JF Exclusive: Video/Audio ya Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine (1978)

JF Exclusive: Video/Audio ya Waziri Mkuu Edward Moringe Sokoine (1978)

Sawa, lakini swali langu la kwanza hukujibu, maana ndio tabia yako nilikwambia wakati huo mimi nilikuwa Dar wewe hata hukusema ulikuwa wapi? Pengine ulikuwa hujazaliwa then unataka kujifanya mjuaji na kuwaanisha watu kwamba lipo jambo ambalo unalielewa. Nimekupa hata jina la Mwandishi wa habari wa Waziri mkuu wakati ule, what else can you expect. Nitakwenda kwenye maktaba yangu nifukue baadhi ya magazeti ambayo ni kumbu kumbu inshallah nikipata nitaweka humu.
Mkuu 'Ole', nimekwishatambua wewe ni mtu wa aina gani. Inatosha sasa.
 
Tukiendelea na mijadala mingine nimeonelea niwashikilishe video hii. Nimeulizwa mara kwa mara kuhusu video/ audio ya Edward Sokoine. Katikati upekuzipekuzi wangu nimekutana na hii. (Kuna mtu aliniuliza chemba kuwa angependa kumuona na kumsikia Sokoine) badala ya kusoma tu habari zake. Hii ni miongoni mwa video nzuri nilizopata kuziona au kuzisikia.



Mkuu MMm hongera sana kwa kutukumbusha kuhusu shujaa wetu na mzalendo namba moja wa Tanzania.

Hixi videos zinaweza kupatikana (kama anavyosema mkuu Paschal) kutoka hivyo vyanzo alivyovitaja.

Ila nimedokezwa kwamba kuna kulipa ada kiasi hivi.
 
"...alionea 'wananchi' kwa sababu alisimamia zoezi la kuwakamata na kuwaweka kizuizini..." umetumia neno 'alionea' kwa maana kwamba hapakuwa na sababu ya kuwakamata hao wananchi? "Ulanguzi" haikuwa sababu, na hasa ukichukulia wakati husika na taifa likikabiliwa na hali ngumu ya kivita?

Na wakati unasema hapa kwamba "Mzee Mwinyi aliondoa tatizo la ulanguzi wa bidhaa bila kulazimika..." huoni kwamba wakati uliruhusu kufanya hivyo? Vita ilikwishapita, kwa hiyo ilikuwa ni sawa kuliweka taifa katika hali tofauti.

"Sokoine alifanya kazi kubwa.wakati wa vita.." Kazi gani, ambayo inafanya makosa aliyofanya huko kabla ya vita yaendelee kumwondolea sifa? Huoni kwamba msimamo wake kabla ya vita, wakati wa vita na baada ya vita, yote kwa pamoja ndio yanayofanya aonekane kuwa mzalendo wa kweli kwa taifa lake?

Sidhani kuwa mtu ambaye hakuwepo wakati wa Sokoine, ataelewa kwa kuambiwa tu 'Sokoine alifanya kazi kubwa wakati wa vita.'

Vita zidi ya uhujumu ujumi haikulenga kumkomoa mtu. Hali ya maisha ya wananchi wote ilikuwa ni ngumu.

Wakati taifa linapokuwa linakabiliwa na hali ngumu, halafu ukawaonea aibu watu wanaohujumu juhudi zinazofanywa ili taifa liondoke kwenye hali ngumu, sijui faida ya kufanya hizo juhudi za kuondokana na hali ngumu.

..wananchi walikamatwa, wakawekwa kizuizini, halafu baada ya hapo bunge likapitisha sheria ya makosa ya uhujumu uchumi.

..mtitiriko huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala wa sheria.

..sasa waliiokamatwa kwa mtindo huo walikuwa ni wengi. Mashauri yao yalichukua muda mrefu. Na wengi wao hawakupatikana na hatia lakini maisha na mali zao ziliharibika.

..Serikali ilikuwa inajihujumu yenyewe kwa kushindwa kufanya marekebisho ya sera zake ili kuweza kukabiliana na changamoto za kiuchumi zilizokuwa zimejitokeza.
 
..wananchi walikamatwa, wakawekwa kizuizini, halafu baada ya hapo bunge likapitisha sheria ya makosa ya uhujumu uchumi.

..mtitiriko huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala wa sheria.

..sasa waliiokamatwa kwa mtindo huo walikuwa ni wengi. Mashauri yao yalichukua muda mrefu. Na wengi wao hawakupatikana na hatia lakini maisha na mali zao ziliharibika.

..Serikali ilikuwa inajihujumu yenyewe kwa kushindwa kufanya marekebisho ya sera zake ili kuweza kukabiliana na changamoto za kiuchumi zilizokuwa zimejitokeza.

Mkuu lakini hao unaowatetea walificha bidhaa na baadae kuzilangua kwa bei ya juu.

Ndo maana kukawepo msako wa walanguzi na wahujumu uchumi.

Au mkuu hukuonja zie shubiri za kupanga mistari na madaftari?

Ugali wa Yanga je, waukumbuka?
 
Sokoine hakutoa maagizo ya kutafuta sifa, Bali yalikuwa ya kazi tuu. Hakuwa na tabia ya kujikomba kwa Rais bali alitenda yaliyo ndani ya nafasi yake ya kazi tofauti na sasa wasaidizi wote wa Rais ni praise team yake bila aibu. Nadhani hata PM naweza sema hivyo.
Hivyo ndivyo ninavyo mjua Sokoine na jinsi walio kuwa wababe katika maeneo yao walivyo muogopa. Wapo ma RC na DC ambao wanalaumiwa sana wakati huu kwa tabia mbaya za kimaadili na utendaji hakika kwa Sokoine hangesubiri sijui mpaka nani aseme yeye angefyeka tuu.
"Quality" nadra sana kuwa nazo viongozi wengi.
Kassim Majaliwa, anajitahidi sana katika mazingira magumu

Mkuu Chakaza, umetoa 'ushuhuda' kama wa 'walokole', ila wao huweka chumvi nyingi. Pongezi kwako na heshima mkuu.
 
Hilo la kushindwa kuendesha uchumi ni analysis nyepesi sana kwa suala very complicated. Linahitaji mjadala unaojitegemea. Hukuwatendea haki hao magwiji wa uongozi.

..hata nyinyi mnaotoa SIFA ZA JUMLA-JUMLA hamuwatendei haki Mwalimu Nyerere na Edward Sokoine.

..sikatai kwamba walikuwa wazalendo, lakini tuseme ukweli kwamba walikuwa na mapungufu makubwa ktk usimamiaji wa uchumi wa nchi.

NB.

..unayafahamu makosa ya Mwalimu Nyerere yaliyosababisha kilimo cha mkonge na korosho kiporomoke?
 
Mkuu lakini hao unaowatetea walificha bidhaa na baadae kuzilangua kwa bei ya juu.

Ndo maana kukawepo msako wa walanguzi na wahujumu uchumi.

Au mkuu hukuonja zie shubiri za kupanga mistari na madaftari?

Ugali wa Yanga je, waukumbuka?

..nakumbuka sana.

..lakini Sokoine alipowakamata haikufanya bidhaa zifurike madukani na foleni ziishe.

..viwanda vyetu vilikuwa havizalishi bidhaa za kutosha.

..Sokoine hata kama alikuwa na nia nzuri hatua alizochukua hazikuleta matokeo chanya.

..Na zaidi hatua alizochukua hazikuzingatia RULE OF LAW.
 
..wananchi walikamatwa, wakawekwa kizuizini, halafu baada ya hapo bunge likapitisha sheria ya makosa ya uhujumu uchumi.

..mtitiriko huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala wa sheria.

..sasa waliiokamatwa kwa mtindo huo walikuwa ni wengi. Mashauri yao yalichukua muda mrefu. Na wengi wao hawakupatikana na hatia lakini maisha na mali zao ziliharibika.

..Serikali ilikuwa inajihujumu yenyewe kwa kushindwa kufanya marekebisho ya sera zake ili kuweza kukabiliana na changamoto za kiuchumi zilizokuwa zimejitokeza.
Mtiririko huo kwa hakika ni "uvunjifu wa haki za binaadam na utawala bora," bila ya shaka yoyote. Hata hivyo, usisahau kuwa Katiba ilikuwa inatoa mamlaka kwa Rais katika mambo kadhaa ambayo yalihitaji kuchukuliwa hatua kama yanahatarisha usalama wa taifa.
Viongozi hawawezi kuacha kuchukua hatua na taifa lipate madhara eti kwa vile "sheria zilikuwa hazijatungwa." La mhimu hapa ni kuwa sheria ilitungwa na wahusika walishazuiwa wasilete madhara zaidi kabla ya sheria kutungwa.

Katika hali ya mapambano (vita), kuna watu wengi na mali huathirika bila ya kuwa wahusika wa moja kwa moja katika vita hivyo (collateral damage). Vita haiwezi kuacha kupiganwa kwa sababu tu ya hofu ya kuumiza wasiokuwa maadui, hii ndio bahati mbaya sana ya matukio kama haya unayoeleza hapa.

Lililo mhimu ni kwamba sheria ilitungwa na wale ambao hawakuhusika waliachwa huru. Kwa hiyo dhana ya 'kuonea' haistahili kutumiwa katika kulaani yaliyofanyika.
 
..sikatai kwamba walikuwa wazalendo, lakini tuseme ukweli kwamba walikuwa na mapungufu makubwa ktk usimamiaji wa uchumi wa nchi.
Ndio maana, mkuu 'Msuluhishi' kakwambia kwamba unatoa "Mahitimisho' bila ya maelezo katika jambo ambalo ni 'complicated' kama hili la uchumi. Huu hapa ni mfano mzuri.
 
..nakumbuka sana.

..lakini Sokoine alipowakamata haikufanya bidhaa zifurike madukani na foleni ziishe.

..viwanda vyetu vilikuwa havizalishi bidhaa za kutosha.

..Sokoine hata kama alikuwa na nia nzuri hatua alizochukua hazikuleta matokeo chanya.

..Na zaidi hatua alizochukua hazikuzingatia RULE OF LAW.
President Julius Nyerere listens to Primier



Vyombo vingi vya habari vya nje vilielezea ajali na kifo chake kwamba aliuawa.

TANZANIAN PREMIER IS KILLED

13/4/1984
TANZANIAN PREMIER IS KILLED; WAS LEADER'S HEIR APPARENT TANZANIAN PREMIER IS KILLED; WAS LEADER'S HEIR APPARENT?
Reuters


Hizi siasa za Afrika ni siasa mbaya sana na ndizo zimepoteza viongozi wengi wazuri na ambao kama wangeendelea kuwepo, basi baadhi ya nchi nyingi za Afrika ikiwepo Tanzania zingekuwa mbali kimaendeleo.

Hayati Mwalimu alianza kuzungumzia kustaafu siasa tangu katikati ya 1980 na hapo ndipo mapigano ndani ya corridors of power yalipoanza.

Kwa kwa mtizamo wangu ni kwamba hayati Sokoine huenda alitumia hiyo vita ya wahujumu uchumi kutaka kujijenga kisiasa na hivyo kusababisha mtafaruku ndani ya CCM ambamo kuna wanasiasa wengine walitamani kuwa maraisi.

Hivyo kufikia mwaka 1983 kuna viongozi kadhaa waandamizi ambao walianza kutajwa na miongoni mwao alikuwemo hayati Sokoine, hayati Rashid Kawawa na Aboud Jumbe Mwinyi, Cleopa Msuya na mzee wetu Salim Ahmed Salim.

Kumbuka Sokoine alifariki akiwa mdogo sana at 46 na hao wazee walikuwa mbele yakle kisiasa na kiuzoefu.

Kuna kitabu chaitwa The Dark Side of Nyerere Legacy ambacho kimeandikwa na Ludovick Mwijage na anaeleza mengi.

Ila naunga mkono juhudi za hayati Sokoine katika kuhakikisha kwamba hakuna wahujumu uchumi na walanguzi wa bidhaa kwa wakti ule.

Hivyo hata sasa tukiona kiongozi anapambana na nguvu nyingi za fedha na bidhaa kufichwa na kisha baadae akaja hadharani kubainisha majaribu juu ya I=uahi wake basi wapata fursa nzuri ya kuwaelewa wale wote wasoitakia mema nchi yetu.

Nina mengi sana ya kuyaeleza lakini naomba niishie hapo.
 
Ndio maana, mkuu 'Msuluhishi' kakwambia kwamba unatoa "Mahitimisho' bila ya maelezo katika jambo ambalo ni 'complicated' kama hili la uchumi. Huu hapa ni mfano mzuri.

..hata nyinyi mnaosifia mnatoa sifa za jumla-jumla ktk masuala ambayo ni complicated.
 
Tukiendelea na mijadala mingine nimeonelea niwashikilishe video hii. Nimeulizwa mara kwa mara kuhusu video/ audio ya Edward Sokoine. Katikati upekuzipekuzi wangu nimekutana na hii. (Kuna mtu aliniuliza chemba kuwa angependa kumuona na kumsikia Sokoine) badala ya kusoma tu habari zake. Hii ni miongoni mwa video nzuri nilizopata kuziona au kuzisikia.


Alikijua kizungu? Yan kiingereza kimempiga tu chenga Magufuli Mungu wangu😀
 
President Julius Nyerere listens to Primier



Vyombo vingi vya habari vya nje vilielezea ajali na kifo chake kwamba aliuawa.

TANZANIAN PREMIER IS KILLED

13/4/1984
TANZANIAN PREMIER IS KILLED; WAS LEADER'S HEIR APPARENT TANZANIAN PREMIER IS KILLED; WAS LEADER'S HEIR APPARENT?
Reuters


Hizi siasa za Afrika ni siasa mbaya sana na ndizo zimepoteza viongozi wengi wazuri na ambao kama wangeendelea kuwepo, basi baadhi ya nchi nyingi za Afrika ikiwepo Tanzania zingekuwa mbali kimaendeleo.

Hayati Mwalimu alianza kuzungumzia kustaafu siasa tangu katikati ya 1980 na hapo ndipo mapigano ndani ya corridors of power yalipoanza.

Kwa kwa mtizamo wangu ni kwamba hayati Sokoine huenda alitumia hiyo vita ya wahujumu uchumi kutaka kujijenga kisiasa na hivyo kusababisha mtafaruku ndani ya CCM ambamo kuna wanasiasa wengine walitamani kuwa maraisi.

Hivyo kufikia mwaka 1983 kuna viongozi kadhaa waandamizi ambao walianza kutajwa na miongoni mwao alikuwemo hayati Sokoine, hayati Rashid Kawawa na Aboud Jumbe Mwinyi, Cleopa Msuya na mzee wetu Salim Ahmed Salim.

Kumbuka Sokoine alifariki akiwa mdogo sana at 46 na hao wazee walikuwa mbele yakle kisiasa na kiuzoefu.

Kuna kitabu chaitwa The Dark Side of Nyerere Legacy ambacho kimeandikwa na Ludovick Mwijage na anaeleza mengi.

Ila naunga mkono juhudi za hayati Sokoine katika kuhakikisha kwamba hakuna wahujumu uchumi na walanguzi wa bidhaa kwa wakti ule.

Hivyo hata sasa tukiona kiongozi anapambana na nguvu nyingi za fedha na bidhaa kufichwa na kisha baadae akaja hadharani kubainisha majaribu juu ya I=uahi wake basi wapata fursa nzuri ya kuwaelewa wale wote wasoitakia mema nchi yetu.

Nina mengi sana ya kuyaeleza lakini naomba niishie hapo.

..Nyerere alikuwa akimpenda nani zaidi kati ya Sokoine na Salim Salim?

..Mzee Kawawa hakuwa anautamani Uraisi.


..Kawawa alibebeshwa misalaba ya watu wengine na hakuwa na kinyongo.
 
..Nyerere alikuwa akimpenda nani zaidi kati ya Sokoine na Salim Salim?

..Mzee Kawawa hakuwa anautamani Uraisi.


..Kawawa alibebeshwa misalaba ya watu wengine na hakuwa na kinyongo.

Nafikiri aliwapenda wote.

Sokoine JMT na Salim kwa Zanzibar.

Rejea kesi ya A. Jumbe ilopelekea kulazimishwa kujiuzulu.
 
..hata nyinyi mnaotoa SIFA ZA JUMLA-JUMLA hamuwatendei haki Mwalimu Nyerere na Edward Sokoine.

..sikatai kwamba walikuwa wazalendo, lakini tuseme ukweli kwamba walikuwa na mapungufu makubwa ktk usimamiaji wa uchumi wa nchi.

NB.

..unayafahamu makosa ya Mwalimu Nyerere yaliyosababisha kilimo cha mkonge na korosho kiporomoke?
Mkuu JokaKuu ni kweli kabisa Nyerere na Sokoine kwa namna fulani walifanya makosa katika ujenzi wa uchumi wetu.
Lakini nadhani hata upungufu wa wataalamu wa kutosha ulichangia mengi kwenda kombo maana ukichunguza hawakuwa na dhamira chafu kama hawa wa sasa.
Wataalamu wa kutosha lakini hawatumiwi na wakitumiwa hawasikilizwi. Wizi sasa hivi umekuwa wa kimtandao unao ongozwa na chama kama alivyo weka hadharani Mkapa.
EPA na Escrow ni wizi wa kuifanya ccm ibaki madarakani. Ndio maana hata ripoti ya CAG kuhusu 1.5 trillion zisizo onekana CCM badala ya kuisimamia serikali itoe majibu yenyewe ndio inatetea hadi kumtuma Polepole akokotoe eti hesabu za CAG kuwa hajui matumizi ya hiyo hela!
Kwa hiyo pengine nchi wakati huo ingekuwa na wataalamu kama sasa mambo yangekuwa mengine tofauti na haya ma batch ya manyang'au yaliyo madarakani
 
Nafikiri aliwapenda wote.

Sokoine JMT na Salim kwa Zanzibar.

Rejea kesi ya A. Jumbe ilopelekea kulazimishwa kujiuzulu.

..nimeuliza alikuwa akimpenda yupi zaidi ya mwenzake?

..alimpenda Sokoine zaidi, au alimpenda Salim Salim zaidi?
 
Asante sana, Mleta mada. Nimefarijiaka haswa. Mungu akubariki.
 
Back
Top Bottom