Je, Viongozi hao kuhudhuria hafla za makanisani ni mpango wa kuwagawa wakristo kwa sababu ule upande wako pamoja kuhusu DP World?

Je, Viongozi hao kuhudhuria hafla za makanisani ni mpango wa kuwagawa wakristo kwa sababu ule upande wako pamoja kuhusu DP World?

Tanzania ni kubwa na muhimu kuliko makundi yenu ya kiimani

Kama vitisho endeleeni kutisha Kondoo wenu sio Rais na Serikali yake

Wakumbusheni Viongozi wenu wa kiimani tunawaheshimu sio kwa kuwa hatujui madhaifu yao, bali kwa kuwa wanaheshimiwa na wale tunaowaheshimu tu.

Mmeshakumbushwa kwa lugha laini sana 'Hakuna mwenye ubavu wa kuleta choko choko ' na pia mmetolewa wasiwasi pia kuwa hakuna ' Mwenye ubavu wa kuuza rasilimali za Nchi'

Mkiheshimu Mamlaka nanyi mtaheshimiwa na mkileta vitisho na Propaganda mtapuuzwa tu hata na wafuasi wenu
Kwahiyo kondoo, Raisi na Serikali yake wametishika? 😜

Waambie wasiogope bana, lakini na Serikali pia isiwatumie vibaya viongozi wa dini kuwahadaaa kinafiki kwamba kila hafla ya serikali viongozi wa dini hupewa nafasi ya mwanzo kusema au kuomba mpaka ikulu.

😜 Lakini waikiikosoa serikali tu pale ambapo wanaona kunaweza kuhatarisha umoja na amani kitaifa, utaskia ooh wanachanganya dini na siasa 😜.

Kwahiyo mnavowaalika kwenye majukwaa yenu ya kisiasa na dhifa za kitaifa na kuwapa nafasi za mbele kabisa huwa mnachanganya mahindi na mchele au ni nini?

Au mambo yakiwa shwari sio mchanganyo wa dini na siasa ila mkiambiwa ukweli ndio kuchanganya dini na siasa.

Kwani pale Mahakama kanda ya Mbeya ilipotoa hukumu ya kesi ya Mwambukusi kupinga mkataba wa dipi weldi , iliposema mkataba wa uwekezaji wa dipi weldi na Serikali ya Tz hauna shida ila zipo kasoro zinaweza kurekebishwa, je hii tunaitaje?

Kwani hawa viongozi wa katoliki mbona ni kama vile hawana shida na mkataba wenyewe ispokua wanachodai ni hizo kasoro kurekebishwa tu na mambo yaende.....

Na hawa wakatoliki inaonekana ni wasomi mno, wanachofanya ni Maandamano ya kisayansi na kisaikolojia tena yasiyo na na kibali cha mwanadamu bali Mungu. Hii ni hatari sana, na serikali imeshindwa na kamwe haitaweza kabisa kuyazuia. Na naskia yatuendelea kwa majuma 6 zaidi.

Na Viongozi wa Maandamano wamejiorodhesha hadi majina 🤓 ni Maaskofu 37, halafu waandamaji ni maparoko, waamini wote wakatoliki waliohudhiria misa Jpili, viongozi wa Jumuiya na familia zote za kikatoliki, dah! akili nyingi bana saa zingine 😜

Sasa utawaweka jela gani, halafu naskia na wao wanajilaumu kutokuchukua nafasi za uongozi chaguzi zilizopita licha ya kuhamasishana kupiga kura.
Wanajutia if you don't want to take part in political administration don't blame to be ruled by a fool.

Safari hii sijui itakuajee 2024-2025....
 
Wasalaam JF,

Nichukue fursa hii kuhoji uwepo wa JKM kwenye hafla ya wasabato je yeye mwanasiasa alienda kufanya nini kwenye hafla ya dini ya wengine? Je, Huyo Rais wenu alienda makanisani kufanya nini?

Hii mbinu ya kudhani mtawagawa wakristo wakati nyie mmekula kiapo cha pamoja cha kuunga juhudi za kujinasibu na DP World.

Tunafahamu karibia waislam asilimia 95% kwenye mitandao wana unga mkono hilo limkataba la kuuza Tanganyika. Je, Kinachofanyika sasa ni jitihada za kuwagawa wakristo ili mpate ushindi wa dhuluma?

Wakristo washajua hilo toka waislam wamejipumbaza Kwa kueneza udini na kutamka bayana nao wakristo wana akili nyingi tena sana. Hao wasabato na walutheri wamewapaka mafuta kwa mgongo wa chupa, waumini hawapo hivyo Umoja wa Imani yao katika utashi wa kulipenda taifa na Mali zake ni mkubwa mno.
Wakristo sio mazuzu wanawachora tu. Anaegawa taifa ni huyo aloleta hio IGA ya DP World.

Shukrani 🙏
Akili ndogo haiwezi shindana na akili kubwa hata siku moja
 
Tanzania ni kubwa na muhimu kuliko makundi yenu ya kiimani

Kama vitisho endeleeni kutisha Kondoo wenu sio Rais na Serikali yake

Wakumbusheni Viongozi wenu wa kiimani tunawaheshimu sio kwa kuwa hatujui madhaifu yao, bali kwa kuwa wanaheshimiwa na wale tunaowaheshimu tu.

Mmeshakumbushwa kwa lugha laini sana 'Hakuna mwenye ubavu wa kuleta choko choko ' na pia mmetolewa wasiwasi pia kuwa hakuna ' Mwenye ubavu wa kuuza rasilimali za Nchi'

Mkiheshimu Mamlaka nanyi mtaheshimiwa na mkileta vitisho na Propaganda mtapuuzwa tu hata na wafuasi wenu
Ishu ni kuzijibu hoja zao.
Ukitaka kujua nguvu za Imani subiria uchaguzi
 
Back
Top Bottom