Jifunze kumpa mwanamke wako hela bila sababu, utanishukuru baadaye

Jifunze kumpa mwanamke wako hela bila sababu, utanishukuru baadaye

Broo, acha kujikaza. Umeshauriwa uache mara moja, siku ukijua unapohonga kuna mwamba anakojolea bila
Hata senti utalia na kusaga meno.

Wana "psycho" wameendelea kugundua kuwa wanawake wanawadharau sana wanaume wenye tabia kama yako. Wanawachukulia kuwa ni dhaifu wasioweza kushawishi pasipo kutumia pesa.

Umeambiwa mfanye binti awe Royal kwako bila kutumia pesa yoyote, hizo huduma unazotoa anastahili mke sio demu 😂 😂
Nakazia ujumbe wako mkuu.Umenena vyema Sana.
 
Kinachonifurahisha ni kwamba, hawa mnaowapa pesa na kuwalipia kodi ndio wanaotutunuku bure huku mitaani.

Binti mmepanga sehemu moja anashushwa na Prado Ila baada ya dk 20 anakwambia ameboeka uende chumbani kwake umpe kampani [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Sasa mkuu kila mtu ana offee alicho nacho, wewe endelea ku offer hyo company, na wenye hela waendelee kuwapa hizo hela mwisho wa siku dada zetu wasiwe na makasiriko duniani.

NB: Mm ntakua na offee Vocha/Bundle la mwezi nimewai [emoji16]
 
Hakika, nami niliwah kosana na mwanamke sababu ya hivi, nikataka kumuonesha kwamba tunafurahia dunia, full kulala hotelin na mivyakula, sad enough akaniambia hagau una matumizi mabaya sana ya fedha na hivyo mm sipend mtu wa hivyo, nikadahan anatania ila akapunguza mahusiano had tukasauliana. Ukipata mtu anaejielewa anakuona zuzu boya sana ilihal ww ulitaka kuonekana mwamba.
Huyo demu hakukupenda mkuu. Alikutafutia tu sababu, kama angekua amekupenda seriously, Angekurekebisa na mngesonga mbele.
 
Ukishamtumia hiyo hela anaenda kumgawia mpenzi wa moyo wake. Enzi nikiwa mpumbavu sana nilishawahi kumpeleka shopping ya nguo mwanamke niliyempenda ila jioni yake akazivaa zile nguo na kutoka na mpenzi wa moyo wake. Niliumia sana. Bahati nzuri KARMA huwa inasahau address ya CCM tu... huyo manzi kwa sasa ni single mama mwandamizi.
[emoji16][emoji16] Ah umenishtua kuna mtoto wa mtu hapa nilitaka nimnunulie Jersey, Sasa wacha ni ghairi.
 
Tanzania iwekeze kwenye elimu tu na ibadilishe mfumo wa elimu kabisa. Ndipo itaanza kuona maendeleo baada ya miaka 15 mpaka 20 ya mabadiliko ya aina ya elimu yetu.

Kama hatutobadili mfumo wa limu nje ndani, maendeleo ya kweli tusahau, tutabaki kuwa ombaomba tu.

Kwa o,mbaomba namaanisha tegemezi, mfumo wetu wa elimu siyo wa mtu binafsi kujitegemea, ni wa kila mtu kutegemea afanyiwe.
Big Brain 👊🙏
 
Si anakupa utelezi mkuu au kwako sio big deal?
Iyo ni starehe ya wote, kama anajiuza tukubaliane bei twende lodge tukamalizane kama anataka meaniful relationship anawajibika kujihudumia mahitaji yake yote kwa standard ya maisha aliyoichagua mpaka pale tukapoanza kuishi pamoja kama mke na mume. Kumsaidia mpenzi wako kupo lakini ukiwekewa kama ndio sharti la kupewa penzi then you are a simp
 
Kindly refer to the heading above..


Na hii sio mwanamke wako tu, hata yule ambaye unamtaka. Kwa mfano; [emoji116]

Money transfer successful! TSH 200,000.00 was sent to NMB Bank account no 41510040XXX (MILLICENT MZURI) ref:XXX4298373. Thanks for using Exim Mobile, call 0800 780 111 for any assistance needed.

Au,

AirtelMoney
Umetuma Tsh270,000.00 kwenda kwa MILLICENT MZURI. Salio lako jipya ni Tsh2,100,000.00. Muamala No: CI240503.1856.N57337

Hiyo miamala yote uwe umemtumia hata bila kuombwa. Kwa mfano huo muamala wa kwanza unakuwa umeutuma jana usiku wa saa saba wakati amelala, akiamka asubuhi anakutana na notification tu. Aisee, mapenzi utayasimulia katika muktadha wa tofauti sana.

Pengine huo muamala wa pili uwe umemtumia leo week end baada ya binti kukwambia anaenda kwenye birthday ya rafiki yake. Halafu muamala unafuatiwa na SMS hii, "baby pls manage that little token from me. Love always" [emoji4] .

Hawa wanawake tunawalaumu bure tu. Tatizo ni kwamba hatuwapi PESA. Kwao pesa ndio kila kitu; nguvu za kiume, uaminifu, utulivu, upole, utu wema, usikivu, unyenyekevu n.k (mengine ongezea mwenyewe).

Sasa wewe hela hutumi, binti anajikaza anakuomba unaanza stori, sijui "ooh baby nipo mbali msibani huku tandahimba ndanindani nina cash tu na mawakala wako mbali" [emoji23], wakati siku hizi kuna sim banking, mobile money transfer n.k

Hata kama huna sim banking, mwanaume unakosaje akiba kidogo kwenye simu kwa ajili ya dharura?!!! Kwanza siku hizi kutembea na cash ni ushamba.

Wanaume tutafuteni pesa. Dunia haina huruma kwa masikini wote lakini hasa sisi WANAUME.

N:B
'MILLICENT MZURI' NI JINA LA KUSADIKIKA TU.
Wanawake hawahitaji hela.
 
Back
Top Bottom