Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani?

Je, wajua kuwa Zanzibar haikuridhia Muungano? Ina Maana Gani?

Pasco,

Kwa nini unahangaika wakati majibu ambayo yanaweza kumaliza utata unaweza kuyapata bila mihangaiko? wewe mfate Mzee Hassa Nasoro Moyo na Mzee Aboud Jumbe wahoji na tuleteee hapa, utakuwa umekata mzizi wa fitina badala ya kuteletea ngonjera za mkataba wa kimatifa nini, hivi unajua hata wewe na jamaa wa Uganda mkisaini makubaliano tayari ni mkataba wa kimataifa huo?
 
3. Mkataba wa Kimataifa ni nini, una sifa gani na Jee Muungano watu ni mkataba wa kimataifa?.
Mkataba wa Kimataifa, ni mkataba kati nchi moja na nchi nyingine, au mikataba yote ya jumuiza za kimataifa ambayo nchi ama hutakiwa kuridhia, au kulazimishwa kuiheshimu hata kama haikuridhia. Mikataba hii au itifaki mbalimbali (protocals), hupaswa kuridhiwa kabla haijawa sheria kwa nchi husika.

Mfano Tanzania iliridhia mkataba wa mahakama ya kimataifa ya Biashara, ICC. Dowans iliposhinda ile kesi, imepaswa kuisajili hukumu hiyo kwenye mahakama zetu (ratification), ili hukumu hiyo igeuke sheria zetu, (domestic law) na kutekelezwa. Watu humu walipiga sana kelele, nilipouangalia mkataba ule humu jf, nikawaambia wana jf wenzangu, hatuna pa kutokea, tozo ile italipwa tuu mara baada ya tozo hiyo kusajiliwa, kinachoendelea sasa ni delaying tactics ambayo nayo tutailipia dearly!.

Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar, ni mkataba halali wa kimataifa wenye sifa muhimu za mkataba, japo una mapungufu mengi kubwa likiwa ni kitu kinachoitwa "Privity of Contrac" ambapo mkataba ulikuwa kwa lugha ya Kiingereza na signatory mmoja alikuwa msomi anaejua kusoma na kuandika kiingereza, wakati signatory wa pili hakujua kusoma, kuandika wala kiingereza, hivyo alisaini kwa dole gumba!.

Ufafanuzi zaidi kuhusu Muungano kuwa ni mkataba wa kimataifa, unapatikana pia katika ukurasa wa kwanza wa andiko la
Prof. Shivji kwenye kitabu cha "The Legal Foundation of the Union in Tanzania and Zanzibar Constitution, DUP, 1990.

Kwa faida ya wasoma kimombo, tembelea
THE UNION BETWEEN TANGANYIKA AND ZANZIBAR
hapa unatakiwa kufafanua nani alikuwa Privity to the contract? maana waliosaini wote wawili walikuwa ni wahusika wakuu wa huo mkataba, sasa anaye ingia hapo nu kuwa si muhusika katika huo mkataba ni nani? Karume au Nyerere? maana kuwa privity to the contract ni pale mtu kudai haki katika kitu ambacho si muhusika mkuu katika mkataba.
sasa ukisema wananchi wa tanganyika au wazanzibar, unatakiwa sasa tuangalie mambo mengine, uhalali wa karume kuwa kiongozi na kuingia mikataba, uhalali wa serikali ya Tanganyika wakati huo katika kuingia mkata au kuto kuingia. na unaweza kwenda mbele zaidi mpaka wakati wa Jumbe , na muungano wa ASP na TANU na kuunda CCM , mbaka uuandaji wa Baraza la Wawakilishi.
 
Pasco...point of information please, zingatia hii;
Ni katiba ya mwaka 1980 iliyounda Baraza la Wawakilishi na kuwezesha uchaguzi wa kwanza tokea mapinduzi ya mwaka 1964. Lazima tusisahau kuwa mara tu baada ya mapinduzi, Jamhuri ya Unguja na Pemba iliyoanzishwa haikuwa na katiba, haikuwa na bunge na haikuwa na baraza la Mawaziri, mihimili hii yote ilipigwa marufuku na majukumu yake yote kukasimiwa kwa Baraza la Mapinduzi kwa njia ya "decree".

Nafikiri kosa kubwa linalofanywa na wengi ni kushindwa kuzingatia tofauti katika majukumu na taratibu kiutendaji kati ya iliyokuwa Baraza la Mapinduzi la 1964 na Baraza la Wawakilishi la 1980 tunapojadili kuridhiwa kwa Muungano na vyombo hivi viwili. Tanganyika tulikuwa na vyombo vilivyoendeshwa kwa kwa misingi ya katiba rasmi ya nchi tofauti na Zanzibar iliyokuwa chini ya constitutional decree.

Mag3, ndio maana wengine tunasubiri hilo somo maana hadi hivi sasa hakuna mahali popote ameonesha kuwa Muungano haukuwa umeridhiwa Zanzibar.
 
Mag3, ndio maana wengine tunasubiri hilo somo maana hadi hivi sasa hakuna mahali popote ameonesha kuwa Muungano haukuwa umeridhiwa Zanzibar.
Mwanakijiji, huyu jamaa sijui kama anajua anachoongelea au anachanganya mambo...hapa tunamtaka aseme ni chombo kipi huko Zanzibar kilitakiwa (kiutaratibu) kiridhie Muungano mwaka 1964 na hakikufanya hivyo. Asiongelee vyombo ambavyo havikuwepo wakati huo na kwa nini hata vilipokuja kuundwa miaka mingi tu baadaye havikuhoji hadi leo. Tunamsubiri Pasco tena kwa hamu.
 
Last edited by a moderator:
Hivi hii kauli ya kusema tuwaulize Watanzania na Wazanzibar yatoka wapi? Mtanzania ni yupi? Na Mzanzibar ni nani? Bila shaka Mtanganyika aliyeungana na Mzanzibar ndiyo huitwa Watanzania. Hii dhambi ya ubaguzi ya kumwita Mtanganyika ni Mtanzania na Mzanzibar kumpa haki yake ya kuitwa Mzanzibar inauma sana !!
 
Martin Bailey quoted Nyerere when he addressed the mass rally at Dar es Salaam on November 15, 1964:

We sent our police to Zanzibar. After overcoming various problems we united. We ourselves voluntarily agreed on union. Karume and I met. Only the two of us met. When I mentioned the question of the union Karume did not even give it a second thought. He instantly asked me to call a meeting of the press to announce our intention. I advised him to wait a bit as it was too early for the press to be informed. (p. 31).

This is a clear testimony that the union of Zanzibar and Tanganyika was the creation of Karume, a racist dictator nominal Muslim from Nyasaland (Malawi) and Nyerere, an autocratic devout Christian from Tanganyika.

Source: Nyerere Against Islam In Zanzibar And Tanganyika
 
Labda nianze

Pasco, usijiumize sana babangu, unajikamua bure Kwa nondo unazotaka kujikunja nazo .. Kiini cha suluhu umeshakigusia kwamba serikali haiwezi kufanya maamuzi yake pasipo kuwauliza wananchi wake, Na hii ni Kwa kupitia kura ya Maoni..
Nadhani kuna dhana kwamba Upande mmoja wa Muungano hawautaki uchumba huu.. Kwa upande wa Bara wananchi wengi hawana uelewa chanya Wala hasi kuhusu muungano .. Wanachojua Zansibar hawatutaki sisi wabara.. Kwa mantiki hiyo kuna Hoja ya baadae ya kujadili mfumo wa upigaji kura..

Bara yenye wakazi zaidi ya milioni 48 sasa Na Zanzibar yenye wakazi milioni 1.2 ambao ni asilimia 2.4 ya wakazi wa inayoitwa JMT, kura lazima itakuwa Na uwalakini.. Kama watu wote Zanzibar watapiga kura ya kuukataa Muungano, na wakazi milioni 3 tu wa bara wakaukubali, je Hoja ya muungano itabaki MTAMBUZI?

nadhani labda mjadala makini tuuelekezee kwenye suluhisho la nini kifanyike Na sio uhalali Wa Muungano..

Kama Muungano una madudu, kwanini madudu hayo yasimwagwe hapa Na tukayadadavua na kupata suluhu linaloweze kuwa msaada Kwa viongozi ambao wanaumiza vichwa Na mzimu huu unaoitwa MUUNGANO?

Tutapiga kwa asilimia kupata jibu. Kama zanzibar ni nchi na wamepiga kura wote tutachukua asilimia yao ni ngapi according to their population yani1.2/1.2x100=100% na Tanganyika itakua 3/48x100=6.25% kwa hiyo zanzibar watakua wameshinda.
 
Mwanakijiji, huyu jamaa sijui kama anajua anachoongelea au anachanganya mambo...hapa tunamtaka aseme ni chombo kipi huko Zanzibar kilitakiwa (kiutaratibu) kiridhie Muungano mwaka 1964 na hakikufanya hivyo. Asiongelee vyombo ambavyo havikuwepo wakati huo na kwa nini hata vilipokuja kuundwa miaka mingi tu baadaye havikuhoji hadi leo. Tunamsubiri Pasco tena kwa hamu.
Tatizo la Pasco ni kwamba anataka kujaribishia taaluma ya sheria hapa jamvini, ndio maana hataki kuuacha mjadala uwe huru na kuja na vikwazo kibao........mara msiniulize maswali, oh nitajadiri kila kipengere.........., kuna puppets wa .........., Kwa kweli hana majibu ya "contraversial issues" anazoziibua zaidi ya ubabaishaji tu.
 
kwani tanganyika iliridhia muungano?

Hata kama Tanganyika iliridhia , lile lilikuwa ni bunge lililochaguliwa na watu , jee kule Zanzibar, Baraza la Mapinduzi kalichagua nani ?? Na lilikuwa linamwakilisha nani ?? Au nyerere
 
Pasco...point of information please, zingatia hii;
Ni katiba ya mwaka 1980 iliyounda Baraza la Wawakilishi na kuwezesha uchaguzi wa kwanza tokea mapinduzi ya mwaka 1964. Lazima tusisahau kuwa mara tu baada ya mapinduzi, Jamhuri ya Unguja na Pemba iliyoanzishwa haikuwa na katiba, haikuwa na bunge na haikuwa na baraza la Mawaziri, mihimili hii yote ilipigwa marufuku na majukumu yake yote kukasimiwa kwa Baraza la Mapinduzi kwa njia ya "decree".

Nafikiri kosa kubwa linalofanywa na wengi ni kushindwa kuzingatia tofauti katika majukumu na taratibu kiutendaji kati ya iliyokuwa Baraza la Mapinduzi la 1964 na Baraza la Wawakilishi la 1980 tunapojadili kuridhiwa kwa Muungano na vyombo hivi viwili. Tanganyika tulikuwa na vyombo vilivyoendeshwa kwa kwa misingi ya katiba rasmi ya nchi tofauti na Zanzibar iliyokuwa chini ya constitutional decree.

Pasco anasahau au hajui vizuri ni vipi Zanzibar ilikuwa ikiendeshwa baada ya mapinduzi tukufu...:sick:
 
Hata kama Tanganyika iliridhia , lile lilikuwa ni bunge lililochaguliwa na watu , jee kule Zanzibar, Baraza la Mapinduzi kalichagua nani ?? Na lilikuwa linamwakilisha nani ?? Au nyerere
unataka kusema zanzibar hakuna serikali na wala haikuwepo hapo mwanzo
 
unataka kusema zanzibar hakuna serikali na wala haikuwepo hapo mwanzo

serikali iliyowekwa na Nyerere ilikuwepo maana ile serikali iliyochaguliwa na watu ilikuwa imekamatwa na kufungwa katika majela ya Nyerere Tanganyika , wakati huo ni kabla ya Muungano
 
serikali iliyowekwa na Nyerere ilikuwepo maana ile serikali iliyochaguliwa na watu ilikuwa imekamatwa na kufungwa katika majela ya Nyerere Tanganyika , wakati huo ni kabla ya Muungano
Kwa maana hiyo huyatambui Mapinduzi ya Januari, 1964, huitambui Serikali ya Mapinduzi iliyoongozwa na Raisi Abeid Karume, na hulitambui Baraza la Mapinduzi. Sasa ipi serikali unayoitambua kabla ya Muungano? Ilichaguliwa na nani na iliongozwa na nani? Hao viongozi wake waliofungwa katika majela ya Nyerere Tanganyika ndio akina nani?
 
Ngoja niendelee kuwa mvumilivu hadi mada ziishe!
Wala hata usianze kujisuasua, hizi ni rasha rasha tu, wengine tunamsubiria Pasco ashushe nondo alizoahidi tumpe vidonge vyake.
 
Last edited by a moderator:
Kwa maana hiyo huyatambui Mapinduzi ya Januari, 1964, huitambui Serikali ya Mapinduzi iliyoongozwa na Raisi Abeid Karume, na hulitambui Baraza la Mapinduzi. Sasa ipi serikali unayoitambua kabla ya Muungano? Ilichaguliwa na nani na iliongozwa na nani? Hao viongozi wake waliofungwa katika majela ya Nyerere Tanganyika ndio akina nani?

mimi nikiyatambua nisiyatambue ndio iwe nini humu JF ???UKWELI KITU CHENGINE NA KUTAMBUA KITU CHENGINE,

HEBU WAULIZE HAO WANAOKUFUNDISHA NI NANI ALIMCHAGUA KARUME HATA AKAWA RAISI ???

MAJIBU YA MASUALI YAKO MENGINE SOMA HICHI KITABU LABDA WEWE ULIKUWA HUJAKIONA HUMU JF


Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru! Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia by Harith Ghassany in History
 
mimi nikiyatambua nisiyatambue ndio iwe nini humu JF ???UKWELI KITU CHENGINE NA KUTAMBUA KITU CHENGINE, HEBU WAULIZE HAO WANAOKUFUNDISHA NI NANI ALIMCHAGUA KARUME HATA AKAWA RAISI ??? MAJIBU YA MASUALI YAKO MENGINE SOMA HICHI KITABU LABDA WEWE ULIKUWA HUJAKIONA HUMU JF

Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru! Zanzibar na Mapinduzi ya Afrabia by Harith Ghassany in History

Hicho kitabu kasome wewe, mimi kwa umri wangu sihitaji kusoma kitabu chochote kujua hali ilivyokuwa Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi. Ila kwa kukuondoa wasi wasi hadithi za Harith Ghassany nimezisoma kama nilivyosoma hadithi za alfu lela ulela. Kama ndiyo msingi wako wa kujenga hoja, umepotea...wasome na watu wengine wameandika nini, utaelimika zaidi! Mathalan, kwa mfano tu, je umewahi kusoma kitabu alichoandika Field Marshall John Okello au yawezekana hata humjui!
 
kulikuwa hakuna muda wa kuridhia huo muungano by enactment of laws by the revolutionary goverment? kama hawakuridhia kwa kufanya hivyo lakini wakaendelea kuishi kama wamefanya hivyo, then mkataba ni halali by implication.
mimi nike jifanya ni agent wako na wewe ukaniacha niishi hivyo, then mimi ni agent wako by implication.

sawasawa kabisa mpendwa,

ubarikiwe sana na Bwana

Glory to God!
 
Back
Top Bottom