Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Jeshi la wananchi laonywa lisivunje katiba ya nchi kwa kufanya majukumu yasiyo yake kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi

Ni kwambie tu ndugu yangu. Wengine hata hatujazaliwa tulitukanwa tukiwa tumboni mwa mama zetu. Tukazaliwa tunatukanwa hadi tunakua. So kwangu mimi matusi wala sijali na siumii. Na si njia ya kunifanya niache kusimamia nacho kiamini.

Naona watanzania wengi wa siku hizi wanadhani matusi ndo njia pekee ya kujadili ili umnyamazishe mtu. Mfano tunaongelea mada. Badala uje na mawazo yako unakejeli watu sijui darasa la saba. Hivi uoni utakuwa umetukana hadi kwenu kwani watanzania wengi wameishia la saba. Hivyo ilo tusi umejumuisha na wazazi au nduguzo.

Lakini ujue kusoma unapata taaluma ya kidarasa, ila kuna watu wameelimika zaidi ya udhaniavyo. Unajua wanasayansi wengi hawakua wasomi?

Unajua waliofanikiwa wengi matajiri wakubwa si wasomi? Nenda hata huko Ulaya wanao enjoy na life si wasomi. Jifunze kutodharau.
Mkuu yaishe[emoji107]
 
Shida unatetea uwendawazimu [emoji53][emoji53]
Naongea nacho kijua. Sikurupuki. Nina experience ya kutosha! Nina exposure, na naweza kusema nafahamu mengi! Zamani nikiwa kama wewe sikujua na nilidhani mimi navyojua ndo kila kitu.

Ila uzoefu. ulinifanya kufungua macho. Naingia kazini nilifundishwa na huyo mtu unae msema darasa la saba. Tena wamama wazee hawa ndo walio nifundisha kazi.

nimefanya kazi nje nchi kadhaa nimefundishwa na hao hao ambao hawana elimu kubwa. Make hata ulaya wapo. Na ndiyo walio nisaidia ktk future.

Jifunze kuheshimu kila mtu. Utajua mengi.
 
Kuna kitu naanza kuhisi

Ukifikiri kwa makini lile tamko la JWTZ kuhusu sare za jeshi naliona kama lina mlengo mwingine tofauti na ambavyo limewasilishwa.

Kwanini kusalimisha sare kuambatane na msako wa nyumba kwa nyumba kukagua watu ambao hawajakabidhi sare?

Vipi kama hao wanajeshi wana agenda yao nyingine?

Kupitia sakata la bandari na jinsi upinzani walivyo chachamaa kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ubovu wa mkataba.

Huku wakihamasisha wananchi waukatae pamoja na kuongeza nguvu ya kudai katiba mpya, na mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa.

Vipi kama ujio wa wanajeshi mtaani hauna lengo la kukusanya sare bali kuwatisha raia ambao hivi karibuni wamekuwa wakihamasishwa kufanya maandamano ya kupinga mkataba?
maandamano afanye nani bongo ndugu yangu! Njaa iliyopo jumlisha madeni hata nguvu tu ya kufatilia nakosa
 
Jwtz,imejaa vijana, failures wa form 4,kule juu imejaa makada wa CCM, wanasubili wateuliwe wawe ma RC, DC, mabalozi nk! Yaani, mtu kasoma military science! Amefikia cheo cha major nk, lakini,badala, ya kuwaza Mambo makubwa kama kuanzisha jeshi, LA, pamoja LA SADC, au East Africa, au kutafuta kazi, UN, the hague nk, au kufungua kampuni la ulinzi, kama Wagner au black water,anawaza uteuzi, kuwa mwenyekiti wa CCM akishastaafu!
Akili hakuna kabisa,
Yule msemaji wao, ukimuangalia vzr,nafikiri kirusi cha ngoma kimefika kwenye ubongo! Anaongea kama kibaka, au konda anaetishia wanafsunzi wasipande daradara kama hawana sarsfu ya 200
 
Namheshimu sana Mwabukusi na ninamuunga mkono katika baadhi ya mambo kama DPW. Au kupinga badndari zetu kugawiwa bure kwa DPW.
Ila ktk ili nadhani hatofautishe utendaji wa kazi za jeshi na polisi. Pia hatofautishe sheria zetu jinai na taratibu za kijeshi.

Ajiulize, kwanini jeshi lina mahakama yake ya kijeshi. Kwanini mwanajeshi akivunja sheria lazima kwanza taratibu zao za kijeshi zifuate avuliwe uanajeshi ndipo taratibu za kawaida za kijinai zifuatwe.

Anatakiwa ajue taratibu za kijeshi na intelligency za kijeshi. Jeshi halikurupuki kufanya jambo. Si mara ya kwanza jeshi kufanya zoezi kama hili. Nakumbuka miaka ya nyuma mkoa fulani zoezi ili lilifanyika na lilisaidia kuzuia uharifu. Yaani ukichekea watu hati sheria za kijinai unaweza shangaa unajeshi lisilo rasmi nchini. Au watu tayari wanamiliki silaha.

Na zoezi ili ufanywa na Military police. Wanajua taratibu tuache wafanye kazi.
Wee kilaza sheria za jeshi zinawahusu wao wenyewe na kamwe haziwahusu raia kwa mujibu wa katiba!

Raia hawezi kupelekwa kwenye mahakama za kijeshi lakini mwanajeshi akitenda jinai uraiani anavuliwa jeshi na kupelekewa mahakama za kiraia na polisi.

Usijifanye mjuaji kumbe ni chawa tu kazi kutisha watu!
 
WAKILI MWABUKUSI ANATAKA MKUU WA MAJESHI AZUIE UVUNJIFU WA KATIBA.

"Nchi inaongozwa kwa mujibu wa sheria na katiba. Kazi ya kukamata wa halifu ni ya Jeshi la Polisi. Jeshi la wananchi halina mamlaka kisheria na kikatiba kuingia kufanya msako mitaani kwa kisingizio cha kutafuta sare zao. Jukumu lao ni kulinda mipaka ya nchi. Cha ajabu hawajatuambia walizipeleka lini huko mitaani au zilichukuliwa na nani au waliibiwa lini? This is more than a comic [Huu ni usanii]!

Mwanajeshi hana mamlaka ya kupekua mtu katika makazi yake au maungo ya raia. Hii ni kazi ya Polisi wetu. Isipokuwa pale kunapokuwa na hali ya hatari au tishio dhahiri la mapinduzi.

Sheria inaruhusu kukataa ukamataji haramu na iwapo jeshi litaingia kwa namna hii ni haki ya wananchi kukataa ukamataji au upekuzi haramu usiofuata sheria ikiwemo kumshtaki Mwanasheria mkuu na Mkuu wa Majeshi ili kulinda sheria na Katiba ya Nchi na kudai fidia ya usumbufu.

Kama jeshi limeibiwa sare zake likaripoti Polisi. Polisi wafanye uchunguzi na wakibaini kosa Polisi ndiyo wenye utaalamu wa kupeleleza uhalifu wa wizi. Jeshi au wanajeshi hawako juu ya sheria [hivyo] wapunguze mihemko.

Kumekuwa na ujasiri wa uvunjaji katiba na sheria na kuwatisha wananchi katika taifa letu katika uongozi huu wa sasa na kwa hili hatutakubali na tutalitolea tamko rasmi kupinga vurugu hizi katika utumishi wa umma.

Mkuu wa Majeshi awajibike haraka kuzuia ukora huu wanaotaka au kupanga kuufanya!

Najisikia aibu sana kuishi na kushuhudia viroja hivi. Mungu bariki Watanganyika! Mungu ibariki Tanzania! Mungu waadhibu na kuwakemea madhalimu wote.

Boniface Kajunjumele Mwabukusi!
Ni kweli sare za jeshi hazitakiwi kuvaliwa nasi raia....

Namuunga mkono MWABUKUSI kuwa JWTZ liheshimu katiba....

Liheshimu katiba....

Wasiingilie kazi ya JESHI LETU LA POLISI.....

#SiempreJMT[emoji120]
 
Watanzania tuache kuchekea ujinga. Jwshi linapaswa kufanya mambo serious na sio kuanza kusumbua raia. Jeshi linapaswa kuwa sehemu ya raia kukimbilia pale ambapo vyombo vingine vyote vimeshindwa
[emoji2956]
 
Back
Top Bottom