Je, wapinzani ni wakombozi?

Je, wapinzani ni wakombozi?

To me the question is, tunajuaje kilichobora ambacho chapaswa kuchukua nafasi badala ya CCM na viongozi wake? Je tunatafuta chama au watu?

Kama mfumo wa CCM ungekuwa unaruhusu kupatikana kwa watu safi, kisha wakatuongoza Watanzania bila kuwa influenced na maslahi ya Chama au kundi la watu ndani ya Chama then tatizo lingekuwa dogo.Lakini mfumo unaotumika kuwapata,kuwaingiza viongozi wa CCM madarakani ni mchafu, hakuna msafi atakayepatikana.

Watanzania tunatafuta watu na si chama, lakini ni vizuri pia tukaelewa watu hawa bora tunaowahitaji hawapatikani ndani ya chama kibovu,kichafu ,kilichokwisha oza(CCM).Mkebe wa kufyatulia keki yetu ni mbovu, hivyo hata tukifyatua keki ingine kwa mkebe uleule dosari itakuwa palepale.Tunahitaji keki isiyo na dosari na hii itapatikana kwenye mkebe usiokuwa na dosari.
 
Kwa wapinzani tuloikuwa nao hivi sasa sidhani kama watakuwa tofauti na CCM!Wengi wetu tuna angalia viongozi wa ngazi ya juu wa Upinzani hatuwajui viongozi wa ngazi za wilaya hadi mkoa.Wengi mpo nje ya Nje mnawasikia Mbowe,Slaa,Zitto au Lipumba .Mrema!Lakini wengi wa viongozi wa ngazi ya chini wa vyama vya wapinzani hamuwajui.Jamani kuna viongozi wa ngazi ya chini wa wapinzani wamechoka kiuchumi wa njaa hao sijapata kuona sasa itokee vyama vyao vinatawala watakuwa kama fisi mwenye njaa watatafuna nchi hao!CCM itakuwa mtoto!
Lakini sio mbaya tuwajaribu!Huenda wataleta maendeleo katika nchi!
 
Kwa wapinzani tuloikuwa nao hivi sasa sidhani kama watakuwa tofauti na CCM!Wengi wetu tuna angalia viongozi wa ngazi ya juu wa Upinzani hatuwajui viongozi wa ngazi za wilaya hadi mkoa.Wengi mpo nje ya Nje mnawasikia Mbowe,Slaa,Zitto au Lipumba .Mrema!Lakini wengi wa viongozi wa ngazi ya chini wa vyama vya wapinzani hamuwajui.Jamani kuna viongozi wa ngazi ya chini wa wapinzani wamechoka kiuchumi wa njaa hao sijapata kuona sasa itokee vyama vyao vinatawala watakuwa kama fisi mwenye njaa watatafuna nchi hao!CCM itakuwa mtoto!
Lakini sio mbaya tuwajaribu!Huenda wataleta maendeleo katika nchi!

Watanzania karibu wote wamechoka sana kiuchumi kwa sababu ya sera mbaya za mafisadi wa ccm na sio viongozi wa upinzani tu walioko choka mbaya!
 
..maendeleo ya tanzania yataletwa na wananchi wenyewe kwa kuchagua viongozi waadilifu na si kufuata ushabiki wa chama au kupewa vijisenti!

..ukitazama vizuri hata baadhi kwenye huo upinzani given a chance watakuwa mafisadi tu!

..tunahitaji viongozi nchi hii,regardless ya chama wanachotoka!
 
so inamaana hata wakipewa nchi wapinzani yatakuwa yale yale?...au?
 
..maendeleo ya tanzania yataletwa na wananchi wenyewe kwa kuchagua viongozi waadilifu na si kufuata ushabiki wa chama au kupewa vijisenti!

..ukitazama vizuri hata baadhi kwenye huo upinzani given a chance watakuwa mafisadi tu!

..tunahitaji viongozi nchi hii,regardless ya chama wanachotoka!

hapo nakuelewa kaka na ni kweli kabisa kuwa kuna kina mrema wananjkaa ile mbaya je tukiwapa nchi si ndo watataka kurudisha mwili faster?
 
gang chomba,

Ndiyo maana nasisitiza tuwe na institutions zilizo na nguvu ya kufanya checks and balance, tuwe na katiba inayomuadibisha rais pamoja na mabadiliko mengine mengi, tuwe na bunge makini na siyo rubber stamp yetu hii, wananchi wenyewe wawe na elimu ya uraia pamoja na kuelimika kiujumla.

Tukiwa na institutions thabiti basi itakuwa haijaliki nani anachukua nchi, kama mfisadi au msafi, sheria, katiba, bunge, magazeti na wananchi watamkalia kooni mpaka mwenyewe atakuwa hana pa kupumlia.

Lakini tukisema wapinzani ni safi tuwape nchi bila kuwa na institutions za nguvu siwezi kushangaa wakiingia Ikulu wakajikuta kwenye vishawishi vya rushwa na challenge za kutatua matatizo magumu, sintoshangaa wakirudi nyuma na kujiingiza katika ufisadi.

This is just human nature, kwamba binadamu ni kama walivyosema waswahili, punda haendi bila kiboko, tukileta uzuri tutajikuta tunarudi pale pale.Inabidi tulete mabadiliko katika taasisis zetu ili mabadiliko ya utawala yawe na maana.
 
hapo nakuelewa kaka na ni kweli kabisa kuwa kuna kina mrema wananjkaa ile mbaya je tukiwapa nchi si ndo watataka kurudisha mwili faster?

Kwa argument kama hii, ni bora ccm waendelee kunyonya na kusaza kwa vile hatujui kina Mrema wakipewa nchi watafanya nini. Dr Watson alisema kitu somewhere na ninakitafuta kuona kama kina uhusiano hapa!
 
We Pundit, jibu swali kuhusu hoja yako ya chupa nzee mvinyo ule ule.

Kipi bora, chupa mpya mvinyo ule ule au mvinyo ule ule na li chupa zee mpaka ni hatari kulitumia kunywa mvinyo ule ule maana chupa linaweza lika kukata mdomo?
 
Kwa argument kama hii, ni bora ccm waendelee kunyonya na kusaza kwa vile hatujui kina Mrema wakipewa nchi watafanya nini. Dr Watson alisema kitu somewhere na ninakitafuta kuona kama kina uhusiano hapa!

mmmmh mwafrika wa kike hapo swala la CCM kuendelea kutawala milele mi kidogo nakupinga ila naungana na puundit alivyosema sheria ziwe kali kuanzia kwa rais mpaka katibu tarafa sasa hapo ndo ufisadi na rushwa na mambo mengine ya maudhi yatakwisha nchi hii.
 
gang chomba,

Ndiyo maana nasisitiza tuwe na institutions zilizo na nguvu ya kufanya checks and balance, tuwe na katiba inayomuadibisha rais pamoja na mabadiliko mengine mengi, tuwe na bunge makini na siyo rubber stamp yetu hii, wananchi wenyewe wawe na elimu ya uraia pamoja na kuelimika kiujumla.

Tukiwa na institutions thabiti basi itakuwa haijaliki nani anachukua nchi, kama mfisadi au msafi, sheria, katiba, bunge, magazeti na wananchi watamkalia kooni mpaka mwenyewe atakuwa hana pa kupumlia.

Lakini tukisema wapinzani ni safi tuwape nchi bila kuwa na institutions za nguvu siwezi kushangaa wakiingia Ikulu wakajikuta kwenye vishawishi vya rushwa na challenge za kutatua matatizo magumu, sintoshangaa wakirudi nyuma na kujiingiza katika ufisadi.

This is just human nature, kwamba binadamu ni kama walivyosema waswahili, punda haendi bila kiboko, tukileta uzuri tutajikuta tunarudi pale pale.Inabidi tulete mabadiliko katika taasisis zetu ili mabadiliko ya utawala yawe na maana.

..hili ndio deal!
 
Kwa argument kama hii, ni bora ccm waendelee kunyonya na kusaza kwa vile hatujui kina Mrema wakipewa nchi watafanya nini. Dr Watson alisema kitu somewhere na ninakitafuta kuona kama kina uhusiano hapa!


..no,big no!

..point si nani anapewa,la hasha! point ni anayeshinda ni nani na jinsi gani atatekeleza ahadi zake kwa watanzania na kutimiza wajibu wake;kuongoza nchi na si kuifuja nchi.
 
mmmmh mwafrika wa kike hapo swala la CCM kuendelea kutawala milele mi kidogo nakupinga ila naungana na puundit alivyosema sheria ziwe kali kuanzia kwa rais mpaka katibu tarafa sasa hapo ndo ufisadi na rushwa na mambo mengine ya maudhi yatakwisha nchi hii.

nani atabadilisha hizo sheria kama ccm wamekataa kuzibadili?
 
...This is just human nature, kwamba binadamu ni kama walivyosema waswahili, punda haendi bila kiboko, tukileta uzuri tutajikuta tunarudi pale pale.Inabidi tulete mabadiliko katika taasisis zetu ili mabadiliko ya utawala yawe na maana.

Lakini asili ya binadamu ni kama asili ya Punda? Establish hilo kwanza. Wahenga hawakusema - ni Pundit kasema - binadamu ni kama Punda. Kwa hiyo kabla sija jaribu ku apply hiyo maxim ya Wahenga, nithibitishie kwamba binadamu ni kama Punda!
 
gang chomba,

Ndiyo maana nasisitiza tuwe na institutions zilizo na nguvu ya kufanya checks and balance, tuwe na katiba inayomuadibisha rais pamoja na mabadiliko mengine mengi, tuwe na bunge makini na siyo rubber stamp yetu hii, wananchi wenyewe wawe na elimu ya uraia pamoja na kuelimika kiujumla.

Tukiwa na institutions thabiti basi itakuwa haijaliki nani anachukua nchi, kama mfisadi au msafi, sheria, katiba, bunge, magazeti na wananchi watamkalia kooni mpaka mwenyewe atakuwa hana pa kupumlia.

Lakini tukisema wapinzani ni safi tuwape nchi bila kuwa na institutions za nguvu siwezi kushangaa wakiingia Ikulu wakajikuta kwenye vishawishi vya rushwa na challenge za kutatua matatizo magumu, sintoshangaa wakirudi nyuma na kujiingiza katika ufisadi.

This is just human nature, kwamba binadamu ni kama walivyosema waswahili, punda haendi bila kiboko, tukileta uzuri tutajikuta tunarudi pale pale.Inabidi tulete mabadiliko katika taasisis zetu ili mabadiliko ya utawala yawe na maana.

hizo institutions za nguvu nani ataziweka? Hebu tuwe kwenye real world kidogo hapa. CCM wamesema kamwe hawatabadili katiba wala kubadili uendeshaji wa serikali na institutions zingine. Hao ccm wanamajority ya nguvu bungeni, wanatumia nafasi ya upresident wa nchi kuchukua pesa hazina na kutumia kwenye kampeni na kisha the whole circle inaanza all over again.

Hii kwangu naipenda lakini naiona kama ndoto na just a talk. Ohh tubadili katiba na kujenga institution, how kama umewapa ccm dola na wanaitumia wanavyopenda?
 
Nilijua hiyo itasababisha controversy,

actually binadamu ni worse than Punda, angalau Punda anaweza kusema ung'amuzi wake wa mambo ni mdogo.Binadamu hata baada ya ung'amuzi mkubwa wa mambo bado anakuwa fisadi by nature.Ndiyo maana ukomunisti umeshindwa Urusi, wakati wengine wakipanga foleni kupata mikate ya rationing, wakuu wa chama cha kikomunisti walikuwa wanajivinjari katika ma Dacha yaliyo kwenye posh suburbs za Muskva.Na hata maduka yao yalikuwa tofauti kwani walikuwa na Supermarket zao zina kila kitu kutoka west.

Lord Acton alisema power corrupt, absolute power corrupts absolutely.Binadamu is worse than Punda na hawezi kutegemewa ku act responsibly bila ya kuwekewa sheria, at least as far as the context of government is concerned ambako all sorts of weird groupthink and mob psychology zinatokea na kuwafanya hata watu rational waanze kufanya mambo ya ajabu within a group.
 
kwani mbona hata kibaki alikuwa hataki katiba kubadilishwa lakini mbona wakeii wakamkalia kooni mpaka imerekebishwa?
ni woga uliowajaa watanzania walio wengi na kwa kisingizio cha amani CCM wanazidi kujinufaisha matumbo yao
 
kwani mbona hata kibaki alikuwa hataki katiba kubadilishwa lakini mbona wakeii wakamkalia kooni mpaka imerekebishwa?
ni woga uliowajaa watanzania walio wengi na kwa kisingizio cha amani CCM wanazidi kujinufaisha matumbo yao

mkuu angalia formation ya bunge la kenya na ulinganishe na la Tanzania!
 
Nilijua hiyo itasababisha controversy,

actually binadamu ni worse than Punda, angalau Punda anaweza kusema ung'amuzi wake wa mambo ni mdogo.Binadamu hata baada ya ung'amuzi mkubwa wa mambo bado anakuwa fisadi by nature.Ndiyo maana ukomunisti umeshindwa Urusi, wakati wengine wakipanga foleni kupata mikate ya rationing, wakuu wa chama cha kikomunisti walikuwa wanajivinjari katika ma Dacha yaliyo kwenye posh suburbs za Muskva.Na hata maduka yao yalikuwa tofauti kwani walikuwa na Supermarket zao zina kila kitu kutoka west.

Lord Acton alisema power corrupt, absolute power corrupts absolutely.Binadamu is worse than Punda na hawezi kutegemewa ku act responsibly bila ya kuwekewa sheria, at least as far as the context of government is concerned ambako all sorts of weird groupthink and mob psychology zinatokea na kuwafanya hata watu rational waanze kufanya mambo ya ajabu within a group.

Pundit bado nasubiria kuona ukisema namna ambavyo institution zitabadilishwa kabla ya kuwapa wapinzani uongozi.
 
mkuu angalia formation ya bunge la kenya na ulinganishe na la Tanzania!

mi ninachojaribu kuamini ni kuwa endapo wananchi wataamka na kufuata njia zoote wanazohisi zitawasaidia kuhakikisha katiba inabadilishwa basi itaweza kubadillishwa hata kama bunge lina wambunge watano tu wa upinzani. ila kama ndo tutabweteka na kuwasubiri wabunge ndo tutangoja milele na tutakufa bila kelele.
 
Back
Top Bottom