Jerry Silaa na matumizi mabaya ya Madaraka: Waziri kapata wapi mamlaka kuwaweka mahabusu watanzania?

Jerry Silaa na matumizi mabaya ya Madaraka: Waziri kapata wapi mamlaka kuwaweka mahabusu watanzania?

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Vifungu vya 7 na 15 vya Sheria ya Tawala za Mikoa ya mwaka 1997 imempa mamlaka Mkuu wa mkoa kuweka Mtu mahabusu Kwa masaa 48 (kif.7). Mkuu wa wilaya sheria imemruhusu kumweka Mtu ndani Kwa masaa 24 (kif.15) pale inapothibitika Mtu Huyo anàhatarisha Amani ya mbele yake.

Nimejaribu kuisoma sheria hiyo yote lakini sijaona kifungu kinachompa Waziri yeyote mamlaka ya kumweka Mtu mahabusu. Lakini ni kawaida nchini na jana tu Waziri wa Ardhi Jerry Slaa akiwa Kihonda Morogoro aliamuru mwananchi akamatwe na OCD na kuwekwa ndani Kwa kutoa maelezo Kwa kirefu wakati Waziri alimtaka atoe Kwa kifupi.

Kabla ya kutoa amri hiyo alimkatisha Msemaji na kumwambia hataki hotuba anataka majibu kitu ambacho mzungumzaji alishindwa na kuendelea kutoa maelezo na hivyo kumuudhi MHESHIMIWA WAZIRI na kuamuru akamatwe na OCD mara moja.

Swali langu Nataka kujua kama kuna sheria nyingine tofauti na nikiyoitaja inayompa Waziri mamlaka ya kuweka watu mahabusu kadri wanavyojisikia.


 
Katika hili tukio ambapo waziri wa ardhi Jerry Silaa anaamuru OCD kumkamata mzungumzaji kosa la anayezungumza ni nini?View attachment 3042185
Jerry Silaa amelewa sifa. Uongozi wa vitisho hauna nafasi kwenye kizazi hiki. Sijaona kosa la wananchi wote hao wawili.

Nahisi Waziri Silaa amekuja na majibu yake (preconceived ideas), kumbe kunako ground mambo ni vice versa. Hawezi kuukabili ukweli na ndiyo maana anaamua kuwatoa wenye ukweli kwenye mkutano. This is bullshit
 
Back
Top Bottom