Jeshi la Polisi lapewa siku 90 kuhakikisha mitambo ya LUGUMI inafanya kazi vituo vyote

Jeshi la Polisi lapewa siku 90 kuhakikisha mitambo ya LUGUMI inafanya kazi vituo vyote

Ni baada ya Kamati ya Bunge iliyopewa kazi ya kufuatilia Sakata la Lugumi kuthibitisha kuwa vifaa mashine hizo zimefungwa katika vituo vyote.

Agizo hilo limetolewa na Bunge kupitia kwa Naibu Spika, Dr. Tulia Ackson wakati akiahirisha Bunge la 11 leo mjini Dodoma
==========



Habari wakuu,

Leo akihitimisha bunge, naibu spika ametolea ufafanuzi utekelezaji wa mfumo wa kielektroniki wa utambuzi wa alama za vidole(AFIS), hoja iliyojengwa kutokana na mkaguzi wa hesabu za serikali(CAG) kwa kutokamilika kwa mradi huo.

Agizo la bunge lilimtaka afisa masuhuli wa jeshi la polisi kuhakikisha mfumo wa AFIS unafanya kazi ndani ya kipindi cha miezi sita. Ripoti ilieleza mfumo wa AFIS ulikuwa unafanya kazi katika vituo 14 pekee kati ya vituo 108 hivyo agizo la kamati halikuwa limetekelezwa kikamilifu.

Spika ametoa agizo kwa serikali kuhakikisha mfumo huo unafanya kazi ndani ya miezi mitatu ili kuboresha uwezo wa jeshi la polisi kuwa na utambuzi wa haraka wa wahusika wa matukio ya kihalifu katika vituo vyote nchini. Pili masuala yote yaliyobainika kuwa na dosari za kiutendaji yapatiwe ufumbuzi haraka.

Spika anatarajia sasa suala hilo litafikia mwisho na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali atafunga hoja yake baada ya kujiridhisha na utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa.

Kumbe jpm hapambani na ufisadi bali mahasim wake ccm ni ile ile
 
Ñchi hii hata wezi wa fedha nyingi hadi billioni 37 wanapewa muda wa kuficha wizi wao kwa kuruhusiwa kupandikiza kompyuta mbovu hivi hivi kadamnasi. Nani alichota pesa ya Lugumi? Iweje mtu aliyefunga kompyuta 14 tu katika miaka mi 3 aweze kufunga mifumo madhubuti ya kompyuta 98 ndani ya siku 90? Aliyehamisha hela kupitia mradi wa Lugumi atajwe.
 
Ni pure siasa za usanii....

Sasa ndiyo naanza kuelewa alikuwa na maana gani huyo Lugumi alipotamba siyo kila jipu Magu ana uwezo wa kulitumbua.......

Hivi kwa mwendo huu wa Bunge la mfumo wa Chama kimoja la huyo mdada, ni nani atathibitisha kama mashine hizo zimefungwa?

Na Je ni sheria gani ya nchi hii inayoruhusu mwizi arejeshe mali akizoiba halafu ataachiwa huru?!

Usihofu ndugu yangu CAG namuaminia taenda tena huko na akikuta bado ataripoti kama kawaida yake.
 
Eeh Mungu wangu. Nimegundua kwa nini vikundi vya kigaidi hujitokeza, nimegundua ni kwanini yule kijana wa Kiarabu alijichoma Moto mbele ya ofisi za Serikali, nimegundua ni kwa nini mtiifu wa ccm anaweza kujiunga Chadema, nimegundua kwa nini anataka aombewe. Jamani issue ya Lugumi ndo imeisha hivi hivi bila mtu kutiwa hatiani!!!?? Kweli? Nchi inaenda wapi? Mbona sioni tofauti ya JK na JPM? Mungu bora uiangamize Taifa hili tujue moja. Izame kama gharika.
 
Usishangilie upuuzi wewe .... hio ni pesa yetu sote. hivi watu wengine sijui akili zenu mnaweka wapi aiseee, shame on you, mnaleta siasa hata kwenye mambo ya muhimu....
Watu wa aina hii hata akisikia mamaa ya watoto anaselebuka na kiongozi wa chama chake atajisikia fahari kuwa ndio ukada wenyewe huo. Huwezi kumbadili huyo, ni brain washed
 
kweli tanzania hakuna kiongozi wa kweli wa kutukomboa wote ni wasanii tuu, hivi huyu lugumi anatofauti gani na mkurugenzi aliyefukuzwa TRA, engineer wa mkoa aliyefukuzwa na makonda, mkurugenzi wa TCRA n.k. Iweje yeye wampe muda wa kusawazisha makosa yake wakati hata mtoto mdogo anatambua kama wamepiga pesa
 
Kuna mambo mengine kuchangia ni kuongeza hasira tu kitu ambacho ni kibaya sana kiafya.
 
kweli tanzania hakuna kiongozi wa kweli wa kutukomboa wote ni wasanii tuu, hivi huyu lugumi anatofauti gani na mkurugenzi aliyefukuzwa TRA, engineer wa mkoa aliyefukuzwa na makonda, mkurugenzi wa TCRA n.k. Iweje yeye wampe muda wa kusawazisha makosa yake wakati hata mtoto mdogo anatambua kama wamepiga pesa

Usikute Pombe na Kitwanga wote wana hisa ndani ya Lugumi. At last ile true colour ya hapa kazi tu inajipambanua tartiiibu.
 
Hii ndo maana halisi ya "huu mchezo hautaki hasira na Sio kila jipu ni la kutumbua"

Hahahaahaahahahahahahaha Only in Tanzania,hongera sana Lugumi kwa kutimiza makubaliano yako kwenye mkataba. Safari bado ni ndefu tutafika tuu chini ya Sirikali yetu tukufu.
 
Lugumi ni nani nchi hii?hata mzee wa mbwembwe kachemka?
 
hilo ndilo bunge letu.....sema ndiooooooo!!
 
Back
Top Bottom