Jifunze kutokuamini watu ili uepuke kuumizwa

Jifunze kutokuamini watu ili uepuke kuumizwa

Agresive

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2018
Posts
890
Reaction score
1,236
Ndugu wana jamvi hbr ya leo.

Naandika kwa msisitizo kuwa jitahidi sana sana upunguze kuamini watu katika jambo lolote punguza imani ya kuamini watu ili kuepeuka kuumizwa na kupoteza pesa.

Watu wengi wameumizwa kipesa na kimapenzi na watu waliowaamini, haijalishi ni mtu wako kiasi gani punguza kuamini watu kwa kuwa kuna watu wameumizwa na watu ambao walidumu nao katika biashara miaka kadhaa lakini mwisho wa cku waliwaibia.

Vifuatavyo ni visa vya watu kuumizwa na watu waliowaamini na hawa ni watu nawajuwa so ni visa vya kweli.

1. Miaka 5 nyuma rafiki yangu wa karibu nilimpa buku 10 hakunirejeshe mpaka leo.

2. Mdogo wangu Mwenge sokoni hapa Dsm alikuwa na rafiki yake wanafanya biashara ya viatu akamtuma mzigo kama mara 5 analeta bila shida, cku moja akamwambia amepata chimbo Kenya kuna bei nafuu dogoo akampa 3M mpaka leo miaka 5 jamaa hajarudi tena.

3. Mdogo wangu mwingine ana duka la Pharmacy Angola pharmacy mfanyakazi aliaminiwa akaingiza hasara ya milioni 17 aliiba kutokana na uzembe wa usimamizi.

4. Mfanyakazi staff moja alimpa dogo 250K za kitanda cha chuma 5×6 dogo akatengeneza cha kwanza kikawa hakifiti na godoro kikarudishwa atengeze kingine mpaka leo fundi katoroka kijiwe coz alikuwa na madeni mengine mwaka wa 2 sasa hayupo.

5. Mzee mmoja Moshi alikuwa na rafiki yake sana akampa mashamba yake kama dhamana achukulie mkopo Bank jamaa hakumaliza mashamba yule mzee mwaka juzi alikuwa anahaha mashamba yasiuzwe, na jamaa haonekani.

6. Muuzaji wa magari mtaani ukisikia kisa chake mpaka kushuka na kuingia kwenye madeni ya 1B ambayo kwa sasa amelipa bado kama milioni 100 baadhi ya hasara ni kuamini watu.

7. Unamtumia Manzi kwa kumuamini unatuma Nauli half haji.

8. Mwaka juzi niliingia hasara ya zaidi ya milioni 9 kwa kumuamini mtu, nilivyomshika nikapeleka polisi bahati mbaya AKAFA pesa nikapoteza utamdai marehemu?

9.Mwezi 7 nyuma rafiki yangu alimuazima mtu waliyezoea muda mfupi Laptop jamaa kamzurum na kahama mkoa.

10. Mjomba wangu kiukoo cku moja alipakia karanga gunia 100, wakafika njiani wakalala dreva kaamka ucku katoroka na mzigo, Ilikuwa Lori kalipiga mkono likasimama akapakia mzigo so hakuchukua tahadhari hata no za Gari.

11. Wanaume wengi tumelea mimba si zetu na watoto si wetu kisa kuamini wapenzi na wake zetu.

NDUGU WANA JF hii ni mifano michache kati ya mingi niliyonayo ambayo nimeona kwa macho yangu, unamuamini mtu mwisho wa cku anakuumiza.

WATU WENGI WAAMINIFU NDIYO HUWA WANAUMIZWA KWA KUWA HUHISI WATU WOTE NI WAAMINIFU KAMA WALIVYO WAO, KUNDI HILI HUUMIZWA ZAIDI ZAIDI.

Binafsi suala la kuamini watu nimeachana na kupunguza kwa asilimia 85%.

Suala la kukopesha pesa mtu nimeacha mwisho nitakupa 30k hata ukinizurumu basi siyo issue.

Nasisitiza tena acha kuamini watu kupita kiasi, mtu unaweza kufanya naye biashara miaka 4 ila mwisho wa cku ukampa 30M asionekane tena.
 
Umeshare kitu cha msingi sana, Na watu weusi ndio wanaongoza. Big YES nawachukia watu weusi, wamenikwamisha at some moments.

Sijui wanafikiriaje kuhusu maisha
ukifanya uchunguzi watu wengi tumeumizwa na watu tuliowaamini, suala la kuishi kwa kuamini watu kisa umejuana kitambo tunapaswa kuwa makini na mipaka Dunia ilipofikia tupunguze kuamini watu.
 
Ukiogopa kutibiwa huwezi kusonga mbele,huwezi kufanya kila kitu mwenyewe
 
Yamenikuta mara kibao tu [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Pole sana mkuu, kikubwa punguza kuamini watu na jifunze kutokana na makosa
Nilimuamini sana mtoto wa Aunt yangu yaani binamu kila mara aliomba nimsaidie mtaji laki nampa, sikumoja aliniomba Laki 3 nikampa haikurudi hiyo. Baadae niliendelea kumuamini kwakuwa ni ndugu yangu tukakutana nyumbani ilikuwa likizo yangu kumbe binamu kanigeuza kitega uchumi alivyo ona nimekuwa mgum akaanzisha valangati hapo hapo mpaka sasa nimesha gombana nae.
 
Nilimuamini sana mtoto wa Aunt yangu yaani binamu kila mara aliomba nimsaidie mtaji laki nampa, sikumoja aliniomba Laki 3 nikampa haikurudi hiyo. Baadae niliendelea kumuamini kwakuwa ni ndugu yangu tukakutana nyumbani ilikuwa likizo yangu kumbe binamu kanigeuza kitega uchumi alivyo ona nimekuwa mgum akaanzisha valangati hapo hapo mpaka sasa nimesha gombana nae.
Ndivyo maisha yalivyo, na tunaumizwa na wale tunaowamini sana, pole sana , ni kweli tunapaswa kuamini watu lakini tunapaswa kuchukua tahadhari sana.
 
Back
Top Bottom