Jengo la mahakama ya Wilaya Chato

Jengo la mahakama ya Wilaya Chato

Mahakama ipo katika mpango wa kuboresha mahakama zake za wilaya.....
kaangalie mahakama ya Wilaya Kibaha nenda Mahakama mpya ya Ilala.....
na sehemu kadhaa tu....
Ooh .....

Kumbe Ni nchi nzima????

Safi
 
Chato itajengwa na wana Chato wenyewe acheni tuijenge Chato yetu na nyinyi simamieni miradi inayoelekezwa kwenye maeneo yenu ifanyike kikamilifu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kali balaa ila mahakama hata iwe nzuri kiasi gani haivutii ni kama jeneza tu hata liwe zuri namna gan huwez kulitamani
Kata ninayoishi kuna kituo kidogo cha polisi, ni kizuri sana hadi mahabusu kuna tiles, mahabusu wa vituo vingine huwa wanaombwa wapelekwe kule bahati mbaya sana mahabusu ni ndogo haiwezi kuaccommodate watu wengi
 
Mhe.Rais mimi najua wewe sio mbunge wa Chato bali ni Rais wa nchi. Maana yangu ni kwamba linapofika suala la maendeleo simamia bila kupendelea.

Ukiangalia jengo hili jipya la Mahakama ya Wilaya ya Chato hivi ni wilaya gani nyingine yenye jengo la mahakama ya kisasa kama hili? Kama ni kwa nia njema ningetamani kuona majengo ya namna hii ya kisasa kwenye mahakama zote za wilaya nchi nzima lakini jengo hili nimeliona Chato tu anakotoka Rais.

Mdude Nyagali
#Sumu_ya_nyigu
#freedom_fighter

View attachment 1294907View attachment 1294907View attachment 1294907

Hata uwe mzalendo vipi.....hakuna anayeweza kwenda kutafuta pesa na akapata afu akanunua Tv kwa jirani kabla ya kununua ya kwake.
 
Hata uwe mzalendo vipi.....hakuna anayeweza kwenda kutafuta pesa na akapata afu akanunua Tv kwa jirani kabla ya kununua ya kwake.

Nyerere?????

Kwanini alifeli kuijenga Butiama
 
Titi linawasha
Hizi nguvu mnazotumia kwenye mambo madogo kama haya munge elekeza kwenye mambo muhimu makubwa.
Hilo jengo la kawaida sana tatizo ni hizo ngazi au au urembo wa nguzo za kwenye baraza?

Wilaya nyingine ni za zamani sana, mahakama zake zilijengwa zamani hivyo huwezi kufananisha na wilaya mpya inayojengwa majengo au miundombinu ya kisasa.
Akili ya kawaida tu inatosha kutambua hii sababu ya utofauti wa miundombinu mipya.

Mnataka mwaka 2015/2019 lijengwe jengo kama la mwaka 1961/1986?
Hata huku mitaani maeneo ya miji au makazi mapya huwa na majengo mazuri ya ramani na urembo wa kisasa.

Hii ndio shida ya kuwa na watu wako wa propaganda na kampeni wenye elimu ndogo kama akina mdude.
Sijawahi kuona ukosoaji wa kitoto namna hii enzi za ujana wa akina Mnyika, Halima Mdee, Zitto Kabwe n.k.
Na hao wote utaona elimu yao ni tofauti na akina Mdude. Kibaya zaidi hata wenye elimu ya juu wanaingia mkenge kuuunga juhudi za ukosoaji wa mambo madogo sana na kuacha makubwa ya msingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyerere?????

Kwanini alifeli kuijenga Butiama

Nyerere alikuwa mshamba mshamba.

Wewe ukiwa Raisi kwa sasa.... ni mfano lakini😁 ina maana huwezi kijenga nyumba y kisasa zaidi eti kisa Nyerere jana mjengo wa maana kule Kwao?
 
Back
Top Bottom