Jengo la mahakama ya Wilaya Chato

rr4

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2015
Posts
3,797
Reaction score
5,510
Mhe.Rais mimi najua wewe sio mbunge wa Chato bali ni Rais wa nchi. Maana yangu ni kwamba linapofika suala la maendeleo simamia bila kupendelea.

Ukiangalia jengo hili jipya la Mahakama ya Wilaya ya Chato hivi ni wilaya gani nyingine yenye jengo la mahakama ya kisasa kama hili? Kama ni kwa nia njema ningetamani kuona majengo ya namna hii ya kisasa kwenye mahakama zote za wilaya nchi nzima lakini jengo hili nimeliona Chato tu anakotoka Rais.

Mdude Nyagali
#Sumu_ya_nyigu
#freedom_fighter

 
Hizi nguvu mnazotumia kwenye mambo madogo kama haya munge elekeza kwenye mambo muhimu makubwa.
Hilo jengo la kawaida sana tatizo ni hizo ngazi au au urembo wa nguzo za kwenye baraza?

Wilaya nyingine ni za zamani sana, mahakama zake zilijengwa zamani hivyo huwezi kufananisha na wilaya mpya inayojengwa majengo au miundombinu ya kisasa.
Akili ya kawaida tu inatosha kutuambua hii sababu ya utofauti wa miundombinu mipya.

Mnataka mwaka 2015/2019 lijengwe jengo kama la mwaka 1961/1986?
Hata huku mitaani maeneo ya miji au makazi mapya huwa na majengo mazuri ya ramani na urembo wa kisasa.

Hii ndio shida ya kuwa na watu wako wa propaganda na kampeni wenye elimu ndogo kama akina mdude.
Sijawahi kuona ukosoaji wa kitoto namna hii enzi za ujana wa akina Mnyika, Halima Mdee, Zitto Kabwe n.k.
Na hao wote utaona elimu yao ni tofauti na akina Mdude. Kibaya zaidi hata wenye elimu ya juu wanaingia mkenge kuuunga juhudi za ukosoaji wa mambo madogo sana na kuacha makubwa ya msingi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…