Kurunzi
JF-Expert Member
- Jul 31, 2009
- 9,753
- 10,747
MCHEZO WA MAAMUZI (CAFCC)..
Ni mchezo wa mamuzi kwa timu zote mbili , Marumo gallants wakiitaji ushindi wa magoli mengi kwa kujiweka nafasi nzuri ya kufuzu kwenda hatua ya fainali huku Yanga Sc kwao ni mchezo wa kuamua hatma yao kwenye fainali .
Marumo gallants kwenye mchezo wa mwisho akiwa kwenye ardhi ya nyumbani alipata ushindi mbele ya Pyramid , lakini haiwezi kuwa sehemu ya kuifanya Marumo gallants kuingia kinyonge kwenye mchezo huu.
Kwa jinsi mchezo ulivyo kuwa wa muhimu kama yanga sc ataruhusu goli katika mchezo huu basi nafasi yake ya kwenda fainali inakuwa ndogo sana, huku Yanga Sc wao mchezo ukiisha wakiwa wamepoteza kwa magoli dhidi ya mawili basi nafasi yao kwenda fainali itapotea.
Prof Nabi na mfumo wake mama akiwa ugenini 4-2-3-1 , viungo wawili wa chini “Double Pivot” huku namba 10 wawili (Aziz Ki na Mudathir) dhumuni kubwa ni kuwa na idadi kubwa ya wakabaji (viungo) , nafikiri itakuwa moja ya silaha yake kubwa siku ya leo.
Yanga Sc mchezo uliopita dhidi ya Marumo gallants hapa nyumbani hawakuwa na game nzuri , walionekana kuwa na changamoto kubwa kwenye eneo la kiungo walishindwa kucontrol mchezo , pia hawakuwa bora sana kwenye kutumia makosa ya Marumo gallants kuwaadhibu.
NB; Ni Wananchi dhidi ya Marumo gallants , Mchezo wa kuamua hatma zao kwenda Fainali.
Napatikana instagram kama Michezo_kusini
Ni mchezo wa mamuzi kwa timu zote mbili , Marumo gallants wakiitaji ushindi wa magoli mengi kwa kujiweka nafasi nzuri ya kufuzu kwenda hatua ya fainali huku Yanga Sc kwao ni mchezo wa kuamua hatma yao kwenye fainali .
Marumo gallants kwenye mchezo wa mwisho akiwa kwenye ardhi ya nyumbani alipata ushindi mbele ya Pyramid , lakini haiwezi kuwa sehemu ya kuifanya Marumo gallants kuingia kinyonge kwenye mchezo huu.
Kwa jinsi mchezo ulivyo kuwa wa muhimu kama yanga sc ataruhusu goli katika mchezo huu basi nafasi yake ya kwenda fainali inakuwa ndogo sana, huku Yanga Sc wao mchezo ukiisha wakiwa wamepoteza kwa magoli dhidi ya mawili basi nafasi yao kwenda fainali itapotea.
Prof Nabi na mfumo wake mama akiwa ugenini 4-2-3-1 , viungo wawili wa chini “Double Pivot” huku namba 10 wawili (Aziz Ki na Mudathir) dhumuni kubwa ni kuwa na idadi kubwa ya wakabaji (viungo) , nafikiri itakuwa moja ya silaha yake kubwa siku ya leo.
Yanga Sc mchezo uliopita dhidi ya Marumo gallants hapa nyumbani hawakuwa na game nzuri , walionekana kuwa na changamoto kubwa kwenye eneo la kiungo walishindwa kucontrol mchezo , pia hawakuwa bora sana kwenye kutumia makosa ya Marumo gallants kuwaadhibu.
NB; Ni Wananchi dhidi ya Marumo gallants , Mchezo wa kuamua hatma zao kwenda Fainali.
Napatikana instagram kama Michezo_kusini