JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

JF Photo Library: Mada maalum ya Picha za Zamani

FB_IMG_1727951002950.jpg
 
1. Hiyo picha ni msafara kwenda Monduli, Arusha kumzika aliyekuwa Waziri Mkuu wa tatu wa Tanzania, Edward Moringe Sokoine, 1984. Edward Moringe Sokoine alifariki April 12, 1984 kwa ajali ya gari. Hapo ni Uhuru Road, Arusha siyo Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

2.
20241013_021822.jpg
April 12, 1984 Edward Moringe Sokoine akitokea Dodoma kwa gari yake, Mercedes-Benz na msafara mkubwa uliosheheni magari ya usalama, aligongwa na gari (Land Cruiser) mali ya DUMISAN DUBE raia wa South Africa na kupelekea kifo chake.

3. Dumisani Dube alikuwa akitokea Mazimbu, alibeba chakula kwa ajili ya wakimbizi wenzake wa kisiasa kutoka South Africa waliokuwa wameweka kambi yao eneo la Dakawa. Waliendesha harakati zao za kupigania uhuru kutoka eneo la Mazimbu na Dakawa.

4. Ajali ilitokea saa 7 mchana. Msafara wa Sokoine ulikuwa ukitoka bungeni, Dodoma. Baada ya gari la Sokoine kupata ajali, magari mengine yaliyokuwa nyuma yaligonga gari hilo likiwa chini. Hali iliyochangia Sokoine kuumia zaidi na maumivu pamoja na dereva wake.

5. Dumisani Dube aliyumbisha gari na kumzubaisha dereva wa gari la Sokoine na hivyo kuacha njia na kupinduka. Maafisa usalama walimbeba Sokoine na dereva wake hadi Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu. Wote walikuwa hawajitambui.

6. Dumisani Dube alikuwa mwanachama wa African National Congress (ANC) na mpigania uhuru wa South Africa. Gari lake liligonga gari la Edward Moringe Sokoine eneo la Luhindo, Dakawa, Morogoro. ANC walifikiri uhusiano wao na Tanzania utatereka baadae.

7. Kumbuka; Wafuasi wa African National Congress (ANC) walikuwa wameweka kambi Mazimbu na Dakawa, Morogoro. Dumisani Dube alikuwa raia RSA. Rais wa ANC, Oliver Tambo na SG, Alfred Nzo walikwenda Arusha kuwakilisha ANC katika msiba wa Sokoine.

8. Dumisani Dube, ambaye alikimbilia Tanzania kutoka Afrika Kusini miaka ya ubaguzi na kujiunga na ANC, kundi linalopigana na ubaguzi wa rangi Afrika Kusini, alikiri shtaka la kuua bila kukusudia na kuomba msamaha kwa mahakama kwa kusababisha ajali hiyo.

9. Dumisani Dube hakuwa na leseni ya udereva (driving license) na alikiri kuendesha gari kwa uzembe na kusababisha ajali. Kesi hiyo ilifanyika Morogoro. Dumisani Dube alihukumiwa kutumikia kifungo cha miaka 13 gerezani kwa kusababisha ajali na kifo.

10. Dumisani Dube alikuwa akiendesha Toyota Landcruiser 1F. Gari hizo zilipachikwa jina la Dumisani Dube baada ya kifo cha Edward Moringe Sokoine. Alishikiliwa kwa muda, baadae alichiwa kwa msamaha na kurejeshwa nchini kwao, South Africa.

PS; Aina ya kifo chake, kwanini kuna hisia za kupangwa na siyo ajali, kwanini inahusisha succession struggles kuelekea 1985? Huo ni mjadala mwingine mpya wa muda mwingine. Huko tunaweza kuwajadili Rashid Kawawa, Aboud JUMBE na Cleopa Msuya na wengine.

MMM, Brigedia Mtikila.
 
Leo nimebahatika kupata picha ya kengele na mahali ilipokuwa hiyo kengele . Shule ya msingi niliyosoma
Nilipata hisia za ajabu mno.. Kumbukumbu za nyuma na marafiki wa utotoni🥵
Screenshots_2024-10-14-21-23-14.png
 
This was 1st Dec 1970, 𝗔𝗙𝗥𝗜𝗖𝗔𝗡 𝗙𝗜𝗘𝗦𝗧𝗔 𝗡𝗔𝗧𝗜𝗢𝗡𝗔𝗟 In Olympia show in Paris. After this show the name changes to 𝗔𝗙𝗥𝗜𝗦𝗔 𝗜𝗡𝗧𝗘𝗥𝗡𝗔𝗧𝗜𝗢𝗡𝗔𝗟 and some members left like Ndombe Opetum to form his band 𝗔𝗙𝗥𝗜𝗭𝗔𝗠.

From L to R; 𝐊𝐚𝐫𝐫𝐞 𝐌𝐮𝐰𝐨𝐬𝐨, 𝐏𝐞𝐩𝐞 𝐍𝐝𝐨𝐦𝐛𝐞 & 𝐑𝐨𝐜𝐡𝐞𝐫𝐞𝐚𝐮.

In the background, From L to R; 𝐋𝐨𝐤𝐚𝐬𝐬𝐚 𝐘𝐚 𝐌𝐛𝐨𝐧𝐠𝐨, 𝐌𝐢𝐜𝐡𝐞𝐥𝐢𝐧𝐨 𝐌𝐚𝐯𝐚𝐭𝐢𝐤𝐮 𝐕𝐢𝐬𝐢, 𝐀𝐭𝐭𝐞𝐥 𝐌𝐛𝐮𝐦𝐛𝐚 𝐊𝐢𝐚𝐤𝐨𝐧𝐝𝐮𝐚 & Drummist 𝐒𝐞𝐬𝐤𝐚𝐢𝐧 𝐌𝐨𝐥𝐞𝐧𝐠𝐚.

©️🅙︎🅐︎🅑︎🅤︎🅛︎🅐︎🅝︎🅘︎ 🅐︎🅡︎🅒︎🅗︎🅘︎🅥︎🅔︎🅢︎
FB_IMG_1732425598568.jpg
 
Back
Top Bottom