JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

FB_IMG_1688873856540.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siisemi kwa kuteta naasema hadharani
Kinachonifanya niseme ni kilio cha rohoni
Naa kiu ya kusubiri jibu lako ooh ( Max Bushoke )
FB_IMG_1688874943289.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sijui sababu gani likaitwa hivyo wahenga naomba tufamishane
Liliitwa bomba la muhimbili
Zamani tulipokuwa wadogo starehe yetu mwisho wa wiki au mwezi wa ramadhani kwenda ferry
Basi lazima tutembeee kwenye hili bomba wakati maji yametoka tatizo wakati maji yanarudi ilikuwa hatari sana
Wahenga wengi wanakumbuka kuhusu michezo yetu ya hatari
FB_IMG_1688883448332.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Juma Thomas Zangira mtanzania wa kwanza kushtakiwa kwa kesi ya ujasusi nchiniView attachment 2676802
JUMA THOMAS ZANGIRA: MTANZANIA WA KWANZA KUSHTAKIWA KWA KOSA LA UJASUSI (ESPIONAGE)


1. Usuli:

Takribani miongo minne na ushee hivi iliyopita, ilitokea kesi ya Ujasusi iliyomkabili Mtanzania, Juma Thomas Zangira. Kesi hiyo ya kihistoria na ya aina yake ilimstua si tu aliyekuwa Rais wa Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Baraza zima la Mawaziri, bali pia ilizua kimuhemuhe kikubwa nchini na ilitaradadi vilivyo kwenye vyombo vya habari enzi hizo; Radio Tanzania Dar Es Salaam (RTD) na magazeti ya Uhuru, Mzalendo, Daily News & Sunday News.

Leo, Jumamosi tulivu ya Julai 1, 2023, ikiwa imetimia miaka 46 toka SASP Ali Juma Guguru apokee taarifa za kiintelligentsia Julai 27, 1977 kuwa Bw. Zangira alikuwa anajihusisha na ujasusi uliokuwa ukimpatia maokoto, "Mzee wa Atikali" amewiwa kuielezea kiunagaubaga kesi hiyo iliyokuwa kesi ya kwanza ya Ujasusi nchini.
"Mzee wa Atikali", kwa kutumia hadubini yake, amefukunyua makavasi na makabrasha anuai na kupata habari kedekede kuhusu kesi hiyo. Aidha, "Mzee wa Atikali " amedahili na kufanikiwa kupata taarifa nyingi za kusisimua toka kwa waliohusika kwa namna moja au nyingine na mchakato wa kesi hiyo.


2. Wasifu wa JUMA THOMAS ZANGIRA

Bw. Juma Thomas Zangira alikuwa ni Afisa Uhusiano wa Kilimanjaro hotel, Afisa Usalama wa Taifa na mmoja wa Watanzania wachache waliokuwa wamepata mafunzo ya aina yake ya ukomandoo toka nchi mbalimbali duniani. Huyu alikuwa ni Komandoo aliyewiva ambaye alikuwa shupavu sana na mwenye ujuzi mkubwa wa mapambano katika ukanda huu wa Afrika. Mkono wake wa kushoto ulikuwa na nguvu kama bondia hodari wa zamani wa Marekani, Sonny Liston. Aidha, Bw. Zangira alikuwa ni mbobevu sana kwenye masuala ya intelligentsia na alikuwa ametunukiwa nishani nyingi kwa umahiri wake. Hivyo, alikuwa ni tegemeo kubwa kwa Taifa lake la Tanzania.

Kutokana na unyeti wa kazi zake, serikali ilimfungulia ofisi ya "Travel Agency" ya kupokea na kusafirisha wageni wa nje, pale "Ground floor" ya Kilimanjaro hoteli.

Miaka ya 1960s & 1970s, Tanzania ilikuwa kiota cha wapigania uhuru toka nchi za Kusini mwa Afrika na Makao makuu ya Kamati ya Ukombozi ya Afrika yalikuwa Dar es Salaam. Hii ilipelekea vyama vya ukombozi Kusini mwa Afrika kufungua ofisi zao hapa nchini mf. FRELIMO, ZANU, SWAPO, PAC & ANC na viongozi wengi wa nchi hizo waliishi nchini mf Edward Mondlane, Samora Machel, Robert Mugabe, Sam Nujoma nk. Viongozi hawa na wageni mbalimbali walikuwa hawakauki hotelini Kilimanjaro. Hivyo, ofisi ya Bw. Zangira iliwekwa pale mahsusi ili kupata taarifa mbalimbali nyeti na yeye akawa ndiye jicho na sikio la serikali.

3. Taarifa ya Ujasusi wa Bw. ZANGIRA

Jumatano, Julai 27, 1977, saa 1.30 asubuhi, SASP Guguru alipokea taarifa za kiintelligentsia kuwa Bw. Zangira alikuwa akijihusisha na ujasusi!. SASP Guguru alipigwa na butwaa na awali hakuamini maskio yake!. Ilielezwa kwamba badala ya kutafuta na kuchakata taarifa za wageni zenye ukakasi ili ziisadie serikali, Bw. Zangira alikuwa anasaka siri za serikali na za vyama vya ukombozi na kuzituma kwenye mataifa ya Kusini mwa Afrika.

4. "Surveillance Team" Yaundwa

Baada ya kupatikana taarifa hizo, ikaonekana kwamba kwavile Bw. Zangira ni Komandoo mahiri, isingekuwa busara kumuendea kichwakichwa. Hivyo, ikabidi mpango kamambe uandaliwe. Hatimaye, ikakubalika iundwe timu "Surveillance Team" ili kumnasa. Timu hiyo ikaundwa mara moja ikiwa na wajumbe toka taasisi mbalimbali likiwemo Jeshi la Polisi. Abdallah Msika, ambaye wakati huo alikuwa "Detective Sergeant" kabla ya kuja kuwa Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi miaka ya hivi karibuni kabla hajastaafu, ndiye aliyeteuliwa toka Jeshi la Polisi. Bw. Msika alikuwa amesoma hadi darasa la 8 "Malangali Middle School" kisha akaenda "Nursing" Muhimbili kabla ya kujiunga na Jeshi.

Timu hii ikajiapiza kuwa, aslan abadan, ni lazma ifanikishe jukumu hilo kwa weledi na uzalendo mkubwa kwa Taifa lao. Kisha, ikatayarisha adidu za rejea na kuanza kufuatilia kwa ukaribu nyendo zote za Bw. Zangira toka alipokuwa akitoka nyumbani kwake asubuhi hadi usiku. Bw. Zangira alikuwa akiishi mtaa wa Nkrumah ambako kulikuwa na ghorofa lililokuwa makao makuu ya FRELIMO, mkabala na "Co-Cabs", yeye akikaa ghorofa ya pili. Timu ilikuwa na magari na ilifanya kazi kwa zamu isipokuwa Msika ambaye alilazimika kuwepo muda wote kwani ndiye aliyekuwa na jukumu la kumkamata.

5. Barua za Bw. ZANGIRA Zanaswa

Timu ilifanikiwa kubaini kwamba Bw. Zangira alikuwa akiwasiliana na genge lake lililokuwa nje ya nchi kwa njia ya posta. Hivyo, barua zake zote alizokuwa akituma na alizokuwa akitumiwa kama majibu zilikuwa zinatolewa kopi na kurudishiwa kwa ustadi mkubwa.

6. Bw. ZANGIRA Akamatwa Kininja !

Baada ya Timu kumfuatilia Bw. Zangira kwa muda mrefu na kukusanya ushahidi usio na mawaa, Timu ilitoa taarifa na mara moja ikatolewa amri akamatwe.

Siku ya ukamatwaji, Timu hiyo ilifika nyumbani kwake na kumsubiri kwa nje. Akiwa hajui hili wala lile, Bw. Zangira alianza kuelekea kazini kwake hoteli ya Kilimanjaro kupitia Posta. Timu ikawa inamfuata huku ikihakikisha kuwa lije jua, ije mvua lazma Bw. Zangira awekwe chini ya ulinzi. Bw. Zangira alipofika eneo la Posta mpya, akaenda yaliko masanduku ya barua. Msika, aliyekuwa amefundishwa vilivyo jinsi ya kumkabili na namna ya kukwepa mkono wake hatari wa kushoto, akawa anamnyatia kwa umakini wa hali ya juu. Bw. Zangira, kwa bashasha kubwa, akaitoa barua toka kwenye sanduku la barua. Afanalek, ile anageuka tu ili aondoke, ghafla Msika akamvaa na kumwambia "hands up" huku wale wenzie nao wakisogelea huku wakimuonesha Bw. Zangira mitutu ya bunduki! Ilikuwa ni kama sinema ya "James Bond 007"!. Bw. Zangira akanywea kama kobe aingizavyo kichwa ndani ya jumba lake!. Ukomandoo wote ukawa kwishnei na akawa anafuata kila alichoelezwa. Akatii sheria bila shuruti! Hatimaye, aliingizwa ndani ya gari huku akitweta na akiwa chini ya ulinzi mkali ambapo watu wawili walikuwa kushoto na wawili kulia kwake "sandwich"!.

Alipofikishwa "Central Police Station" ikaamuliwa akasachiwe nyumbani kwake. Zoezi hilo lililoongozwa na Maafande, Alfred Tibaigana na Adadi Rajab, lilifanyika kama utaratibu wa sheria unavyoeleza. Kisha, Bw. Zangira alihojiwa na akapelekwa gereza lenye ulinzi mkali la Ukonga.

7. RTD Yamtangaza Bw. ZANGIRA !

RTD ikautangazia umma kukamatwa kwa Bw. Zangira kwa tuhuma za ujasusi. "Bongolanderz" nchi nzima hawakuamini kile walichokuwa wakikisikia toka redioni kwani hawakuwahi kusikia tukio kama hilo na hawakujua Tanzania ina Jasusi !.

Kesho yake, magazeti ya "Uhuru" na "Daily News" yakaeleza jinsi Rais Nyerere na Baraza zima la Mawaziri lilivyosikitishwa na mkasa huo. Baada ya hapo, taratibu zote muhimu za kuitayarisha kesi zikataradadi.

Siku ya Jumapili, Septemba 25, 1977, RTD, katika taarifa yake ya habari saa mbili usiku, ikaeleza kwamba Bw. Zangira atapelekwa mahakamani kesho yake, Jumatatu. Kisheria, Ujasusi ni kosa kubwa ambalo ni lazma lisikilizwe na Mahakama Kuu na lazma wawepo Wazee wa Baraza kumsaidia Jaji kama yalivyo makosa mengine makubwa kama vile Mauaji au Uhaini .

8. Bw. ZANGIRA Afikishwa kwa Pilato

Jumatatu kuntu ya Septemba 26, 1977, Bw. Zangira alifikishwa Mahakama Kuu, toka gereza la Ukonga akiwa amefungwa pingu na akiwa chini ya ulinzi mkali.

Kutokana na upekee na unyeti wa kesi hii, ilibidi Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP)wa wakati huo, Bw. Damian Meela, aiendeshe mwenyewe kesi hiyo. Aidha, kutokana na ukweli kwamba kesi hiyo ilikuwa ni ya aina yake, ikabidi isikilizwe na Jaji Mkuu wa wakati huo, Mhe. Francis Nyalali, mwenyewe. Mhe. Nyalali alisaidiwa na Wazee wa Baraza watatu ambao ni Bw. Zuberi Ally, Bw. Hussein Hamis na Bw. Simba Salum. Bw. Zangira alikuwa akitetewa na wakili mashuhuri Thomas Mkude, wa lililokuwa Shirika la Sheria Nchini (TLC). Wakili Msomi Mkude baadaye alikuja kuwa "Chief Corporation Counsel" wa TLC na kisha akawa Katibu Mkuu Wizara ya Sheria na Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na kisha akaja kuwa Jaji wa Mahakama Kuu. Hivyo, walioshiriki kwenye kesi hiyo iliyomkabili Bw. ZANGIRA walikuwa "WAMBA" watupu !.

9. Kesi ya Bw. ZANGIRA Yarindima !

Siku ya kwanza ya kesi, Septemba 26, 1977 saa 3 asubuhi, umati mkubwa wa "Bongolanderz" ukiwa umefurika mahakamani, DPP Meela alimsomea Bw. Zangira Mashtaka Matatu :

Shtaka la Kwanza lilikuwa ni Kukusanya Habari kisha kuzitoa kwa raia wa Uingereza aliyeitwa John Wilson kwa nia ya kuvuruga usalama wa nchi yetu na kwamba taarifa hizo zingeweza kutumiwa na mataifa ya nje yanayoichukia Tanzania kuvuruga usalama wa nchi yetu.

Kosa la Pili lilikuwa ni Kumpatia Bw John Wilson habari ambazo zingeharibu jitihada za TANU na vyama vya ukombozi vya SWAPO, FRELIMO, PAC, ANC na ZANU.

Kosa la Tatu lililokuwa ni Kutoa Taarifa za OAU kwa John Wilson.

Mashtaka haya yote matatu yalidaiwa ni kinyume na Kifungu cha 9(1)(a) na 9(2)(1), Sheria ya Usalama wa Taifa, 1970.

Katika kesi hiyo, Bw. Zangira alikana mashtaka yote hayo matatu ambayo ilidaiwa aliyatenda kati ya mwaka 1971 na 1977. DPP Meela akaita mashahidi nane.

Shahidi wa kwanza alikuwa ni SASP Ali Juma Guguru ambaye alieleza kwamba Julai 27, 1977 alipokea habari za ujasusi na ikaundwa timu. Moja ya majukumu ilikuwa ni kuchunguza nani alikuwa anatumia sanduku la posta Na. 3900 DSM. D/Sergeant Abdallah akatumia mbinu za medani na kugundua kwamba aliyekuwa analitumia si mwingine bali ni Bw. Zangira.

SASP Guguru alieleza kuwa siku tatu tu baadaye, yaani Julai 29, 1977, saa 2 asubuhi, Bw Zangira aliondoka nyumbani kwake akawa anaenda ofisini kwake Kilimanjaro hoteli kwa kupitia Posta mpya bila kujua kuwa alikuwa anafanyiwa "surveillance" kali ya nyendo zake.

Bw. Zangira alipofika Posta akafungua sanduku lake la barua na akachukua barua moja aliyoikuta. Kufumba na kufumbua, akakamatwa na polisi! Bw. Zangira alikiri kuwa barua hiyo ni yake na ilipofunguliwa ilikuwa na £ 150. Barua hiyo ilikuwa imeandikwa na John Wilson wa Parkside, Derry Hills, Calne, Wits, UK ikimtaka Bw. Zangira atafute na kumpa habari juu ya namna uhusiano kati ya China na Tanzania ulivyokuwa ukiharibu uhusiano wa Tanzania na majirani. Pia ilimtaka aeleze kuhusu vyama vya ukombozi ambavyo makao yake makuu yalikuwa Dar es Salaam. Aidha, ilimtaka kutotumia jina lake halali na kwamba atalipwa £ 150 kwa mwezi na akileta habari zaidi ataongezwa.

Nyumba ya Bw. Zangira ilisachiwa na ofisi yake nayo ilisachiwa na zikapatikana barua 33. Barua zote hizo zilipokelewa mahakamani kama vidhibiti. Ilibainika kwamba Bw. Zangira alikuwa anatuma barua kwenda Uingereza kwa Bw. John Wilson. Barua inapofika kule, huwekwa bahasha mpya na kutumwa mataifa ya Kusini mwa Afrika. Aidha, mtiririko huo huo hufuatwa barua zitumwapo kwa Bw. Zangira.

Barua ya kwanza iliandikwa tarehe 29.11.1971 na ikafuatiwa na zingine tarehe 18.2.1972, 29.2.1972, 11.3.1972, 25.3.1972 na 12.4.1972. Barua hizo zilihabarisha taarifa mbalimbali za kijasusi huku zilionesha Bw. Zangira alikuwa ametumiwa jumla £ 485. Baadhi ya barua hizo zilikuwa zikimpongeza Bw. Zangira kwa kazi nzuri alizokuwa amefanya na zingine zikimlaumu kwa kukaa kimya kwa muda mrefu. Zingine zilimtaka atoe habari za OAU na ziliko kambi za wapigania uhuru nchini. Aidha, zingine zilimtaka aeleze kama Rais Julius Nyerere alikuwa akipendwa na wapigania uhuru na ni Mtanzania gani angekuja kuchukua nafasi yake.

Bw. Zangira pia alitakiwa kutoa taarifa za ofisi zote za ubalozi na maeneo ziliko na ni zipi zinawaunga mkono wapigania uhuru. Barua hizo pia zilionesha alikuwa akipokea fedha mara kwa mara na kuna wakati alimwandikia Bw. John Wilson akiomba apewe fedha za kujengea nyumba na kununua gari kutokana na kazi kubwa aliyokuwa ameifanya ya kupeleka taarifa nyeti. Alijibiwa kwamba apekeke "Account No" na avute subira. Mwisho, barua zilionesha pia alisafiri kwenda Kenya (22.7.1974) na Malawi (7.4.1976) ambako aliambiwa na John Wilson hoteli ya kufikia na watu atakaokutana nao.

Baada ya kesi hiyo kusikilizwa kwa siku nne mfululizo, Upande wa Mashtaka ulimaliza kuita mashahidi wake hivyo ukafunga kesi yake.

10. Bw. ZANGIRA Aanza Kujitetea

Ijumaa, Septemba 30, 1977, Bw. Zangira akaanza kujitetea. Katika utetezi wake, Bw. Zangira alikiri kuwa barua hizo zote ni zake na kweli alikuwa akimuandikia barua Bw. John Wilson ila alikuwa akifanya hivyo kama Mwandishi wa Habari kwani hizo zilikuwa ni habari za kawaida tu na zikipatikana magazetini. Aidha, alidai habari alizokuwa akituma zilikuwa za biashara tu. Alieleza zaidi kuwa zamani alikuwa akifanya kazi Subuzani Tours & Safaris, Arusha ambako alikuwa akipeleka watalii mbugani.

Bw. Zangira alieleza kuwa mwaka 1971 alimpeleka mtalii Wiltshire Mikumi na kwamba Bw. Wiltshire alimwambia ana rafiki yake yuko Uingereza anatafuta Mwandishi wa habari hivyo akampa Bw. Wiltshire "Contacts" zake. Baada ya wiki chache akaanza kupokea barua kutoka kwa Bw. John Wilson. Alieleza zaidi kuwa alikuwa akilipwa kwa habari zote alizokuwa akipeleka toka 1971 hadi 1977.

Bw. Zangira alizua kicheko mahakamani alipoeleza kuwa alishangazwa alipostukia anakamatwa, yeye akiwa Mwandishi wa habari, asubuhi ya Julai 29, 1977 mara tu baada ya kuchukua barua toka kwenye sanduku lake la barua iliyotoka kwa John Wilson. Huo ndio ukawa mwisho wa utetezi wake.

11. Wazee wa Baraza Watoa Maoni

Mhe Jaji Mkuu Nyalali aliwafafanulia Wazee wa Baraza maelezo yote ya kesi na akauchakata ushahidi na kisha akawataka watoe maoni yao. Baada ya hapo, Wazee wawili (Simba Salum na Hussein Hamis) walitoa maoni kuwa wanaona ushahidi umethibitisha mashtaka wakati Mzee wa tatu (Zuberi Ali) aliona mashtaka hayakuthibitishwa.

Mhe. Nyalali akaihairisha kesi hiyo hadi Jumatano, Oktoba 5, 1977 ambayo ilipangwa kuwa ndiyo siku ya hukumu.

12. "Bongolanderz" Waisasambua Kesi

Kwavile "Bongolanderz" nchi nzima, toka Naliendele- Mtwara hadi Kahororo- Bukoba, walikuwa wakiifuatilia kwa umakini kesi hii, kila mmoja alikuwa akitoa maoni yake kuhusu hatma ya Bw. Zangira kwa kuzingatia ushahidi uliokuwa ukitolewa mahakamani kwa mujibu wa magazeti yaliyokuwa yakiripoti kesi hiyo.

12. Bw. ZANGIRA Atiwa Hatiani

Siku ya hukumu, asubuhi na mapema, "Bongolanderz" lukuki walifika Mahakama Kuu kujionea wenyewe kitakachojiri. Ulinzi ulikuwa mkali sana na wote waliotaka kuingia ndani, walisachiwa sana. Kufumba na kufumbua, Mahakama ikawa imejaa hadi pomoni. Hatimaye, Mhe. Nyalali akasoma hukumu iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu. Hukumu hiyo iliyoandikwa kwa weledi mkubwa ilikuwa ndefu na ilimchukua Mhe Nyalali masaa matatu kuimaliza. Mwishowe, Mhe Nyalali alimtia hatiani Bw. Zangira kwa makosa yote matatu aliyoshtakiwa nayo.

Mhe Nyalali, pamoja na mambo mengine, alieleza:

"John Wilson alikuwa ni jasusi aliyekuwa akitumiwa na mataifa fulani ili kuangamiza usalama wa Taifa letu. Utetezi wa Bw. Zangira kuwa alikuwa akimtumia Bw. Wilson habari za biashara hauna hoja. Hizo habari hazikuwa za kumfaa mfanyabiashara yeyote bali haini Smith na kaburu Vorster wa Afrika Kusini. Vilevile, kama ni za biashara iweje atakiwe kutumia jina bandia? Tanzania ni moja ya nchi zilizo mstari wa mbele Kusini mwa Afrika hivyo kitendo cha Zangira kutoa siri za vyama hivyo na OAU ni sawa na Uhaini".

12. DPP Aomba Adhabu Kali

Baada ya Mhe. Nyalali kumtia hatiani Bw. Zangira, DPP Meela aliiomba mahakama itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine hasa ukizingatia umuhimu wa Tanzania kwenye ukombozi wa Kusini mwa Afrika.

13. Wakili MKUDE Aomba Huruma

Bw. Mkude aliiomba mahakama imhurumie mteja wake na izingatie ukweli kwamba hilo lilikuwa ni kosa lake la kwanza na pia alikuwa akitegemewa na nduguze.

14. Bw. ZANGIRA Afungwa Miaka 20

Mhe Nyalali, baada ya kusikiliza na kuzingatia kwa makini maelezo ya DPP Meela na Wakili Mkude, alitoa kifungo cha miaka 20 !. Urefu wa kifungo hiki ulishangaza "Bongolanderz" wengi kwani kifungo cha urefu huo kilikuwa hakijazoeleka enzi hizo. Mara baada ya kuhukumiwa, ndugu, jamaa na marafiki wa Bw. Zangira walitoka mahakamani na simanzi kubwa huku Bw. Zangira akichukuliwa chini ya ulinzi mkali kwenda kuanza maisha mapya Lupango!


15. Tamati

Hii ndio kesi ya kwanza ya Ujasusi nchini na leo, Julai 1, 2023, imetimia miaka 46 toka taarifa za kiintelligentsia zilifikie Jeshi la Polisi kuwa Bw. Juma Thomas Zangira, Komandoo aliyekuwa akiaminiwa sana na serikali, alikuwa anakengeuka majukumu yake na akawa Jasusi, kazi aliyoifanya kuanza mwaka 1971. Kama Wahenga walivyonena "Za Mwizi ni 40", hatimaye akakamatwa mwaka 1977 na kupewa Mvua 20.


Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante sana mkuu.
 
Marijani Rajabu (3 Machi 1955 - 23 Machi 1995) alikuwa mwanamuziki maarufu katika miondoko ya muziki wa dansi kutoka nchini Tanzania.

Marijani Rajab enzi ya utoto wake


Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa

Marijani Rajabu
Amezaliwa
Machi 3, 1955
Kariakoo, Dar es Salaam, Tanzania


Asili yake
Kigoma, Tanzania

Amekufa
23 Machi, 1995
Dar es Salaam, Tanzania

Aina ya muziki
Muziki wa dansi

Miaka ya kazi
1970-1995
Studio
RTD
Ame/Wameshirikiana na
The Safari Tripers


Historia yake na muziki

Kushoto mwenye miwani David Musa, wa tatu Marijani Rajabu na kulia mwisho Jumanne Uvuruge mtunzi wa wimbo wa Georgina.

Historia ya gwiji huyu ilianzia siku alipozaliw,a tarehe 23 Machi mwaka 1955, katika eneo la Kariakoo. Mama yake alikuwa mama wa nyumbani wakati baba yake alikuwa anafanya shughuli za uchapishaji. Maisha yake ya utoto yalikuwa ya kawaida ila alikuwa akipenda sana uimbaji wa Tabu Ley na mwimbaji mmoja wa Guinea Sorry Kandia. Alisoma shule ya Msingi ikiambatana na elimu ya Madrasa.

Mwaka 1970 Akiwa bado shuleni, utaona umri wake ulikuwa miaka 15 tu, alijiunga na STC Jazz, ikiwa chini ya mpiga gitaa maarufu wakati huo Raphael Sabuni, kabla ya hapo bendi hii ilikuwa ikijulikana kama The Jets.

Katika bendi hii Marijani aliweza kutoka nje ya Tanzania kwa mara ya kwanza ambapo alikwenda Nairobi na kurekodi nyimbo zilizotoka katika label ya Phillips. Hili jambo la mwanafunzi kusafiri na bendi likaleta shida na kwa vile (STC) ilikuwa mali ya umma akaachishwa kazi na mwaka1972 alijiunga na The Trippers ya David Mussa ambayo kwa wakati huo ilikuwa inapiga zaidi nyimbo za hoteli na za kukopi na muimbaji wao kiongozi wakati huo alikuwa Ali Rajabu.

Marijani akiwa na The Trippers

Hapa ndipo ubora wake ulifunguka haswa na kuweza kuinyanyua Trippers, ambayo sasa ilibadili jina na kuwa Safari Trippers kutokana na msimamo wa serikali wakati huo wa kutaka majina ya nyumbani yatumike bala ya yale ya kigeni na kuwa moja ya bendi maarufu za wakati huo. Waliweza kutoa vibao vilivyopendwa mfululizo na kuweza kuzunguka nchi nzima. Vibao kama Rosa Nenda Shule, Georgina, Mkuki Moyoni, viliweza kuuza zaidi ya nakala 10,000 za santuri na hivyo kuwezesha bendi kuwa na vyombo vyake vizuri.

Bendi wakati huo ikiwa na wanahisa wanne, ambao kwa bahati mbaya wakati bendi ndio iko juu, wakakosa kuelewana na ukawa ndio mwisho wa bendi hiyo. Marijani alishiriki kutunga, kuimba nyimbo karibu zote za Trippers sanjari na kupiga gitaa kwa baadhi ya nyimbo. Mfano wimbo Olila ambao alipiga rhythm na kuimba.

Marijani na DAR International

Mwaka 1976, Marijani na baadhi ya wanamuziki wa Trippers waliamua kuihama bendi na kwenda baadaye kuasisi Dar es salaam International chini ya umiliki wa Mzee Zakaria Ndabemeye. Baadhi ya wanamuziki hao ni pamoja na Abel Baltazar kutoka Msondo, Kassimu Mponda kutoka Trippers, Abdallah Gama, Joseph Mulenga,Haruna Lwali na George Kessy Omojo waliokuwa wanapiga muziki Magot pale, Said Mohamed kutoka Polisi Jazz, Cosmas Chidumule kutoka Urafiki, Belesa Kakere kutoka Biashara Jazz, Joseph Bernard kutoka Trippers, Ali Rajabu kutoka Trippers, na King Michael Enock kutoka Dar es Salaam Jazz.

Akiwa Dar Inter alishiriki kutunga nyimbo mbili, Betty na Sikitiko. Hata hivyo kama waswahili wanavyosema mafahari wawili hawakai zizi moja ndivyo ilivyotokea kati yake na Abel Balthazal kiasi cha hatimaye Marijani kufukuzwa ndani ya bendi kutokana na ubishi kuhusu wimbo aliotunga Marijani, kuna maelezo kuwa wimbo ulionekana unafanana na wimbo fulani toka Kongo na hivyo Marijani akatakiwa aubadilishe na ndipo ugomvi ukaanza.

Hata hivyo mwishoni mwa mwaka 1978, Marijani alirejeshwa tena kundini kutokana na rundo la wanamuziki wa Dar Inter kuihama bendi kwa kishindo kikubwa na kwenda kuifungua bendi mpya kabisa ya Orchestra Mlimani Park. Aliporejeshwa Marijani alikuja na wanamuziki wengi wapya wakati huo kama akina Christopher Kasongo, Mohamed Tungwa, Mafumu Bilal, Hamis Milambo, Athuman Momba, Mzee Alex Kanyimbo na wengine na kuja na mtindo wa Super Bomboka.

Katika kudhihirisha hasira zake kwa Abel, Marijani alimtungia Abel wimbo wa kumnanga ukiitwa Kidudu Mtu ambao hata hivyo RTD waliukataa kuurekodi, jambo lililokuwa kawaida enzi hizo kwa redio kukataa wimbo. Sifa nyingine ambayo Marijani alikuwa nayo ni kuibua wanamuziki chipukizi kama alivyofanya mwaka 1983 alipomuibua kutoka Tanga kijana Mkuu Waziri Kungugu Kitanda Milima almaaruf Fresh Jumbe ambaye kwa hakika kabisa Marijani hakujutia kumchukua kijana huyo.

Alimuamini kupita maelezo kiasi kwamba wakati mwingine alikuwa akimuachia bendi aongoze na yeye anapumzika nyumbani. Mbali na Fresh, wanamuziki wengine ni kama vile Tino Masinge, Mohamed Mwinyikondo, Juma Choka na wengine kibao. Baada ya kurekodi Zuena na Mwanameka na nyimbo nyingine katika album hiyo alichoambulia ni malipo ya nauli toka RTD ya sh 2500/- tu. Kilichosikitisha zaidi ni kuwa nyimbo zao tisa ziliuzwa kwa kampuni ya Polygram bila ridhaa yao.

Hata hivyo safari ya Dar International ilikoma mwaka 1987 kutokana na sababu za kawaida za kufa kwa bendi lakini kubwa ni uchakavu wa vyombo. Hata hivyo Marijani aliendelea kufanya muziki na kwa kipindi kifupi amewahi kucheza na Kurugenzi ya Arusha na Mwenge Jazz ambayo alirekodi nayo wimbo mmoja wa Ukimwi na hata kupitia bendi ya Watafiti ambayo hatimaye ilikuja kuwa 38..

Mwaka huohuo wa 1987 Marijani na Muhidin Maalim Gurumo waliliongoza kundi la wanamuziki zaidi ya 50 kutunga nyimbo maalum hasa kwa maadhimisho ya miaka 10 ya CCM na 20 ya Azimio la Arusha. Kundi hilo lilijulikana kwa jina la Tanzania All Stars. Aidha mwaka 1994 aliwahi kurekodi zong zing na marehemu Eddy Sheggy.

Bendi yake ya mwisho ilikuwa ni Africulture ama Mahepe Ngoma ya Wajanja, iliyokuwa mali ya Rogers Malila, alikokuwa na wanamuziki kadhaa kama akina Hassan Kunyata, Mgosi na wengine. Bado Marijani ataendelea kukumbukwa na wapenda muziki kote nchini na hata Afrika kwa ujumla kwa nyimbo zake zenye mafundisho na tamu huku akienzi utamaduni na ngoma za kwao Kigom
FB_IMG_1689528829887.jpg
FB_IMG_1689528826753.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom