Usiishie tu kuandika blah... Blah hapa na kujizolea misifa kwa Hawa wazazi wenzio wa kisasa.
Hebu elezea kinaga ubaga umeweza vipi kuwafanya watoto wako kuwa na hiyo discipline ya Hali ya kujua kiasi kwamba wanajua kwamba hili ni kosa, hivi ni sahihi bila kuchapwa hata mara moja udogoni kwao?
Au which convenient approach did you employ to instill discipline to your children such that today intelligently they have become way better than those ones who were raised under the so-called corporal punishment ??? And furthermore what disciplinary actions were you taking against them everytime they misbehaved?
Asante kwa kuendeleza mjadala ila umeanza na ukali kidogo anyway kwa mimi hainisumbui sana
Unajua kuna disciplined aina nyingi na kupiga ni last option
Kumuadhibu kwa mangumi au makofi ya nguvu au fimbo za hasira yote sio nzuri na hiyo ndio napinga kabisa kwa nguvu zote
Lazima ujue binadamu wote ni tofauti kuna wengine hawajawahi kuwapiga watoto nina maana baina ya wazazi
Unakuta anaewadhibu ni mama na baba hapigi kabisa au kinyume
Kwa mimi siwapigi wanangu bali naongea nao sana
Who wana utundu wa kitoto ambao watoto wote wanafanya lakini nikiwaambia sasa ni mda wa kulala huwa hakuna ubishi na nimejaribu kuwalaza mda huo huo kila siku mpaka wamezoea na ukiwaacha ikifika mda utaona wana sinzia
Kuna wakati natoka nao na kwenda kutembea nao hata say Lisaa limoja na nusu au mawili tukirudi wamechoka
Sioni kitu kikubwa wanachofanya mpaka niwapige kipigo kikubwa hapana
Watoto ni kuwakataza mabaya na kuwafundisha mema kila wakati
Nacheza nao na sio kwamba eti mimi niko serious kila saa hapana
Nawanunulia toys zaidi na vitabu vingi pia rangi za kuchora na hata baiskeli zao kwa kila mmoja na weekend nawapeleka farm ambapo tutakuwa na lunch huko na watacheza na jioni kurudi
Sasa niambie unampiga kwa kosa lipi au mradi nipige tu
Sio waizi, hawatoki nje bila ruhusa na huwezi kuwakuta wanazurura hovyo nje kwa sababu wana vitu vingi vya kufanya na hata kuchezea nyumbani