Jifunze kilimo cha nyanya

Jifunze kilimo cha nyanya

Wakulima salama? Mimi ni mkulima mtarajiwa wa nyanya, naomba ushauri wenu na uzoefu, nahitaji kulima nyanya kwny greenhouse, natarajia kuotesha kwny kitalu week mbili zijazo, sasa naomba msaada wa aina nzuri ya mbegu kwa ajili ya kilimo kwny greenhouse, lakini je nikiotesha nyanya kwny kitalu hadi kuvuna kwa mwezi huo wa pili je siwezi kukutana na mavuno ya msimu wa mvua? Hali na bei ya soko itakuwaje? Naomba uzoefu wenu wadau!

Ahsante sana !!

Sent from my HTC Desire 828 using JamiiForums mobile app

Habari

Vipi umepima udongo wa kwenye green house?

Muhimu upime haswa kujua kuhusu magonjwa haswa ya mnyauko bacteria au fungus hii itakuepusha na hasara kubwa sana ya baadae, ili kama kuna matatizo basi ujue utatumia system gani ya kilimo kama utasia direct kwenye udongo au kama utatumia mifuko na udongo wa kutibu.

Ukiwa na udongo usio na matatizo yoyote na ukipata mbegu bora unaweza vuna nyanya kwa miezi sita mpaka nane kwa hapa tunapoenda bei ya nyanya itashuka from mwezi wa nne mpaka wa tisa hivi na wewe ukisia sasa hivi utaanza kuvuna from mwezi wa tano ukiitunza vyema mpaka November au December means wakati bei inapanda na wewe ndio utakua umemaliza kuvuna kama vipi tazama soko kwanza la nyanya, hoho au tango sababu ukiweka tango ni miezi mitatu atleast mpaka kuisha hivyo baada ya kutoa tango unaweza sasa ukaweka nyanya. Tazama soko kabla hujaweka kitu sema pia unalimia mkoa gani wenyeji watakupa details zaidi za uliko pia, mimi niko Arusha kipindi hiki watu wanaandaa mashamba ya nyanya za miradi, huwa zinavuruga soko sana.

Mbegu bora

Tango:

Mydas -rijk zwaan
Massa - rijk zwaan

Tango ya green house lazima iwe parthenocapic yaani isiyohitaji uchavushaji sababu kwenye green house hakuna nyuki ukipanda variety ya tofauti na hizo hapo juu utakua umeotesha maua tu.

Nyanya
Tylka - syngenta
Monteazul -rijk zwaan
Victory -east west seed
Anna f1 etc

Nyanya lazima iwe nyanya ndefu (indeterminate) kwa mavuno ya muda mrefu.

Hoho

Red jet
Pasirella
Ilanga (rijk zwaan)
Balton pia wanazo za rangi
Syngenta pia wanazo

Inabidi ulime za rangi ili usiwe na mzigo sawa na wanaolima nnje
 
f0bcb0a5-f435-41bf-ad3e-f07d83244205.jpg
IMG_1093.jpg
IMG_0134.jpg
IMG_0110.jpg


Hizo system mbili tofauti za ukulima ila kote unaweza tumia udongo,kwenye mifuko unatibu udongo kwanza au unaweza pia ukatumia mchanganyiko wa vitu vingi kutengeneza udongo wa kutumia kwa ratio stahiki mfano samadi2:udongo 1:mchanga 1 etc
 
Mkuu nlieka picha ya nyanya zangu zilipofikia unishauri nn kitafuata,,leo ni cku ya 21

Sijaziona ila kwa siku ishirini na moja ni muda wa kuweka mbolea za kukuzia kama vile can,npk etc.
Mbolea gani umeweka ya mwisho na umeweka lini?
 
Sijaziona ila kwa siku ishirini na moja ni muda wa kuweka mbolea za kukuzia kama vile can,npk etc.
Mbolea gani umeweka ya mwisho na umeweka lini?
can nliweka km siku 10 zilizopita,, nitahitaji kuweka tena mbolea yoyote? vp kuhusu dawa
95e1cfb247629dead3e1ff5f2194ffd9.jpg
 
can nliweka km siku 10 zilizopita,, nitahitaji kuweka tena mbolea yoyote? vp kuhusu dawa
95e1cfb247629dead3e1ff5f2194ffd9.jpg

Weka winner baada ya siku 14 toka uweke can. Dawa tazama kuna wadudu wowote kama hakuna basi dawa hakuna haja piga tu dawa ya ukungu on weekly basis ya kukinga ndio inatakiwa kama dawa yenye mancozeb,copper,sulphur,chlorothalonil etc
 
Weka winner baada ya siku 14 toka uweke can. Dawa tazama kuna wadudu wowote kama hakuna basi dawa hakuna haja piga tu dawa ya ukungu on weekly basis ya kukinga ndio inatakiwa kama dawa yenye mancozeb,copper,sulphur,chlorothalonil etc
vp kuhusu farmzeb na linkmill hapo kweny ukungu
 
Sijaziona ila kwa siku ishirini na moja ni muda wa kuweka mbolea za kukuzia kama vile can,npk etc.
Mbolea gani umeweka ya mwisho na umeweka lini?
Mkuu je unaweza kupanda kitunguu kwenye greenhouse,yaani sehemu zenye kustawi kitunguu kama ruaha mbiyuni unaweka greenhouse ili kukiepusha na kupata magonjwa,ukungu nk.
 
Mkuu je unaweza kupanda kitunguu kwenye greenhouse,yaani sehemu zenye kustawi kitunguu kama ruaha mbiyuni unaweka greenhouse ili kukiepusha na kupata magonjwa,ukungu nk.

Yes unaweza na kina kua vyema tu. Ila je itakulipa? Kilimo cha green house tunafanya cost analysis ndani ya miaka mitano iwe imerudisha cost ya kuijenga sababu mostly baada ya miaka mitano kuna vitu vinaanza kuchoka kama net,udongo,drips etc na kama ya mbao unakuta pia zimeliwa na mchwa. Sasa lazima ulime kitu ambacho per square mita kina weza kulipa gharama ya each sqm 1 ya green house au kwa lugha rahisi unalima zao ambalo unajua litarudisha gharama ya kuliweka shambani na faida ya kulipa gharama ya green house.

Ukilima kitunguu huwezi rudisha cost ya green house ndio kiuchumi tunasema lima nyanya,tango na hoho ila kama utapata zao lingine ambao unasoko lake na unahakika ni pesa nyingi unaweza pia ukalilima ndani ya Green house,niko Arusha watu wanalima maua haswa roses na chrynthathemum kwenye green house,watu wanalima berries kwenye green house so kikubwa sio zao kustawi but ni ile return yake.

Wako ambao wanajenga green house kwa ajili ya kuifanya store sababu anajua anachohifadhi kinarudisha cost ya green house yake
 
Mvua hakuna, na kwenye mbolea km sina winner naweza rudia can au niache tuu?

Kama huna winner tumia npk yoyote uirotate na can yaan ukiweka npk this time kipindi kingine unaweka can.
Iliyobora zaidi ni mop hii unaichanganya na can ukiipata utafurahi sana.
 
Kumbe gharama ya mbegu ya nyanya inakimbuzana na gharama yavm dhahabu
 
Kama huna winner tumia npk yoyote uirotate na can yaan ukiweka npk this time kipindi kingine unaweka can.
Iliyobora zaidi ni mop hii unaichanganya na can ukiipata utafurahi sana
ok, so mbolea naweka mara ngap hadi kuanza kuchuma??
 
Heeeee hiyo ni gharama ya mbegu tu?
Mbegu zipo za bei tofauti tofauti unanunua ambayo unauwezo nayo,
Hata ukitaka mbegu ya bure unapata ukiona watu wanachuma nyanya unachukua masalo unaenda kukamua unapata mbegu
Hujalazimishwa kununua mbegu za gharama hizo za kisasa
Kumbe gharama ya mbegu ya nyanya inakimbuzana na gharama yavm dhahabu
 
ok, so mbolea naweka mara ngap hadi kuanza kuchuma??
Mbolea huweki kwa kuhesabu idadi, ukishaweka za kupandia na kukuzia unakuwa unakagua hali ya shamba, unaangalia nyanya zako shamba zinakuwa zinavyotakiwa kama zitahitaji mbolea utaweka tena
Ila ukishaweka mara moja inatosha utakuwa unapiga mbolea za juu "booster" labda shamba liwe halina rutuba ya kutosha
 
Back
Top Bottom