Jeshi la Polisi linawashikilia watu 4 kwa tuhuma za mauji ya Mtumishi wa TRA Amani Simbayao kutoka tukio la Tegeta

Jeshi la Polisi linawashikilia watu 4 kwa tuhuma za mauji ya Mtumishi wa TRA Amani Simbayao kutoka tukio la Tegeta

Heri kukaa gerezani miaka 100 ukiwa unapigania haki ya Taifa kulingana na hofu iliyojengwa na watawala kwa kushindwa kutekeleza majukumu waliyotakiwa kiyatekeleza ambayo ni ulinzi wa raia kuliko kukaa uraiani siku moja kwa hofu na wasiwasi wa nani atafuatia kutekwa,

Nakutuma chawa kawaambie hao wanaokulipa kuwa waongeze magereza kwani hawawezi kuzima moto kwa kuumwagia mafuta ya taa wala hawawezi kuficha donda lisilotibiwa kwa kulifunika na nguo litaoza na kunuka tu, wajiandae kutoa funza. Naweka nukta
Ukae gereza
Kama hakuna video iliyorekodiwa hakuna kesi hapo ya kumfunga mtu.
Hizo video mbona ziko nyingi tu,alafu nani kakuambia mahakama inapokea ushahidi wa video peke yake?
 
Heri kukaa gerezani miaka 100 ukiwa unapigania haki ya Taifa kulingana na hofu iliyojengwa na watawala kwa kushindwa kutekeleza majukumu waliyotakiwa kiyatekeleza ambayo ni ulinzi wa raia kuliko kukaa uraiani siku moja kwa hofu n wasiwasi wa nani atafuatia kutekwa,

Nakutuma chawa kawaambie hao wanaokulipa kuwa waongeze magereza kwani hawawezi kuzima moto kwa kuumwagia mafuta ya taa wala hawawezi kuficha donda lisilotibiwa kwa kulifunika na nguo litaoza na kunuka tu, wajiandae kutoa funza. Naweka nukta
Thenk yuu, kii bod woria.
 
Kwani magari yenye makosa barabarani si yanakamatwa na Polisi Traffic?
 
Udhalimu haujawahi shinda vita dhidi ya haki. Ni suala la muda
 
Muliro na askari wako mnaua njaa vijana wa bodaboda na pia mnaleta kero kwa wafanyabiashara wa Tegeta kwa ndevu stand,hakuna bodaboda/bajaji stand wote wamekimbia wanahofia kukamatwa.

Tangia tukio la kupigwa kipigo cha mbwa koko "so called TRA staffs" hali imekuwa mbaya stand ya Tegeta kwa ndevu ,askari polisi wanakamata watu ovyo ovyo tu ,ukikutwa umesimama stand unasubiri daladala au unataka kununua kitu unadakwa unaingizwa kwenye difenda unaunganishwa kwenye kesi ya mauaji.

Askari wetu bado hawajajifunza kabisa issue za upelelezi? Ya nini kukamata kamata watu ovyo hata kama hawahusiki? Tukio la bomu la ubalozi wa marekani 1998 napo mlikamata watu ovyo ovyo lakini walivyokuja wenyewe FBI wakawaambia watoeni wote hao hakuna aliyehusika.
 
Ni watuhumiwa.
Nadhani Kibatala yuko tayari na hii ni ndondo.

Mahakamani;
Kibatala; Umesema wewe ni..
Polisi; ni sahihi.
Kibatala; Cheo chako ni mkaguzi wa polisi?
Polisi; ni sahihi.
Kibatala; Ifahamishe mahakama ni kwa nini huko hapa!
Polisi; niko hapa km shahidi wa kesi no...inayohusu mauaji ya Simba.
Kibatala; watuhumiwa wa mauaji hayo ni akina nani?
Polisi; watuhumiwa ni.....ambao wako mbele ya mahakama.
Kibatala; Ithinitishie mahakama.
Polisi; fulani na fulani ni boda wanao paki kijiwe kile,huyu huwa anaenda kupiga stori pale lkn fulani alikuwa amefuata huduma ya usafiri pale kijiweni.
Kibatala; Ilikuwaje wakatenda kitendo kile?
Polisi; Gari no likiendeshwa na Simba lilisimama mbele gari no ili kumuomba dereva wa gari no...sigara ndipo dereva wa gari no...akapiga kelele za kuomba msaada kwa kuhisi kutekwa.
Kibatala; hapa sasa Kibatala anahamia kwa Tarimo Bonge Kiluvya,Una taarifa za jaribio la kutekwa kwa LIMO hotel...kule Kiluvya?
Polisi; ndio?
Kuna watu wanashikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tukio lile?
Polisi; ndio.
Kibatala; Ieleze mahakama ilikuwaje Tarimo hakutekwa.
Polisi; Baada ya watekaji wale kutaka kumuingiza Bonge ndani ya gari aliomba msaada kwa kupiga kelele ndipo watu wakakasogea na wengine wakachukua picha mjengeo,kuona vile watekaji wakakimbia na sura zao zilionekana dhahili kwenye picha ile.
Kibatala; Unaweza kuionesha mahakama hiyo picha?
Polisi; hapa sina hiyo picha.
Kibatala anamuonesha; Una maanisha picha hii?
Polisi; Ndio.
Kibatala;Sasa turudi Tegeta kwa ndevu,kwakuwa umekiri kuhusu kuwepo hali ya utekaji watu na kwamba dereva wa gari no..aliomba msaada ili asitekwe,sasa tupatie ushahidi unaothibitisha ya kuwa ktk watu wooooote waishio Tegeta kwa Ndevu ni hawa watuhumiwa walioonekana wakimsulubi mshukiwa wa utekaji.
Polisi; Flani alikutwa akiwa na mkanda wa Simba,yule alikuttwa na kofia na huyu alikutwa na alama zenye mkwaluzo inayoashiria pulukushani.
Watu woooote kichekoooo.
Kibatala; unaweza ukaionesha mahakama hivyo vidhibiti?
Polisi; ndio,analeta kofia,miwani.
Kibatala; analeta kofia na miwani vikifanania na kuuliza swali,unaweza kutofautisha kati ya....na....na pia....na....?
Polisi; Hapana.
Kibatala; ieleze mahakama ni kwa nini hukuona tofauti.
Polisi; Kofia zinafanana rangi,size na zimetengezwa kiwanda kimoja alikadharika miwani pia ina fanana kwa kila kitu.
Kibatala; Mh Jaji naomba kuishia hapo.
 
Mbuzi wa kafara. Hao maafisa wa TRA ndio waliopaswa washikiliwe kwa kuzua taharuki kwenye jamii. Nimeona hata plate namba za gari ni tofauti na gari yenyewe
WATEKAJI wale, hakuna ofisa wa TRA
 
Kesi ya mauaji? Wamekwiiishaaaaa, minimum gerezani miaka 10 ya kukaa rumande, halafu wanaenda kukaa deathrow, kwa kuwa ulimshambulia Afisa wa serikali, kupata msamaha wa Rais ni ndoto, basi angalau zingekuwa za Mzee Alinacha, zao Zita kuwa ndoto za marehemu(kwa kuwa huwa hawaoti).

Wanaowahamasisha wako JF wanaweka vibando vyao vya 500 wawaingize chaka wengine, akili za kuambiwaaa
Kwasasa dawa yenu WATEKAJI ni kupigwa mawe hadi kufia eneo la tukio, hakuna namna tena
 
Tatizo wananchi hawana imani na serikali pamoja na wafanyakazi wake.
TUMEPOTEZA AMANI.✍🏿
 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne Muliro anazungumza na Vyombo vya Habari.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaaam linawashikilia wanaotuhumiwa wanne, Deogratius Paul Massawe (40), Bakari Idd Bakari (30), wote ni kuli wa Tegeta kwa Ndevu, Omary Issa mpigadebe wa Tegeta DAWASCO na Rashid Mtonga (29) kazi yake ni Bodaboda kwa mauaji ya mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Amani Simbayao.

Watuhumiwa hao, pamoja na wengine ambao bado wanashikiliwa kwa tuhuma hizo, wanahojiwa kwa kina, ikiwa ni pamoja na kumjeruhi mtumishi mwingine aliyefahamika kwa jina la Adriano Fredrick.

Watuhumiwa hawa ambao bado wanashikiliwa na Wanahojiwa kwa kina wakati wanawashambulia maafisa hao waliharibu pia gari la Serikali la TRA, gari namba STL 9922 aina ya Toyota Land Cruiser

======

View attachment 3171365
Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es salaam linawashikilia watuhumiwa wanne 1. Deogratius Paul Masawe miaka 49 kuli , mkazi wa Tegeta kwa ndevu 2. Idd Bakari miaka 30, kuli mkazi Tegeta kwa ndevu.3.Omar Issa miaka 47 ,myao, mpiga debe mkazi wa Tegeta Dawasco 4.Rashid Mtonga myao , miaka 29 kazi ya bodaboda , mkazi wa Bunju.

Wanatuhumiwa kufanya mauaji ya mtumishi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania aitwaye Amani Kamguna Simbayao pia kumjeruhi Adriano Fredrick wa TRA. Watuhumiwa hao na wengine ambao bado wanahojiwa kwa kina walikamatwa baada ya kuwashambulia maafisa hao wa TRA wakati wakitekeleza majukumu yao ya kisheria. waliliharibu pia gari namba STL 9923 aina Toyota Land Cruiser Hardtop nyeupe mali ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.

Tukio hilo lilitokea tarehe 05 Desemba, 2024 majira ya saa 03 :00 usiku Tegeta kwa Ndevu Kinondoni baada ya Maafisa hao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania kukamata gari namba T 529 DHZ aina ya BMW rangi nyeupe lililodaiwa kuwa na makosa ya kikodi

Jeshi la Polisi Kanda maaalum ya Dar es Salaam linawaonya vikali na halitavumilia watu ambao wanataka kujenga tabia ya kuwashambulia watumishi wa Serikali wakati wakitekeleza majukumu yao licha ya kuwa wanakuwa wamefuata taratibu zote za kisheria.Jeshi halitasita kuchukua hatua kali za haraka na za kisheria dhidi ya wahusika kwa kuwafikisha kwenye mamlaka zingine za haki.

Imetolewa na;

Muliro J. Muliro -SACP

Kamanda Kanda Maalum ya Polisi

Dar es Salaam
Sawa ila waliomuua mzee kibao hawajakamatwa wala hawajulikani hadi leo lakini wakiuliwa vipenyo na vificho wenu mnakamata hadi inzi qmamae zenu wadanganyika.
 
Walau hii wiki sasa inaenda kuisha hatujasikia tukio la utekaji.

Hongera sana wakazi wa Tegeta kwa ndevu kwa kuonyesha mfano kwa hao vibaka waliojificha nyuma ya mamlaka ya mapato.

Kila mkoa wakifanya hivyo basi heshima kwa wananchi itarudi.
 
Jumba bovu............limewaangukia wana........hapo hata kama huusiki utapigwa mpaka ukubali.........shida sio kitu kingine maana kifo ni kifo .................shida ni ukubali tu hili mambo yawe mepesi..................lakini si walipigwa na halaiki kama video mjengeo zilivyoonesha au?? Wanasheria kazi kwenu
 
Kifo cha mzee kibao hata mtuhumiwa wa mchongo hajapatikana - Dunia hii
 
Back
Top Bottom