Jifunze kuhusu utapeli mitandaoni na namna ya kuwatambua

Jifunze kuhusu utapeli mitandaoni na namna ya kuwatambua

Ghost MVP

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2022
Posts
439
Reaction score
736
Siku hizi kumekuwa na utapeli mkubwa sana kwa njia ya mtandao, leo nitaelezea njia ya biashara na namna unavyoweza tapeliwa.

Biashara ni nyingi sana mtandaoni kama biashara ya nguo, viatu, simu, laptop na nyingine nyingi. Wapo wafanyabiashara ambao siyo matapeli na wapo matapeli.

Namna ya kujua mfanyabiashara ni tapeli fuata njia hizi:
  • Wengi wao huwa wanatumia bei ambayo itakushawishi kununua, ambayo ni rahisi kulinganisha na bei halisi.
  • Baadhi husema wapo Zanzibar wakijua mteja lazima atakuwa Bara na huwezi kwenda dukani kwao.
  • Ni wepesi sana kukushushushia bei ila ni wazito kukuelekeza mahala sahihi wanapopatikana.
  • Namba zao huwa za WhatsApp tu, hawapatikani kwa kuwapigia kwasababu wanaepuka ku-trackiwa.
  • Picha za ushahidi wa kutuma mzigo huwa hazioneshi sura zao wala picha ya duka vizuri, wala jina la duka, na picha huwa za mikono tofauti.
  • Wanataka uwatumie pesa ndiyo wakutumie mzigo, au ulipie nusu ndiyo upokee mzigo wako, na ukituma tu umekwisha.
  • Namba ya kutuma pesa huwa ni tofauti na anayotumia WhatsApp.
  • Huwa wanakuuliza mahala unapopatikana ili waweze kukutajia mbali ambapo huwezi kwenda.
Na sababu nyingine kibao.

Ukijaribu kumtafuta kwa namba tofauti anaweza kukupa maelezo tofauti kabisaa, na hawaweki location ya link kwenye account zao, ili usiweze jua wapo wapi.

Hivyo unapotaka nunua kitu mtandaoni usikubali kutuma pesa kwanza hata iweje, mwambie akuletee mzigo umpe pesa yake, kwasababu unaweza tapeliwa au kuletewa bidhaa feki/isiyo na kiwango.

Kwenye picha ni mmoja wa watu hao ambapo amejichanganya na kusema yupo sehemu tofauti kwasababu alijua ni mteja mwingine.

Weka comment majina ya wafanya biashara matapeli, user name zao za mitandaoni na useme walikufanyaje ukajua ni tapeli ili waweze komeshwa.

Screenshot_20221125-002941.jpg
20221125_002758.jpg
20221125_002900.jpg
20221125_002829.jpg
 
Siku hizi kuna wale wa michezo ya mitandaoni..pesa inatafutwa nyie🙌
 
Tangu nimetapeliwa 2014 sijawahi tapeliwa na siji tapeliwa maana nilipata darasa.

Zaid zaid huwa nawasanua watu kwamba hapo unaenda kulia na kweli akipuuza lazima alie.
By that time ilikua ni issue za ajira hizi, jamaa alijifannya yupo utumishi ananisomea mpaka namba za vyeti vyangu dah maisha haya.

Mwisho wa siku nikaambiwa tuma pesa jina linakuja Festo Manipa.

Siji sahau kahela kangu ni bora ningekula kuku rost.!!!
 
Hawashirikiani na wanaosimamia sheria za wizi mtandaoni kwa maana hawachukuliwi hatua zozote wangechukuliwa hatua wasingeendelea kutapeli wananchi.
 
Siku hizi kuna wale wa michezo ya mitandaoni..pesa inatafutwa nyie🙌
Utapeli utakithiri kama mamlaka husika haitachukulia swala hili kw auzito, TCRA wafungie line zao wanazotumia na kuwatafuta
 
Tangu nimetapeliwa 2014 sijawahi tapeliwa na siji tapeliwa maana nilipata darasa.

Zaid zaid huwa nawasanua watu kwamba hapo unaenda kulia na kweli akipuuza lazima alie.
By that time ilikua ni issue za ajira hizi, jamaa alijifannya yupo utumishi ananisomea mpaka namba za vyeti vyangu dah maisha haya.

Mwisho wa siku nikaambiwa tuma pesa jina linakuja Festo Manipa.

Siji sahau kahela kangu ni bora ningekula kuku rost.!!!
🤣🤣🤣🤣Pole sana! Je unadhan namba ya vyeti vyako aliijuaje? Huoni ni mtu anaekufahamu vizuri?
 
Back
Top Bottom