Jeshi la polisi chini ya Sirro limeshindwa kuwaweka hadharani wauaji wa muuza chipsi Yusufu Deus, IGP UJAYE TENDA HAKI.

Jeshi la polisi chini ya Sirro limeshindwa kuwaweka hadharani wauaji wa muuza chipsi Yusufu Deus, IGP UJAYE TENDA HAKI.

AbaMukulu

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2018
Posts
2,053
Reaction score
3,586
Naamini IGP Sirro anakaribia kustaafu utumishi wake kwenye jeshi la polisi uliodumu kwa zaidi ya miaka 30. Japo amefanya mengi lakini yapo ambayo bado ananyyoshewa kidole kwayo. Japo ni mengi lakini naomba niwasilishe swala hili moja tuu kwa leo. JESHI LA POLISI CHINI YA SIRRO limeshindwa kuwaweka hadharani wauaji wa kijana Yusufu Deus. Kama ambavyo iliripotiwa kabla ya kifo chake kwamba kijana huyu alitekwa kwanza na watu ambao jeshi la polisi linasema hawajafahamika. Baadae alikuja kuachiwa na watekaji hao rejea mahubiri ya mchungaji eliona kimaro.


Video ya mchungaji eliona Kimaro akielezea tukio hilo



Baada ya kurejeshwa alikuja tena kupatikana akiwa ametegeshwa kama mtu aliejinyonga katika eneo lake la biashara. Kwa mazingira yale ya sehemu alipojinyongea inaonyesha dhahiri aliuliwa sehemu nyingine na mwili wake kuletwa pale. Wauaji wakaufunga kamba shingoni lakini miguu ikiwa inagusa chini kabisa.

Kwa nini ninalilaumu jeshi la polisi chini ya Sirro kwa kushindwa kuwaweka hadharani wauaji wa kijana Deus Yusufu?

Tukirejea wakati marehemu Deus yusuf ametekwa, watekaji waliacha alama za kimawasiliano kati yao na ndugu wa marehemu. Watekaji hao walikuwa wanawasiliana na ndugu wa marehemu kuhusu kupewa kiasi cha hela. Ndugu wa marehemu alionyesha mawasiliano hayo kwa polisi wa kitengo cha cyber pale Mabatini. Askari huyo anaitwa John. Askari huyu na wengine hawakuonyesha ushirikiano licha ya ndugu wa marehemu kuwaonyesha sms ambazo alikuwa anachati na watekaji hao. Askari Polisi walimwambia ndugu wa marehemu aende mwenyewe kwenye eneo walilokubaliana na watekaji halafu kitakachotokea awataarifu askari. Hili haliingii akili kabisa kwa walinda amani hawa kuonyesha kutozingatia maadili ya kazi yao.


Unaweza ukasamehe yote hayo baada ya ndugu yako kupatikana. Lakini siku chache baada ya kuachiwa unakutwa mwili wake ukining'inia eneo lake la kazi. Mazingira yote yakionyesha marehemu hakujinyonga mwenyewe. Mauaji yake yalifanyika eneo lingine na ili kupoteza ushahidi mwili ukaletwa pale tuu ili ionekane amejinyonga.

Kama jeshi lilifanya uzembe wakati wa kutekwa kwake basi hapa lisingetakiwa kurudia uzembe wa awali. Hakuna mtekaji wala muuaji hata mmoja aliekamatwa zaidi ya mama ambae walikuwa wanatumia wote sehemu ya biashara. Watekaji licha ya kutumia namba za simu zilizosajiliwa kwa alama za vidole lakini jeshi la polisi limeshindwa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani wauaji.

Miongoni mwa namba iliyotumika na watekaji hao ni 0629004596. Namba hii ilikuwa imesajiliwa kwa jina la ISACKY RAYMOND KILEO. Lakini sasa hivi usajili umebadilishwa kwenda kwa jina la REMIGIUS REMIGIUS HYERA. Jeshi la polisi liapaswa liuambie umma wa Watanzania huyu ISACKY RAYMOND KILEO ameshiriki vipi kwenye tukio hili. Ni uzembe wa hali ya juu na upuuziwaji mkubwa wa maisha ya mtanzania.

Ni vyema IGP ajaye aiitishe uchunguzi mpya kwenye swala hili. Kwanza la mauaji ya kijana huyu na pili uzembe wa watendaji wa jeshi la polisi kwenye kuokoa maisha ya kijana huyu.
Ninaamini kama jeshi la polisi lingeonyesha ushirikiano kwa ndugu basi watekaji hawa wangepatikana na INGEWEZEKANA KUNUSURU MAISHA YA KIJANA YUSUF DEUS.
 
F,*ck police f*ck siro.
Ujue hii Tanzania Kuna vitu vinatokea mwananchi wa kawaida kabisa anasema uchunguzi ungeanzia hapa na pale na unaona ni kweli lakini unashangaa taasisi Kama Mambo ya ndani jeshi la police wanasema Uchunguzi mpaka apatikane ndugu wa marehemu wakujitolea.
 
Namba tajwa hapo juu ilionyesha usajili huu wa ISACKY RAYMOND KILEO kipindi cha tukio hilo DESEMBA 2020. had March 2021 bado usajili ulikuwa unaonyesha jina hilo

Screenshot_2021-01-01-08-16-18.png
 
F,*ck police f*ck siro.
Ujue hii Tanzania Kuna vitu vinatokea mwananchi wa kawaida kabisa anasema uchunguzi ungeanzia hapa na pale na unaona ni kweli lakini unashangaa taasisi Kama Mambo ya ndani jeshi la police wanasema Uchunguzi mpaka apatikane ndugu wa marehemu wakujitolea.
Utendaji huo wa hovyo unatakiwa ubadilike. Ni ajabu kabisa polisi hawawezi kufuata lead za wahalifu wakati ziko wazi kabisa
 
Kwa rekodi ya failures nyingi kwenye vifo vyenye utata ambavyo mpaka leo havina majibu ..kama ni nchi nyingine the entire top leaders walitakiwa wawe wameshajiuzulu kitambo sana
Unasema kweli kabisa ndugu. Majeshi ya polisi ya wenzetu wamewekeza sana kutatua vifo vyenye utata. Labda sababu sisi tunaajiri failures wa form 4.
 
Kwa rekodi ya failures nyingi kwenye vifo vyenye utata ambavyo mpaka leo havina majibu ..kama ni nchi nyingine the entire top leaders walitakiwa wawe wameshajiuzulu kitambo sana
Kila nchi kuna changamoto kama hizo na hakuna aliyejiuzulu kwakua kujiuzulu siyo suluhisho bali ni kuendelea na uchunguzi.
Siamini kama TPF wamefanya uchunguzi mpaka mwisho bali bado unaendelea.
 
Kila nchi kuna changamoto kama hizo na hakuna aliyejiuzulu kwakua kujiuzulu siyo suluhisho bali ni kuendelea na uchunguzi.
Siamini kama TPF wamefanya uchunguzi mpaka mwisho bali bado unaendelea.
Sense of responsibility! Huwezi kuzuia makosa yasifanyike lakini unaweza kuchukua hatua yakifanyika.. Utachukua hatua gani! ? Hilo ndio la nuhimu
 
Kana sikosei mchungaji Kimaro alikuja kuomba radhi kwamba alichokuwa amekisema sio sahihi, kwamba marehemu alikuwa amemdanganya vitu vingi na uhalisia hauko hivo
But end of the story kuna binadamu mwenzetu uhai wake umekatishwa hapa, common mkuu muda mwingine think out of box...mada inaelekeza udhaifu wa jeshi la police, na hawa jamaa wapo very selective kwenye utendaji wao,kama ur not political connected your nothing
 
Naamini IGP Sirro anakaribia kustaafu utumishi wake kwenye jeshi la polisi uliodumu kwa zaidi ya miaka 30. Japo amefanya mengi lakini yapo ambayo bado ananyyoshewa kidole kwayo. Japo ni mengi lakini naomba niwasilishe swala hili moja tuu kwa leo. JESHI LA POLISI CHINI YA SIRRO limeshindwa kuwaweka hadharani wauaji wa kijana Yusufu Deus. Kama ambavyo iliripotiwa kabla ya kifo chake kwamba kijana huyu alitekwa kwanza na watu ambao jeshi la polisi linasema hawajafahamika. Baadae alikuja kuachiwa na watekaji hao rejea mahubiri ya mchungaji eliona kimaro.


Video ya mchungaji eliona Kimaro akielezea tukio hilo



Baada ya kurejeshwa alikuja tena kupatikana akiwa ametegeshwa kama mtu aliejinyonga katika eneo lake la biashara. Kwa mazingira yale ya sehemu alipojinyongea inaonyesha dhahiri aliuliwa sehemu nyingine na mwili wake kuletwa pale. Wauaji wakaufunga kamba shingoni lakini miguu ikiwa inagusa chini kabisa.

Kwa nini ninalilaumu jeshi la polisi chini ya Sirro kwa kushindwa kuwaweka hadharani wauaji wa kijana Deus Yusufu?

Tukirejea wakati marehemu Deus yusuf ametekwa, watekaji waliacha alama za kimawasiliano kati yao na ndugu wa marehemu. Watekaji hao walikuwa wanawasiliana na ndugu wa marehemu kuhusu kupewa kiasi cha hela. Ndugu wa marehemu alionyesha mawasiliano hayo kwa polisi wa kitengo cha cyber pale Mabatini. Askari huyo anaitwa John. Askari huyu na wengine hawakuonyesha ushirikiano licha ya ndugu wa marehemu kuwaonyesha sms ambazo alikuwa anachati na watekaji hao. Askari Polisi walimwambia ndugu wa marehemu aende mwenyewe kwenye eneo walilokubaliana na watekaji halafu kitakachotokea awataarifu askari. Hili haliingii akili kabisa kwa walinda amani hawa kuonyesha kutozingatia maadili ya kazi yao.


Unaweza ukasamehe yote hayo baada ya ndugu yako kupatikana. Lakini siku chache baada ya kuachiwa unakutwa mwili wake ukining'inia eneo lake la kazi. Mazingira yote yakionyesha marehemu hakujinyonga mwenyewe. Mauaji yake yalifanyika eneo lingine na ili kupoteza ushahidi mwili ukaletwa pale tuu ili ionekane amejinyonga.

Kama jeshi lilifanya uzembe wakati wa kutekwa kwake basi hapa lisingetakiwa kurudia uzembe wa awali. Hakuna mtekaji wala muuaji hata mmoja aliekamatwa zaidi ya mama ambae walikuwa wanatumia wote sehemu ya biashara. Watekaji licha ya kutumia namba za simu zilizosajiliwa kwa alama za vidole lakini jeshi la polisi limeshindwa kuwakamata na kuwafikisha mahakamani wauaji.

Miongoni mwa namba iliyotumika na watekaji hao ni 0629004596. Namba hii ilikuwa imesajiliwa kwa jina la ISACKY RAYMOND KILEO. Lakini sasa hivi usajili umebadilishwa kwenda kwa jina la REMIGIUS REMIGIUS HYERA. Jeshi la polisi liapaswa liuambie umma wa Watanzania huyu ISACKY RAYMOND KILEO ameshiriki vipi kwenye tukio hili. Ni uzembe wa hali ya juu na upuuziwaji mkubwa wa maisha ya mtanzania.

Ni vyema IGP ajaye aiitishe uchunguzi mpya kwenye swala hili. Kwanza la mauaji ya kijana huyu na pili uzembe wa watendaji wa jeshi la polisi kwenye kuokoa maisha ya kijana huyu.
Ninaamini kama jeshi la polisi lingeonyesha ushirikiano kwa ndugu basi watekaji hawa wangepatikana na INGEWEZEKANA KUNUSURU MAISHA YA KIJANA YUSUF DEUS.

Siro akistahafu inabidi atafute kimtaamtaa
 
Katika watu hopeless nchi hii kwa rushwa ni polisi. Hawa watu huwa hawajali kabisa weledi katika kazi zao. Wanataka hela tu
 
Kila nchi kuna changamoto kama hizo na hakuna aliyejiuzulu kwakua kujiuzulu siyo suluhisho bali ni kuendelea na uchunguzi.
Siamini kama TPF wamefanya uchunguzi mpaka mwisho bali bado unaendelea.
Soma uzi vizuri ndugu.
Jeshi la polisi lilifanya uzembe wakati marehemu ametekwa, hiyo mosi.
Pili wamekuja kufanya uzembe kutafuta wauaji wake wakati nyayo zao zimeachwa kwenye tukio hili.
 
Kana sikosei mchungaji Kimaro alikuja kuomba radhi kwamba alichokuwa amekisema sio sahihi, kwamba marehemu alikuwa amemdanganya vitu vingi na uhalisia hauko hivo
Alisema uhalisia uko vipi?
Je hili ndio lanawafanya jeshi la polisi lisiwatafute wauaji wake?
 
Watanzania na sisi sijui nani katuloga yani tunakaa kimyaa mpaka yatupate. Maana leo kwa yusuph kesho hatujui kwa nani.

Polisi yenyewe ndo hao wanaua raia na kupora hela.
 
Back
Top Bottom