Jifunze kilimo cha nyanya

Mkuu miche yangu nlopandikiza shamba majani yake yanaelekea kwnye rangi ya njano na kuna miche mingine imekufa kwa kuoza kuanzia chini mpk katikat ya mche

Ni ugonjwa gani huu na nafanyaje kuukabili,, Msaada wako tafadhali..
 
Mkuu miche yangu nlopandikiza shamba majani yake yanaelekea kwnye rangi ya njano na kuna miche mingine imekufa kwa kuoza kuanzia chini mpk katikat ya mche

Ni ugonjwa gani huu na nafanyaje kuukabili,, Msaada wako tafadhali..
Umepanda lini shambani? Mbona kama imepandwa vibaya haijashindiliwa vzr yani imechomekwa juu juu tu
Yani mengine hata udongo haina kwenye mizizi, nyanya ukipanda hovyo lazima ife nahisi ni tatizo ni upandaji wako
 
Mkuu miche yangu nlopandikiza shamba majani yake yanaelekea kwnye rangi ya njano na kuna miche mingine imekufa kwa kuoza kuanzia chini mpk katikat ya mche

Ni ugonjwa gani huu na nafanyaje kuukabili,, Msaada wako tafadhali..


Mosi naona haukupandia mbolea yaani hukuweka DAP sababu hutupa phosphate ya kukuza mizizi na ammonium ya kutupa nitrate itupe rangi ya majani na shina lenye afya. Pia baada ya siku tatu huwa tunaishtua na CAN ili iendelee kulipa shina afya zaidi.

Pili baada ya kupanda hukupiga dawa za ukungu,huwa tunachanganya ridomil gold gm 20 kwa lita 20 za maji kisha unanyesha kwenye shina la mmea,hii husaidia kuzuia fungus kushambulia shina la mmea wako

Tatu ulipandikiza zaidi ukavuka kiwango ambacho kilikua kwenye kitalu,hivyo udongo ukagusa shina la kijani changa la mmea hii hulea tatizo la soft rot,haina dawa huwa tunaikinga kwa kupanda usawa ule ule uliokua kitaluni na pia kwa kupiga ridomil gold. Tafuta miche mingine ya kujazia sababu tiba hapo hakuna.
Ahsante
 
Upo sahihi mkuu hata mm sijaona kama kuna ugonjwa hapo shida ni upandaji wake

Kuhusu mbolea mm uwa napanda nasubiri kama siku 3 kuangalia miche ipi imeshika na ipi imekufa, iliyokufa narudia kupanda baada ya hapo ndio naweka mbolea tena uwa nachanganya mbolea ya kupandia na kukuzia, nachanganya DAP,CAN na YARAMILA

Huyu anaoneka kosa lipo kwenye kupanda, kuanzia kutoa miche kwenye kitalu kupeleka shamba, unaweza usiweke mbolea miche ikakua ila kwa kuchechemea sio kufa kabisa kama miche ya huyu
 
Mche kama huu haujapandwa vzr, umechomekwa juu juu tu. Na shamba linaonekana udongo wake wa kichanga
 
Umepanda lini shambani? Mbona kama imepandwa vibaya haijashindiliwa vzr yani imechomekwa juu juu tu
Yani mengine hata udongo haina kwenye mizizi, nyanya ukipanda hovyo lazima ife nahisi ni tatizo ni upandaji wako
Ina siku 9 leo,,kuhusu upandaji sijajua mana kuna watu walinisaidia kupanda mi nlipanda miche michache, Ila pia udongo ni wa asili ya kichanga
 
Sawa mkuu, lakini mi nlipandia samadi ya ng'ombe nliyoweka wiki 1 kabla ya kupandikiza

Pili skustulia na Can na wala sijawah piga dawa yoyote toka niipandikize na leo ni siku ya 9 japo siku 1 kabla ya kupandikiza nlipiga belt zikiwa kitaluni

Tatu sasa kuhusu huo unjano na miche naiona km haina afya Nafanyaje mkuu?

Nne kuna mtaalamu amenambia ni Fungus na nipige Megasin kuzunguka shina na kwa juu pia, vp kuhusu hilo?

Ahsante.
 
Iliyokufa ni michache lkn tatizo kuu naloliona ni huu unjano kwenye majani mkuu, Nafanyaje ?
 
Iliyokufa ni michache lkn tatizo kuu naloliona ni huu unjano kwenye majani mkuu, Nafanyaje ?
Iliyokufa ing'oe panda upya, kama shamba lina kichanga kingi chimba shimo lefu kwenda chini
Unjano ni ukosefu wa mbolea, weka mbolea na mwagia maji mengi
 
Shukrani mtoa mada mimi nimelima mbegu aina hii
Na sasa ziko hivi kwenye kitalu
Na nyingine nimesha hamishia shambani ni hizi

Sasa ninajua ndio mbegu bora kulingana na muuzaji kumbe kuna bora zaidi aisee!
Lakini natoa shukrani kwa wadau nimepata elimu hapa nitajua pakuanzua.

Swali langu leo ni siku ya nne tokea kuandikiza, na huku dar kuna mvua inaendelea kunyesha je hazitaathirika?

Pili ni dawa gani nipige kuzuia wadudu na pia kama masika itazikuta zimeiva kuna athari ? Kila la heri.
 

Huo mchanganyiko unapoteza mbolea nyingi sana dap ina nitrate,can ina nitrate na kwenye npk kuna nitrate. Madhara ya nitrate ikizidi ni mmea unakua haraka sana but unazalia juu sana na matunda hafifu. Pia dap inapaswa iwekwe kabla ya kupanda ukichelewa ni siku unapanda sababu phosphate ni madini yanayotolewa taratibu na yanasafiri taratibu pia yanahitaji mapema sana ili ikuze mizizi,ukiweka dap mapema hata mimea mingi kufa itapungua sababu inahitaji chakula pale inapohamishwa.

Kuepuka huo mchanganyiko bora utumie otesha inamadini yote hayo maana ina npk
 

Mbolea ya ng'ombe ina madini kidogo sana yaani tani moja ya samadi ni sawa na mfuko wa kg 50 wa urea kwa kuangalia nitrate level ingawa hili pia hutegemea mfugo umelishwa nini.

Ukitaka ulime kwa kutumia samadi basi sqm 1 uweke ndoo moja kubwa means ekari moja ambayo ni sqm 4000 basi uweke ndoo elf 4 hapo utasema una samadi.

Huo unjano ni lack ya nitrate hivyo weka mbolea weka can au yara mila winner
 

Drench dawa ya ukungu itakusaidia sababu ndio suluhisho kwako ushauri wangu drench ridomil gild gm 20 kwa litre 20 za maji
 
Kuna aina mbili za mbegu za nyanya, kuna za kawaida na za kisasa au chotara "hybrid"

Sasa kwenye mbegu za kawaida zipo aina nyingi na hybrid pia zipo aina nyingi za mbegu
Ww umepanda mbegu ya kawaida mkulima, kwa mbegu za kawaida riogrand safari ndio mbegu nzuri sio hiyo mkulima ukiweza panda hybrid achana na mbegu za kawaida utatumia nguvu kubwa mapato yake yanakuwa madogo
 

Piga dawa ya ukungu yenye kiuatilifu cha kukinga na kutibu kama yenye ivory 72,ebony72,ridomil gild,linkomil,milraz,othelo top,score,ortiva etc
 
Nyanya kama hazitakufa mvua haiwezi kuathiri ila uwe unakagua sn shamba kila siku na upige dawa za wadudu

Hapo mavuno baada ya miezi mitatu inaweza kuwa masika imeisha au bado itategemea
 
Mkuu unaonekana upo vzr kwenye mbolea, nitakutafuta nikianza kupanda
 
Nyanya kama hazitakufa mvua haiwezi kuathiri ila uwe unakagua sn shamba kila siku na upige dawa za wadudu

Hapo mavuno baada ya miezi mitatu inaweza kuwa masika imeisha au bado itategemea
Nashuru sana mkuu, kila la heri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…