Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Je mkuu Una Elimu sahihi ya malezi (parenting Education) au unatumia mfumo wa kuwa Mimi nilichapwa na Mimi nabidi kuchapa.?

Ni vizuri ukadeal na AKILI ya mtoto na sio mwili wake.
 
Hizo nchi ambazo watoto hawachapwi zina mmonyoko mkubwa wa maadili pia ,sisi tunajiona hatuna maadili ila ukitembelea kwa wenzetu utaona bado sisi tuna maadili sana😁
kabisa, halaf sio kila kosa mtoto anakandwa mimi naongea mwisho mara mbili akirudia the same mistake namkanda kidogo akija kufanya kosa extra large namkanda vizuri sana hata akienda kwa bibi yake unapata pongezi mtoto unamlea vizuri anakusikiliza ukimwambia jambo hajui naleaje.
 
Je mkuu Una Elimu sahihi ya malezi (parenting Education) au unatumia mfumo wa kuwa Mimi nilichapwa na Mimi nabidi kuchapa.?

Ni vizuri ukadeal na AKILI ya mtoto na sio mwili wake.
mimi silei mtoto kama nilivyolelelwa kwa sababu hata mm stiki nilizilamba vizuri sana na kwanamna flani zilinisaidia sasa mm nalea lakini akinikosea kosa naona kabisa anastahili kupigwa nampiga kwa kweli
 
Wenzetu hao tunaowataka kuwaiga , wao wenyewe wanatamani waishi kama sisi , kukuta toto linamwambia mzazi kwamba ni shoga kwa wenzetu ni kawaida sana ,hii mambo sioni kama kwetu ina afyaπŸ€”
 
mimi silei mtoto kama nilivyolelelwa kwa sababu hata mm stiki nilizilamba vizuri sana na kwanamna flani zilinisaidia sasa mm nalea lakini akinikosea kosa naona kabisa anastahili kupigwa nampiga kwa kweli

Unawajengea nidhamu ya uwoga watoto wako .

Ikiwa hawawezi kukusikiliza mpaka utumie viboko basi ujue hata wakikusikiliza ni kwakuwa wanaogopa viboko.
 
Wenzetu hao tunaowataka kuwaiga , wao wenyewe wanatamani waishi kama sisi , kukuta toto linamwambia mzazi kwamba ni shoga kwa wenzetu ni kawaida sana ,hii mambo sioni kama kwetu ina afyaπŸ€”
kizazi cha sasa watu tunaendeshwa na mfumo wa kisasa, mambo ya kuiga,hivi unamnyimaje mtoto kiboko? ameshaona madhara ya kunyima mtoto kiboko? asilimia kubwa ya watoto wasiopigwa japo sio wote wakiwa wakubwa wengi huwapanda wazazi wao vichwan na ukute mtoto huyo alilelewa na mzazi mmoja tu hilo ndio balaa, lea mtoto kama vile kesho hautakuwepo awese kuishi mazingira yoyote yale.
 
Wenzetu hao tunaowataka kuwaiga , wao wenyewe wanatamani waishi kama sisi , kukuta toto linamwambia mzazi kwamba ni shoga kwa wenzetu ni kawaida sana ,hii mambo sioni kama kwetu ina afyaπŸ€”
Hiyo Ajenda ya ushoga mnaitumia Kama defense mechanism Ila mnashindwa kutazama upande chanya wa wenzetu

Hao wenzetu wefanikiwa kuzalisha watoto bora ambao wapo productive tangia wakiwa wadogo hauwezi ukalinganisha na sisi

Ila nyie kila mada mnakimbilia muchomekea Ajenda ya Ushoga
 
Unawajengea nidhamu ya uwoga watoto wako .

Ikiwa hawawezi kukusikiliza mpaka utumie viboko basi ujue hata wakikusikiliza ni kwakuwa wanaogopa viboko.
tupo jamii ya changanyikeni, asilimia kubwa ya watoto wasiopigwa kwao ndio watovu wa nidham hasa wakiwa wanacheza pamoja na wenzao wanaokandwa na unaiona tofauti
 
No mkuu nmetolea mfano tu , mmonyoko wa maadili ni mkubwa sana kwa wenzetu tofauti kabisa na kwetu , pia hata wao wanapenda sana jinsi sisi tulivyo naongea kitu ninachokijua na sio nilichosikia mkuu .
 
No mkuu nmetolea mfano tu , mmonyoko wa maadili ni mkubwa sana kwa wenzetu tofauti kabisa na kwetu , pia hata wao wanapenda sana jinsi sisi tulivyo naongea kitu ninachokijua na sio nilichosikia mkuu .

Waafrica na wazungu

Kuhusu maadili hatuwafikii

Ebu tazama tu viongozi wetu wanaiba mpaka unaogopa sasa unajiuliza maadili ya MTU mweusi ni yapi hayo

Sisi ni wahuni Sana hatuna maadili yoyote

Tumebaki kusema kuwa hatufanyi ushoga basi hayo ndo maadili
 
😁😁😁😁😁Sisi umaskini tu ndio unatusumbua.

Njaa huwa ina tabia ya kuja na maelekezo mkuu😁😁😁😁
 
😁😁😁😁😁Sisi umaskini tu ndio unatusumbua.

Njaa huwa ina tabia ya kuja na maelekezo mkuu😁😁😁😁


Siku ya kwanza kwenda shule mzazi anakuambia uwe makini wasije wakakuibia .

Hapo ukiangalia unaenda boarding school πŸ€”πŸ€”πŸ€—πŸ˜ maadili sisi hatuna
 
Inategemea na aina ya mtoto. Nina watoto wawili, wa kwanza sikumlea kwa fimbo maana hakuwa anakupa sababu ya kumchapa. Nilimchapa mara moja tu au mbili kama sikosei. Yupo vizuri anajiendesha mwenyewe bila kuendeshwa, anajua nini anafanya.
Huyu mwingine jamani ee mungu nisaidie.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…