Je, utamkumbuka Hayati Magufuli kwa mambo gani?
Ni ukweli tulikuwa tunampenda sana ,na haya mambo yavyoendela humu nchini,ata wale waliokuw hawampendi zamani sasa wanazidi kuongezaka kumpenda.

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app
Hayo ni mapenzi ya kinafiki, mtu aondoke ndipo aanze kupendwa. Hakuna rais wa TZ kati ya wote sita anayeweza kupendwa kwa dhati akiwa ikulu, ni unafiki tu unatusumbua.
 
Siku SGR na Stigers gorge vikikamilika ndio siku ambayo wananchi wa taifa hili wataomba kwa vinywa vyao itengwe siku maalumu kila mwaka ya kumkumbuka kama tunavyofanya kwa Mwalimu Nyerere
 
Wapo wanaomsema kwa mazuri yake magufuri na tupo sisi pia huwa hatutaki hata kulisikia jina lake likitamkwa popote pale, sisi waislamu akitamka sheitwani huwa tuna utaratibu wa kumlaani na tunasema kwa sauti laanatullah maana yake laana za mwenyezi mungu ziwe juu yake. Magufuri akitamkwa sehemu yoyote ile kimoyomoyo huwa nasema laanatullah 😎😎 yule jamaa alipoteza dira za watu na mpaka leo watu wanavidonda mioyoni mwao vilivyosababishwa na machungu waliyoyapitia kwenye utawala wa magufuri.
 
Mtabiri.., Wapiga Deals, na Walamba Asali hata kama walikuwa hawapo kipindi kile sasa hivi wapo maradufu...

Pia wale aliosema watauza vyuma vya madaraja alikosea kidogo, ni watu wake (Chama Chake) wanauza Nchi..., (Hata Ndugai Kipofu aliweza kuona)
 
View attachment 1734652
Picha: Hayati Rais Magufuli enzi uhai wake

This is a special thread and a tribute to the late J.P.M.

Najua tupo katika kipindi cha masikitiko kama taifa, Jemedari wetu amefariki dunia, kama lisemavyo neno la Mungu katika kitabu cha biblia kuwa mfalme hawezi kuokolewa kwa na jeshi lake kubwa bali ni Bwana hutuponya na mauti (Zaburi 33:16), yaliyoandikwa yametimia Mungu amlaze mahala pema peponi.

Hakika tutammiss, kama ule usemi usemao umuhimu wa mtu huonekana zaidi asipokuwepo.

Yafuatayo ni mambo aliyonikosha J. P. M (R. I. P).

1. Nidhamu kwenye taasisi za serikali, kuanzia matumizi, utendaji wa kazi na utoaji wa huduma.

2. Msimamo bila kujali nchi nyingine zimeamuaje, kimsingi maamuzi mengi yalifanywa kuzingatia maslahi ya nchi sio mkumbo ( i.e chanjo ya corona).

3. Super-Mega projects zenye maslahi ya muda mrefu, S.G.R, Nyerere, Mwendokasi n.k.

4. Kuwanyoosha majirani zetu walizoea kutuibia na kutuchezea michezo ya ajabu ajabu.

5. Kuleta siasa za kuambiana ukweli na sio za kubembelazana hovyo.

6. Kukomesha ujambazi na matukio ya kihalifu majumbani.

7.

Itaendelea...

PIA SOMA>> TANZIA - Rais John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar
Nitamkumbuka Kwa kuua wapinzanzani wake kisiasa kwakua hakua na uwezo wa kujenga hoja kisiasa Bali uongo na unafiki ulimjaa
 
View attachment 1734652
Picha: Hayati Rais Magufuli enzi uhai wake

This is a special thread and a tribute to the late J.P.M.

Najua tupo katika kipindi cha masikitiko kama taifa, Jemedari wetu amefariki dunia, kama lisemavyo neno la Mungu katika kitabu cha biblia kuwa mfalme hawezi kuokolewa kwa na jeshi lake kubwa bali ni Bwana hutuponya na mauti (Zaburi 33:16), yaliyoandikwa yametimia Mungu amlaze mahala pema peponi.

Hakika tutammiss, kama ule usemi usemao umuhimu wa mtu huonekana zaidi asipokuwepo.

Yafuatayo ni mambo aliyonikosha J. P. M (R. I. P).

1. Nidhamu kwenye taasisi za serikali, kuanzia matumizi, utendaji wa kazi na utoaji wa huduma.

2. Msimamo bila kujali nchi nyingine zimeamuaje, kimsingi maamuzi mengi yalifanywa kuzingatia maslahi ya nchi sio mkumbo ( i.e chanjo ya corona).

3. Super-Mega projects zenye maslahi ya muda mrefu, S.G.R, Nyerere, Mwendokasi n.k.

4. Kuwanyoosha majirani zetu walizoea kutuibia na kutuchezea michezo ya ajabu ajabu.

5. Kuleta siasa za kuambiana ukweli na sio za kubembelazana hovyo.

6. Kukomesha ujambazi na matukio ya kihalifu majumbani.

7.

Itaendelea...

PIA SOMA>> TANZIA - Rais John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar
kwakweli nitamkumbuka kwa kupiga marufuku kusema vyuma vimekaza.
 
1.Wasaliti wa nchi na viherere wa kujipendekeza kwa wakoloni kubinywa!

2.,Flyover Dar!

3. Barabara njia NNE ubungo

4. SGR

5. Wakati wa CVD alisema, tuchape kazi, kisha wale wa kujifungia, watakuja t tuwauzia chakula, na mpaka sasa tunakula chakula cha kipindi cha korona, maana tokea hapo, wakulima hawajazalisha tena!



Tuongezee mengine mazuri
 
Mnahangahika kumnadi marehemu ambaye alikataliwa na Muumba kwasababu ya uovu wake.
Mkuu, umekosea Uzi! Unahusu tu, kama kichwani cha habari kisemavyo!

Kwani hujui kusoma na kuelewa!

Hata hivyo, Kwa Mungu hakuna mtenda mema wala mabaya, wote tutakufa ukiwapo na wewe
 
Mkuu, umekosea Uzi! Unahusu tu, kama kichwani cha habari kisemavyo!

Kwani hujui kusoma na kuelewa!

Hata hivyo, Kwa Mungu hakuna mtenda mema wala mabaya, wote tutakufa ukiwapo na wewe
Lakini yule kafa kifo cha mpumbavu.
Mpumbavu huvuna mali akitaraji kukaa kitako ale ndipo anakufa.
Yule kaiba kura kaanza kutawala tu kafa.
Kawarubuni akina Bashiru na Polepole wabadili katiba ya ndani ya chama kimyakimya ili atawale mpaka uzee kafa.
 
Yapo mengi ikiwa ni pamoja na Lissu kupigwa marisasi mchana kweupe kujenga chato airport kuokotwa watu kwenye viroba kuwavesha makalatasi machinga Kisha kuwabatiza jina la wanyonge Huku 20 20 zao akipiga yeye na mganga biswaro na mengine meeeeeengiiiiii kweli atakumbukwa natuseme Kwa saut kuuubwaaa HUYU NI SHUJAAAAAAA.
 
Jamaa aliijua jamii ya kitanzania vyema,alipowaambia watu wa Daresaalam kua 'atakayebaki mjini niwanaume',wapiga dili walijua anatania,acha awabane,walinywea kinoma.
Kwenye inshu ya vyeti feki,alibana kinoma,japo kuna tangazo nimeliona Jana kua wanalipwa na kurudishwa kazini,na huo ni mwanya kwa ma-HR kupiga pesa,na kuingiza watu wao,ila jamaa alibana kinoma.
 
Mbna wale vyeti feki waliojazana jeshin na polisi aliwagwaya.???
Jamaa aliijua jamii ya kitanzania vyema,alipowaambia watu wa Daresaalam kua 'atakayebaki mjini niwanaume',wapiga dili walijua anatania,acha awabane,walinywea kinoma.
Kwenye inshu ya vyeti feki,alibana kinoma,japo kuna tangazo nimeliona Jana kua wanalipwa na kurudishwa kazini,na huo ni mwanya kwa ma-HR kupiga pesa,na kuingiza watu wao,ila jamaa alibana kinoma.
 
Mimi sitamsahau alivyonijibu kwamba kama siwezi kuingia vyoo vya kulipia basi nibaki na mavi yangu nyumbani!
 
Hayatajiki, hayahesabiki; ila mojawapo ni lile la kumchukua Mama kama mgombea mwenza Julai 2015!
 
Back
Top Bottom