ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Jeshi la Polisi limetoa ushahidi wa awali kuhusu kupitea Kwa bwana harasi mara baada ya kumaliza harusi.
Polisi wanadai ushahidi wa awali unaonesha bwana Masawe aliyepotea Aliuza gari aliyokodi Ili Kulipa Madeni na kwamba Polisi wanaendelea kukusanya taarifa Ili Kubaini kama bwana Masawe alijipoteza au ikoje.
Polisi wanadai taarifa zaidi zitatolewa.👇👇
View: https://x.com/millardayo/status/1868976028665663785?t=h7Pm-jybGVTfa2j6gCB6ig&s=19
Ni utata, ndivyo unavyoweza kueleza kuhusu taarifa za kupotea bwana harusi, Peter Masawe ambaye Jeshi la Polisi linaeleza uchunguzi wa awali umebaini alikuwa na madeni na ameuza mali za watu.
Mbali ya taarifa ya Polisi, baadhi ya marafiki wa Masawe anayejulikana zaidi kwa jina la Vincent, wanaeleza wakionyesha wasiwasi kutokana na mzunguko waliotumia walipomtafuta tangu alipopotea.
Victor Mawalla, akizungumza na Mwananchi leo Desemba 15, 2024 amesema alipigiwa simu na Vincent ambaye ni rafiki yake akamweleza alikuwa Mbezi na kuna magari mawili yanamfuatilia, moja alilitaja ni Toyota Land Cruiser (Hardtop).
Amesema alimpatia ushauri aingie kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa.
"Nilivyomwambia hivyo alikubali akinitajia namba za gari lililokuwa likimfuatilia lakini baada ya kufuatilia ikabainika gari alilolitaja limepaki eneo la Ilala," amesema Mawalla.
Amesema baada ya kufuatilia Jeshi la Polisi lilikamata gari na mmiliki ambaye alifika Dar es Salaam akitokea Kahama mkoani Shinyanga kwa ajili ya manunuzi ya vifaa vya magari ambaye alikuwa hafahamu chochote kuhusu kinachoendelea.
Kutokana na taarifa iliyokuwa imetolewa kwenye mitandao juu ya kupotea kwa bwana harusi Jeshi la polisi limetolea taarifa
na taarifa inathibitisha kuwa bwana harusi huyo aliuza gari alilokodi kwa ajili ya harusi huku akimtumia mkewe pesa nyingine apunguze madeni .
My Take
Polisi tunaomba Haki itendeke Kwa matukio yote Ili kuondoa hofu na mashaka kwenye jamii.
Mambo ya kutekana hayafai.
Updates
Kumbe Jamaa alijiteka Ili kukimbia madeni ,akutwa amejificha Pemba 😂😂👇👇
View: https://www.instagram.com/p/DDra5I2sPGp/?igsh=NjhwcndpZ3F0OGJ0
Polisi wanadai ushahidi wa awali unaonesha bwana Masawe aliyepotea Aliuza gari aliyokodi Ili Kulipa Madeni na kwamba Polisi wanaendelea kukusanya taarifa Ili Kubaini kama bwana Masawe alijipoteza au ikoje.
Polisi wanadai taarifa zaidi zitatolewa.👇👇
View: https://x.com/millardayo/status/1868976028665663785?t=h7Pm-jybGVTfa2j6gCB6ig&s=19
Ni utata, ndivyo unavyoweza kueleza kuhusu taarifa za kupotea bwana harusi, Peter Masawe ambaye Jeshi la Polisi linaeleza uchunguzi wa awali umebaini alikuwa na madeni na ameuza mali za watu.
Mbali ya taarifa ya Polisi, baadhi ya marafiki wa Masawe anayejulikana zaidi kwa jina la Vincent, wanaeleza wakionyesha wasiwasi kutokana na mzunguko waliotumia walipomtafuta tangu alipopotea.
Victor Mawalla, akizungumza na Mwananchi leo Desemba 15, 2024 amesema alipigiwa simu na Vincent ambaye ni rafiki yake akamweleza alikuwa Mbezi na kuna magari mawili yanamfuatilia, moja alilitaja ni Toyota Land Cruiser (Hardtop).
Amesema alimpatia ushauri aingie kituo cha polisi kwa ajili ya kutoa taarifa.
"Nilivyomwambia hivyo alikubali akinitajia namba za gari lililokuwa likimfuatilia lakini baada ya kufuatilia ikabainika gari alilolitaja limepaki eneo la Ilala," amesema Mawalla.
Amesema baada ya kufuatilia Jeshi la Polisi lilikamata gari na mmiliki ambaye alifika Dar es Salaam akitokea Kahama mkoani Shinyanga kwa ajili ya manunuzi ya vifaa vya magari ambaye alikuwa hafahamu chochote kuhusu kinachoendelea.
Kutokana na taarifa iliyokuwa imetolewa kwenye mitandao juu ya kupotea kwa bwana harusi Jeshi la polisi limetolea taarifa
na taarifa inathibitisha kuwa bwana harusi huyo aliuza gari alilokodi kwa ajili ya harusi huku akimtumia mkewe pesa nyingine apunguze madeni .
My Take
Polisi tunaomba Haki itendeke Kwa matukio yote Ili kuondoa hofu na mashaka kwenye jamii.
Mambo ya kutekana hayafai.
Updates
Kumbe Jamaa alijiteka Ili kukimbia madeni ,akutwa amejificha Pemba 😂😂👇👇
View: https://www.instagram.com/p/DDra5I2sPGp/?igsh=NjhwcndpZ3F0OGJ0