Jenerali Mabeyo: Tulimpoteza Rais Magufuli, tulisimama kidete kama Jeshi kulinda Katiba

Jenerali Mabeyo: Tulimpoteza Rais Magufuli, tulisimama kidete kama Jeshi kulinda Katiba

jinga kubwa wewe. kila kitu mnaingiza siasa.
Jinga wewe usiyejua kuwa hata jeshi lipo chini ya wizara ya ulinzi inayoongozwa na mwanasiasa…. Muulize CDF kwanini anampigia salute mwanasiasa….
 
Uko sahihi 100%
Huo ni wajibu wao
Hata Sisi walimu tunasimama kidete kuwafundisha wanafunzi
Hatupaswi kusifiwa kwa kufundisha ila tunapaswa kusifiwa kama tukiendesha magari au tukibeba bunduki na kupigania vita
 
Mambo yapo hayo tusiyopaswa kuyajua??
Bunge la Marekani sasa hivi wako kwenye kikao maalum kujadili jinsi Trump alivyotaka kupindua serikali na kila aliyehusika anahojiwa hadharani.
Kwa nini unataka ufafanuzi? Mambo mengine ni siri za nchi na vizuri yabaki kuwa siri za nchi. Wananchi nyie shukuruni nchi ilivuka salama maisha yanaendelea. Siri za nchi, usalama wa nchi waachieni wahusika.
 
View attachment 2270035

====

Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) anayemaliza muda wake Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ametaja kifo cha Rais wa awamu ya tano John Magufuli, na matukio yaliyofuata baada ya tukio hilo, kama moja kati ya changamoto kubwa alizokabiliana nazo kwani Jeshi lilipaswa kusimama kidete kuilinda Katiba ya nchi.

Mabeyo, aliyeanza kutumikia wadhifa huo mnamo Februari 6, 2017, baada ya kuteuliwa na Rais Magufuli, akichukua nafasi ya Jenerali mstaafu Davis Mwamunyange, alieleza hayo wakati wa mahojiano maalum na kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ITV hapo Juni 22, 2022.

“Nadhani [Watanzania] ni mashuhuda [kwamba] kwa mara ya kwanza, [Tanzania] tukampoteza Rais aliyekuwa madarakani,” Mabeyo, 65, alisema wakati wa mahojiano hayo.

“[Hiki] kilikuwa ni kipindi kigumu kidogo. Lakini tulisimama kidete, kwa utulivu mzuri, kama jeshi, tukitimiza wajibu wetu kwa mujibu wa Katiba, kuilinda nchi yetu [na] kuilinda Katiba.

“Na hilo likapita salama. Tukampokea Rais mpya, ambaye tunaendelea naye mama Samia Suluhu Hassan, na naamini kwamba tunaendelea vizuri. Nchi iko salama mpaka sasa. Wananchi wako watulivu, wanaendelea kufuata miongozo kama inavyotolewa na Serikali,” aliongeza Mabeyo.

Rais Magufuli alifariki mnamo Machi 17, 2021, kutokana na matatizo ya moyo, tukio lilioandika historia mpya kwa taifa la Tanzania ya Rais kufariki akiwa madarakani. Habari za kifo cha Rais huyo aliyekonga nyoyo za watu wengi na kuwakera wengine zilitangazwa usiku wa Machi 18, 2021, na aliyekuwa Makamu wake wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Samia aliapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita mnamo Machi 19, 2021, huku Jeshi la Ulinzi (JWTZ), ambalo kazi yake kuu ni kulinda Katiba na mipaka ya nchi, likipongezwa kwa kiasi kikubwa kusimamia uhamisho huo wa madaraka kwa utulivu mkubwa.

Matishio ya ugaidi
Mabeyo, ambaye aliagwa rasmi bungeni hapo Juni 14, 2022, huku Spika wa Bunge Tulia Ackson akimshukuru kwa “utumishi wako uliotukuka” kwa Tanzania, alitaja matishio ya ugaidi ambayo Tanzania imekuwa ikikabiliana nayo kwa miaka ya hivi karibuni kama moja ya “milima” aliyopaswa kuipanda wakati wa uongozi wake.

Matukio haya ni pamoja na yale ya Amboni, mkoani Tanga; Kibiti, mkoa wa Pwani; ugaidi huko mkoani Mwanza; na huko Mtwara kwenye mpaka na Msumbiji ambako magaidi wamekuwa wakifanya maisha ya jamii za karibu na mpaka huo kuwa magumu kwa kutokuwa na uhakika wa usalama wao.

“Kwa kweli, kipindi hicho kilikuwa kigumu sana lakini tunashukuru ushirikiano na wananchi, ushirikiano na vyombo vingine vya usalama, tumeweza kuhimili,” alibainisha Mabeyo kwenye mahojiano hayo.

“Lakini ni bahati mbaya kwamba majirani zetu [Msumbuji] wanakabiliwa sasa na tishio hilo [la ugaidi] kwa kiasi kikubwa. Na sisi kama sehemu ya ukanda wetu huu wa [Nchi za Kusini mwa Afrika] tumekubaliana kwamba tuwasaidie wenzetu,” aliongeza Mabeyo.

Migogoro ya ardhi
Kwenye mahojiano hayo pia, Mabeyo alikiri uwepo wa migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, akisema mingi ya migogoro hiyo inatokana na Serikali kushindwa kulipa fidia kwa wakati lakini pia uvamizi wa maeneo ya jeshi na wananchi.

Migogoro ya ardhi kati ya jeshi na wananchi ni tatizo kubwa ambalo mara kadhaa Serikali imeahidi kutafuta namna bora za kukabiliana nalo.

Hivi karibuni, kwa mfano, Waziri wa Ulinzi Dk Stergomena Tax alikiambia kituo cha habari cha Dar24 kwamba Serikali iliandaa mpango wa miaka mitatu – 2020/2021 mpaka 2022/2023 –kwa ajili ya kutatua migogoro hiyo.

“Kwa sasa wataalam wapo sehemu mbalimbali za nchi ambazo zimeainishwa na kuna baadhi migogogoro imeshatatuliwa na kuna sehemu bado inaendelea kutafutiwa ufumbuzi,” Dk Tax amenukuliwa akisema.

Kwenye mahojiano yake na ITV, Mabeyo alisema jeshi linafanya kila linalowezekana kuhakiksha migogoro iliyopo sasa inatatuliwa na kwamba hakuna migogoro mipya inazalishwa.

Alipoulizwa anatamani kuona jeshi la aina gani muda huu ambao anaenda kustaafu, Mabeyo alisema kwamba anatamani Jeshi la Tanzania liwe la kisasa zaidi, huku likijitegemea na kutoa mchango zaidi katika ujenzi wa uchumi wa nchi.

“Kwa nini wenzetu wanatengeneza zana wanatuletea kutuuzia sisi?” anauliza Mabeyo. “Kwa nini na sisi tusitengeneze zana za kututosheleza sisi wenyewe? [Wenzetu] wana hoteli, wana nyumba nzuri ambazo watu wanakuja wanakaa wanaongeza uchumi wa nchi. Na sisi jeshi letu liwe hivyo.”

Lukelo Francis ni mwandishi wa The Chanzo kutoka Dar es Salaam, Tanzania. Anapatikana kupitia lukelo@thechanzo.com.
chuma hiko bwana!dah mama kiongezee hata mwaka mmoja!!
 
View attachment 2270035

====

Dar es Salaam. Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) anayemaliza muda wake Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ametaja kifo cha Rais wa awamu ya tano John Magufuli, na matukio yaliyofuata baada ya tukio hilo, kama moja kati ya changamoto kubwa alizokabiliana nazo kwani Jeshi lilipaswa kusimama kidete kuilinda Katiba ya nchi.

Mabeyo, aliyeanza kutumikia wadhifa huo mnamo Februari 6, 2017, baada ya kuteuliwa na Rais Magufuli, akichukua nafasi ya Jenerali mstaafu Davis Mwamunyange, alieleza hayo wakati wa mahojiano maalum na kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ITV hapo Juni 22, 2022.

“Nadhani [Watanzania] ni mashuhuda [kwamba] kwa mara ya kwanza, [Tanzania] tukampoteza Rais aliyekuwa madarakani,” Mabeyo, 65, alisema wakati wa mahojiano hayo.

“[Hiki] kilikuwa ni kipindi kigumu kidogo. Lakini tulisimama kidete, kwa utulivu mzuri, kama jeshi, tukitimiza wajibu wetu kwa mujibu wa Katiba, kuilinda nchi yetu [na] kuilinda Katiba.

“Na hilo likapita salama. Tukampokea Rais mpya, ambaye tunaendelea naye mama Samia Suluhu Hassan, na naamini kwamba tunaendelea vizuri. Nchi iko salama mpaka sasa. Wananchi wako watulivu, wanaendelea kufuata miongozo kama inavyotolewa na Serikali,” aliongeza Mabeyo.

Rais Magufuli alifariki mnamo Machi 17, 2021, kutokana na matatizo ya moyo, tukio lilioandika historia mpya kwa taifa la Tanzania ya Rais kufariki akiwa madarakani. Habari za kifo cha Rais huyo aliyekonga nyoyo za watu wengi na kuwakera wengine zilitangazwa usiku wa Machi 18, 2021, na aliyekuwa Makamu wake wa Rais Samia Suluhu Hassan.

Samia aliapishwa kuwa Rais wa awamu ya sita mnamo Machi 19, 2021, huku Jeshi la Ulinzi (JWTZ), ambalo kazi yake kuu ni kulinda Katiba na mipaka ya nchi, likipongezwa kwa kiasi kikubwa kusimamia uhamisho huo wa madaraka kwa utulivu mkubwa.

Matishio ya ugaidi
Mabeyo, ambaye aliagwa rasmi bungeni hapo Juni 14, 2022, huku Spika wa Bunge Tulia Ackson akimshukuru kwa “utumishi wako uliotukuka” kwa Tanzania, alitaja matishio ya ugaidi ambayo Tanzania imekuwa ikikabiliana nayo kwa miaka ya hivi karibuni kama moja ya “milima” aliyopaswa kuipanda wakati wa uongozi wake.

Matukio haya ni pamoja na yale ya Amboni, mkoani Tanga; Kibiti, mkoa wa Pwani; ugaidi huko mkoani Mwanza; na huko Mtwara kwenye mpaka na Msumbiji ambako magaidi wamekuwa wakifanya maisha ya jamii za karibu na mpaka huo kuwa magumu kwa kutokuwa na uhakika wa usalama wao.

“Kwa kweli, kipindi hicho kilikuwa kigumu sana lakini tunashukuru ushirikiano na wananchi, ushirikiano na vyombo vingine vya usalama, tumeweza kuhimili,” alibainisha Mabeyo kwenye mahojiano hayo.

“Lakini ni bahati mbaya kwamba majirani zetu [Msumbuji] wanakabiliwa sasa na tishio hilo [la ugaidi] kwa kiasi kikubwa. Na sisi kama sehemu ya ukanda wetu huu wa [Nchi za Kusini mwa Afrika] tumekubaliana kwamba tuwasaidie wenzetu,” aliongeza Mabeyo.

Migogoro ya ardhi
Kwenye mahojiano hayo pia, Mabeyo alikiri uwepo wa migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, akisema mingi ya migogoro hiyo inatokana na Serikali kushindwa kulipa fidia kwa wakati lakini pia uvamizi wa maeneo ya jeshi na wananchi.

Migogoro ya ardhi kati ya jeshi na wananchi ni tatizo kubwa ambalo mara kadhaa Serikali imeahidi kutafuta namna bora za kukabiliana nalo.

Hivi karibuni, kwa mfano, Waziri wa Ulinzi Dk Stergomena Tax alikiambia kituo cha habari cha Dar24 kwamba Serikali iliandaa mpango wa miaka mitatu – 2020/2021 mpaka 2022/2023 –kwa ajili ya kutatua migogoro hiyo.

“Kwa sasa wataalam wapo sehemu mbalimbali za nchi ambazo zimeainishwa na kuna baadhi migogogoro imeshatatuliwa na kuna sehemu bado inaendelea kutafutiwa ufumbuzi,” Dk Tax amenukuliwa akisema.

Kwenye mahojiano yake na ITV, Mabeyo alisema jeshi linafanya kila linalowezekana kuhakiksha migogoro iliyopo sasa inatatuliwa na kwamba hakuna migogoro mipya inazalishwa.

Alipoulizwa anatamani kuona jeshi la aina gani muda huu ambao anaenda kustaafu, Mabeyo alisema kwamba anatamani Jeshi la Tanzania liwe la kisasa zaidi, huku likijitegemea na kutoa mchango zaidi katika ujenzi wa uchumi wa nchi.

“Kwa nini wenzetu wanatengeneza zana wanatuletea kutuuzia sisi?” anauliza Mabeyo. “Kwa nini na sisi tusitengeneze zana za kututosheleza sisi wenyewe? [Wenzetu] wana hoteli, wana nyumba nzuri ambazo watu wanakuja wanakaa wanaongeza uchumi wa nchi. Na sisi jeshi letu liwe hivyo.”

Lukelo Francis ni mwandishi wa The Chanzo kutoka Dar es Salaam, Tanzania. Anapatikana kupitia lukelo@thechanzo.com.

Chanzo: The Chanzo Initiative
kwani kuna mtu alitaka kuvunja katiba
 
Katiba ya Tanzania ni kifungu gani kinasema Rais lazima awe na degree..

Mbona mbowe hana degree ila anagombea urais ?

Ni wapi Mbowe anagombea urais? Mbowe aliwahi kugombea urais kabla sheria hiyo haijawekwa, kama hujui kitu kaa kimya dogo.
 
Yaani inachekesha na kusikitisha, CDF anasema alikutana na wakati mgumu eti kwa rais kufia madarakani, hivyo akalinda katiba. Ni mara ngapi katiba imevunjwa huku akiangalia? Kimsingi viongozi wa nchi hii wanakaa madarakani kwa kutegemea vyombo vya dola, sasa ni ugumu gani alikutana nao wakati yeye ndio msimamizi wa kiongozi kuingia madarakani?
 
Kwa nini unataka ufafanuzi? Mambo mengine ni siri za nchi na vizuri yabaki kuwa siri za nchi. Wananchi nyie shukuruni nchi ilivuka salama maisha yanaendelea. Siri za nchi, usalama wa nchi waachieni wahusika.

Hamna lolote, ilivuka salama kwenye nini labda? Huo uhuni ndio mnaita siri za nchi?
 
Wewe unatoa.matusi,uliwahi kuona general yupi kwenye nchi.hii kila kukicha anatafuta mahali pa kuongea...?

Hapa kuna tatizo kwa muhusika.
Kuna watu hawajiamini kama ni wazee na wanahitaji kipumzika na wawapishe vijana.

Huko nyuma kuna mzee.alipoambiwa anakalibia kustaf siku hiyo ilibidi avae kikomando.amekimbia kutoka upanga hadi ikulu kumuulia nyerere kua kama.yeye.ni mzee na anatakiwa astaf..nyerere alihofia ujio ule.ilibidi amwambie kua yeye bado kijana achapekazi.

Wenzetu huko kustafu ni furaha anajua napunzika sasa na anawaza nitembelee nchigani kila mwaka kutalii. Sisi waafrika kustafu tunaona kama kudhalilishwa.

Hili ni tatizo.akili zetu sisi waru weusi bado zina ukungu mzito.
Ahahahah tutajie huyo MTU mkuu
 
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ) anayemaliza muda wake, Jenerali Venance Salvatory Mabeyo ametaja kifo cha Rais wa awamu ya tano Hayati Dk. John Magufuli kama moja kati ya changamoto kubwa alizokabiliana nazo katika kipindi cha utumishi wake.

Mabeyo ameeleza hayo katika kipindi cha Dakika 45 kilichorushwa na kituo cha televisheni cha ITV.

Amesema hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Tanzania kumpoteza rais aliyekuwa madarakani hivyo kilikuwa ni kipindi kigumu lakini kama Jeshi walisimama kidete kutimiza wajibu kwa mujibu wa katiba wa kuilinda nchi na katiba.

"Naamini kwamba tunaendelea vizuri, nchi iko salama mpaka sasa. Wananchi wako watulivu, wanaendelea kufuata miongozo kama inavyotolewa na Serikali,” amesema Mabeyo.

Rais Magufuli alifariki dunia Machi 17, 2021, kutokana na matatizo ya moyo jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania, Venance Mabeyo anatarajia kustaafu wadhifa wake mwisho mwa mwezi Juni, 2022

Mabeyo aliteuliwa kushika nafasi hiyo Februari, 2017 na hayati Magufuli.

Source: #MtanzaniaDigital
 
Nchi hua ina jeshi moja tu. hapa bongo ni JWTZ, hizi nyingine hua ni taasisi, Ila bongo utasikia jeshi la polisi, sijui magereza, mara uhamiaji, mara jeshi usu. Yani kazi kuchanganya watu tu. Siasa mbaya Sana.
kama unaamua kujilisha upepo hata hilo moja utakuja kuona halitoshi kuitwa jeshi.

kama kuna sehemu umesoma jeshi la polisi au magereza linalinda mipaka ya nchi na katiba ndipo uchanganyikiwe.
 
Back
Top Bottom