Kuridhia Muungano kwa Tanganyika na Zanzibar, ratification
1. Msingi mkuu wa ratification mkataba wa muungano ni kifungu hiki kwenye hati za muungano.
Article VIII of the Articles of Union provides:" These Articles shall be subject to the enactment of laws by the Parliament of Tanganyika and by the Revolutionary Council of the Peoples Republic of Zanzibar in conjunction with the cabinet of ministers thereof, ratifying the same and providing for the Government of United Republic and of Zanzibar in accordance therewith2. Lengo la kifungu hicho, ni kwa vile muungano ni mkataba wa kimataifa, ili mkataba huo upate uhalali wa kisheria katika nchi husika, lazima mkataba huo uridhiwe na nchi husika, hivyo kifungu hicho kilimaanisha bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi, walipaswa waridhie mkataba huo kwa kuutungia sheria mahsusi ili kuuhalalisha kisheria ndani ya nchi zao!.
3. Baada tuu ya hati za Muungano kutiwa saini ile Aprill 22 kule Zanzibar, Mwanasheria Mkuu Tanganyika enzi hizo, Rowland Brown aliandaa ratification na kupelekwa kwenye kikao cha bunge la Tanganyika, likapitisha ratification ile asubuhi ya Aprili 26, 1964 kwa kutunga sheria No. 243 ambayo ilitangazwa kwenye gazeti la serikali ya Tanganyika, GN No. hivyo kutimiza matakwa ya kile kifungu namba viii cha mkataba wa muungano.
4. Wakati hayo yakiendelea huku Tanganyika, Zanzibar nao kupitia Mwanasheria Wake Mkuu, Wolfgang Dourado, alipaswa kuandaa hiyo sheria ya ratification kule ikiitwa Decree, ili Baraza la Mapinduzi likae na kuipitisha hivyo kuutambua rasmi muungano kisheria. Hili halikufanyika lkwa sababu Dourado alipewa likizo ya siku 7 akapumzike nje ya nchi!. Aliporudi, seven day leter, akakuta game over!. Akaishia kulalamika kichini chini maana angetoa sauti, sijui kama hata unywele ungepatikana!. Ushahidi ni kauli ya Dourado Mwenyewe "I myself have been the Zanzibar Attorney General and Minster responsible for justice between 1984 and 1989. At that time I managed to peruse all the statute books of Zanzibar from 1964 and 1979 when the Revolutionary Council was acting as a legislative Assembly cum the Cabinet. No ratification law or any law to that effect is there. I was not myopic, but even if I was, the first Attorney General of Zanzibar after the Revolution had also testified the same that no law ratifying the Articles of unionexists on the Statute Books of Zanzibar." Dourado aliyasema hayo katika andiko lake la "The Consolidation of Union" alilowasilisha kwenye semina ya Tanhanyika Law Society, Julai 7, 1983 hapa jijini Dar es Salaam.
5. Mpaka Mungu amemuita Dourado mbele ya haki, msimamo wake ulikuwa "No law ratifying the Articles of the union of 1964 exists on the statute books of Zanzibar., I as a Principal Legal adviser to the Zanzibar government was not consulted ……… Zanzibar therefore did not have legal or constitutional advice from its Principal Legal adviser."
6. Badala yake, Solicitor General wa Tanganyika, PRN Fifoot ndiye alieandaa ratification document ya Zanzíbar ambayo aliisaini yeye na kumpatia Karume ile April, 27, 1964, Karume aiwasilishe kwenye bunge la Tanganyika ile siku Nyerere na Karume walibadilishana hati pale Karimjee. Hati ya aliyoiwasilisha Nyerere was a genuine ratified document iliyokuwa ratified na bunge la Tanganyika!. Hati aliyowasilisha Karume, was a fake one as if ni BLM ndilo nalo limefanya hiyo rafication kama lilivyofanya bunge la Tangayika!, It was just a make belive, kuizuga jumuiya ya kimataifa na hapo ndipo hata hao CIA na iteligensia yao wakaingizwa chaka na kubaki kupiga tarumbeta ya ratification kuwa ilifanyika!.
7. Hata kama Fifoot aliiandaa hiyo ratification ya Zanzibar, kwa nini hakumpa Douradau naibu wake, ili aisaini na kuipitisha kwenye kikao cha BLM ili angalau ionekane ilipitishwa Zanzibar?!.Kwa vile Zanzibar hawakuwa na bunge, Baraza la Mapinduzi ndilo lililokuwa Bunge, Baraza la Mawaziri na Mahakama, kwanini ile ratification iliyoandaliwa bara, isipelekwe tuu na kupigwa rubber stamp kwenye BLM ili kuipa uhalali kuwa ni kweli BLM waliridhia na kuratify?!.
8. Siku ile ya April 27, 1964, wakati Nyerere na Karume walipotinga ndani ya bunge la Tanganyika, kubadilishana hati za muungano zilizo kuwa ratified,Nyerere aliwasilisha hati halali ya muungano ilikuwa ratified kihalali na bunge la Tanganyika na kutangazwa rasmi kwenye gazeti la serikali, GN lakini Karume aliwasilisha ile hati iliyosainiwa na Fifoot alijifanya Dourado na kuziwasilisha hati za muungano kwenye bunge la Tanganyika as if ni kweli BLM lilikaa likajadili na kuridhia hizo hati za muungano, na Karume sio tuu amesaini hizo ratification bila kuzipitishia BLM, bali pia amezitungia Decree na kuitangaza katika GN hiyo hiyo ya Tanganyika japo kwenye GN ya Zanzibar sheria hiyo haipo!.
9. Kisheria, kwenye sheria ya mikataba, place of contact maters much as far as domestic laws are concerned, Ule mkataba wa muungano ni international contract, unaweza kusainiwa popote ndio maana Mwalimu Nyerere na time yake, walifunga safari kwenda Zanzibar. Process ya ratification sio international contact, ni domestic contact kutumia domestic laws (municipal) ambapo ratification hupaswa kufanywa na bunge husika likiwa nchi husika. Bunge la Tanganyika lilitimiza wajibu wake hivyo ratification ya Tanganyika ni legal. Kitendo cha ratification ya Zanzibar kuandaliwa na Fifoot wa Tanganyika na kusainiwa nae, halafu Karume kukabidhiwa sheria hiyo wakati sgeria za Zanzibar kwa wakati huo zilikuwa Decrees na kuiwasilisha bunge la Tanganyika, tangazo la ratification kutolewa kwenye GN ya Tanganyika na sio ya Zanzibar, ni mambo yanaifanya hiyo ratification kuwa voidable na sio void!
10. Hoja ya "privity' to contract na "capacity" to contract pia ipo kwa Karume kama Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, alikuwa na capacity to contact kama Karume kwenye zile articles of union, lakini kwenye Ratification, Karume hakuwa na Capacity ya kusaini sheria ambayo haikutungwa na BLM, na kusainiwa na Fifoot badala ya Dourado, na sheria hiyo kutopitishwa na BLM lakini akaiwasilisha as if imeridhiwa na BLM!, na Fifoot hakuwa na capacity to contract kwa niaba ya Dourado!, tena (ninahisi Fifoot alifanya "misrepresentation kujifanya Dourado ndio maana kuna uwezekano mkubwa, Karume hakupewa tena zile original documents!, alikuja mikono mitupu, na kurudi mikono mitupu ndio kule Zanzibar, hizo documents are no where to be seen!!). Emphasis mine!
11. Hata hivyo, kuna mabishano makubwa kati wanazuoni na wasomi mbalimbali wa sheria kuhusiana na hii issue ya ratification. Mwalimu wangu, Prof. Shivji amesema japo hakuna kumbukumbu zozote kuwa BLM liliridhia, kwa vile BLM limeipitisha sheria ya muungano, huko ndiko kuridhia kwenyewe!, kwa hiyo kwa Shivji, muungano uliridhiwa!.
12. Aliyekuwa kiongozi wa kambi ya upinzani kwenye BLW, Hon. Abubakar Khamis Bakary ambaye ndie aliyetoa posa ya ndoa na CCM kule BLW na kuunda SUK ambapo kama mshenga, amezawadiwa uwaziri wa sheria anapingana na Prof. Shivji kwa kusema kuwa sheria ambayo haikutungwa na BLM wala haikupitishwa na BLM, sio sheria halali kwa Zanzibar!.
13. Pamoja na Kutofautiana na Shivji kuhusu uhalali wa ratification, lakini Mhe. Bakari anakubaliana na Shivji kuwa muungano ni halali, kwa sababu, licha yakutokuwepo official ratification kutoka Zanzíbar, hakuna Wanzanzibari wowote waliochukua hatua zozote za kupinga au kulalamika, hivyo hiyo ni dalili kuwa Wanzanzibari wameukubali muungano impliedily not expressly!.
14. Mwanasheria mwingine wa Zanzibar, al maaruf, Ali Salehe, mwandishi na mtangazaji wa BBC, yeye anashikilia, kwa kwa vile muungano haukuridhiwa, lazima uridhiwe ili kuupa nguvu ya kisheria Zanzibar!. Hivyo anasema ratification ifanyike!. Na hapa ndipo na mimi niliposimamia kuwa Wanzanzibari wafanye ratification kama kweli hawautaki tena muungano, BLW likatae ku ratify ili mlango wa kutokea uwe wazi, wide open!.
15. Prof. Haroub Othman ametofautiana na Shivji kwa kusema wajumbe wawili wa BLM, Abrahman Mohamed Babu na Khamis Abudulah Ameir, walimweleza kuwa BLM walijadilili hati za muungano na kuridhia! (bila maandishi wala kumbukumbu?). Prof. Haroub anadai siku anaelezwa hayo walikuwa club ya YASU akiwa anacheza na katoto fulani ambacho kalikuwa bado hata hajabalehe, kakiitwa Ali Juma Shamhuna!.
16. Kufuatia uwepo wa document ya ratification huku bara, na Zanzibar kimataifa ilikufa rasmi siku ile ya April, 26, 1964, hakuna tena anaejali kama hizo ratification documents zili fojiwa huku bara, ndio maana hata tume ya Nyalali, ilizihalalisha na kimataifa everthing is ok na humo humo ndimo hao majasusi wa Marekani, walikolalia na wote wanaoamini muungano uliridhiwa, japo ni kweli kwa bara muungano uliridhiwa kwa kauli na matendo, kwa Zanzibar, uliridhiwa kwa kauli bila matendo!, na sasa tunasikia kauli za kupinga na matendo ya akufukuzaye!.
17. Kiukweli Karume aliliendesha BLM kibabe sana, yeye kama Rais, Jaji Mkuu na Spika, wale wote waliopingana naye, hakuna ajuaye kilichowakuta ili walishughulikiwa kimya kimya na hata miili yao haikubahatika kuonekena (inasemekana walining'inizwa jiwe shingoni na kutoswa baharini!. Kina Babu kuona hivyo, wakajitimkia zao kabla ya kuwakuta, hayajawakuta. Uvumilivu ulipowashinda waliobaki, nao wakamshughulikia Karume!. (Naamini inteligensia ya Mwalimu alishauona mwelekeo wa Karume kwenye majaaliwa ya muungano, hivyo nae akaacha ya kumkuta yamkute, muungano udumu!.
18. Baada ya Karume, Aboud Jumbe akaukwaa urais. Dourado akamjulisha Jumbe kuhusu kukosekana kwan proper ratification na iliyopelekwa UN is fake!, wakaandaa document kuujulisha ulimwengu kuhusu hilo!. Seif Sharif akamtonya Nyerere, Jumbe akashughulikiwa ipaswavyo, huku Dourado akaozea jela!. Tukatangaziwa "kuchafuka kwa hali ya hewa Zanzibar" bila kuelezwa kisa ni absence ya proper ratification!.
19. Wanzanzibar ni watu wazito sana kujifunza, licha ya kujua kilichomkuta Jumbe kilihusu kuutishia muungano, Dr. Salmini nae akataka kucheza karata yake zile siku zake za mwisho mwisho alinukuliwa akisema, wao wanayatambua yale mambo 11 tuu ndio ya halali, hivyo akajenga hoja kubadili katiba aongeze kipindi cha tatu ili ayashughulikie!. Tiss ilimshughulikia yeye na timu yake yote wakatupwa kando!. Hamshaghai kwa nini Salmin baada ya kustaafu hakuitwa popote kuwa mgeni rasmi kwenye shughuli rasmi?, na yule dada yetu naye akaporwa!.
20.Kupitia hoja hizo na nyingine ambazo sikuzitaja, Mimi Pasco wa JF, kwa Mamlaka niliopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Chini ya Kifungu cha "Freedom of Expressions", Sasa Natamka Wazi kuwa Muungano Kati ya Tanganyika na Zanzibar, Haukuwa Ratified Properly in Zanzibar!. Ila pia Nasisitiza, Muungano Huu ni Halali, japo ulikosa uhalali kwa njia ya Expressly in Zanzibar, umepata uhalali huo Impliedly!.