Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Je, unataka kulima mazao ya mbogamboga na matunda lakini unakosa maarifa sahihi? Karibu tushauriane hapa

Kilimo Maarifa.
Asante kwa hizi taarifa.Ninajipanga kulima eka moja kwanza Kijiji cha shauri moyo Rufiji. Nitamwagilia kwa mifereji.Elimu hii itanisaidia.
 
KWA MICHE HIYO 3200 HADI 3500 KWA SUKARI F1 NAWEZA KUPATA MATUNDA MANGAPI? JE KWENYE SHAMBA LA TIKITI NAWEZA CHANGANYA NA MAZAO MENGINE, JE NAWEZA KUPANDA KWENYE SHAMBA NILILOCHIMBA VIAZI NA MAGONJWA YALIYOKUWA KWENYE VIAZI KAMA MNYAUKO YAWEZA KUDHURU TIKITI? NITATUMIA MBOLEA KIASI KUANZIA KUPANDA NA KUKUZIA. ASANTE SANA.
 
Taarifa nzuri [emoji817] ✔
Elimu madhubuti [emoji817] [emoji818]

Swali nitafanyaje ili matunda ya baki mawili tu? Asante
 
UNAYATOA NA MIKONO YALE MATUNDA MENGINE YANAYOENDELEA BAADA YA HAYO 2, LAKINI 3 NI STARDARD KUBAKI YATAKUWA MAKUBWA KULIKO KUACHA 5 AU 7 KAMA WENGINE WANAVYOFANYA YALE YANAYOENDELA BAADA YA YALE 4 YA KWANZA UNAKUTA YANAKUWA MADOGO, NA HATA MENGINE HUWA HAYAFIKII HATUA YA KUKOMAA YANAKAUKA.
Niliwahi sikia Kuna kukata matawi. Je nayo hufanywaje?
 
NEW NEW NEW 22/01/2016
=================================


BAADHI YA TAARIFA ZA ZIADA KWA WAKULIMA WA TIKITI

-Utahitaji kwa wastani gram 250-hadi 350 kupanda kwa eka 1
MBEGU Itakugharimu wastani kati ya TSH130,000 hadi 250,000TSH

-Utakuwa na miche kati ya 3200 hadi 3500 kwa eka 1

-Nafasi ya kupanda
xxx SM 90 Kutoka mche mmoja hadi mwingine, na sm 150=1.5Mita kutoka KATIKATI YA tuta moja hadi lingine-Njia ya umwagiliaji ni DRIP

AU sm 100 kutoka mche mmoja hadi mwingine, na sm 200=Mita 2 Kutoka katikati ya tuta moja hadi Lingine-Njia ya Umwagiliaji ni DRIP

KUMWAGILIA KWA MIFEREJI (Furrow Irrigation)
-Tengeneza jaruba la upana wa mita 2 hadi 3, lenye urefu wowote ule unaoweza kuhimili kutoa huduma urefu wa weza kuwa mita 5 hadi 10mita
-Kisha katikati ya jaruba pafanye pawe sunken-Pabonyee kidogo
-Utapanda mbegu zako kwa nafasi hizo hapo juu Sm 90 au 100 kutoka mche mpaka mwingine, panda pembeni mwa hizo pande nne za jaruba, upande chini kidogo karibu kabisa na kitako (chini) ya jaruba

-Kisha tikiti zitakapoanza kuota utazitrain zote zije kulala hapo katikati (sunken center)

Aina ya Mbegu- Mistari-MUDA WA KUKOMAA UKUBWA (KG) Kampuni

1.SUKARI F1-Mistari ya Punda milia siku 80-90 7-14 kg -East African Seed
2.
-J
ulina F1-Mistari ya punda milia siku 85-90 8-12kg -Kibo seed
3.-Mshindi F1-Mistari ya punda milia Siku 75-80 5-9 kg -East West seed
4. -
Daytona F1-Mistari ya Punda milia siku 75-80 10-12 kg -Kibo seed
5. -
Jubilee/Tiger stripe-Mistari ya pundamilia siku75-85 5-12kg -East African Seed
6..-
Creemson sweet Ni la kijani tu siku 80-85 5-10 kg -Kibo seed

BAADHI YA MBEGU ZINAZOHIMILI MAGONJWA
1.-Juliana is the best huhimii magonjwa mengi ya ukungu na wadudu
2.-Daytona F1-Huhimili sana magonjwa ya ukungu shambani
3.-Creemson Sweet-Hustahimili magonjwa ya Ubwiri Unga/Ubwiri Poda/Powdery Mildew

Mkuuu niendelee kutoa Shukrani nyingi kwa elimu yako. Kuhusu document ya kitunguu nimekuemail. Sasa hapa kwenye tikiti napata shida kuelewa haya matuta ya kutumia furrow. Naomba more elaboration mkuu.
Nakushukuru
 
mseminari mdogo


Unachosema kiongozi kipo pia kinafanyika ila si na wakulima wote, Ila kiutaalamu kinaruhusiwa, Ntaeleza hapa chini

1, Ni kuwa ukishahesabu katika kamba moja ukapata vile vitumba vyenye tikiti viko vitatu , baasi yale maua mengine yanayokuja kuleta tikiti la nne na kuendelea unayaondoa.

Na kiutaalamu tunashauri yale matunda 3 yawe katika main stem-Maana hii main stem (Shina kuu) ndiyo ina tissue muhimu za kusafirishia maji (Xylem) na chakula (Virutubisho) (Phloem), yaani matunda yawe katika shina/kamba mama ile KAMBA iliyotoka chini SIYO MATUNDA yaje kujitengenezea katika secondary brach (Tawi la pili) lililo gawanyika kutoka katika kamba kuu (Kamba mama) hayo huwa mengi yanakuwa madogo kwa sababu ya kukosa lishe, na baadhi huwa yanakufa/nyauka

2, Pia baada ya kupata yale matikiti matatu wapo ambao hukata ile kamba mbele ili chakula kisiendelle kwenda kule mbele ambako hakuna matikiti so unakuwa ni upotevu wa lishe ya bure, hata kama ni dawa za wadudu unakuwa unaspary kule mbele sehemu ambayo haina production inakuwa ni hasara,


Niliwahi sikia Kuna kukata matawi. Je nayo hufanywaje?
 
chayowa

Kiongozi Nashukuru sana


-Kuhusu E-mail


-Email yako nimeiona na nimeshakujibu mkuu-Karibu sana


Kuhusu haya matuta ya Tikiti ya kutumia furrow

-Inakuwa hivi mkuu, Haya ni majaruba yanakuwa kama ya mpunga (kama ulishayaona) yanakuwa mapana, na hayainuki kuja juu, haya yanabonyea katikati au unayafanya yanakuwa flat tu, kwahiyo unachokifanya unavuta udongo kutoka pande zote nne zinainuka kiasi upana huwa tunashauri uwe angalau mita 2 hadi 3 urefu ni ule utakaoweza ila tunashauri angalau uwe mita 5 hivi

-Sasa kinachofanyika kiongozi, yanakuwa kama yale matuta ya nyanya ya kumwagilia kwa njia ya mifereji (furrow), yaani maji unayaingiza kwa block, huku zingine unafunga

-Mbegu za tikiti unazipanda chini/ukingoni mwa tuta karibu kabisa na hiyo furrow ili maji yanapopita kufuaa ile mifereji ya pembeni mwa tuta ile mbegu/miche ya tikiti inapata hayo maji

-Mche wa tikiti ukianza kutambaa sasa ndio unaanza kuutrain uje kulala/kutambalia pale katika ule upana wa mita 2 ulioacha mkuu, kwa hiyo Tikiti zote za pande zote nne unazileta zije kutambalia hapo juu mwa tuta lako

Nadhani umenipata
Email nimeipata mkuu.
Matuta nimeyapata sasa vizuri. Hii ni nzuri kwa sisi ambao ndio tunachipuka tusio na drips kwa sasa.
Pdf ya kitunguu wow.. Tam sana. Hapa ninavyopita niko kama naangalia filam mkuu. Inaeleweka vyema sana sana. Inanionesha shambani kabisa from kuanza hadi kuanza kufunga pesa baada ya kuvuna. Nitaifanyia kazi ilasavyo.
Nashukuru tena mkuu.
 
mseminari mdogo


Unachosema kiongozi kipo pia kinafanyika ila si na wakulima wote, Ila kiutaalamu kinaruhusiwa, Ntaeleza hapa chini

1, Ni kuwa ukishahesabu katika kamba moja ukapata vile vitumba vyenye tikiti viko vitatu , baasi yale maua mengine yanayokuja kuleta tikiti la nne na kuendelea unayaondoa.

Na kiutaalamu tunashauri yale matunda 3 yawe katika main stem-Maana hii main stem (Shina kuu) ndiyo ina tissue muhimu za kusafirishia maji (Xylem) na chakula (Virutubisho) (Phloem), yaani matunda yawe katika shina/kamba mama ile KAMBA iliyotoka chini SIYO MATUNDA yaje kujitengenezea katika secondary brach (Tawi la pili) lililo gawanyika kutoka katika kamba kuu (Kamba mama) hayo huwa mengi yanakuwa madogo kwa sababu ya kukosa lishe, na baadhi huwa yanakufa/nyauka

2, Pia baada ya kupata yale matikiti matatu wapo ambao hukata ile kamba mbele ili chakula kisiendelle kwenda kule mbele ambako hakuna matikiti so unakuwa ni upotevu wa lishe ya bure, hata kama ni dawa za wadudu unakuwa unaspary kule mbele sehemu ambayo haina production inakuwa ni hasara,
Asante nitafanya hivyo.

Sent from my PTM-Z-mini using JamiiForums mobile app
 
Mkuu tunaisubiri kwa hamu hiyo. Hivi mkuu kumwagilia nyanya kitaluni na maji yenye mchanganyiko wa mbolea niufanye angau mara ngapi tofauti na ule wa kawaida wa kila siku asubuhi na jioni?
 
NAOMBA KUULIZA JE NAWEZA KUPANDA NYANYA AINA YA ANNA FI SEHEMU YA WAZI NA SIO KWENYE GREEN HOUSE NA IKAZAA VIZURI. JE EDEN F1 NAWEZA MWEZI WA TISA ILI NIVUNE MWEZI WA KUMI NA MOJA NA MBILI KWA NJIA YA KUMWAGILIA, AU INAFAA MASIKA TU. ASANTE
 
chayowa

SAWA KIONGOZI PDF YA NYANYA IKIWA TAYARI NTASEMA

1. UMWAGIA MAJI YENYE MBOLEA UNAWEZA KUWA UNAUFANYA KWA KILA BAADA YA SIKU 7(kwa wiki mara moja, so unaweza kuwa unafanya kila jumatatu unamwagia asubuhi maji yenye mbolea)- KWA MAZAO AMBAYO HAYAMALIZI MWEZI KITALUNI. Hii iko applied sana kwa mashamba ambayo yamekuwa yakilimwa mara kwa mara-RUTUBA YA UDONGO UNAKUTA IKO CHINI SANA. LAKINI kama shamba ni virgin/HALIJAWAHI KULIMWA, utamwagia MAji yenye mbolea mara 2, ile wiki ya kwanza miche ikiota na ile wiki ya mwisho utakapokuwa unakaribia kuitoa iende shambani

2. NA UNAWEZA KUWA UNAMWAGILIA KILA BAADA YA SIKU 14 KWA MAZAO YANAYOMALIZA ZAIDI YA MWEZI KITALUNI KAMA KITUNGUU etc

Bila shaka umenipata.
Nimekupata sana mkuu.
Nashukuru mno mno
 
kilimomaarifa.tajiri nimelima matikiti sasa yako tayarikuvunwa ila kuna ugonjwa wanaita dot.com yaani matikiti yanakuwa na vidoti kwa chini kule kunakogusa chini je kuna namna yeyote ya kuzuia huu ugonjwa? ili wakati mwingine nikilima niweze kutibu kabla
 
Mkuu Habari,naomba Kufahamu Mambo Yafuatayo: 1.Kuna Dawa Inaitwa Swing Sc Nimeambiwa Ni Dawa Ya Kuzuia Mnyauko(wilt) Kwenye Mimea Kwamba Inapulizwa Kwenye Mashimo Kabla Ya Kupandikiza Sasa Naomba Kujua Ni Kweli? Pia Naomba Kujua Ni Kwa Namna Gani Naweza Kuzuia Athar Za Mvua Kwenye Kitalu Cha Nyanya? Namaanisha Maji Kupita Kiasi Na Ukungu Na Je Net Au Nyasi Zinaweza Kusaidia? Pia Kuna Ugonjwa Wa Kiuno Wa Miche Ya Nyanya Mara Kadhaa Nimeona Ukitokea Hata Kama Kitalu Kilichomwa Moto Kabla Ya Kuatika Mbegu. Nini Husababisha? Na Ninatibu Vipi Ugonjwa Huu Kwa Miche Ambayo Tayari Imeathirika? Na Je Kuna Dawa Yeyote Ambayo Naweza Kupuliza Kama Kinga?
 
POLESANA MKUU; -JARIBU KUWA BRIEF KIDOGO ILI NIKUELEWE ZAIDI, NI VIDOT VYA NAMNA GANI (RANGI, SAIZI ETC)-VIKOJE HIVYO VIDOT???

JE NI SHIDA KAMA HIZI HAPA CHINI??/

1574000-SMPT.jpg
1575412-SMPT.jpg
ndio, ni kama hivyo ila sio vimetobolewa na wadudu, vinakuwa vidoti kama hivyo ila vya brown ambayo ukifanya kama kukanyaga hilo tikiti linatoa maji.
 
Mkuu kilimo nyanya imekubali kitaluni ila vilepeo weupe nimewaona around leo. Nina duduall na dimethoate zaweza kuwadhibiti au nikatafutr nyingine? Nilikuwa jumamosi nizipeleke shambani je niendelee kuwashughulikia hawa jamaa kwanza hadi wafie mbali au naweza hamisha baada ya kupiga dawa tu. Nashukuru mkuu
 
Dah mkuu moyo wabubujika kwa furaha. Mungu akupe faraja ya moyo wako.. Nimefarijika sana. Nakumbuka sana mkuu.. Kiganja kimoja kimenyooka kwenye kita 15 zangu.. Starter soln. Ngoja nipambane.. Nina imani ndio njia inanyooka ya matamanio ya moyo wangu. Kuwa mkulima bora..

Nashukuru
 
Back
Top Bottom