Jet Li amkabidhi mkewe utajiri wake wote asema ataomba kwa mkewe akihitaji kitu

Jet Li amkabidhi mkewe utajiri wake wote asema ataomba kwa mkewe akihitaji kitu

Jamaa anampenda huyu mwanamke kiasi kwamba alimpa taraka mkewe wa awali na kutelekeza watoto wao wawili wa kike baada ya kukutana huyu mrembo. mrembo akamwambia kama akiendelea kuwa na mapenzi naye yale yale kwa miaka kumi basi ndipo atamuoa.
Mnyamwezi akaendelea kuonyesha mapenzi kiasi kwamba kuna kipindi bidada alikuwa na madeni makubwa, jet li akasaini mkataba wa kucheza filamu sita na pesa itakayopatikana iende kulipia madeni ya huyu binti na kumbuka wakati huo hawajaoana ndicho kipindi cha hiyo miaka kumi ya demu kumwangalia jamaa kama ana mapenzi yale yale.
Unajua kwanini jet li movie zake nyingi alikuwa haonyeshi mahaba kwa wanawake? katika kipindi cha hiyo miaka kumi, kuna movie alicheza akiwa ana mpenzi. Baada ya hiyo movie kutoka fununu zikaanza kudai kuwa jet li anatoka na huyo actress. Huyo binti akakasirika na kutaka kuvunja mahusiano yao ambapo jet li alijitetea na kumbembeleza sana. Basi toka wakati huo Jet Li akawa kwenye mikataba yake inahusisha kipengele cha kutokuwa na scenes za mapenzi yaliyopitiliza na binti anayecheza naye.
Jamaa haambiwi kitu kwa huyo mwanamke.
Amelogwa

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
 
Mimi napenda mademu wa kijapan na china ,just walivyo tu halafu umkute mwenye limguu na shape hasa hasa wafilipino wapo hivyo mishep kama yote hata nikichunguliaga sex zao naonaga kawivu😂😁😁😁
 
Mwigizaji Li Lianjie 'Jet Li' amewaacha mashabiki wake midomo wazi baada ya kufunguka kuwa amemkabidhi mke wake Nina Li Chi utajiri na fedha zake zote.

Mwigizaji huyo mwenye utajiri unaokadiliwa kuwa zaidi ya dola milioni 260, kupitia mahojiano yake ya hivi karibuni ameweka wazi kuwa uamuzi huo haukutokana na matatizo yake ya kiafya ambapo anasumbuliwa na ugonjwa wa hyperthyroidism na matatizo ya mgongo bali ni kwa sababu anaimani kubwa kwa mkewe.

"Upendo wake wa kwanza, anastahili zaidi. Kwa hakika, kwa miaka mingi, Nina amekuwa kitu kikubwa kuliko tu kuwa mpenzi wangu yeye ni mshauri, nguzo yangu ya nguvu. Alikuwa daima upande wangu, Li wakati nilipokuwa chini kabisa, alinisimamia. Anasimamia kila kitu ili niweze kuzingatia kazi yangu na afya yangu. Lolote lile, namwamini. Yeye ndiye sababu naweza kuwa ninavyokuwa leo," amesema Jet Li

Nina ambaye ni mke wa Li aliveshwa taji la Miss Asia mwaka 1986, wawili hao walikutana na kuanzisha uhusiano mwaka 1988, aidha moja ya sababu inayomvutia Li kutoka kwa mkewe ni kumtii kuacha shughuli zake za urembo na kujikita zaidi kulea familia.

Uaminifu huo wa Li kwa mkewe uliibua mijadara mbalimbali katika mtandao wa Twitter (X) mashabiki wakiwapongeza wawili hao kwa kuaminiani wakiandika "Hii si kuhusu pesa, somo la upendo ni kuhusu kuthamini mtu ambaye amekuwa upande wako kupitia kila kitu,".

Mkali huyo wa filamu za ngumi ambaye amewahi kuonekana kwenye Mulan, League of Gods, The Founding of a Republic, War na nyinginezo alifunga ndoa na Nina mwaka 1999 na wamebahatika kupata watoto wawili pamoja. Hata hivyo anadai kuwa hata akitaka kununua kitu chochote basi atamuomba mkewe pesa.

NB Wale team kataa ndoa...mpite hivi[emoji125][emoji125]View attachment 3220818

Sent from my TECNO KG5j using JamiiForums mobile app
Hio itawashangaza wengi ambao hamuwajui wachina ila kwa mtu ambaye amesha interact nao huwa wachina wanaheshimu sana mama kuanzia watoto mpaka waume.

Final say huwa ni mama. Hadi huwa nafikiria huenda wanafata sana Matrilineal system.
 
Nimejaribu kuangalia mali zangu nikiambiwa nimkabidhi mama G ,mpaka nimecheka.Mashati mengii na viatu vya mtumba[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
$ milioni 260 pesa ya kibongo
Inakuwa ngapi vile??

Ova
 
Back
Top Bottom