Je, utamkumbuka Hayati Magufuli kwa mambo gani?
JPM ulifahamu yaliyokuwa yanaendelea nchini katika utumishi wako wa miaka ishirini na tano kwenye medani ya siasa. Wakati wa uongozi wako ulijali Sana wananchi wa daraja la chini ambapo tulinunua mchele tsh. 1200/= kwa kilo; kwa utawala wa Sasa unaojipambanua kwa kuingiza magari 60 ya Mwigulu Lameck Nchemba kwa siku moja; kilo moja ya mchele kwa Sasa tunainunua kwa tsh. 3500/=. Hakika tutakumbuka baba ila uliokuwa umeziba mirija yao ya matumizi mabaya ya fedha ya umma daima wataendelea kukulaani bila kufahamu kuwa ulishalala milele na hakuna siku amabayo utaweza kuwajibu.

Wamebaki wanasiasa uchwara akina Hussein Bashe wasiofahamu hata jembe linashikwaje lakini eti leo Bashe ndye waziri wa kilimo. Wananchi tunaumia Sana Tena Sana lakini BEPARI Bashe anajinasibu kuwa mazao sio Mali ya serikali kwa hiyo wakulima waachwe wauze wanavyotaka. Mkulima wa kawaida hanufaiki na kauli ya kijinga, KEJELI, DHIHAKA na KIZANDIKI ya bepari Hussein Bashe bali anawapaka mafuta kwa mgongo wa chupa kwani wanufaika wakuu wa mfumuko Mkubwa na wa kutisha wa Bei ya chakula Ni bepari Bashe na washirika wake.

Wakati wa uongozi wako hakukuwa na nyongeza ya mshahara lakini maisha yaliendelea bila shida kutokana umakini wako wa kudhibiti mfumuko wa Bei ya chakula. Leo mtu anaona vema kuhudumia watoto wa jirani wake wakati nyumbani kwake watoto wa wanalala njaa!. Daima tutakumbuka JPM.
Aisee mbona bashe ni mkulima wa mpunga huko kwao nzega tokea akiwa mwanafunzi? Hilo la bashe kutokujua kushika jembe umelipata wapi?
 
..
 

Attachments

  • JamiiForums839866055.jpeg
    JamiiForums839866055.jpeg
    46.5 KB · Views: 7
  • 1679652251550.jpg
    1679652251550.jpg
    74 KB · Views: 6
  • IMG-20200403-WA0003.jpg
    IMG-20200403-WA0003.jpg
    12.9 KB · Views: 7
Kwa kuwa tunaamini kimwili haupo na sisi ila kiroho upo na sisi, naomba nikupe taarifa hii.

1. Nyumba yetu uliyoiacha ikiwa haivuji kwa zaidi ya 91%, sasa inavuja karibu kila kona kwa zaidi ya 78%.

2. Panya na mchwa uliowafunika na jiwe zito ili wasiendelee kuleta usumbufu katika nyumba yetu, mlinzi wa nyumba amewafungulia na amewapa kazi ya kulinda ghala la chakula chetu.

3. Cha ajabu kabisa na cha kushangaza ni kwamba, mlinzi aliyewakaribisha panya na mchwa chumbani, ndiyo huyo huyo anayetoka hadharani kulalamika eti panya na mchwa wametafuna nguo na kuharibu chakula kilichohifadhiwa.

Mlinzi huyu kazi yake kubwa ni kulalamika tu bila hata kuwachukulia hatua kali hawa panya na mchwa ikiwa ni pamoja na kuwafukuza hapa nyumbani.

Kwa ujumla Baba, hali ya nyumba yetu si shwari kabisa.

RIP Shujaa wetu, JPM.
 
Hii ni ishara ya kuwa unawaamini watu wengine kuliko unavyo jiamini wewe mwenyewe.

Huyu unae msema hawezi kukusia all Isha kufa, kuna sehemu Kuna shida upambane tulio Hai kurekebisha Marehemu Hana msaada kwa tulio Hai hata tumsifu vipi
 
Kwa kuwa tunaamini kimwili haupo na sisi ila kiroho upo na sisi, naomba nikupe taarifa hii.

1. Nyumba yetu uliyoiacha ikiwa haivuji kwa zaidi ya 91%, sasa inavuja karibu kila kona kwa zaidi ya 78%.

2. Panya na mchwa uliowafunika na jiwe zito ili wasiendelee kuleta usumbufu katika nyumba yetu, mlinzi wa nyumba amewafungulia na amewapa kazi ya kulinda ghala la chakula chetu...
Nini kilimtoa Prof. Assad offisini kama so kuhoji ufisadi wa lile chizi lenu
 
Baba wakati wako ulikuwa unakula peke yako na Wananzengo ulio wachagua mwenyewe ila Sasa kila mtu anakula kwa urefu wa kamba yake.

Miradi uliyoiacha inaendelezwa kwa kiwango Cha kuridhisha na itakamilika ila waimba mapambio wako wanamkwamisha mama.

Anajitahidi ila kundi lako halifurahii mafanikio yake.

Demokrasia imetamalaki ila enzi zako hali ilikuwa mbaya.

Uendelee kuongoza Malaika wa kuzimu salama.
 
RIP JPM ama kweli tutakukumbuka 1. 1..TOTO Afya Kodi hamna tena huku baba.

2. Mchele tulionunua 1600 sasa ni 3500 baba.

3. Baba Petrol uliacha 1900 sasa ni 3000.

4. Bwawa la Nyerere halijanza mpaka leo.

5. Baba wajua kwamba tulichanjwa na chanjo ya COVID 19 na mikopo juu?.

6. Nakunong'oneza baba "Eti Mwigulu Nchemba Ndiyo waziri wa fedha, Makamba nishati na Nauye mawasoliano.".

7. Mwanza tulienda Kwa elfu 45 Sasa billa 65000 hufiki.

Ni hayo tu Kwa leo Mzee wetu
 
Ngoja vyeti feki waje uone utakavyooga matusi.

Kuna muda ni heri tu mngemwacha huyu mzee akapumzika kwa amani,kuliko kumtaja taja,mnaganya anazidi kutukanwa kila kukicha.
 
Unamuomba mfu kweli kabisaa?

Au ndiyo kutafuta kiki?
Amefikisha ujumbe kwa njia ya sanaa.

Humo ndani pia kataja,mchwa,panya,nyumba nk. Hivyo vyote si vitu halisi katika katika context ya alichokikusudia kufikishia hadhira. Ni sanaa na usanii ili ujumbe uwafikie wahusika.
 
Amefikisha ujumbe kwa njia ya sanaa.

Humo ndani pia kataja,mchwa,panya,nyumba nk. Hivyo vyote si vitu halisi katika katika context ya alichokikusudia kufikishia hadhira. Ni sanaa na usanii ili ujumbe uwafikie wahusika.
Yeye mwenyewe chawa.
 
Back
Top Bottom