Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Je, Viongozi wa Idara ambao ni Wachagga waachie ngazi!??

Status
Not open for further replies.
Mwanakijiji said:
JokaKuu.. tatizo la mambo ya Ukabila ni kuwa it is not rational. Mtu mwenye kuona ukabila anaitikia jambo hilo kwa hisia na vionjo na siyo kwa akili, kwani ukimuuliza onesha ukabila yeye atakuonesha namba. kama vile mtu mwenye udini akatavyoonesha namba. Wote wawili mkabila na mdini hawaangalii hoja za kiakili kwani wanaitikia kivionjo na hisia.

Ukiangalia humu utaona jinsi gani watu kwa mbali wanavumbi vumbi la ukabila dhidi ya Wachagga, si kwa sababu nyingine yoyote isipokuwa wivu wa kwanini wao wamefanikiwa kuliko watu wengine.

Ni kwa sababu hiyo mimi naamini mtu wa hatari sana kwenye suala hili sasa hivi atasikika Bungeni siku moja akimwaga sumu yake ya ukabila.


Mwanakijiji,

..mimi sina tatizo na mtu atakayetuletea number na kutuhumu ukabila.

..lakini baada ya kuwa na number na kutambua ukabila what do we do next? hatujiulizi ni kitu gani kimewezesha kupatikana kwa hiyo number kubwa ya kabila fulani.

..watu wanalalamika uwepo wa, say wahasibu 20 wa kichaga TRA. wanamtuhumu CEO wa TRA kwa ukabila. hilo linafanyika bila kujiuliza hawa wahasibu 20 wamepatikana vipi. it takes at least 18 yrs to train an entry-level accountant.

..zaidi ni kwanini CEO wa Kichaga at any time anaweza ku-recruit wahasibu 20 wa kabila lake, lakini CEO wa Kimakonde hawezi kupata idadi hiyo ya wahasibu hata kama ana nia ya kuwa mkabila?

..kama tuhuma hizi za ukabila zingetolewa pamoja na mapendekezo ya mbinu za kupambana na ukabila huo mimi ningezielewa. tatizo mara nyingi zinatolewa, si kwa nia ya kuwasaidia wale walioachwa nyuma, bali kwa kuwafanya wale wanaonekana kuwa na "maendeleo" wabaya ndani ya jamii yao.

..halafu hii habari kwamba Wachaga wanajiona superior sijui imetoka wapi. au ni pale mmoja wa wachangiaji aliyesema kwamba Wachaga ni very hard working ndiyo imewakwaza wengine? hivi kuna watu hard working kama Wamachinga wanaotembea toka Kariakoo mpaka Masaki kuuza mashati? na kama kuna ushahidi wa waziwazi wa namna hiyo kwanini mtu akwazike na kusema Wachaga wanajiona superior?

..pia hili jina chasaka...nina hakika kila kabila Tanzania wana neno wanalotumia ku-refer watu wasiotoka eneo lao. kwanini mtu akwazike kuitwa chasaka akitembelea Uchagani, lakini hana tatizo na kuitwa foreigner akienda ughaibuni?

..mimi nafikiri badala ya kushindania viti 6 maalum kwa wabunge wanawake, labda tujielekeze ktk kuangalia ni jinsi gani tutaongeza idadi ya wasomi toka kila kabila/wilaya/mkoa Tanzania.

..tujielekeze katika kuhakikisha kwamba tunatoa elimu ya kiwango sawa ktk kila sehemu ya Tanzania. hilo siyo lengo linalotekelezeka kwa awamu moja ya uongozi, it may take a generation.

NB:

..vilevile huu uchumi wetu nao haukui na ajira haziongezeki. kila Mtanzania amepatolea macho TRA, Tanroads, na taasisi nyingine chache. kwa mfano: nilisoma mahali kwamba kuna vijana wa Kitanzania zaidi ya 100 wana PhD degrees. vijana hao wanalilia wazee waondoke pale UDSM ili wao vijana wapewe nafasi.

..kauli hiyo imenishangaza ukizingatia kwamba inatoka kwa wasomi wetu. kwanini tuwe na kilio kama hicho wakati ndiyo kwanza tumeanzisha Chuo kikuu Dodoma?
 
tukiuliza Maswali Yafuatayo Hapa, Utashangaa Majibu Yake Ambayo Ni Imani Za Watu (hakuna Takwimu Za Kisayansi Kuthibitisha Imani Hizo - Oxymoronic?)

A. Ni Kabila Gani Linapenda Fedha Zaidi Tanzania?
B. Ni Kabila Gani Linapenda Kujitukuza Zaidi?
C. Ni Kabila Gani Linapenda Ufuska?
D. Ni Kabila Gani Wanapenda Kujinyonga?
E. Ni Kabila Gani Hawapendi Kufanya Kazi Ngumu?
F. Ni Kabila Gani Wanapenda Kupiga Wake Zao?
G. Ni Kabila Gani Wanapenda Kuficha Hela Zao Na Hawataki Kuziweka Benki?
H. Ni Kabila Gani Wana Dharau Sana Na Wanyanyasasi Wa Wafanyakazi Wao?

Nawahakikihishia Nikipiga Kura Ya Siri.. Karibu Asilimia 70 Majibu Yenu Yatafanana!
Jibuni Maswali Hayo Hapo Juu Makabila Yote.
 
[QUOTE=Mzee Mwanakijiji;242122]Tukiuliza maswali yafuatayo hapa, utashangaa majibu yake ambayo ni imani za watu (hakuna takwimu za kisayansi kuthibitisha imani hizo - oxymoronic?)

a. Ni kabila gani linapenda fedha zaidi Tanzania?
b. Ni Kabila gani linapenda kujitukuza zaidi?
c. Ni Kabila gani linapenda ufuska?
d. Ni kabila gani wanapenda kujinyonga?
e. Ni Kabila gani hawapendi kufanya kazi ngumu?
f. Ni kabila gani wanapenda kupiga wake zao?
g. Ni kabila gani wanapenda kuficha hela zao na hawataki kuziweka benki?
h. Ni Kabila gani wana dharau sana na wanyanyasasi wa wafanyakazi wao?

Nawahakikihishia nikipiga kura ya siri.. karibu asilimia 70 majibu yenu yatafanana![/QUOTE][/I

Kwii kwwiii kwiii kwiii. Ndiyo maana nilikwambia badilisha maada. Tuongelee imani potofu za watanzania kwa makabila na jamii mbalimbali. Maana majibu yataenda kwa makabila mbalimbali. Lakini maada yako ilikuwa ni kwenye nafasi za kazi. Haikuwa masuala ya mitizamo ambayo tunataniana kwenye vijiwe vyetu vya pombe.
 
Dawa ya kuhakikisha kuwa wanajitoa basi ni kuikodisha nchi kwa Wayahudi ama Wapalestina ili waje wakatutawale na hapo itakuwa ni suluhu kwani hakuna mchagga ,mhaya,mkwere,msukuma,mmanyema,mdigo,msambaa,mmasai,mmatengo, n.k atakaye lalamika .
 
ubaguzi ndani ya JF jamani ni hatari ,watanzania tunaelekea wapi? kama watu tuna kuwa wabaguzi kiasi kwamba tuna nyoshea kidole kabila flani kuwa ni mafisadi?

Mzee Mwanakijiji,tafadhali futa usimi wako maana unonekana hapa kama wewe ni mbaguzi .
 
Nadhani historia ya wachaga kuwa kila sehemu za ajira ni kwa sababu ya elimu.
Kwa hili hatuna wa kumlaumu ila ninataka kuchukua nafasi hii kuwapongeza wazee wa zamani wa kichaga ambao bila ufisadi walikuwa na maono ya kuendeleza mkoa wao.
Walijenga mashule katika kila kata (miaka 30 iliyopita) ili kuhakikisha wana wao wanasoma.
Leo wakati ni sera ya sirikali kujenga shule kila kata wao kwao ilikuwa sera isiyo rasmi (kwa maono ua kileo) miaka 30 iliyopita. Leo wanavuna walichopanda na watu wanakasirika. Waacheni wale maana hivyo vyeo na kazi kila idara wamepata kwa haki wala si kwa kuhonga.
Wakati wao walikuwa na mikakati hiyo wenzetu waliongeza juhudi za kuongeza wake na kuona mifugo yao inaongezeka.
Leo wachaga wana dominate kila eneo na hata katika siasa na watu wanalalamika kwamba wachaga wana dominate hata katika vyama. Hii si kweli.
Bora tuanze kufanya mikakati ya kuelimisha wanetu na hapo tutawafikia wachaga. Sijui ni lini!!!!!!!!!!!!
 
Jokakuu,
..halafu hii habari kwamba Wachaga wanajiona superior sijui imetoka wapi. au ni pale mmoja wa wachangiaji aliyesema kwamba Wachaga ni very hard working ndiyo imewakwaza wengine? hivi kuna watu hard working kama Wamachinga wanaotembea toka Kariakoo mpaka Masaki kuuza mashati? na kama kuna ushahidi wa waziwazi wa namna hiyo kwanini mtu akwazike na kusema Wachaga wanajiona superior?
Mkuu labda hujafuatilia masda hii toka mwanzo na kuyasoma kwa makini yale yaliyoandikwa.. Nitasema hivi sababu zote zilizojengwa kutetea mafanikio ya Wachagga yamelinganishwa na makabila mengine..Kwa mfano huwezi kuzungumzia elimu leo hii kuwa kuna makabila yako nyuma... Yameandikwa haya... wapo waliosema kuhusiana TRA nakadhalika hali wakijua fika kwamba miaka ya Nyerere sio leo tena.. Elimu waliyopata Wachagga zaidi ya makabila mengine ilikuwa miaka ya 50 na 60 sio leo na hawa watu wengi wao wamestaafu, bado kuna watu wanachukulia mifano hiyo kwa makusudi kabisa.. Kama mtru kauliza sababu ya TRA kuwepo na wachagga wengi madarakani ni muhimu jibu lihusiane na sababu zinazoweza kueleweka kwa kila Mtanzania.. Hata kama Uhasibu inachukua miaka 10 au hata 20, Tanzania katika miaka hiyo vyuo vyote vya uhasibu vilikuwa na watu wa makabila mengine kuliko Wachagga na nina hakika hawakufanya hata asilimia 20 ya wanafunzi hata ukitazama vyuo vikuu. Sasa iweje leo mseme makabila mengine hayakusoma wakati hamna takwimu za kuthibitisha dhana hizi.
Tatizo kubwa la watu maskini ni ULAJI tu.. mimi nina hakika kwamba kelele zote za maskini ni kwa sababu sehemu hizo za kazi zina loops za kuiba na kujitajirisha! Kila Mtanzania anataka afanye kazi TRA kwa sababu kuna Ulaji. mishahara Tanzania haitoshi..sehemu za deal ndizo kimbilio la kila mtu...Kama vile Ikulu na Mkoloni.

Jokakuu, ebu tazama maneno kama haya:-
Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini.
Vumbi la mambo yote ya kibaguzi husababishwa na UMASKINI wa hoja. Kichwani sifuri kabisa. Uwe ubaguzi wa kikabila, rangi, jinsia au aina yoyote ile, CHIMBUKO ni MUFILISI wa hoja tu. Sasa huu mufilisi wa hoja unakujaje? Ufisadi is one. Just angalia vituko vya yule Wangwe wa CHADEMA: I am avoiding kuandika, ...yule mkurya wa CHADEMA. It is very easy to use such accolades, but then one has to be VERY THICK indeed to remain with such shallow generalizations.
Ni maneno mazito sana ambayo hata kaburu ama mzungu aliyatumia kwa mwafrika. Maneno haya ni dhahiri yanaonyesha jinsi mtu huyu anavyojisikia - Superior!kashindwa hata ku avoid kwani lilikuwa akilini mwake limejenga hema... sasa nina hakika ukimuuliza atasema kwani UONGO!
Haya huyo Wangwe leo anaitwa MKURYA!..lakini Mbowe au Dr. Slaa hatakiwi kuitwa kwa makabila yao!..kweli suluhu itapatikana!.. haya ndio majibishano ya Chadema na Wangwe! hoja na madai ya mtu mmoja yanatufanya tutazame makabila mengine uwezo wao... hii ni hatari sana.
Binafsi sintapenda kabisa kutumia mifano ya mtu mmoja mmoja kuihukumu jamii nzima na hapa ndicho kinachoendelea iwe kwa Wachagga ama watu wa makabila mengine!
 
Mweshimiwa nimesoma ulicho eleza nikidhani utatoa suluhisho linalokubalika kitaalamu.Lakini suluhisho uliloto limenisikitisha

Yani watu waliosoma waachie uongozi kwasababu niwa jamii fulani wawachie uliowaita wasio soma kwasababu ulizozieleza kwa uhakika tutakuua tunarudi nyuma

Kikubwa swala la wachaga wengi kusoma au kufanikiwa iwe ni changamoto kwa watanzania wote Wafunge mkanda wapeleke watoto shule wasisubiri serikali ijenge shule,ilete walimu,ifundishe watoto kusoma na wakati mwengine iwalazimishe wazazi hao kuwapeleka watoto shule (AIBU)

tupeleke watoto shule wasoma kisha mambo yote hayo yatakwisha sio wasomi waache kusaidia kujunga taaifa eti kwasababu ni wachanga au eti nimafisadi.(asiyefanya kazi na asile)

Regards
 
Mkandara,

..Wachaga wana idadi kubwa ya wasomi kulinganisha na makabila mengine. utakuwa siyo mkweli ukipingana na suala hilo.

..hii habari ya kuwa na sekondari kila kata wenzetu wameanza wakati wa Mzee Ruksa. sisi wengine sekondari za kata bado tunashikana mashati hadi leo.

..vilevile msomi aliyesoma miaka ya 1960 leo hii ndiyo yuko ktk ngazi ya CEO,Balozi,au Katibu Mkuu,Jaji Mahakama Kuu etc. wengi wa walio ktk ngazi hizo wameingia serikalini miaka ya 1973 -- 1979.

..kuna mchangiaji hapa alieleza experience yake alipokuwa Shy Comm. kwamba idadi kubwa ya wanafunzi walikuwa wanatoka Kilimanjaro. sasa Shy Comm ndiyo hupeleka majority ya wanafunzi wa BComm pale UDSM.

..binafsi sikubaliani na mchangiaji aliyeonyesha dharau dhidi ya makabila mengine. zaidi anaonyesha amejawa chuki kuliko hata hiyo superiority complex.

..wakati huohuo napata tabu sana kumuelewa mtu kama Chacha Wangwe ambaye kauli zake zinaonyesha kwamba anaona kinyaa kuona Wachaga wawili watatu wamepewa nafasi za kazi sehemu fulani.

..hebu fikiria KIONGOZI WA KITAIFA mwenye matatizo na kuwepo kwa Wachaga 5 sehemu fulani ya kazi. hebu fikiria KIONGOZI WA KITAIFA anayeona kinyaa kwasababu Chadema "kumejaa" madereva na matarishi wa Kichaga. how many drivers and messengers are there at Chadema's hqs? lakini hiyo ndiyo hoja kuu ya Chacha Wangwe, tena ina mashabiki wengi kwelikweli.

..nadhani wachangiaji wengi wamekuwa 'wastaarabu' kwa kutotaja kabila la Chacha Wangwe ktk mijadala hii. labda sikuwa makini lakini nadhani hiyo ni mara ya kwanza kabila lake limetajwa. zaidi kuna aliyetaja kabila la Dr.Slaa? kuna anayelijua? sitashangaa watu wakidai ni Mchaga.

NB:

..hata kama Wachaga watatoa 5% au 10% ya proffesion yoyote ile, it is still an overwhelming factor ukizingatia kwamba kiidadi hawafikii 5% to 10% ya Watanzania wote.
 
Nani anaweza kunihakikishia kuwa Wachagga wamesoma kuliko makabaila mengine! nipeni hizo dataz!..haiwezekani kabisa nchi yenye population karibu 40 na makabila 120 ukasema Wachagga wamesoma!..wapo wengi lakini hilo sio somo kabisa...

China yenye population zaidi ya Billion mbili wana wasomi pengine sawa na population nzima ya Marekani Je wao wamesoma kuliko Marekani au Norway...jamani hizo kazi zinachukua nafasi gani ya ajira nchini kama sio less than 30%.. Asilimia kubwa ya wananchi wote tunaambiwa ni wakulima ambao hata Wachagga wamo kwa asilimia kubwa kuliko waliosoma.. sawa kabisa na makabila mengine.
Hizi secondary unazozungumzia kuna watu wa makabila kibao wamesoma huko haikuwa swala la kabila fulani kusoma Kilimanjaro hata kidogo. Kifupi sasa wewe ndio unataka kunambia hata elimu hiyo ilitolewa kwa Wachagga. Kuwepo shule Kilimanjaro haina maana waliosoma ni Wachagga,,,matokeo ya taifa yalieleza wazi nani anakwenda secondary gani hata uwe Mtwara..
Mkuu Tumekwenda sote vyuoni tumewaona wachagaa na tunafahamu wingi wao.
Leo msitazame nafasi za kazi nchini na kuutazama mfumo mzima wa Kiutawala mnaanza kuleta habari za Wachagga wamesoma..When?.. bado mnazungumzia miaka ya 50 na 60 au hivi leo.. Nipeni takwimu za chuo kikuu toka mwaka 1990 na vyuo vingine vyote hata tufuate majina tuone ukweli wa haya madai yenu..Kwani taabu nini si hawa ndio maofisa ktk taasisi zetu?..kwanini tuandikie mate hali wino upo toeni takwimu!.
 
Wachaga, waachie ngazi eti wakwere, wandengereko na wanaofanana nao ndio wawe madakitari, majaji nk nk!!!! mhn!! mwnkjj unataka kuua watu!!!!

Acheni wachaga wale jasho lao. Cha msingi ni makabila mengine kupiga shule na kuongeza usongo wa kutafuta maisha (Ndio siri ya wachaga kufanikiwa). Ikibidi tuvunje hata kanuni ili kutoa upendeleo zaidi kwa watu wa makabila ambayo si wachaga.

Badala ya kuwaonea wivu wachaga, tuwachukulie kama mfwano. tuige nyendo zao ili nasi kina matonya tufanikiwe!!!! Vinginevyo ni kama maneno ya mzee mkapa, WIVU WA KIKE NA UVIVU WA KUFIKIRI!!!!!
 
Nani anaweza kunihakikishia kuwa Wachagga wamesoma kuliko makabaila mengine! nipeni hizo dataz!..haiwezekani kabisa nchi yenye population karibu 40 na makabila 120 ukasema Wachagga wamesoma!..wapo wengi lakini hilo sio somo kabisa...

China yenye population zaidi ya Billion mbili wana wasomi pengine sawa na population nzima ya Marekani Je wao wamesoma kuliko Marekani au Norway...jamani hizo kazi zinachukua nafasi gani ya ajira nchini kama sio less than 30%.. Asilimia kubwa ya wananchi wote tunaambiwa ni wakulima ambao hata Wachagga wamo kwa asilimia kubwa kuliko waliosoma.. sawa kabisa na makabila mengine.
Hizi secondary unazozungumzia kuna watu wa makabila kibao wamesoma huko haikuwa swala la kabila fulani kusoma Kilimanjaro hata kidogo. Kifupi sasa wewe ndio unataka kunambia hata elimu hiyo ilitolewa kwa Wachagga. Kuwepo shule Kilimanjaro haina maana waliosoma ni Wachagga,,,matokeo ya taifa yalieleza wazi nani anakwenda secondary gani hata uwe Mtwara..
Mkuu Tumekwenda sote vyuoni tumewaona wachagaa na tunafahamu wingi wao.
Leo msitazame nafasi za kazi nchini na kuutazama mfumo mzima wa Kiutawala mnaanza kuleta habari za Wachagga wamesoma..When?.. bado mnazungumzia miaka ya 50 na 60 au hivi leo.. Nipeni takwimu za chuo kikuu toka mwaka 1990 na vyuo vingine vyote hata tufuate majina tuone ukweli wa haya madai yenu..Kwani taabu nini si hawa ndio maofisa ktk taasisi zetu?..kwanini tuandikie mate hali wino upo toeni takwimu!.

LETA wewe kwanza hizo data zinazoonyesha kuwa NAFASI ZOTE WALIZONAZO HAWAJA QUALIFY?
Kihiyo naye MCHAGGA?
Hata waislam wenyewe wameanza kushitukia elimu sasa hivi kwani zamani ilikuwa ni MADRASSA TUUU!
Na SHULE WALISEMA NI ELIM DUNIA!
Hivyo haikupewa kipaumbele sana.Na wakati wakienda ku apply kazi wanakuta kuwa elimu ya MADRASSA haiwasaidii kupata kazi na hivyo wanabakia kulalamikia UDINI NA UCHAGGA!
 
Wakuu hamuwezi kabisa kutumia kigezo chochote kile kunifahamisha hili...
Nina hakika hakuna mzani na mnajaribu kujenga hoja isiyokuwa na msingi kabisa..
Kwa kutazama population tu Wachagga wanalingana sana na Wahaya na Wanyakyusa hivyo huwezi kusema wamesoma kuliko mkabila hayo tu.. acha Wasukuma ambao wametawanyika ktk mikoa miwili.. By Population. Kisha mnatazama mkoa kama kabila maanake hawa wanaoitwa wamesoma kwa sababu mkoa mzima umejenga kabila...Hivi Arusha au Tanga mtasema ni Kabila gani?

Kwa hiyo tuseme mathlan, Wachagga ni millioni 3 na waliosoma hadi chuo kikuu ni asilimia 20, Wahaya na wanyakusya pia watakuwa tayari wameisha fika hesabu hiyo hiyo ktk asilimia na idadi... si ndivyo navyoamini?... au
Kisha Wasukuma ambao ni millioni 6 kwa mikoa miwili hata kama waliosoma ni aslimia 10 watakuwa katika hesabu ya wingi wa Wachagga....
Hivyo basi tunaposema Wachagga wamesoma sana haina maana ya idadi ambayo ndio inatoa ajira na huwezi kunambia wasukuma hawastahili nafasi zile kwa sababu within themselve wamesoma asilimia 10 tu. Wachagga wamesoma kutokana na takwimu within wao wenyewe.. yaani asilimia 20 imepatikana kwa kutazama kabila hilo kwanza sio kutazama nje.
Na hata ukitazama kwa njia nyingine sisi wakerewe ni wilaya tu haina Mkoa kikabila. labda wapo Wakerewe laki 2 na waliosoma ni asilimia 20 huwezi kusema Wachagga wamesoma kuliko Wakerewe ukitazama idadi ya watu....sisi wote ni asilimia 20..
Huko kusoma sana kwa Wachagga ni kupi? ikiwa karibu kila mkoa una namba kubwa ya population na waliosoma wamezagaa nchi nzima..Kipimo gani mnachotumia kama sio kuangalia hizo nafasi za kazi na kuanza kurudi nyuma kujenga sababu!..Tuanzie kwenye shina la elimu leo hii kisha nipeni hizo talwimu ambazo zinapingana na maelezo yangu.
__________________
 
Wakuu hamuwezi kabisa kutumia kigezo chochote kile kunifahamisha hili...
Nina hakika hakuna mzani na mnajaribu kujenga hoja isiyokuwa na msingi kabisa..
Kwa kutazama population tu Wachagga wanalingana sana na Wahaya na Wanyakyusa hivyo huwezi kusema wamesoma kuliko mkabila hayo tu.. acha Wasukuma ambao wametawanyika ktk mikoa miwili.. By Population. Kisha mnatazama mkoa kama kabila maanake hawa wanaoitwa wamesoma kwa sababu mkoa mzima umejenga kabila...Hivi Arusha au Tanga mtasema ni Kabila gani?

Kwa hiyo tuseme mathlan, Wachagga ni millioni 3 na waliosoma hadi chuo kikuu ni asilimia 20, Wahaya na wanyakusya pia watakuwa tayari wameisha fika hesabu hiyo hiyo ktk asilimia na idadi... si ndivyo navyoamini?... au
Kisha Wasukuma ambao ni millioni 6 kwa mikoa miwili hata kama waliosoma ni aslimia 10 watakuwa katika hesabu ya wingi wa Wachagga....
Hivyo basi tunaposema Wachagga wamesoma sana haina maana ya idadi ambayo ndio inatoa ajira na huwezi kunambia wasukuma hawastahili nafasi zile kwa sababu within themselve wamesoma asilimia 5 tu. Wachagga wamesoma kutokana na takwimu within wao wenyewe.. yaani asilimia 20 imepatikana kwa kutazama kabila hilo kwanza sio kutazama nje.
Na hata ukitazama kwa njia nyingine sisi wakerewe ni wilaya tu haina Mkoa kikabila. labda wapo Wakerewe laki 2 na waliosoma ni asilimia 20 huwezi kusema Wachagga wamesoma kuliko Wakerewe ukitazama idadi ya watu....sisi wote ni asilimia 20..
Huko kusoma sana kwa Wachagga ni kupi? ikiwa karibu kila mkoa una namba kubwa ya population na waliosoma wamezagaa nchi nzima..Kipimo gani mnachotumia kama sio kuangalia hizo nafasi za kazi na kuanza kurudi nyuma kujenga sababu!..Tuanzie kwenye shina la elimu leo hii kisha nipeni hizo talwimu ambazo zinapingana na maelezo yangu.
__________________

Umeshaambiwa utowe udhibitisho kwamba ni kweli matatizo yetu yamechangiwa na WACHAGGA NA WALA SI MAFISADI WENYE MAKABILA NA DINI ZA TOFAUTI!

Na kama thats the case...Then badala ya kuwa OPPORTUNIST..Then weka wazi kuhusu swali la MSINGI LA MKJJ....Viongozi wote wa Idara ambao ni wachagga waachie ngazi?

Jibu hapo juu kama waachie ngazi ama la!

Baada ya hapo then wachagga waliofukuzwa kazi watajitafutia USTAARAB MWINGINE!

Mbona miye niko USA na sina NOMA?

Na mimi kama ningekwa MKABILA NA WENZANGU WACHAGGA WAKO KWENYE KILA IDARA.. SI NINGEKUWA NA KAZI HUKO BONGO?

AMA SIKUPENDELEWA KWASABABU NA MIMI NI MZEE WA VIJISENTI?
AMA MGAGAGIGIKOKO?
 
Mkandara,

..inasemekana wachaga wako 2 mill na Tanzania nzima ina wananchi 30mill. kwa msingi huo Wachaga ni around 6.7% ya Watanzania. now, chukulia kwamba takwimu hizo ni za kweli.

..nimetembelea website ya UDSM ni katika senior staff member wenye majina ya Kichaga ni 13%. kwa maana nyingine they have twice their "share" of senior staff pale UDSM.

..zaidi nikatembelea kitivo cha Mechanical and Chemical Engineering. pale kuna PhDs 18. sasa 6 kati yao wana majina ya Kichaga. ina maana hiyo ni 30%!!

..kama ukichunguza TAALUMA yoyote ile Tanzania na ukakuta Wachaga ni zaidi ya 7%, then they are doing pretty well considering the fact they account for only 6.7% of the country's population.
 
Halafu pia tuongeze tupime shule za msingi na sekondari zimegawanyika vipi kati ya Kilimanjaro na mikoa mingine.
 
Mwanakijiji,

..halafu watu wako too obssesed na wachaga wa tra na chadema.

..kuna Wachaga wengi tu wanashona viatu,mafundi welding, mechanics, wauza bucha, wachoma mishkaki, madereva wa daladala,....husikii wananchi wakiwalalamikia hao.
 
Jokakuu,

Mkuu umetazama kuhusiana na Wachagga against the rest!..Asilimia 6.7 ni aslimia waliyokuwa nayo Wanyanyusa, Wahaya na pengine mikoa yote mikubwa..Nilichotanguliza hapo juu nina hakika hesabu ya Wahaya na wanyakyusa haipo nyuma sana labda wanazidiwa kwa asilimia 0.0005. tofauti ambayo huwezi kupitisha hukumu kwamba wengine hawakusoma..

Sasa nikuulize ktk mfano huo huo utasema nini kuhusiana na Wakerewe ambao ni asilimi 0.65 ya Population na wana wasomi 2 ktk kitengo cha chuo hicho! hali tofauti ya kiasilimia ilitakiwa kwa kila Wachagga 10 awepo Mkerewe 1. Hapa kuna Wachagga 8 tu....Je, ndio kusema wakerewe wamesoma kuliko Wachagga?... mkuu sikubaliani na hilo nipe hesabu ya chuo kikuu chote! na laukama Wachagga watajenga aslimia kubwa kuliko makabila basi nitakubaliana nanyi katika ajira kwani navyofahamu mimi kinachotakiwa ktk ajira ni uwezo wa mtu sio namba za graduate ktk kila kabila. Kama Wachagga ni asilimia 30 ya wasomi wetu basi kuna uwezekano wa Wachagga kushika asilimi 30 ya ajira ktk hizo nafasi za juu nchini...ikiwa zaidi basi kuna sababu nyingine kabisa pengine wao wanapenda kuajiriwa serikalini zaidi ya mashirika.
Hakuna sababu hata moja ya kubweteza udhaifu huu wa kufikiri ambao ndio chanzo cha utumwa wetu. Kama ajira zimetolewa kutokana na wale walioenda kuomba na waka pick watu hawa kutokana na uwezo wao hili swala la Ukabila linatoka wapi?.. na ikiwa walipendelewa nafazi zile kwa sababu ya Kabila lao basi bila shaka dhana ya watu italeta mantiki.. hakuna kati yenu anayeweza kutupa ukweli hivyo hata hizi dhana za Ukabila ni kilio cha maskini..Nina hakika waajiriwa nchini ktk ngazi za wasomi hao Wachagga hawatengenezi 51% ya viongozi ktk mashirika na taasisi isipokuwa watu wanatazama baadhi sehemu za Ulaji kama ulivyotazama kitengo kimoja ktk chuo Kikuu.. kelel zote ni ktk kutafuta ulaji pale TRA na kweli Wachagga wamewahi na uwezo wanao..Sasa kwa kutazama nani kapata ktk ujanja bila shaka Mchagga mshindi hata mseme kitu gani hakuna justfication ya usomi ktk ajira nchini inayokwenda na kabila...Ni maisha tuliyokuwa sote tunafahamu kwamba Tanzania ajira lazia uwe na mtu kifua! uwe Mchagga au Mkerewe.kosa moja watu wanafunga goli sii kosa lao ni kosa la system nzima.
Kukosa kwao (walalahoi) kupata kazi sehemu ya Ulaji ndio chimbuko la malalamishi yote haya wametafuta hoja kama hizi kujenga chuki kama alivyofanya Wangwe.. Binafsi nina hakika NI ULAJI tu ndio ulimsukuma wangwe kuweka madai yale na wanaompinga wanatazama ULAJI badala ya kutoa sababu za msingi..ndio maana wanarushiana wao madongo. hoja bado imesimama pale pale.
Wale wanaotetea hili wanatumia pia Ukabila wa kujionyesha wao bora ati wamesoma!..Hizi ndio kasumba chafu sana kwani Tanzania nzima bado kabisa watu tuko nyuma ktk elimu.. Ni wakati wa kuwahimiza vijana wetu waende shule sii wachagga wala wamakonde sote kwa pamoja tuna tatizo la elimu nchini na ajira hakuna!...Ni vijana wangapi wa kichagga leo hii Machinga tena toka wakati wa Nyerere nakumbuka vizuri vijana wanaopiga kiwi viatu mijini, kuuza magazeti, sigara vituoni, michubuo, sabuni za Gardenia walikuwa vijana wa Kiachagga.. Biashara hiyo haikutokana na elimu hata kidogo..
Tena mara nyingi sana makabila ama nchi ambazo vijana wake wametapakaa kila sehemu kutafuta riziki hutokana na shida nyingi nyumbani.. Wa Ethiopia, na Wasomali wengi tulijenga imani kwamba wao waliamka zamani bila kufahamu kwamba vita kati ya wao kwa wao ndio chimbuko kubwa la wao kukimbia nchi zao. Huko nje kama wageni wakajijenga Upya wakatafuta elimu na makazi mapya.
Kwa hiyo nitazidi kusema hii mada haiwezi kujenga hoja ya msingi kama watu mtaendelea kuonyeshana vidole..
 
A MODEST PROPOSAL

Na. M. M. Mwanakijiji

Kuna vumbi la chuki, fitina, wivu, kisasi, na hisia za kibaguzi dhidi ya jamii ya Wachagga nchini. Kuna kila dalili kuwa jamii ya Wachagga nchini siyo tu inaanza kutengwa lakini uwepo wake katika nafasi mbalimbali za uongozi inazua hoja ya ukabila kwa haraka zaidi yawezekana kuliko kabila jingine lolote nchini. Katika Tanzania yetu, wachagga wameanza kunyoshewa kidole siyo kwa siri tena bali kwa wazi kabisa tena na watu ambao wakati mwingine hawapati hata kigugumizi.

Ubaguzi huo msingi wake mkubwa ni idadi ya wachagga katika nafasi mbalimbali za uongozi na hasa kuhusiana na elimu yao. Kuanzia mara tu baada ya uhuru jamii ya wachagga mojawapo ya jamii ambayo watu wake wengi wamesoma sana na kufanikiwa kielimu na kiuchumi imekuwa ikinyoshewa kidole cha kupendelewa.

Mtu yeyote ambaye anaweza akafanya uchambuzi yakinifu hatoshangaa kukuta wataalamu wa kichagga katika nafasi mbalimbali za uongozi au taaluma nchini. Kwenye vyuo vikuu, kwenye idara za serikali na hata kwenye taasisi binafsi kumejaa watu wenye asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hususan watu wa jamii ya Kichagga.

Endapo itatangazwa nafasi yoyote ya kitaalamu usishangazwe ukiona kuwa waombaji wengi wana majina ya "Kichagga".

Ni kwa sababu hiyo basi kuna kila dalili kuwa kutokana na wingi wao katika nafasi muhimu na vyeo mbalimbali (hata ndani ya Jeshi la Polisi) Wachagga siyo tu ni wengi lakini wanaonekana kufanikiwa zaidi. Hili ni tishio kwa baadhi ya watu. Ni tishio kwa watu ambao hawako tayari kuangalia jitihada za watu katika kufanikiwa kwao na matokeo yake kushutumu ukabila kila idadi ya Wachagga kwenye kitengo fulani inazidi mmoja.

Ushauri wangu ni kuwa, kwa vile Wachagga wameshasoma sana na kuendelea katika biashara karibu mikoa mingi nchini. Na kwa vile wanaendelea kufanikiwa pia katika nafasi mbalimbali za uongozi nchini, basi itakuwa vizuri kama watajitolea kuachilia nafasi hizo ili kuwapa nafasi watu wa makabila mengine.

Kwa vile ni wao wanaonekana kulalamikiwa kutokana na mambo ya kifisadi aidha kwa moja kwa moja au kwa kuashiria basi ni vizuri wawape watu wengine nafasi hizo hata kama watu hao hawajasoma sana. Hii yote itakuwa ni katika kudumisha mshikamano, umoja na udugu wa Taifa letu.

Endapo Wachagga wataachilia nafasi mbalimbali kama UCEO, Ukurugenzi, Ukuu wa Idara n.k watasababisha watu wawapende na kuwakubali kuwa ni wazalendo wa kweli. Sitoshangaa kuwa ndugu zetu wa Jamii ya Kichagga wakikaa pembeni, basi ufisadi utakoma serikalini, idara zitaongozwa na watu wazuri, na mara moja na daima Tanzania itaanza kukua katika uongozi.

Kwa kupendekeza nashauri wabunge wote ambao ni Wachagga au wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro kuachia ngazi mara moja ili watu wa makabila mengine wapewe nafasi hizo. Siyo wao tu bali pia wabunge ambao wameoa au kuolewa uchagani vile vile wafuate nyazo hizo.

Wakishamaliza hao, wakuu wote wa idara za serikali ambao wana asili ya mkoa wa Kilimanjaro na hasa wa jamii ya kichagga (wamarangu, wamachame, wa Rombo, na wa Kibosho) na wao waamue kuachilia nafasi hizo kwa ndugu zao Wamakua, Wamwera, Wa Ndali, Wadigo n.k Katika hili Wapare hawahusishwi.

Tukishamaliza wakuu hao wa idara za serikali ningependekeza madaktari wote wenye kumiliki hospitali binafsi ambao ni wachagga au wameoa/kuolewa uchagani na wenyewe waamue kuingia ubia na watu wa makabila mengine kama wangengereko, wambuu, na wanjiro ili hayo makabila madogo na wenyewe wapate nafasi ya kujifunza fani hizi muhimu.

Zaidi ya yote, majaji na mahakimu wote ambao wana asili ya Uchaggani na wenyewe waamue kujitoa katika nafasi hizo kwani wingi wao pia unaonekana sana na hivyo kuwa kikwako kwa watu wa makabila mengine kufanikiwa zaidi katika nyanja ya sheria. Kwanza kabisa wale majaji wa Kichagga wa mahakama ya Rufaa na Mahakama Kuu wawe wa kwanza kuweka manyanga chini.

Katika kufanya hivyo jamii ya Watanzania ambao inaona ukabila wa wachagga katika sehemu nyingi itaridhika kwani kwa mara ya kwanza tutakuwa tumeshughulikia chanzo cha matatizo yetu mengi.

..mwkjj,

..with all due respect, hii post ina-betray basic human being intelligence.

..ama kweli ufumbuzi pekee uliopo sasa katika kukabiliana na matatizo tulionayo ni kujengeana chuki za kikabila,halafu tuuane na tukisha-pass past our foolish mind sets tujiokote na kuwa watumwa wa wenzetu,once again.

..i'm pissed!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom