Jifungie zako ndani, tazama filamu hizi

Movie gan hizo?? Zaman nlikuwa napenda movie za aina hii ila kwa sasa nmeachana nazo..! Sasa napenda movie za ucheshi na stori za maisha...!
Kuna movie moja inaitwa THE BANKER itafute hii kama ww ni kijana mpambanaji bas itakutia moyo sana
Ya Denzel Washington?
 
Mkuu uko vizuri[emoji122][emoji122]
 
Daah hii kali
 
Mkuu unaonaje kama ungekuwa unatuwekea na links za ku-download kabisa maana sio wote humu wana utaalam wa kuzitafuta!!
Jaman njoon ofisini kwangu BoBmovies Sinza madukani ...buku lako tu[emoji16][emoji16]
 
Duuuh kazi ninayo...yaan haya ndo mambo yangu Wit[emoji848][emoji848][emoji15]
 
Inahusu nini mkuu?
NOPE (2022)


Mzee Otis anafariki kifo chenye kujawa na utata, kwa mujibu wa maelezo ya polisi mzee huyo alitobolewa na shilingi iliyodondoka toka juu angani, wakiamini shilingi hiyo ilitoka kwenye ndege ikamfikia mzee huyo jichoni na kumpasua ubongo.

Bada ya kifo hicho, watoto wawili wa marehemu Otis wanakaimu ranchi ya mzee wao kwa lengo la kuiendeleza hapo wakishughulika na kuwatazama na kuwafunza farasi ambao walikuwa wanawauzia Hollywood kwaajili ya maigizo.

Lakini biashara hii, mikononi mwa hawa watoto, haionekani kuwa na faida, pengine kwasababu warithi hawa hawakuwa na ujuzi kama ule alokuwa nao baba yao. Kwasababu hiyo basi, mtoto wa kike anaegemea zaidi kupata mwanya huko Hollywood huku kaka yake akitazamia namna ya kujikuza kiuchumi.

Muda si mrefu, watoto hawa wawili wanakuja kubaini kuna kitu cha kushangaza angani! ... Ni kama wingu kubwa hivi lakini lenye umbo la ajabu mithili ya ndege wanazotumia viumbe kutoka sayari zingine (UFOs), wingu hilo la ajabu linawaogopesha farasi wao wa kwenye ranchi na hata binadamu pia.

Kijana wa kiume, Otis junior, anaona kitu hiko kinaweza kuwa fursa kwao. Endapo wakifanikiwa kukirekodi kwenye kamera na kikathibitishwa kuwa ni kweli basi wanaweza kupata fedha nyingi sana kwasababu kuna tovuti na vyombo vingi vya habari vingeinunua habari hiyo.

Lakini kabla hawajaanza kupata hata senti mkononi, wanabaini wingu lile si kitu cha mzaha kabisa, ni zaidi ya kile walichokuwa wanakifikiria na kukitegemea. Ni kitu chenye njaa na roho za watu!

Mambo yanabadilika juu chini, chini juu, kwani sasa badala ya kuwaza kutengeneza pesa, wanahaha kutetea uhai wao ambao upo mashakani chini ya kitu ambacho huenda kilitoa uhai wa baba yao!





 
Duuh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…