Nikifa MkeWangu Asiolewe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2024
- 6,944
- 14,351
Mkuu hivyi unadhani ulivyo wewe namimi tunalingana kiuchumi?Nunua vitu vya jumla weka ndani acha kumtuma mtoto vitu rejaja dukani mara sukari robo, mara kiberiti kimoja, mara chumvi pakiti moja n.k
Ninyi mnapinga viboko peleke kwenye shule ambazo hazipigi Watoto. Kwanza Kila siku wanapewa mkate na mayai huko na uji wa blue band pelekeni huko sisi tupeleke kwenye mboko.Nashukuru hapa tuko na mama Dkt. Gwajima D atusaidie kupeleka muswada bungeni wa kufuta sheria ya viboko mashuleni, tena iwe ni kosa la jinai kumpiga viboko mtoto akiwa shule.
Kama hawawezi kufundisha watoto bila kuwararua na viboko ni HERI HIZO SHULE ZIFUNGWE KABISA.
Kuna shule za binafsi nyingi zikiwemo zinazomilikiwa na Mh. Anna Tibaijuka zinaendeshwa bila viboko na zinafanya vizuri tu kimaadili na kitaaluma. Tuige hiyo model, nendeni mkafanye utafiti kujua wamewezaje.
Viboko havijengi maadili, vinajenga NIDHAMU YA WOGA.
Waziri tunaomba mkafute ile sheria ya kikoloni.
Hii hafai kabisa yanaitwa mateso na manyanyaso makubwa Kwa mtoto.Ni kweli mkuu wengi hawakubali na kusema ooh tunawadekeza hell no
Mtoto kuonywa na kupigwa kidogo ni sawa ila sio mpaka unamchoma moto mikono kisa kadokoa nyama au kaiba mia
Kuna wazazi washenzi mkuu na hao ndio sikubaliani nao kabisa
Unamfunga kamba mtoto masaa na kumfungia chumbani siku nzima
Mkuu kuna ukatili wa watoto we acha tu
Hata humu unaweza kukuta watu wanapiga hivyo
Tuendelee kutoa darasa ili nao wabadilike
Mzazi hata siku moja hutembei barabarani na mwanao bali kuwakunjia uso tu
Akikuomba buku unamtukana
.aisee tunaona mengi sana mitaani
Wengine wanasema wazungu hawapigi sio kweli wakiwa wadogo wanawapiga kwa kuwafundisha ingawa wanajua wanaweza kunyang"anywa watoto
Ila nidhamu ipo
Kina mama kwa afrika ndio wanaongoza kwa ukatili wa watoto sasa sijui kisa mimba za nje ya ndoa sijui
😀😀😀Maadili ya bongo ni kutokuwa shoga tu,
Wewe mradi sio shoga hata ukiwa teja, fisadi, jambazi, mkwepa kodi, malaya, mbamikiaji kesi, muongo n.k sio ishu sana.
Wapo mkuu wanaopiga kisa tu baba kamtelekeza mama na msala unampata mtotoHii hafai kabisa yanaitwa mateso na manyanyaso makubwa Kwa mtoto.
Mbona kiasi yafaa sana
Sijawahi kuwapiga watoto wangu kwa sababu nimepigwa sana na ninaona kuna wakati nilikuwa napigwa hata nikitoka kucheza mpiraAisee kuna watu wanapiga ht vitoto vichanga.
Wengine wanataka wtt wadogo wa act km watu wazima mtt asifanye utundu hata kdg anachapwa.
Wengine mtt akiwa na ufaham mdogo juu ya jambo fulani, wanachapa na matusi juu.
Mie adhabu ya kuchapa naipinga vikali mno
Hii mada ndipo ilipofikia, kuwa shoga sidhani.Au labda shoga?
Unazo pesa za kumpeleka mtoto wako shule wanayokula mkate, mayai na uji wa blue band?Ninyi mnapinga viboko peleke kwenye shule ambazo hazipigi Watoto. Kwanza Kila siku wanapewa mkate na mayai huko na uji wa blue band pelekeni huko sisi tupeleke kwenye mboko.
Badala ya kushauri apeleke mswaada wa katiba mpya
Kama mnaona mboko hazifai futeni na magereza.
Boreshini uchumi sasa muache kudunda watoto kwa sababu wamepoteza buku ya sukari.Mkuu hivyi unadhani ulivyo wewe namimi tunalingana kiuchumi?
Hujui Kuna familia Kila siku hununua mafuta 300 na sabuni ya kufulia na kuogea ndo hiyo hiyo? Kwa comment Yako inaonyesha wazi hujui hata uchumi wa watanzania walio wengi
Huko mamtoni unaweza kuta wana maisha mazuri tu ambayo hapa bongo labda wasingekaa wayapate lakini ndio hivyo wameamua kujitenga na wanoko na wengine ambao wangekuwa tegemezi tu kutaka kutumiwa remittance money kila wakati.Hii mada ndipo ilipofikia, kuwa shoga sidhani.
Ki ukweli malezi ya watoto ni suala mtambuka. Nakumbuka wakati nakua miaka ya tisini mwanzoni nilikuwa na kampani ya wahuni wahuni tu ambao walikuwa wanawaza HipHop na kutoboa maisha kama Black Americans.
Wengi wa washikaji zangu walizamia mamtoni, wamezamia kama wana 10+ hadi leo haijulikani kama wapo hai au wamekufa.
Wawili tu ndio tunawasiliana, mmoja yupo Ujerumani mwingine yupo Norway. Nilikuwa na kampani ya wahuni pale Upanga kabla ya kuhamia Ilala mwaka 1993.
MaishaKupiga mtu yeyote yule(hasa asie na uwezo wa kukurudishia) ni hatua ya juu kabisa ya uonevu.
Jiulize, wewe ukikosea, ni nani huwa anakupiga?
Kwa amri ipi? tuboreshe maisha kwa uchumi upi wa nchi?Boreshini uchumi sasa muache kudunda watoto kwa sababu wamepoteza buku ya sukari.
Soma vzr nilicho andikaUnazo pesa za kumpeleka mtoto wako shule wanayokula mkate, mayai na uji wa blue band?
MinHata hawa watoto wa miaka ya 2000 wengi wao hawakupitia viboko , je umeona tofauti yoyote kimaadili?
Mkuu kiukweli hao wanatumia maandiko ya Dini wanatumia vibaya maandiko wengi wao:Kwanza maandiko yanasema kweli tuwape watoto kipigo Tena ukiwa huna hasira na si kila kosa ni Lazima kipigo!Hivi sasa vipigo sio kwa ajili ya kumwadabisha mtoto,Bali ni mtu ana stress zake huko, mtoto akikisea hasira zake anammbebesha mtoto.Kwa nchi yetu Tanzania vipigo kwa watoto inaonekana ni jambo la kawaida sana, na huku baadhi wakipongeza jambo hilo kwa kuona ndio msingi bora wa malezi kwa watoto unaowafanya kuwa na maadili, hofu, kusikiliza na kutekeleza maagizo ya wazazi aidha kwa kutaka au kutokutaka kwa kuogopa kuadhibiwa kwa vipigo.
Kuna baadhi wamekuwa wakijisifu kuwa wao hawacheki na watoto kwani wao ni fimbo mkononi huku wakirejea maandiko kutoka kwenye vitabu vya dini kuwa Usimnyime mtoto mapigo na hivyo kuona kaaa walipewa ruksa ya kuwadunda watoto vilivyo kutoka kwa Muumba wao.
Hali hiyo imekuwa ikifanya watu wanaolea watoto bila kuhusisha vipigo kutuhumiwa kuwa wanawaharibu watoto, wanawadekeza na kwamba wanafata utamaduni wa wazungu ambao hauwezi kufanya kazi kwa watoto wa kiafrika hususani Watanzania, Wazazi wa aina hiyo wamekuwa wakituhumiwa kuzalisha watoto watakaokuja kuwa wa ovyo wasio na maadili wenye matendo mabaya.
Je, watu wote wasio na maadili waliopo ni zao la wazazi ambao hawakuwapiga watoto wao?
Je, hakuna watoto waliopigwa na hawakuwa na maadili licha ya vipigo vikali?
Ni kweli kipigo ndio suluhisho la maadili na usikivu kwa watoto?
Ni kweli hakuna watoto wanaolelewa bila vipigo na kuja kuwa watu wema?
Pamoja na yote wanaosifu vipigo kwa watoto huwa hawataki kabisa kuzungumzia athari hasi ya vipigo hivyo kwa watoto, na pengine hawatambui kuwa zipo. Je, hakuna namna ya kuweza kuwalea watoto bila kuhusisha vipigo?
Pia soma: Je, ni kweli Adhabu ya Viboko inasaidia kuongeza Nidhamu na Uelewa kwa Mtoto?
Takwimu zipi na nikupatie za kazi gani? Sijaelewa mkuuMin
Utupatie mchanganuo wa hizi takwimu ulizikusanya vipi?