Jehanamu ni uhalisia au ni jambo la kupumbaza akili za watu?

Jehanamu ni uhalisia au ni jambo la kupumbaza akili za watu?

Mkuu huo moto upo

Ni kweli Mungu uliyemtaja hapo juu ni Mungu wa upendo, wa amani wa furaha n.k

Anasema Mwenyeezi Mungu katika Qur'an... Angalipenda angetutiisha wote (tutii amri zake) kama alivyowatiisha malaika,

Lakini aliamua kutupa uhuru kila mmoja afuate njia aipendayo bila kushurutishwa

Dunia ni kama shule tu, utapewa mitihani ukiifanya vizuri unakua rewarded umefaulu ukiifanya vibaya unakua rejected mwishoni

Anauliza Mwenyezi Mungu katika Qur'an anadhani mwanadamu ataachwa hivi hivi kwa kusema kwake tu ameamini? Bla shaka atatiwa katika mitihani hakuna janja janja muzee

Kama si hivyo dunian pangekua mahala pa ajabu sana

Dhulma ingetawala, mauwaji yangeshamiri, uzinzi, ubakaji, unyonyaji, fitna, na takataka zote uzijuazo zingeongezeoa mara milioni ya hizi uzionazo sasa
Asante kwa mchango wako lakini Nina swali kuhusu kutiishwa kwa malaika maana shetani naye alikuwa malaika mku
Aliye kufanya kua na hiyo akili ni nani?
Hiyohiyo ENERGY ambayo wengine wanaisingizia kwamba itatufanya mishikaki kwa milele yote
 
Watu waovu kama Makaburu, Putin, Iddi Amin na Adolf Hitler hawataonja Jehanamu?
Yani mwisho wao ndio hapa hapa duniani?!
Kunyimwa furaha ya milele inayotajwa kama uzima wa milele ndiyo adhabu ya kutosha. Hao uliowataja na wengine wote waovu malipo Yao ni hayo ila siyo Hekaya za Mungu wa kuchoma watu mishikaki ambayo yeye mwenyewe hana hata hamu ya kuila!!
 
WAOVU WANA MALIPO YAO.
Kama utawala wa duniani unatoa adhabu kwa wakosefu kwanini utawala wa mbinguni usitoe adhabu kwa wakosefu?
Mwenyezi mungu atuepushe na jehannam
Hilo liko wazi wala sipingani nalo. Lakini nasisitiza Tena A FINITE OFFENCE DEMANDS A FINITE PENALTY. Hizi habari za Mungu kukaanga watu kwenye moto ni Hekaya za kujazana ujinga. Kwenye ulimwengu wa roho hakuna moto. Moto ili uwe moto unahitaji Oksijeni! Hiyo kwenye ulimwengu wa roho hakuna.
 
Mkuu huo moto upo

Ni kweli Mungu uliyemtaja hapo juu ni Mungu wa upendo, wa amani wa furaha n.k

Anasema Mwenyeezi Mungu katika Qur'an... Angalipenda angetutiisha wote (tutii amri zake) kama alivyowatiisha malaika,

Lakini aliamua kutupa uhuru kila mmoja afuate njia aipendayo bila kushurutishwa

Dunia ni kama shule tu, utapewa mitihani ukiifanya vizuri unakua rewarded umefaulu ukiifanya vibaya unakua rejected mwishoni

Anauliza Mwenyezi Mungu katika Qur'an anadhani mwanadamu ataachwa hivi hivi kwa kusema kwake tu ameamini? Bla shaka atatiwa katika mitihani hakuna janja janja muzee

Kama si hivyo dunian pangekua mahala pa ajabu sana

Dhulma ingetawala, mauwaji yangeshamiri, uzinzi, ubakaji, unyonyaji, fitna, na takataka zote uzijuazo zingeongezeoa mara milioni ya hizi uzionazo sasa
Asante sana kwa mchango wako. Lakini moto huo uko wapi? Kwenye huu ulimwengu wetu au ulimwengu wa roho??
 
Mbingu huwa ipo wapi? Tuanzie hapo kwanza, tusije tukawa tunajitengenezea vitu vya kufikirika tu
Swali Zuri kabisa. Kwa wengi wetu eti mbinguni ni huko juu ya mawingu😆
Ujinga mtupu! Wakati fulani nilimlaumu mwanaanga ( Astronaut) wa Urusi, Yuri Gagarin kwa kauli yake kwamba alipoenda huko anga za juu hakumuona Mungu. Alikuwa sahihi maana Mungu hakai huko. Mbinguni ni hali iliyo kwenye plane of existence tofauti na yetu.
 
Mkuu,
Kama unaamini ni uongo tu unaoambiwa, basi endelea kwa wakati wako kufanya dhambi. Baada ya kufa utuletee mrejesho mambo yakoje huko. Kwa maana nyingine, ipi bora: kujiweka sawa kwa kuamini unachoambiwa, au kusubiri mpaka kufa ujionee mwenyewe, na kama moto upo kweli sijui utafanyaje?
Hujazikia hata msemo wa mitaani unaosema AKILI ZA KUAMBIWA ONGEZA NA ZAKO?
 
Uhakika wa hayo utaujua pale utakapo tayari umekufa.
 
Ipo laliki mm naamin kuna mungu mwingine atajitokeza kutusaidia haiwez kuwa ya milele never.
Miungu iko mingi sana. Biblia inasema hata sisi binadamu ni miungu. Milele kwenye ulimwengu wa riho haina uhusiano na dakika au masaa tunayoyajua. Tunamsingizia Mungu vitu visivyomhusu
 
Mbingu zipo SABA( 7)
Kama sayari zipo kwanini mbingu zisiwepo?
Aliyefanya yote hayo ndo amesema mbingu zipo kwanini usiamini?
Kwa hiyo mbingu ni physical place?? Kama ndiyo sema ilipo niongee na NASA tutume chombo cha anga za juu! Niambie pia iko Kwenye galaxy ipi.
 
Mbigu ipo hapo hapo ulipo but in another side😆.dimensions
Una akili sana wewe. Wengine hata hizo dimensions ni kitendawili kwao basi wanaishia kusema tu ni ulimwengu wa roho. Ukimuuliza roho ni nini hana jibu. Big up mkuu!
 
Acha kuzunguka zunguka kwa mambo ambayo hujaulizwa. Nimekuuliza mbingu ipo wapi? Haya, kama umesema mbingu ziko 7, ndo nauliza hizo mbingu zipo sehemu gani???

Nahitaji majibu, maana tunakaririshwa uomgo huko makanisani na misikitini
Nimemjibu pia kwa namna ya swali. Haya mambo ya kukariri Hekaya za wageni yamewatia watu kwenye utumwa mbaya sana
 
Sasa hao wanaotwambia ipo huko juu wanamdanganya nani??
Aliyekuambia mbingu ipo huko juu ni taahira wa elimu ya kila aina. Kwanza kwenye space juu ni wapi. Maana relatively hata hapo ulipo upo kichwa chini miguu juu japo unatembea na kufanya mambo yako. Kwa sababu ya udogo wa mwili waKo relative to the massive earth huwezi kuhisi hilo.
 
Tuwaulize wao sasa watuelekeze vizuri[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Hakuna juu. Juu ipo juu ya kichwa chako tu. Leo ukisema juu ni pale baada ya masaa kadhaa pale uliposema ni juu tayari ni chini. Haya mambo ya dini usipoweka na elimu ya Dunia utaambulia patupu
 
Kama vile upande mwingine huamini mateso huanzia kaburini kwa wenye dhambi eti watakumbana na joka nalo litawanyofoa macho!ikiwa adhabu zipo duniani(sharia ya kidini)na kaburini(nyoka na wadudu)hiyo jehanamu ya nini?
Hakuna mtu mwenye akili timamu ataamini hizo hadithi. Ni Hila za wajanja kutiana hofu tu
 
Back
Top Bottom