Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Je, Watoto wanaolelewa bila vipigo hawana maadili?

Nunua vitu vya jumla weka ndani acha kumtuma mtoto vitu rejaja dukani mara sukari robo, mara kiberiti kimoja, mara chumvi pakiti moja n.k
Mkuu hivyi unadhani ulivyo wewe namimi tunalingana kiuchumi?

Hujui Kuna familia Kila siku hununua mafuta 300 na sabuni ya kufulia na kuogea ndo hiyo hiyo? Kwa comment Yako inaonyesha wazi hujui hata uchumi wa watanzania walio wengi
 
Nashukuru hapa tuko na mama Dkt. Gwajima D atusaidie kupeleka muswada bungeni wa kufuta sheria ya viboko mashuleni, tena iwe ni kosa la jinai kumpiga viboko mtoto akiwa shule.

Kama hawawezi kufundisha watoto bila kuwararua na viboko ni HERI HIZO SHULE ZIFUNGWE KABISA.

Kuna shule za binafsi nyingi zikiwemo zinazomilikiwa na Mh. Anna Tibaijuka zinaendeshwa bila viboko na zinafanya vizuri tu kimaadili na kitaaluma. Tuige hiyo model, nendeni mkafanye utafiti kujua wamewezaje.

Viboko havijengi maadili, vinajenga NIDHAMU YA WOGA.

Waziri tunaomba mkafute ile sheria ya kikoloni.
Ninyi mnapinga viboko peleke kwenye shule ambazo hazipigi Watoto. Kwanza Kila siku wanapewa mkate na mayai huko na uji wa blue band pelekeni huko sisi tupeleke kwenye mboko.

Badala ya kushauri apeleke mswaada wa katiba mpya

Kama mnaona mboko hazifai futeni na magereza.
 
Ni kweli mkuu wengi hawakubali na kusema ooh tunawadekeza hell no
Mtoto kuonywa na kupigwa kidogo ni sawa ila sio mpaka unamchoma moto mikono kisa kadokoa nyama au kaiba mia
Kuna wazazi washenzi mkuu na hao ndio sikubaliani nao kabisa

Unamfunga kamba mtoto masaa na kumfungia chumbani siku nzima
Mkuu kuna ukatili wa watoto we acha tu
Hata humu unaweza kukuta watu wanapiga hivyo
Tuendelee kutoa darasa ili nao wabadilike
Mzazi hata siku moja hutembei barabarani na mwanao bali kuwakunjia uso tu
Akikuomba buku unamtukana
.aisee tunaona mengi sana mitaani
Wengine wanasema wazungu hawapigi sio kweli wakiwa wadogo wanawapiga kwa kuwafundisha ingawa wanajua wanaweza kunyang"anywa watoto
Ila nidhamu ipo
Kina mama kwa afrika ndio wanaongoza kwa ukatili wa watoto sasa sijui kisa mimba za nje ya ndoa sijui
Hii hafai kabisa yanaitwa mateso na manyanyaso makubwa Kwa mtoto.

Mbona kiasi yafaa sana
 
Aisee kuna watu wanapiga ht vitoto vichanga.
Wengine wanataka wtt wadogo wa act km watu wazima mtt asifanye utundu hata kdg anachapwa.
Wengine mtt akiwa na ufaham mdogo juu ya jambo fulani, wanachapa na matusi juu.
Mie adhabu ya kuchapa naipinga vikali mno
Sijawahi kuwapiga watoto wangu kwa sababu nimepigwa sana na ninaona kuna wakati nilikuwa napigwa hata nikitoka kucheza mpira
Hayo walikuwa wanafanya wazazi kudhani kuwa tutakuwa na nidhamu
Ila wengi waliharibika mpaka kuwa nunda, hata mimi nina watoto wakubwa na wengine wamemaliza vyuo ila wananipa heshima ya hali ya juu na upendo juu
Sina mtoto mwizi wala muongo kwa sababu nimewafundisha kama nilivyofundishwa ila bila fimbo

Najua kuna wazazi humu wanaona kupiga ni njia rahisi ya kumnyamazisha mtoto
Jamani hata mbuzi wadogo huwa wanakimbia kimbia wakiwa wadogo
Watoto wakicheza tushukuru Mungu wana afya njema na wanahitaji michezo
Kuna mwanangu alivunja kikombe alishtuka sana nikamwambia kaa mbali na hapo na ni ajali usijali
Sasa ukute mwingine atapigwa siku nzima na hata baadae haombwi msamaha kwa hasira za kijinga
Kikombe tu unamtoa mpaka damu mtoto daa
Wanangu wanalala wakiwa na furaha na lazima nihakikishe hilo
Na wakitoka shule ni kuwapokea kwa heshima bila maswali mengi hujui wamepata nini huko shule na pia wamechoka

Nakuomba uwaelimishe sana wanaopiga badala yake kuwa karibu na kuwafundisha
 
Au labda shoga?
Hii mada ndipo ilipofikia, kuwa shoga sidhani.

Ki ukweli malezi ya watoto ni suala mtambuka. Nakumbuka wakati nakua miaka ya tisini mwanzoni nilikuwa na kampani ya wahuni wahuni tu ambao walikuwa wanawaza HipHop na kutoboa maisha kama Black Americans.

Wengi wa washikaji zangu walizamia mamtoni, wamezamia kama wana 10+ hadi leo haijulikani kama wapo hai au wamekufa.

Wawili tu ndio tunawasiliana, mmoja yupo Ujerumani mwingine yupo Norway. Nilikuwa na kampani ya wahuni pale Upanga kabla ya kuhamia Ilala mwaka 1993.
 
Ninyi mnapinga viboko peleke kwenye shule ambazo hazipigi Watoto. Kwanza Kila siku wanapewa mkate na mayai huko na uji wa blue band pelekeni huko sisi tupeleke kwenye mboko.

Badala ya kushauri apeleke mswaada wa katiba mpya

Kama mnaona mboko hazifai futeni na magereza.
Unazo pesa za kumpeleka mtoto wako shule wanayokula mkate, mayai na uji wa blue band?
 
Mkuu hivyi unadhani ulivyo wewe namimi tunalingana kiuchumi?

Hujui Kuna familia Kila siku hununua mafuta 300 na sabuni ya kufulia na kuogea ndo hiyo hiyo? Kwa comment Yako inaonyesha wazi hujui hata uchumi wa watanzania walio wengi
Boreshini uchumi sasa muache kudunda watoto kwa sababu wamepoteza buku ya sukari.
 
Hii mada ndipo ilipofikia, kuwa shoga sidhani.

Ki ukweli malezi ya watoto ni suala mtambuka. Nakumbuka wakati nakua miaka ya tisini mwanzoni nilikuwa na kampani ya wahuni wahuni tu ambao walikuwa wanawaza HipHop na kutoboa maisha kama Black Americans.

Wengi wa washikaji zangu walizamia mamtoni, wamezamia kama wana 10+ hadi leo haijulikani kama wapo hai au wamekufa.

Wawili tu ndio tunawasiliana, mmoja yupo Ujerumani mwingine yupo Norway. Nilikuwa na kampani ya wahuni pale Upanga kabla ya kuhamia Ilala mwaka 1993.
Huko mamtoni unaweza kuta wana maisha mazuri tu ambayo hapa bongo labda wasingekaa wayapate lakini ndio hivyo wameamua kujitenga na wanoko na wengine ambao wangekuwa tegemezi tu kutaka kutumiwa remittance money kila wakati.
 
Bila fimbo Mtoto wa kibongo haendi Ila sio kila kitu unatumia fimbo,muadhibu Kwa mafundisho Mazuri upendo na fimbo Ila kadiria asiwe nunda! Si mnaona watoto wenu mnaowafundisha kizungu wanatukana Hadi watu mtaani! Analelewa kizungu anaishi kiswahili
 
Kwa nchi yetu Tanzania vipigo kwa watoto inaonekana ni jambo la kawaida sana, na huku baadhi wakipongeza jambo hilo kwa kuona ndio msingi bora wa malezi kwa watoto unaowafanya kuwa na maadili, hofu, kusikiliza na kutekeleza maagizo ya wazazi aidha kwa kutaka au kutokutaka kwa kuogopa kuadhibiwa kwa vipigo.

Kuna baadhi wamekuwa wakijisifu kuwa wao hawacheki na watoto kwani wao ni fimbo mkononi huku wakirejea maandiko kutoka kwenye vitabu vya dini kuwa Usimnyime mtoto mapigo na hivyo kuona kaaa walipewa ruksa ya kuwadunda watoto vilivyo kutoka kwa Muumba wao.

Hali hiyo imekuwa ikifanya watu wanaolea watoto bila kuhusisha vipigo kutuhumiwa kuwa wanawaharibu watoto, wanawadekeza na kwamba wanafata utamaduni wa wazungu ambao hauwezi kufanya kazi kwa watoto wa kiafrika hususani Watanzania, Wazazi wa aina hiyo wamekuwa wakituhumiwa kuzalisha watoto watakaokuja kuwa wa ovyo wasio na maadili wenye matendo mabaya.

Je, watu wote wasio na maadili waliopo ni zao la wazazi ambao hawakuwapiga watoto wao?
Je, hakuna watoto waliopigwa na hawakuwa na maadili licha ya vipigo vikali?

Ni kweli kipigo ndio suluhisho la maadili na usikivu kwa watoto?
Ni kweli hakuna watoto wanaolelewa bila vipigo na kuja kuwa watu wema?

Pamoja na yote wanaosifu vipigo kwa watoto huwa hawataki kabisa kuzungumzia athari hasi ya vipigo hivyo kwa watoto, na pengine hawatambui kuwa zipo. Je, hakuna namna ya kuweza kuwalea watoto bila kuhusisha vipigo?

Pia soma: Je, ni kweli Adhabu ya Viboko inasaidia kuongeza Nidhamu na Uelewa kwa Mtoto?
Mkuu kiukweli hao wanatumia maandiko ya Dini wanatumia vibaya maandiko wengi wao:Kwanza maandiko yanasema kweli tuwape watoto kipigo Tena ukiwa huna hasira na si kila kosa ni Lazima kipigo!Hivi sasa vipigo sio kwa ajili ya kumwadabisha mtoto,Bali ni mtu ana stress zake huko, mtoto akikisea hasira zake anammbebesha mtoto.
 
Back
Top Bottom