Jenerali Ulimwengu apinga kutumia siku 100 kumtathimini Rais

Jenerali Ulimwengu apinga kutumia siku 100 kumtathimini Rais

Jenerali ulimwengu ambaye ni mwanahabari nguri amepinga vikali hatua ya kumpa bi Samia Suruhu siku 100 za kumjadili.

Amesema kwanza hatupaswi kutumia njia hiyo sababu ni njia ambayo wamarekani ndiyo wanaitumia kwa viongozi wao iweje na sisi tuige wakati hatuya simamii malengo yetu.

Pia ameendelea kusema, hategemei jipya sababu bi Samia alikuwa msaidizi wa rais aliyepita na chama ni kile kile cha muda mrefu, hivyo matamko yoyote hayawezi kuleta jipya.

Jenerali amesema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha redio cha sauti ya Marekani VOA.


View attachment 1838069
PICHANI: Jenerali Ulimwengu, picha haina uhusiano na mada.
Tulikuwa pamoja na Jenerali Ulimwengu jioni ya leo kwenye mahojiano yaliyoongozwa na Mkamiti Kibayasi wa VOA

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo la Gwandumi lilikuwa ni kumsifia jenerali akashindwa kufunguka na kila akitaka kufunguka anapiga break akishtuka kuwa mama Samia ni amiri jeshi so awezi kumwaga madini as jenerali.
Namsifia kwa kuwa Jenerali Ulimwengu ni Mwalimu wangu katika uchambuzi wa hoja zenye mashiko. Haina maana kwamba nilimsahau Rais. Nilimwimbia hata kawimbo! Namheshimu sana Rais SSH pasipo kuacha kumkosoa lakini kwa staha.

Kama ulisikiliza hadi mwisho nilimchambua sana Rais Samia kwa hatua alizopatia na alizokosea, ikiwemo kuweka kando katiba mpya na bora. Mojawapo ya jinsi nilivyomkosoa ni pale nilipolinganisha katiba yetu mbovu na gari bovu.

Huwezi ukasema nitalitengeneza nikimaliza safari kwa kuendesha hivyo hivyo likiwa bovu. Unalitengeneza kwanza ndipo unaendelea na safari, safari ya kiuchumi. La sivyo utakwama tu kwa kutaka kuendesha uchumi kwa katiba mbovu!

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Jenerali ulimwengu ambaye ni mwanahabari nguri amepinga vikali hatua ya kumpa bi Samia Suruhu siku 100 za kumjadili.

Amesema kwanza hatupaswi kutumia njia hiyo sababu ni njia ambayo wamarekani ndiyo wanaitumia kwa viongozi wao iweje na sisi tuige wakati hatuya simamii malengo yetu.

Pia ameendelea kusema, hategemei jipya sababu bi Samia alikuwa msaidizi wa rais aliyepita na chama ni kile kile cha muda mrefu, hivyo matamko yoyote hayawezi kuleta jipya.

Jenerali amesema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha redio cha sauti ya Marekani VOA.


View attachment 1838069
PICHANI: Jenerali Ulimwengu, picha haina uhusiano na mada.
Hata kutokutathminini ni kutathmini. Ukisema alikuwa msaidizi wa aliyepita kwa hiyo hawezi kwa tofauti nako ni kutathmini. Hi ya America ni akili kuyumba kwa sababu zisizo wazi, we ignore that.
 
Basi tumpime Kwa siku 200.

Huyu jenerali keshakuwa koplo.

Sasa kama hutaki kitumia kipimo Cha siku 100 kwakua ni Cha Marekani.

Na wakati huo huo ukililia Demokrasia ambayo imeasisiwa na hao hao marekani, sijui unataka tukueleweje??

Siasa za mahaba au ni kukosa hoja ?
 
Basi tumpime Kwa siku 200.

Huyu jenerali keshakuwa koplo.

Sasa kama hutaki kitumia kipimo Cha siku 100 kwakua ni Cha Marekani.

Na wakati huo huo ukililia Demokrasia ambayo imeasisiwa na hao hao marekani, sijui unataka tukueleweje??

Siasa za mahaba au ni kukosa hoja ?
Hoja ya ulimwengu ni kwamba hatuvisimamii vipaumbele vyetu Kama wenzetu.
 
Hii dunia ina watu sijui mnawaza kwa kutumia nini? Unajua utofauti wa asimia 100 na siku 100 ivyo ni vitu viwili tofauti sana kimaana na kimahesabu mkuu. Mbona kwenye teknolojia tunasema gb 1= mb 1024 kwanini tusiseme 1000 mb ? Usifananishe vitu bila kutumia reasoning na kujenga hoja


Hoja ni hii; kwanini usishangae na kuhoji dunia kutumia 💯% badala ya any other number na Ushangae Watz kutumia siku 💯 na sio siku 20, 40, nk kumtathimini Mama samia ??--- cha ajabu zaidi mnatumia hiyo 💯% kuhalalisha kupinga siku 💯 za Mama madarakani.

Maana yangu ni hii; kupanga ni kuchagua, kama tumepanga na kuamua kutathimini Uongozi wa mama katika kipindi cha siku 100 kitu ambacho nchi zingine nazo hufanya hapo hakuna kosa jinsi wanamahesabu walivyoamua kutumia 💯% na sio 200% nk, jinsi wanamahesabu walivyoamua kutumia 360° kupima nyuzi za duara, kama jinsi watu walivyoamua kufanya siku 40 za marehemu (arobaini ya marehemu) nk, pia kuna usemi usemao za mwizi ni arobaini na sio hamsini nk, sasa cha ajabu nini kuwepo kwa Siku 💯 za MAMA SAMIA na watu wakazitathimini???--- au mlitaka siku hizo zingeanzishwa na Wazungu ndipo muone ni siku bora jinsi Wazungu walivyotuloga kwenye Birth days parties, tunaona birth day parties ni sikukuu ya ibada nk.

Usiwe na akili iliyoganda kama mafuta ya mgando.
 
Jenerali ulimwengu ambaye ni mwanahabari nguri amepinga vikali hatua ya kumpa bi Samia Suruhu siku 100 za kumjadili.

Amesema kwanza hatupaswi kutumia njia hiyo sababu ni njia ambayo wamarekani ndiyo wanaitumia kwa viongozi wao iweje na sisi tuige wakati hatuya simamii malengo yetu.

Pia ameendelea kusema, hategemei jipya sababu bi Samia alikuwa msaidizi wa rais aliyepita na chama ni kile kile cha muda mrefu, hivyo matamko yoyote hayawezi kuleta jipya.

Jenerali amesema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha redio cha sauti ya Marekani VOA.


View attachment 1838069
PICHANI: Jenerali Ulimwengu, picha haina uhusiano na mada.
Jipya litakuwepo kwasababu huyu ni Samia Suluhu
 
Hoja ni hii; kwanini usishangae na kuhoji dunia kutumia [emoji817]% badala ya any other number na Ushangae Watz kutumia siku [emoji817] na sio siku 20, 40, nk kumtathimini Mama samia ??--- cha ajabu zaidi mnatumia hiyo [emoji817]% kuhalalisha kupinga siku [emoji817] za Mama madarakani.

Maana yangu ni hii; kupanga ni kuchagua, kama tumepanga na kuamua kutathimini Uongozi wa mama katika kipindi cha siku 100 kitu ambacho nchi zingine nazo hufanya hapo hakuna kosa jinsi wanamahesabu walivyoamua kutumia [emoji817]% na sio 200% nk, jinsi wanamahesabu walivyoamua kutumia 360° kupima nyuzi za duara, kama jinsi watu walivyoamua kufanya siku 40 za marehemu (arobaini ya marehemu) nk, pia kuna usemi usemao za mwizi ni arobaini na sio hamsini nk, sasa cha ajabu nini kuwepo kwa Siku [emoji817] za MAMA SAMIA na watu wakazitathimini???--- au mlitaka siku hizo zingeanzishwa na Wazungu ndipo muone ni siku bora jinsi Wazungu walivyotuloga kwenye Birth days parties, tunaona birth day parties ni sikukuu ya ibada nk.

Usiwe na akili iliyoganda kama mafuta ya mgando.
Jamaa acha kuandika vitu usivyovijua . Hujui kuwa siku 100 za raisi madarakani ni sera inayotumiwa na wamarekani katika kutathmini utendaji? Hujui kuwa joe Biden alipomaliza siku 100 walifanya evaluation? Hujui pia tume copy kwa wazungu? Unanishangaza sana kusema eti hadi wazungu waanzishe, [emoji23][emoji23] kumbe hujui kuwa tume copy kutoka marekani . Kama sio mfuatiliaji wa vitu ni busara kukaa kimya wala hakuna atakayejua hujui kuliko kuongea ku prove vitu ambayo hujui
 
Jamaa acha kuandika vitu usivyovijua . Hujui kuwa siku 100 za raisi madarakani ni sera inayotumiwa na wamarekani katika kutathmini utendaji? Hujui kuwa joe Biden alipomaliza siku 100 walifanya evaluation? Hujui pia tume copy kwa wazungu? Unanishangaza sana kusema eti hadi wazungu waanzishe, [emoji23][emoji23] kumbe hujui kuwa tume copy kutoka marekani . Kama sio mfuatiliaji wa vitu ni busara kukaa kimya wala hakuna atakayejua hujui kuliko kuongea ku prove vitu ambayo hujui


Wewe unajua kusoma na kutafakari unachosoma au umezoea ku crame???--- hiyo ndiyo shida ya elimu zetu. Hebu soma hiki nilichoandika;

kama tumepanga na kuamua kutathimini Uongozi wa mama katika kipindi cha siku 100 kitu ambacho nchi zingine nazo hufanya
 
Mzee wangu Mungu ampe maisha marefu ,hakuwi niangusha, watu Kama awa bila kujali misimamo yao ilitakiwa rais madarakani kuwaomba kuwa washauri wake, sio kuchukua watu ili mradi wanakupongeza tu kumbe ni wanafiki
Unaweza ukawa bingwa wa kukosoa ila sio bingwa wa kushauri.
 
Jenerali Ulimwengu: Wazalendo wote wanatakiwa kumuunga mkono Rais Samia

Samia alikuwa msaidizi wa rais aliyepita na chama ni kile kile cha muda mrefu, hivyo matamko yoyote hayawezi kuleta jipya.
 
Jenerali ulimwengu ambaye ni mwanahabari nguri amepinga vikali hatua ya kumpa Rais Samia Suluhu siku 100 za kumjadili.

Amesema kwanza hatupaswi kutumia njia hiyo sababu ni njia ambayo wamarekani ndiyo wanaitumia kwa viongozi wao iweje na sisi tuige wakati hatuya simamii malengo yetu.

Pia ameendelea kusema, hategemei jipya sababu bi Samia alikuwa msaidizi wa rais aliyepita na chama ni kile kile cha muda mrefu, hivyo matamko yoyote hayawezi kuleta jipya.

Jenerali amesema hayo alipokuwa akifanya mahojiano na kituo cha redio cha sauti ya Marekani VOA.

View attachment 1838069
PICHANI: Jenerali Ulimwengu, picha haina uhusiano na mada.
Juzi tu ameandika na kumsifu samia akimtaka a 'demagufulify' the country. Mtu huyu mwenye asili ya rwanda ni mnafiki kupindukia. Tangu avuliwe na mkapa uraia wa tanzania aliyokua amejipachika kinyume cha sheria anatoa cheche mbaya mdomoni kuhusu ccm na serikali zake.
 
Back
Top Bottom