Jeshi la Polisi, naomba mtujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe

Jeshi la Polisi, naomba mtujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Jeshi la Polisi hatimaye limemfikisha Mbowe mahakamani Kisutu "kisirisiri" likimtuhumu kwa Makosa ya jinai ya ugaidi.

Naliomba Jeshi hilo litujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe.

1. Ni kwanini wamempeleka mahakamani Kisutu kisirisiri, bila kumuarifu yeye mtuhumiwa, ili aweze kutumia haki yake kisheria, ya kuwa na mawakili wake kwenye kesi hiyo?

2. Hapo awali RPC wa Mwanza, alitueleza kuwa wamemkamata Mbowe, kutokana na kuandaa kongamano la Katiba mpya ya nchi, ni kwanini kwenye "charge sheet" ya mahakamani, kosa hilo liwe halipo na badala yake, aonekane Mbowe kuwa alipanga njama za kigaidi za kutaka kulipua vituo vya mafuta?

3. Hapo awali Jeshi la Polisi lilituambia kuwa wanamshikilia Mbowe, kwa tuhuma kuwa alipanga njama za kuwaua viongozi wa serikali, ni kwanini walipomfikisha mahakamani, kosa hilo pia halipo?

4. Kama Mbowe anaunganishwa na watuhumiwa wengine wa ugaidi watatu waliokamatwa mwaka Jana mwezi wa 8, ni kwanini basi ichukue muda mrefu kiasi hiki hadi hivi sasa inakaribia mwaka mmoja, kwa Jeshi la Polisi kumkamata Mbowe, kwa kesi hiyo ya hatari sana?

5. Jeshi la Polisi halijataja vituo vya mafuta, ambavyo Mbowe alivi-target kuvilipua na lini tukio hilo lilikusudiwa kufanywa, hivi hiyo inaweza kutufanya sisi wananchi tuendelee kuliamini Jeshi letu la Polisi?

Hivi sisi wananchi tukiamini kuwa hii kesi ni ya kisiasa na ya kubambika, ambayo lengo lake ni Jeshi hilo ku-side upande wa watawala wa CCM, tutakuwa tumekosea kweli?
 
Jeshi la Polisi hatimaye limemfikisha Mbowe mahakamani Kisutu, likimtuhumu kwa Makosa ya jinai ya ugaidi.

Naliomba Jeshi hilo litujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe...
Jeshi la Polisi sio kiwango security kijana, wana taratibu zao za kazi, wamemfikisha Mbowe mahakamani taarifa wametoa, hawawezi kufanya utakacho wewe, watafanya kama taratibu zao zinavyotaka, ebu tulieni kama Mbowe ni msafi mbona uraiani utamuona tu.
 
Jeshi la Polisi sio kiwango security kijana, wana taratibu zao za kazi, wamemfikisha Mbowe mahakamani taarifa wametoa, hawawezi kufanya utakacho wewe, watafanya kama taratibu zao zinavyotaka, ebu tulieni kama Mbowe ni msafi mbona uraiani utamuona tu.
Taratibu zao za kazi, ndiyo kumbambikia Mbowe makosa ya ugaidi?
 
Jeshi la Polisi hatimaye limemfikisha Mbowe mahakamani Kisutu, likimtuhumu kwa Makosa ya jinai ya ugaidi.

Naliomba Jeshi hilo litujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe...
Hujui prosecution inavyofanyika. Prosecutors can move to add new charges, amend or drop existing charges anytime. Prosecutors wanahitaji tu kuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha (beyond reasonable doubt) tuhuma zao dhidi ya mtuhumiwa!
 
Jeshi la Polisi sio kiwango security kijana, wana taratibu zao za kazi, wamemfikisha Mbowe mahakamani taarifa wametoa, hawawezi kufanya utakacho wewe, watafanya kama taratibu zao zinavyotaka, ebu tulieni kama Mbowe ni msafi mbona uraiani utamuona tu
Mama kaanza udhalimu kama mwendazake, atalia muda si mrefu
 
Hivi sisi wananchi tukiamini kuwa hii kesi ni ya kisiasa na ya kubambika, ambayo lengo lake ni Jeshi hilo ku-side upande wa watawala wa CCM, tutakuwa tumekosea kweli?
Mkuu Mystery, mbona unatumia nguvu zako nyingi hivi kutafuta majibu ya maswali yasiyohusika na kesi?

Hakuna kesi, Mbowe ni Mfungwa wa Kisiasa.

Inabidi sote tulitambue hilo jinsi lilivyo, na tulitangaze jinsi lilivyo kuliko kuendelea kupoteza wakati na maswala yasiyokuwepo.

Mbowe ni Mfungwa wa Kisiasa, na atakaa jela hadi hapo wenye madaraka watakapoamua kumwachia, au watakapopata joto la kutosha kuwafanya wabadili maamuzi yao.

Sasa sijui kama CHADEMA wamejipanga vipi kulikabili hili, maanake wao ndio walio na uongozi wa kuwatangulia wanachama wao na wananchi wasiopendezwa na hali hii ya nchi yetu kwa ujumla.

Kuna akina Mbowe wangapi waliobaki huko CHADEMA kuendeleza mapambano haya. Hilo ndilo la muhimu lililobaki kujibiwa.
 
Hujui prosecution inavyofanyika. Prosecutors can move to add new charges, amend or drop existing charges anytime. Prosecutors wanahitaji tu kuwa na ushahidi wa kutosha kuthibitisha (beyond reasonable doubt) tuhuma zao dhidi ya mtuhumiwa!
Je hiyo uliyoiita kuwa ushahidi (beyond reasanoble doubt) ni kweli hao Polisi wanao ushahidi wa kuthibitisha kuwa Mbowe ni gaidi?
 
1. Ni kwanini wamempeleka mahakamani Kisutu kisirisiri, bila kumuarifu yeye mtuhumiwa, ili aweze kutumia haki yake kisheria, ya kuwa na mawakili wake kwenye kesi hiyo?
Kwa sababu CHADEMA walitangaza rasmi kupitia Mwakamu Mwenyekiti Taifa na Mwanasheria wa Chama Mstaafu kwamba Mbowe hatajibu mashtaka, hataandika statement, hataomba dhamana, hatajitetea wala hatatetewa, CHADEMA hawatamwombea dhamana, hawatafanya chochote, serikali wakitaka kumfunga wamfunge, kumpoteza wampoteze, kwa sababu wanavyozidi kumweka ndani ndivyo serikali wanavyozidi kuchafuka duniani na kwamba watamwachia wao wenyewe.

That’s their calculus.
They released that statement point blank.
 
Jeshi la Polisi hatimaye limemfikisha Mbowe mahakamani Kisutu, likimtuhumu kwa Makosa ya jinai ya ugaidi.

Naliomba Jeshi hilo litujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe...
CCM ni genge la kigaidi linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendelea kutawala
 
Jeshi la Polisi sio kiwango security kijana, wana taratibu zao za kazi, wamemfikisha Mbowe mahakamani taarifa wametoa, hawawezi kufanya utakacho wewe, watafanya kama taratibu zao zinavyotaka, ebu tulieni kama Mbowe ni msafi mbona uraiani utamuona tu
Je taratibu zao za kazi, ni kumpeleka mtuhumiwa mahakamani bila kuzingatia haki zake za msingi, kama vile kuwakilishwa na mawakili wake mahakamani?
 
CCM ni genge la kigaidi linalotumia mabavu ya vyombo vya dola kuendelea kutawala
Hivi CCM hawajifunzi tu kutokana na matukio ya historia ya nyuma?

Hata utawala wa makaburu wa Afrika Kusini, ulimtia hatiani na kumfunga jela maisha, shujaa wetu Nelson Mandela, kwa makosa hayo hayo ya ugaidi.

Nini kilitokea baada ya hapo?

Baada ya kusota jela miaka 27, alikuja kuachiwa huru mwaka 1990 bila ya masharti yoyote na utawala huo wa makaburu na baadaye akawa mwafrika Kusini mweusi wa kwanza, kuchaguliwa katika uchaguzi uliokuwa huru wa kwanza kuandaliwa nchini Afrika Kusini!
 
Kesi iko mahakamani yote hayo utayajua wakati wa hatua ya ushahidi.
 
Jeshi la Polisi hatimaye limemfikisha Mbowe mahakamani Kisutu "kisirisiri" likimtuhumu kwa Makosa ya jinai ya ugaidi.

Naliomba Jeshi hilo litujibie maswali yafuatayo kuhusu ugaidi wa Mbowe...
CCM ni wananchi au siyo wananchi?

Je, CHADEMA ni wananchi au siyo wananchi?

Wananchi ni nani?
 
Ma
Hivi CCM hawajifunzi tu kutokana na matukio ya historia ya nyuma?

Hata utawala wa makaburu wa Afrika Kusini, ulimtia hatiani na kumfunga jela maisha, shujaa wetu Nelson Mandela, kwa makosa hayo hayo ya ugaidi...
Mandela ili kuachia huru kulikuwepo na masharti mengi muno, muno mpaka sasa ndiyo yanayo itafuna Afrika ya kusini! Mojawapo ya sharti ovyo ni wazungu kubaki na ardhi yote waliyo pora!

Sijui Mandela wa CHADEMA atawekewa masharti gani?
 
Je hiyo uliyoiita kuwa ushahidi (beyond reasanoble doubt) ni kweli hao Polisi wanao ushahidi wa kuthibitisha kuwa Mbowe ni gaidi?

Usiniulize mimi. Mahakama ndiyo itategua hicho kitendawili. Ikiridhika na ushahidi utakaotolewa itamtia hatiani mtuhumiwa. Vinginevyo, itamuachia huru!
 
Huna akili wewe pimbi kila suala mnataka kuhusisha na siasa. Mbowe ni binadamu kama watu wengine, hivyo anaweza kuwa culprit.
Kwa hiyo hili ndiyo jibu kutoka kwa mtu "mwenhye akili"? Mbona ni kama jibu la mtu "mwenda wazimu"?
Ningependa kukudadavulia jinsi ulivyo kama mwenda wazimu kwa kutoa jibu kama hilo, lakini naona haitasaidia chochote kwa mtu mwenye akili kama zako.
 
Back
Top Bottom