Je, wajua kwamba Katiba hii mbovu inamruhusu Rais kuteua Watu wa familia yake kushika vyeo mbalimbali?

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kwa katiba tuliyo nayo mhe Samia anaweza kuteua familia yake yote na kuipa vyeo tofauti tofauti. Anaweza kumpa mtu yeyote cheo cha aina yeyote muda wowote. Uwe unataka ama hutaki.

Kwa mfano anaweza kuamua kumteua:-
- Mumewe kuwa waziri wa fedha.

- Mwanawe kuwa mhazini mkuu wa serikali

- Mjukuu wake kuwa gavana wa BoT

- Jirani yake kuwa IGP

Usisahau pia ana uwezo wa kuamuru achotewe kiasi chochote cha fedha afanyie kazi zake binafsi.

Katiba gani hii? No! No! No! Not at all!.

Tunahitaji katiba mpya.
 
Kama huyo mtoto wake atatenda kwa weledi na anasifa zote sioni tatizo kabisa ni haki ya kila mtanzania, shida wanateuliwa watu ambao hawana weledi wowote.
 
Mimi Kabudi aliposema juzi eti hii katiba ni nzuri ndio nimeishiwa nguvu kabisa.

Hii katiba ni ya hovyo.
Na mimi na sisitiza katiba ni zuri, hao wenye katiba nzuri wakoje ukilinganisha na sisi ,katiba cannot garantee you good on the tablet
Work had usifuate mkumbwa mtu kupanua mdomo na wew unamuuigilizia
 
Na mimi na sisitiza katiba ni zuri, hao wenye katiba nzuri wakoje ukilinganisha na sisi ,katiba cannot garantee you good on the tablet
Work had usifuate mkumbwa mtu kupanua mdomo na wew unamuuigilizia
Huwezi kujua hao wenye katiba nzuri wanakuzidi nini hadi kwanza unue kama hii katiba sio nzuri. Ukishajua hilo ndio unaweza kuelewa.

Jambo la pili, nataka nikupe mfano mdogo tu wa hii katiba ubovu wake ulipo. Kwenye kifo cha Magufuli hapa ndio hii katiba imeonyesha jinsi ilivyo ya hovyo.

Ni ya hovyo kwa msingi kwamba tutaongozwa na mtu ambae hatukumchagua wala kusikiliza sera zake na hoja zake yeye kama yeye kwa miaka 5. Unatakiwa kujua kua kwenye uchaguzi ambae hua anachaguliwa ni rais, makamo wa rais yuko pale tu kama kukamilisha logistics lakini hua sio wa muhimu na ndio maana nchi nyingine anagombea rais mwenyewe kisha akishinda anateua makamo wa rais.

Kwa katiba nzuri tulipaswa kuitisha uchaguzi ndani ya muda flani tuchague tena rais mwingine na sio hii ya kuokota embe kwenye mnazi. Assume hii nchi urais ukiwa miaka 10 term 1, watu wataongozwa na mtu ambae hawakumchagua kwa miaka 10, hiyo ni hatari sana. Ndio maana unaona hata sasa mama hajui anachokifanya maana ni suprise kwake.
 
Mkuu unatakiwa utulie kwenye mada moja moja,kule kwa majaliwa umeondoka umekuja kuanzisha uzi huku anyway acha na hapa tuwe pamoja.
Naomba uniambie ni katiba ya nchi gani hairuhusu mtu kumchagua ndugu yake au mtu wake wa karibu kuwa katika nafasi husika pale endapo tu atakidhi vigezo husika ?

Hapo kwenye vigezo ndio point ya msingi.

Kwa sababu raisi hana uwezo wa kumchukua kaka yake ambaye yupo mtaani akamchagua akawa IGP lazima IGP awe askari wa cheo fulani.

Hiko kitendo cha kuwa askari wa cheo fulani ndio kigezo chenyewe.

Sasa kama amekidhi vigezo vya kuwa IGP yaani ni askari wa cheo fulani alafu ni ndugu yake naomba uniambie ni katiba ya Nchi gani hapa duniani inakataza jambo hilo ?


Lakini pili ukitaka katiba ambayo raisi hatoruhusiwa kumchagua ndugu yake ama mtu wake wa karibu katika nafasi fulani basi naomba UNIPE SABABU MBILI TU KWA NINI HII ISIWE KATIKA INAYOMBAGUA RAISI KATIKA KUTEUA ?

kwa nini isiwe katiba baguzi dhidi ya raisi ?
 
Roho mbaya inakusumbua sasa kama wana sifa zinatakiwa wasipewe kisa wanaudugu na Rais au Kiongozi husika .

SISI TUNA WATU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…