under threat kutoka kwa wanyama wengine wakubwa kama Simba, chui, fisi, Rock python na wengineo. Anawajambia kuwatishia.
Nyegere ni carnivora mkuu
 
Nitajie jina lako nikuingize kwenye guiness book of records,,,
Mkuu,hiyo haina sifa ya kuingia kwenye guiness book of records ila ipo tu kwenye record ya maisha yangu kilichonisaidia siku ile ni kwamba sikujua napambana na mnyama gani kwa hiyo sikuwa na hofu pili ni ule mpini mfupi wa mudu niliweza kuudhibiti na kuutumia barabara na isitoshe nilikuwa na taa mkononi pengine mwanga wa taa ulikuwa unamchanganya na mwisho kabisa nilikwa nimefunga taulo kiunoni labda kalidhani mimi ni ke vinginevyo kangejua mimi ni me ilikuwa rahisi kuondoka na ikulu yagu
 
Back
Top Bottom