Sasa unalindaje kitu kisichojengwa mkuu. Hata nyumba inabidi kwanza uijenge alaf ndo uilinde.Mi nalinda taifa na siyo kujenga
Hata mimi najiuliza hivyo, by the way kuna wajuzi wa mambo zaidi yetu tunaoona kwa macho ya nyama.Niaje waungwana
Japo hakuna mtu mwenye dhamana ya kumpangia raisi kile anachoamua, lakini katika hili la kumtoa Silaa ardhi na kwenda kumtupa huko kwenye habari kwa kweli Rais wetu amefanya kosa la kiufundi sana.
Jerry alikuwa ashaanza kuwashughulikia vibaka na matapeli wa ardhi wote, yaani mmoja baada ya mwingine hadi kupelekea wengine kutupwa ndani. Sasa leo anapotolewa na kupelekwa wizara nyingine ni kuwapa nafasi wale wote waliokuwa washaanza kurudisha ardhi walizotapeli kabla kiama hakijawashukia waendelee nazo na pengine kuendelea kutapeli na zingine kwani aliekuwa anawapa tumbo joto kaondolewa na kupelekwa kungine.
Najiuliza, kwanini hiyo wizara ya habari asingepewa hata Mwana FA, ili Silaa aendelee kuwanyoosha wezi na vibaka wa ardhi za watu!
Anyway acha tuone mwisho wa game utakuaje. Lakini mama kama unatusikia na kufanikiwa kusoma uzi huu tafadhali TUNAOMBA (kwa herufi kubwa) UMRUDISHE JERRY SILAA W/ ARDHI 🙏🙏
Duu inawezekana matapeli wa ardhi wako hadi .......................Ukiona hivyo mkono mrefu wa matapeli umemfikia raisi
Mfumo ukiwekwa vizuri ndio itakuwa mwarobaini wa hizi changamoto zinazojitokeza mara kwa maraNdivyo utendaji wa serikalini mwetu ulivyo. Utendaji unategemea mtu kwa sababu mfumo uko corrupted.
Unajua kwa nini alikuwa anatumia muda mwingi mikocheni, mbweni, kariakoo, Mwanza,Morogoro, Dodoma,Arusha? Huko alikuwa analazimisha Makamishna wa Ardhi wampe viwanja vya bure, na akienda maeneo potential kama Mikocheni na kwingine, apewe cha juu kwa kumtisha tajiriUshahidi wa kupokea mlungula uko wapi mkuu? Au na ww umekuwa miongoni mwa watu wanaookota maneno mitaani na kuleta humu bila ushahidi na facts za kueleweka?
Yani kwa uzoefu wako hapa jukwaani nilitegemea ungekuja na ushahidi wa hiki ulichoandika ili sisi wote tumuhukumu. Kumbe ni porojo za kisiasa tu ambazo zinaonekana hazina ukweli wowote.
Sababu iko wazi, ameenda tofauti na falsafa ya chama chake, washazoea dhulma halafu jerry hataki dhulmaSijui kwanini wamemtoa 🐼
Je, yeye ndio mwenye uwezo wa kushughulika kiuwajibika na hakuna mtu mwingine?Yule mzee aliyekuwa anajieleza kisha akamkatisha na kuita polisi wamkamate ni mwanajeshi?kwa hiyo unataka kusema yule mzee ndio ameenda kushitaki juu kwenye mfumo?
But anyway serikali yetu inafeli sana kuhamishahamisha watendaji hovyo yaani hawako strategic hata kidogo mtu ambaye alikuwa anafuatilia kwa ukaribu chanzo cha migogoro ya ardhi akawa anawashughulikia matapeli wanamtoa wanampeleka wizara nyingine ina maana kwenye Watanzania zaidi ya milioni 60 hakuna mtu wa kumuweka kwenye wizara ya habari na akafiti?
Ndio maana miaka yote tunarudi palepale.
Sasa hivi matapeli wa ardhi na nyumba wataanza kufanya sherehe
Kashindwa kutanzua dhuluma iliyotokea kwa wananchi wa Mbopo kudhulumiwa ardhi na DDC na KMC watu waliwekeza wakanyang'nywa mbele ya mtutu wa bunduki yeye kimya.Sababu iko wazi, ameenda tofauti na falsafa ya chama chake, washazoea dhulma halafu jerry hataki dhulma
Labda wanatakiwa viongozi wanaoshinda wanalala ofisini, alafu mwisho mwezi analipwa mamilioni yanayotokana na kodi zetu.Tanzania hii.. Mtu anayepinga ufisadi , ndio huzushiwa ajali kila aina ya kisiasa , hata ya kimwili... Ilikuwa hamna sababu yenye mashiko kumuondoa Jerry .... Yaani sijui wanatakiwa viongozi wa aina gani?
Bado umerudi kule kule kwenye porojo zako ambazo hazina ushahidi.Unajua kwa nini alikuwa anatumia muda mwingi mikocheni, mbweni, kariakoo, Mwanza,Morogoro, Dodoma,Arusha? Huko alikuwa analazimisha Makamishna wa Ardhi wampe viwanja vya bure, na akienda maeneo potential kama Mikocheni na kwingine, apewe cha juu kwa kumtisha tajiri
Sehemu kama Kintinku, Gairo, au Manyoni na Mpanda humuoni
Ni kweli mkuu.ila bibi anazingua, yaani kumtoa kijana namimi imeniuma sana. Kijana alikuwa na nia ya kuwasaidia wananchi kwa moyo wake wote nikimtazama. Sasa anakuja kutuwekea watoto wa viongozi ambao wamepewa nafasi hizo kwa heshima za wazazi wao na si kwa kuwa na sifa.....yaani nikisikia ukoo tu mfano; makamba, pinda, nnauye, mavunde, ndejembi, kikwete, nani sijui...yaani hawa wote ni vilaza hamna kitu.....ni majina ya baba zao ndio yapo ...upendeleo wa watawala na kulipana fadhila. Lakini ukisikia ukoo unaitwa makonda, slaa, chalamila, mtaka, mpina, majaliwa, mwamri, unajua wazi kuwa ni watu wa kazi kazi
Wanaweza wakawepo wengine wa kuiendesha wizara ya ardhi lakini kwa nini tupoteze muda wa kumtafuta mwingine wakati tayari alishapatikana anayeiwezea hiyo,it doesnt make any sense.Je, yeye ndio mwenye uwezo wa kushughulika kiuwajibika na hakuna mtu mwingine?
Au wangempa Ask Gwajima?
Huyo Ndejembi hatumfahamu lakini nafikiri anatokea Dodoma huyu mwenye nasaba na Malecela
Mkuu inawezekana hii Dunia hakuna kitu watu wanashindwa isipokuwa kufufua aliyekufa tu.Inawezekana wapo au hawapo, lakini wakatumia rupia kuwafanya washauri wa mama wamshawishi mama amtoe Silaa kule awekwe mtu wao.