Je, wajua nini hutokea katika Ulimwengu wa Roho wawili wanapoungana katika NDOA Takatifu?

Je, wajua nini hutokea katika Ulimwengu wa Roho wawili wanapoungana katika NDOA Takatifu?

taa yangu inawaka kila sekunde imejaa mafuta mafuta hayapungui maana imeandikwa mwanamke atamlinda mume wake kwa maombi mimi ni mlinzi wa mume wangu kwa ilo sina shaka
Ubarikiwe sana,

Pia usisahau kuombea na ndoa za wengine ambapo ndoa zao hazielewiki, zenye nagomvi, waombee na kuwashauri hasa WALIO karibu Yako,

Maana jirani Yako akiwa salama, usalama wako utaongezeka pia.

Lakini nimefurahi Kupata comment ya aina Yako, maana wengi wananishambulia, jambo ambalo linaonyesha kipengele Cha ndoa kina Hali Tete Kwa sasa.

Amen
 
Acha kupotosha Imani Sahihi inayofichwa.
Hujiulizi Ibrahimu angekua na mihamko ya kingono Kwa nini alikaa miaka mia moja bila kuoa Mwanamke Mwingine na kuzaa .?
Kwa nini hakuoa mapema tu akiwa kijana na kuzaa?
Kwa nini alikaa na MKE wake Sara mpaka wakazeeka na hakumsaliti kwenda kuoa MKE mwingine mpaka akafikisha miaka mia moja ? Kwa nini alisubiri mpaka Mkewe ndiye akamlazimisha amwingilie Hause Girl na amzalie mtoto.? Hapo huoni kuwa Yule alikua ni Nabii mwenye Imani sana na mwadilifu Kwa kiwango Cha juu sana.
Unafikiri waliomwita baba Wa Imani walikurupuka tu?

Manabii wakubwa wote walizaliwa na wanawake WASIOKUA na uzazi Wa kuzaa Zaa Watoto wengi ikiwemo Yesu.
Yesu hakuwa na Ndugu Wa mama mmoja zaidí ya Binam zake na Watoto Wa Joseph Kwa mamá Mwingine.
Kwa Mila za kiyahudi watoto Wa baba mmoja ni ndugu halisi Wa Damu. Kama walivyo watoto Wa mama mmoja.

Kwanza umepotosha habari za Miaka ya ibrahimu..
Umepotosha Juu ya Hagari..

Hivi mbona mnapenda kupotosha Sana na huwa mnapotosha kwa faida ya Nani...

Ibrahimu kamuoa Hagar akiwa na miaka 85..
Na ibrahimu kapata mtoto wa Kwanza akiwa na miaka 86..
Labda nikukumbushe kitu..
Hagari alikuwa mtoto wa Mfalme wa Misri ilo kwanza lifahamu..na alipewa Ibrahimu baada ya mfalme kutaka kulala na Sara baada ya kupata majanga ili kumuomba msamaha akampa mali nyingi pamoja na mtoto wake ili awe kijakazi wa Sarai...

Sheria ya Waebrania Mtumwa au Kijakazi huwekwa huru baada ya miaka 10..
Kwahyo Sara kwakuwa hakuzaa aliona Bora ampe Hagari kuwa mke wa ibrahimu..
Na sio kumuingilia kwa zinaa bali kama mke wake..

Nyie huwa mnasoma biblia au mnasimuliwa biblia?

Swala la binamu nafikiri nililijibu ukifatikia post no (#103) kuwa kulingana na maandiko kwa lugha ya Kiyunani Kaka zake na yesu Biblia imetaja kama ἀδελφοὶ" (adelphoi) ns kama unajua kiyunani (Greek) utagundua hiyo ni kwa Ndugu wa damu peke yake yaani ndugu wa wazazi sawa..
na binamu huitwa ανηψιός (anepsiós)
ila kulingna na biblia Bila Tafsiri wale hawakuwa binamu wala watoto wa mama mkubwa wala wa mjomba...

Mi nafikiri Arguments Nzuri ingekuwa hivi wale ni Watoto wa Maria au watoto wa Mke mwingine wa Yusufu?
hapa ningekuelewa na tungeanza kuongea lugha zinazoelekea kufanana ila nakushauri soma
 
Jamani Yesu ni Mwana Wa Mungu.
Yesu ni zaidí ya Nabii.
Yesu ni zaidí ya wafalme Wa Dunia .
Yesu ni Zaidí ya Uzao wote Wa Adamu Wa Kale.
Sasa jiulizeni ni Nabii Yupi mkuu alitakiwa na Mwanamke mwenye uzao Wa watoto wengi kwenye Biblia?

Manabii wote wakiotengwa Tangu tumboni mwa mama Zao walizaliwa peke Yao Tena mara nyingine na wanawake walioonekana kuwa Tasa lakini baba Zao walikuwa na Watoto wengine Kwa mama wengine.
Tafakarini. Haya.
Hawataki watu wajue kuwa Joseph alikua ni mume Wa wanawake wengi Wa ndoa Halali Kwa mujibu Wa Mila na Tamaduni za kiyahudi. Kwa Warumi wake wengi haikubaliki ndio Maana hawakuzingatia hiyo historia.
Sio Wote Mkuu Usiseme wite sema asilimia kubwa
 
Ubarikiwe sana,

Pia usisahau kugombea na ndoa za wengine ambapo ndoa zao hazielewiki, zenye nagomvi, waombewe na kuwashauri hasa WALIO karibu Yako,

Maana jirani Yako akiwa salama, usalama wako itaongezeka pia.

Lakini nimefurahi Kupata comment ya aina Yako, maana wengi wananishambulia, jambo ambalo linaonyesha kipengele Cha ndoa kina Hali Tete Kwa sasa.

Amen
Ni kweli mimi nimepitishwa kwenye ndoa kusudi niweze kuwashauri wengine na kuwaombea pia ndoa inachangamoto kubwa sana ni kuzidi kuomba maana tumeambiwa ombeni bila kukoma kila saa ni kuomba.
 
Ubarikiwe sana,

Pia usisahau kugombea na ndoa za wengine ambapo ndoa zao hazielewiki, zenye nagomvi, waombewe na kuwashauri hasa WALIO karibu Yako,

Maana jirani Yako akiwa salama, usalama wako itaongezeka pia.

Lakini nimefurahi Kupata comment ya aina Yako, maana wengi wananishambulia, jambo ambalo linaonyesha kipengele Cha ndoa kina Hali Tete Kwa sasa.

Amen
Yaani ukiongea hivi napenda sana kwa sababu mtu anayeshauri kuhusu Ndoa nampenda na namuona matured iwe kidini (Kama nikisema iwe hivyo) au ki Nature ila kwingine huwa tunapishana ila kuna mambo uko vizuri snaa..
Yoyote Ambaye anapinga Ndoa (Hayuko tu kinyume na Mungu wako) ila pia yupo kinyume na Mazingira na Nature
 
Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee ulio dumu kwa muda mrefu ni huu

Hebu fikiri unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea.

Ameumba dunia kwaajili yetu na ataiangamiza dunia kwaajili yetu.

Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza,
Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na UWEZO wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie Pepo tu tukale bata

Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyo taka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani(magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani.

Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake

Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair

Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima.

Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu

Yaani kuna Fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwaajili ya dhambi za watu wote duniani.... seriously ?
Akaitwa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani.

Fundi kampenta huyu hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu fundi huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”.

Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk

Hebu fikiria huko Arabia kuna Maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakao pinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mbikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu.

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa
Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoa agiza ili ukale bata sana baada ya kufa

Asante. Jibu la utapeli wako hilo hapo
Mkuu Mungu yupo kweli, ila wanadamu ndiyo WANAMUABUDU Mungu ambaye ni wa uongo. Hii mifumo ya kibinadamu kuhusu suala la Mungu achana nayo. Mtafute Mungu wako utampata.
 
Ni kweli mimi nimepitishwa kwenye ndoa kusudi niweze kuwashauri wengine na kuwaombea pia ndoa inachangamoto kubwa sana ni kuzidi kuomba maana tumeambiwa ombeni bila kukoma kila saa ni kuomba.
Mungu azidi kuibariki ndoa Yako, mpate maisha marefu yenye kheri,awape afya njema hata katika Ule umri wa uzee.

Ndoa yenu iwe ya kupigiwa mfano na JAMII yote inayowazunguka,

Na wengi wavutwe Kwa Yesu Kwa ushuhuda wenu.

Amen
 
Mkuu Mungu yupo kweli, ila wanadamu ndiyo WANAMUABUDU Mungu ambaye ni wa uongo. Hii mifumo ya kibinadamu kuhusu suala la Mungu achana nayo. Mtafute Mungu wako utampata.
Tatizo mukiulizwa mnaleta mlivyokalilishwa.
Mungu ni nini? Yuko wapi? Anafanya nini! Namtafuta wa nini! Hamjibu
 
Mungu azidi kuibariki ndoa Yako, mpate maisha marefu yenye kheri,awape afya njema hata katika Ule umri wa uzee.

Ndoa yenu iwe ya kupigiwa mfano na JAMII yote inayowazunguka,

Na wengi wavutwe Kwa Yesu Kwa ushuhuda wenu.

Amen
Ameeeeeeeeeeeeen, Napokea baraka katika jina la Yesu aliye hai Ameeeeeeeeeeeeeeeeeeen
 
Acha kupotosha Imani Sahihi inayofichwa.
Hujiulizi Ibrahimu angekua na mihamko ya kingono Kwa nini alikaa miaka mia moja bila kuoa Mwanamke Mwingine na kuzaa .?
Kwa nini hakuoa mapema tu akiwa kijana na kuzaa?
Kwa nini alikaa na MKE wake Sara mpaka wakazeeka na hakumsaliti kwenda kuoa MKE mwingine mpaka akafikisha miaka mia moja ? Kwa nini alisubiri mpaka Mkewe ndiye akamlazimisha amwingilie Hause Girl na amzalie mtoto.? Hapo huoni kuwa Yule alikua ni Nabii mwenye Imani sana na mwadilifu Kwa kiwango Cha juu sana.
Unafikiri waliomwita baba Wa Imani walikurupuka tu?

Manabii wakubwa wote walizaliwa na wanawake WASIOKUA na uzazi Wa kuzaa Zaa Watoto wengi ikiwemo Yesu.
Yesu hakuwa na Ndugu Wa mama mmoja zaidí ya Binam zake na Watoto Wa Joseph Kwa mamá Mwingine.
Kwa Mila za kiyahudi watoto Wa baba mmoja ni ndugu halisi Wa Damu. Kama walivyo watoto Wa mama mmoja.
Mkuu Ibrahim alikuwa ana pigana miti na Sara daily .angekuwa hataki ngono asingeoa.ila alikuwa mwaminifu sababu ya uchamungu.hata leo kuna wakristo wengi wana mke mmoja tu na hawazai nje nikiwemo mm
 
Acha kupotosha Imani Sahihi inayofichwa.
Hujiulizi Ibrahimu angekua na mihamko ya kingono Kwa nini alikaa miaka mia moja bila kuoa Mwanamke Mwingine na kuzaa .?
Kwa nini hakuoa mapema tu akiwa kijana na kuzaa?
Kwa nini alikaa na MKE wake Sara mpaka wakazeeka na hakumsaliti kwenda kuoa MKE mwingine mpaka akafikisha miaka mia moja ? Kwa nini alisubiri mpaka Mkewe ndiye akamlazimisha amwingilie Hause Girl na amzalie mtoto.? Hapo huoni kuwa Yule alikua ni Nabii mwenye Imani sana na mwadilifu Kwa kiwango Cha juu sana.
Unafikiri waliomwita baba Wa Imani walikurupuka tu?

Manabii wakubwa wote walizaliwa na wanawake WASIOKUA na uzazi Wa kuzaa Zaa Watoto wengi ikiwemo Yesu.
Yesu hakuwa na Ndugu Wa mama mmoja zaidí ya Binam zake na Watoto Wa Joseph Kwa mamá Mwingine.
Kwa Mila za kiyahudi watoto Wa baba mmoja ni ndugu halisi Wa Damu. Kama walivyo watoto Wa mama mmoja.
Huu ujinga mnajaziwaga wapi? Kuna sheli ya pumba na uongo?
 
Salaam / Shalom!!

INTRODUCTON.

(Mwanzo 2:18,21-24) na (Mathayo 19:3-9).

NDOA ni muunganiko wa KIMWILI kati ya mume mmoja na mke mmoja KIMWILI na kiroho.

Asili ya NDOA ni Mbinguni, NDOA ni usafi, NDOA ni utakatifu.

Kila mtu aliyezaliwa Huwa anae mtu mmoja ambaye Huwa ndiye ubavu wake. Na hao kukutana, ni Hadi wamwombe Mungu, Kuzini kabla ya Kuoa kunamweka mtu katika position ya Kuoa au Kuolewa na mtu mume au mke asiye ubavu wako sahihi.

Matatizo mengi ya NDOA na magomvi ni sababu ya Kuoa au Kuolewa na mtu asiye chaguo Kutoka Kwa MUNGU.

Mwanaume anapofikia uamuzi wa Kuoa, shetani huleta wanawake wengi karibu Yako, na Mungu Huwa tayari amemleta mtu sahihi, ukiitumia macho ya MWILI kuchagua mke, utaangukia Kuoa uliyeletewa na shetani, ndomana Kila aliyeoa Huwa na simulizi, hujikuta katika wakati ambapo huhitaji achague, wakati kiuhalisia, atokaye Kwa Mungu, ubavu wako Huwa ni MMOJA tu!!!

Utaniuliza, kwanini wanawake ni wengi kuliko wanaume, kwamba tukioana mke mmoja, mume mmoja, wanawake watabaki bila waume, Hilo Lina sababu na majibu yake, Si Leo.

Utaniuliza pia ikiwa aliumbwa Adam mmoja na Hawa mmoja, kwanini idadi ya wanawake iwe kubwa kuliko wanaume? Hilo nalo majibu yake Si Leo!!

Ulimwengu wa Giza NDOA Yao ni kinyume na NDOA aliyoasisi Mungu, Ulimwengu wa Giza hakuna NDOA, wachawi, mama na mwanae wanajamiiana, USHOGA ,USAGAJI,kujamiiana na wanyama na Kila UOVU,umeanzia katika Ulimwengu wa Giza,Kisha kuletwa duniani, huko hawana mipaka, ni tafrani tupu.

Ili kuivuruga Dunia, Ulimwengu wa Giza hufanya jitihada juu chini Ili kwenda kinyume na maagizo ya Mungu Ili watu wasioane na kufikia baraka za wawili wanapoungana katika NDOA Takatifu.

Ibilisi na shetani ajua akivuruga NDOA Takatifu atavuruga uzao wa mwanadamu, sababu watoto wakipatikana na kutunzwa vizuri katika taasisi aliyoasisi Mungu, watazaliwa watoto watakaomcha Mungu.

MADA: NINI HUTOKEA WAWILI, MUME NA MKE WANAPOUNGANA NA KUWA MWILI MMOJA KIMWILI NA KIROHO?

Katika mwili, anaposimama Mchungaji kufungisha NDOA Takatifu kati ya mke na mume KIMWILI,

Pia, Katika Ulimwengu wa Roho pia wawili Hawa huunganika, Mungu akiwa shahidi.

Muunganiko huo hutokea Kwa Mfano wa nyota mbili zenye uelekeo tofauti angani, zinapokutana na kupata crash, nyota na Nuru kubwa huzaliwa sababu ya muunganiko huo. Na mng'ao huongezeka sana, sababu nyota mbili kuungana na kuwa moja kubwa inayong'aa zaidi.

Mamajusi, alipozaliwa Yesu, wao waliona Nyota yake, na ilionyesha nini Yesu amebeba, lakini Kwa watakatifu, hatuchunguzi Nyota, sisi huomba Mungu atuzidishie mafanikio Kutoka KIBALI tulichozaliwa nacho.

Kila mtu ana KIBALI, KIBALI Kutoka Kwa MUNGU ndiyo Bahati na mafanikio ya mtu huzaliwa nazo Toka tumboni, Mtu mume na mke sahihi wanapoungana katika NDOA Takatifu huunganisha KIBALI Cha mke na KIBALI Cha mme na kuwa kitu kimoja. Nguvu na uwezo wa mafanikio ya mke na mume sahihi Huwa hayazuiliki, baraka Huwa ni mara mbili, na hatua zao Huwa za haraka sana.

Narudia, hakuna mchawi au Pepo awezaye kuzuia mafanikio ya mtu mume na mke waliofunga NDOA sahihi Walio mwili mmoja, kuwatenganisha hao ni Hadi uvunje NDOA kwanza ndipo uweze kuwatenganisha.

Mafanikio Yako kijana yapo katika NDOA, watoto na uzao sahihi umo katika NDOA sahihi, jambo muhimu la kuzingatia, ni upate Mume au mke sahihi aliye Ubavu wako.


HITIMISHO
NDOA na iheshimiwe na watu wote, vijana wajitunze na kutunza bikira zao kabla ya Kuoa na Kuolewa Ili kupata baraka za NDOA.

Usipojitunza, usipotunza Bikra Yako, utapata wa kufanana nae, Pipa na mfuniko.

Kwa Leo niishie hapa.

Mungu na Awabariki.

NOTE: Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wa maisha ya, fuatisha Sala ifuatayo:

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO,NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE NA NIMEDHAMIRIA KUZIACHA, NIPE UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI,FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, NA ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA. AMEN

Karibuni.

Amen
Swali rahisi tu:

Huko kwenye ulimwengu wa roho ni wapi? Mtu kama mimi ambaye sijaokoka nawezaje kufika huko?
 
Swali rahisi tu:

Huko kwenye ulimwengu wa roho ni wapi? Mtu kama mimi ambaye sijaokoka nawezaje kufika huko?
Umewahi kuota ndoto?

Na unaweza kunisimulia ndoto ulizoota ambazo unazikumbuka ambazo ulipoamka Uliona ni kama tukio halisi kabisa lilitokea?
 
Umewahi kuota ndoto?

Na unaweza kunisimulia ndoto ulizoota ambazo unazikumbuka ambazo ulipoamka Uliona ni kama tukio halisi kabisa lilitokea?
Kama tukio halisi kabisa lilitokea? Mh!

Ndoto zangu nyingi ni za kuruka juu huko na kutua japo mara moja moja huwa napata shida ya kutua hasa nikiwa nimezidisha ugali au kama nimekula kwa kuchelewa sana. Pia kupigana na watu ambao siwajui...mara nyingi nawakanda japo mara moja moja huwa wananizidi naanza kukimbia mbio halafu naamka nikiwa nimelowa jasho hatari huku natweta.

Na mara chache chache niko chuoni au shuleni masomoni mara zali natandikwa viboko au nazusha varangati mpaka nafukuzwa au naambiwa kwenda kuwaleta wazazi.

Ndoto hizi ndiko huko kwenye ulimwengu wa roho? 😳
 
Salaam / Shalom!!

INTRODUCTON.

(Mwanzo 2:18,21-24) na (Mathayo 19:3-9).

NDOA ni muunganiko wa KIMWILI kati ya mume mmoja na mke mmoja KIMWILI na kiroho.

Asili ya NDOA ni Mbinguni, NDOA ni usafi, NDOA ni utakatifu.

Kila mtu aliyezaliwa Huwa anae mtu mmoja ambaye Huwa ndiye ubavu wake. Na hao kukutana, ni Hadi wamwombe Mungu, Kuzini kabla ya Kuoa kunamweka mtu katika position ya Kuoa au Kuolewa na mtu mume au mke asiye ubavu wako sahihi.

Matatizo mengi ya NDOA na magomvi ni sababu ya Kuoa au Kuolewa na mtu asiye chaguo Kutoka Kwa MUNGU.

Mwanaume anapofikia uamuzi wa Kuoa, shetani huleta wanawake wengi karibu Yako, na Mungu Huwa tayari amemleta mtu sahihi, ukiitumia macho ya MWILI kuchagua mke, utaangukia Kuoa uliyeletewa na shetani, ndomana Kila aliyeoa Huwa na simulizi, hujikuta katika wakati ambapo huhitaji achague, wakati kiuhalisia, atokaye Kwa Mungu, ubavu wako Huwa ni MMOJA tu!!!

Utaniuliza, kwanini wanawake ni wengi kuliko wanaume, kwamba tukioana mke mmoja, mume mmoja, wanawake watabaki bila waume, Hilo Lina sababu na majibu yake, Si Leo.

Utaniuliza pia ikiwa aliumbwa Adam mmoja na Hawa mmoja, kwanini idadi ya wanawake iwe kubwa kuliko wanaume? Hilo nalo majibu yake Si Leo!!

Ulimwengu wa Giza NDOA Yao ni kinyume na NDOA aliyoasisi Mungu, Ulimwengu wa Giza hakuna NDOA, wachawi, mama na mwanae wanajamiiana, USHOGA ,USAGAJI,kujamiiana na wanyama na Kila UOVU,umeanzia katika Ulimwengu wa Giza,Kisha kuletwa duniani, huko hawana mipaka, ni tafrani tupu.

Ili kuivuruga Dunia, Ulimwengu wa Giza hufanya jitihada juu chini Ili kwenda kinyume na maagizo ya Mungu Ili watu wasioane na kufikia baraka za wawili wanapoungana katika NDOA Takatifu.

Ibilisi na shetani ajua akivuruga NDOA Takatifu atavuruga uzao wa mwanadamu, sababu watoto wakipatikana na kutunzwa vizuri katika taasisi aliyoasisi Mungu, watazaliwa watoto watakaomcha Mungu.

MADA: NINI HUTOKEA WAWILI, MUME NA MKE WANAPOUNGANA NA KUWA MWILI MMOJA KIMWILI NA KIROHO?

Katika mwili, anaposimama Mchungaji kufungisha NDOA Takatifu kati ya mke na mume KIMWILI,

Pia, Katika Ulimwengu wa Roho pia wawili Hawa huunganika, Mungu akiwa shahidi.

Muunganiko huo hutokea Kwa Mfano wa nyota mbili zenye uelekeo tofauti angani, zinapokutana na kupata crash, nyota na Nuru kubwa huzaliwa sababu ya muunganiko huo. Na mng'ao huongezeka sana, sababu nyota mbili kuungana na kuwa moja kubwa inayong'aa zaidi.

Mamajusi, alipozaliwa Yesu, wao waliona Nyota yake, na ilionyesha nini Yesu amebeba, lakini Kwa watakatifu, hatuchunguzi Nyota, sisi huomba Mungu atuzidishie mafanikio Kutoka KIBALI tulichozaliwa nacho.

Kila mtu ana KIBALI, KIBALI Kutoka Kwa MUNGU ndiyo Bahati na mafanikio ya mtu huzaliwa nazo Toka tumboni, Mtu mume na mke sahihi wanapoungana katika NDOA Takatifu huunganisha KIBALI Cha mke na KIBALI Cha mme na kuwa kitu kimoja. Nguvu na uwezo wa mafanikio ya mke na mume sahihi Huwa hayazuiliki, baraka Huwa ni mara mbili, na hatua zao Huwa za haraka sana.

Narudia, hakuna mchawi au Pepo awezaye kuzuia mafanikio ya mtu mume na mke waliofunga NDOA sahihi Walio mwili mmoja, kuwatenganisha hao ni Hadi uvunje NDOA kwanza ndipo uweze kuwatenganisha.

Mafanikio Yako kijana yapo katika NDOA, watoto na uzao sahihi umo katika NDOA sahihi, jambo muhimu la kuzingatia, ni upate Mume au mke sahihi aliye Ubavu wako.


HITIMISHO
NDOA na iheshimiwe na watu wote, vijana wajitunze na kutunza bikira zao kabla ya Kuoa na Kuolewa Ili kupata baraka za NDOA.

Usipojitunza, usipotunza Bikra Yako, utapata wa kufanana nae, Pipa na mfuniko.

Kwa Leo niishie hapa.

Mungu na Awabariki.

NOTE: Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wa maisha ya, fuatisha Sala ifuatayo:

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO,NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE NA NIMEDHAMIRIA KUZIACHA, NIPE UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI,FUTA JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, NA ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA. AMEN

Karibuni.

Amen
Yakobo aliyekuwa na wake wanne na bado alikuwa rafiki mkubwa wa Mungu ,Sulleiman wanawake 1000
umeandika vitu vingi ambavyo havina uhalisia
hata Musa hakuwa na mke mmoja
 
Kama tukio halisi kabisa lilitokea? Mh!

Ndoto zangu nyingi ni za kuruka juu huko na kutua japo mara moja moja huwa napata shida ya kutua hasa nikiwa nimezidisha ugali au kama nimekula kwa kuchelewa sana. Pia kupigana na watu ambao siwajui...mara nyingi nawakanda japo mara moja moja huwa wananizidi naanza kukimbia mbio halafu naamka nikiwa nimelowa jasho hatari huku natweta.

Na mara chache chache niko chuoni au shuleni masomoni mara zali natandikwa viboko au nazusha varangati mpaka nafukuzwa au naambiwa kwenda kuwaleta wazazi.

Ndoto hizi ndiko huko kwenye ulimwengu wa roho? 😳
Ndio,

Ndoto pekee ni Ulimwengu wa Roho.

Mtu ni jumla ya MWILI, NAFSI NA ROHO.

Mtu ni ROHO anayo NAFSI na anaishi ndani ya MWILI.

Ukilala, Roho hupata muda wa kuzurura ipatakapo na hakuna umbali katika Ulimwengu huo wa Roho.

Roho inapokuwa imeenda kuzurura, Huwa Kuna kamba ya Sllver ambayo Huwa imeunganishwa mtu wa ndani (Roho) na mtu wa nje (Mwili).

Ni vibaya sana kumstua mtu aliye usingizini, maana utailazimisha Roho irudi Kwa haraka, jambo ambalo waeza sababisha kamba hiyo kukatika na mtu asiamke mazima.

Kwa kuwa mtu ni ROHO, awe ameokoka au hajaokoka huingia kwenye Ulimwengu wa Roho automatically kupitia ndoto.

Ile ya mawazo ya mchana kujirudia ndotoni, hufanywa na Akili ambayo Iko kwenye NAFSI.

Kuna viwango vya kuingia katika Ulimwengu wa Roho.

Kuingia katika Ulimwengu wa Roho Kwa kudhamiria ni LAZIMA uingie kupitia either Ulimwengu wa Giza au kupitia Ulimwengu wa Nuru.

Ukiokoka, utawezeshwa kuingia huko Kwa uweza wa Roho mtakatifu, macho ya mtu wa ndani yatafunguliwa uone wazi wazi yanayoendelea humo bila hata kusubiri kulala USINGIZI.

Njia ya pili ni kupitia Ulimwengu wa Giza, mchawi akikupania mchana, atasubiri muda ufike na ataficha sura yake Kwa msaada wa Pepo na atakuja kupitia Ulimwengu wa Roho, nawe Kwa kuwa u Roho, utata ndoto za kushambuliwa au kukimbizwa na wanyama.

Wakati naandika haya, napata ufunuo kuwa unayajua zaidi mambo katika Ulimwengu wa Giza kupitia asili na Mila za kikabila na ukoo uliotokea.

Nakusihi, uokoke, umpe Yesu maisha Yako, Ujazwe Roho mtakatifu Ili uwe raia wa Mbinguni.

Uona wazi wazi tena Bure maana Vipawa vya Yesu ni Bure na havina majuto.

Amen
 
Kama tukio halisi kabisa lilitokea? Mh!

Ndoto zangu nyingi ni za kuruka juu huko na kutua japo mara moja moja huwa napata shida ya kutua hasa nikiwa nimezidisha ugali au kama nimekula kwa kuchelewa sana. Pia kupigana na watu ambao siwajui...mara nyingi nawakanda japo mara moja moja huwa wananizidi naanza kukimbia mbio halafu naamka nikiwa nimelowa jasho hatari huku natweta.

Na mara chache chache niko chuoni au shuleni masomoni mara zali natandikwa viboko au nazusha varangati mpaka nafukuzwa au naambiwa kwenda kuwaleta wazazi.

Ndoto hizi ndiko huko kwenye ulimwengu wa roho? 😳
Pia umegusia ndoto za kuota uko shuleni.

Mungu ni Roho, husema nawe mchana, na akiona husikii, hukuletea ndoto usiku, Atasema na mtu wa ndani live Kisha mtu wa ndani atakukumbusha ujumbe kupitia ndoto.

Mungu anakukumbusha kupitia ndoto ya mambo ya shule kuwa zipo hatua ambazo hukuzifanya vizuri zamani ambazo ndizo zinaleta mkwamo katika Maisha Yako kiuchumi, kijamii kimahusiano nknk.

Nilipoomba Mungu anipe mke sahihi, Mimi sikujubiwa Kwa ndoto, nilipata maono live, mchana kweupe, nikajikuta katika Ulimwengu wa Roho,nikiletewa picha ya mtu sahihi kwangu iliyokuwa ikifunguka mbele yangu Polepole kama ambavyo picha hufunguka unapoifungua kwenye mtandao.

Jifunze pia kuandika ndoto ambazo ukiamka unajikuta unatoka JASHO, HOFU au kukosa amani, au furaha tele na kuzitafutia majibu Kwa kushare na watu sahihi.
 
Ila ndoa ni chanzo cha utumwa kwetu wanaume. Ndio chanzo cha kutumaliza hata tusiishi miaka mingi duniani. Ndio chanzo cha msongo wa mawazo na tuzeeke vibaya
Hayo humpata mtu endapo atachagua Mke sie sahihi....sifa kuu Moja wapo ya Mke au Mume anayetoka Kwa Mungu hua ni Mcha Mungu mke anakua mwenye kumtii mumewe na mume anakuwa mwenye upendo wa dhati Kwa mkewe
 
Yakobo aliyekuwa na wake wanne na bado alikuwa rafiki mkubwa wa Mungu ,Sulleiman wanawake 1000
umeandika vitu vingi ambavyo havina uhalisia
hata Musa hakuwa na mke mmoja
Soma (Marko sura ya 10-12)

Yesu amefafanua vizuri. Tamaa na Vichwa ngumu vya WANADAMU ndo sababu ya watu Kuoa wake wengi,

Na Musa akaruhusu hayo ingawa haikuwa maelekezo ya Mungu.

Yesu akawajibu Kwa kuwarudisha Edeni, akamwambia Mungu aliasisi NDOA ya mke na mume mmoja baasi, tofauti na hapo ni UZINZI na UASHERATI.

Waislamu wanadai wanaamini INJILI, ila katika suala la NDOA, wameamua kubali kwenye torati.

Yesu ni Mungu, hivyo maelekezo yake ni Amri, sharti tuyafuate.

Amen
 
Back
Top Bottom