Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Vifungu vya 7 na 15 vya Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 imempa mamlaka Mkuu wa mkoa kuweka Mtu mahabusu Kwa masaa 48 (kif.7). Mkuu wa wilaya sheria imemruhusu kumweka Mtu ndani Kwa masaa 24 (kif.15) pale inapothibitika Mtu Huyo anàhatarisha Amani ya mbele yake.
Nimejaribu kuisoma sheria hiyo yote lakini sijaona kifungu kinachompa Waziri yeyote mamlaka ya kumweka Mtu mahabusu. Lakini ni kawaida nchini na jana tu Waziri wa Ardhi Jerry Slaa akiwa Kihonda Morogoro aliamuru mwananchi akamatwe na OCD na kuwekwa ndani Kwa kutoa maelezo Kwa kirefu wakati Waziri alimtaka atoe Kwa kifupi.
Kabla ya kutoa amri hiyo alimkatisha Msemaji na kumwambia hataki hotuba anataka majibu kitu ambacho mzungumzaji alishindwa na kuendelea kutoa maelezo na hivyo kumuudhi MHESHIMIWA WAZIRI na kuamuru akamatwe na OCD mara moja.
Swali langu Nataka kujua kama kuna sheria nyingine tofauti na nikiyoitaja inayompa Waziri mamlaka ya kuweka watu mahabusu kadri wanavyojisikia.
Nimejaribu kuisoma sheria hiyo yote lakini sijaona kifungu kinachompa Waziri yeyote mamlaka ya kumweka Mtu mahabusu. Lakini ni kawaida nchini na jana tu Waziri wa Ardhi Jerry Slaa akiwa Kihonda Morogoro aliamuru mwananchi akamatwe na OCD na kuwekwa ndani Kwa kutoa maelezo Kwa kirefu wakati Waziri alimtaka atoe Kwa kifupi.
Kabla ya kutoa amri hiyo alimkatisha Msemaji na kumwambia hataki hotuba anataka majibu kitu ambacho mzungumzaji alishindwa na kuendelea kutoa maelezo na hivyo kumuudhi MHESHIMIWA WAZIRI na kuamuru akamatwe na OCD mara moja.
Swali langu Nataka kujua kama kuna sheria nyingine tofauti na nikiyoitaja inayompa Waziri mamlaka ya kuweka watu mahabusu kadri wanavyojisikia.