Jifunze kutokuamini watu ili uepuke kuumizwa

Jifunze kutokuamini watu ili uepuke kuumizwa

Upo sahihi kbsa mkuu, hapa Duniani hutakiwi kumuamini mtu kwa asilimia 💯 zaidi yako wewe mwenyewe.
 
[emoji23][emoji23] tanzania ye2 tu hii , ila yule ni vile tulikuwa kama mandugu , tumebebana since chuo ,alifanikiwa mbele yangu kimaisha kwa muda nilikaa kwake , tukajuana muda , sema alivoniosha mpaka leo siamini
Maisha ni fumbo hujuw kesho yupi atakupa huzuni na yupi atakupa furaha
 
Mm sikopeshi mtu awe ndugu au mtu baki.
Nina wadai watu wengi na hakuna dalili za kulipa.
Mtu nikimuonea huruma sana kumkosesha aje na mkewe amwache kwangu nimtumie hadi atakapo rudisha pesa yangu.
Sitaki ukhanithi mimi kwenye pesa.
 
2019 nilimpa rafiki mkopo wa millioni 400 , mwamba alikuwa na hardware kubwa hapa dar , by then tumejuana since chuo , ilipofika miezi mitano baadaye muda wa malipo , aliingia mitini naskia siku hizi anabangaiza njombe na iringa, iliniuma sana kwa kuwa almost inipeleke bankruptcy then ,namshukuru mungu niliponea mufilis

Pesa ndefu sana hiyo
 
Ndugu wana jamvi hbr ya leo.

Naandika kwa msisitizo kuwa jitahidi sana sana upunguze kuamini watu katika jambo lolote punguza imani ya kuamini watu ili kuepeuka kuumizwa na kupoteza pesa.

Watu wengi wameumizwa kipesa na kimapenzi na watu waliowaamini, haijalishi ni mtu wako kiasi gani punguza kuamini watu kwa kuwa kuna watu wameumizwa na watu ambao walidumu nao katika biashara miaka kadhaa lakini mwisho wa cku waliwaibia.

Vifuatavyo ni visa vya watu kuumizwa na watu waliowaamini na hawa ni watu nawajuwa so ni visa vya kweli.

1. Miaka 5 nyuma rafiki yangu wa karibu nilimpa buku 10 hakunirejeshe mpaka leo.

2. Mdogo wangu Mwenge sokoni hapa Dsm alikuwa na rafiki yake wanafanya biashara ya viatu akamtuma mzigo kama mara 5 analeta bila shida, cku moja akamwambia amepata chimbo Kenya kuna bei nafuu dogoo akampa 3M mpaka leo miaka 5 jamaa hajarudi tena.

3. Mdogo wangu mwingine ana duka la Pharmacy Angola pharmacy mfanyakazi aliaminiwa akaingiza hasara ya milioni 17 aliiba kutokana na uzembe wa usimamizi.

4. Mfanyakazi staff moja alimpa dogo 250K za kitanda cha chuma 5×6 dogo akatengeneza cha kwanza kikawa hakifiti na godoro kikarudishwa atengeze kingine mpaka leo fundi katoroka kijiwe coz alikuwa na madeni mengine mwaka wa 2 sasa hayupo.

5. Mzee mmoja Moshi alikuwa na rafiki yake sana akampa mashamba yake kama dhamana achukulie mkopo Bank jamaa hakumaliza mashamba yule mzee mwaka juzi alikuwa anahaha mashamba yasiuzwe, na jamaa haonekani.

6. Muuzaji wa magari mtaani ukisikia kisa chake mpaka kushuka na kuingia kwenye madeni ya 1B ambayo kwa sasa amelipa bado kama milioni 100 baadhi ya hasara ni kuamini watu.

7. Unamtumia Manzi kwa kumuamini unatuma Nauli half haji.

8. Mwaka juzi niliingia hasara ya zaidi ya milioni 9 kwa kumuamini mtu, nilivyomshika nikapeleka polisi bahati mbaya AKAFA pesa nikapoteza utamdai marehemu?

9.Mwezi 7 nyuma rafiki yangu alimuazima mtu waliyezoea muda mfupi Laptop jamaa kamzurum na kahama mkoa.

10. Mjomba wangu kiukoo cku moja alipakia karanga gunia 100, wakafika njiani wakalala dreva kaamka ucku katoroka na mzigo, Ilikuwa Lori kalipiga mkono likasimama akapakia mzigo so hakuchukua tahadhari hata no za Gari.

11. Wanaume wengi tumelea mimba si zetu na watoto si wetu kisa kuamini wapenzi na wake zetu.

NDUGU WANA JF hii ni mifano michache kati ya mingi niliyonayo ambayo nimeona kwa macho yangu, unamuamini mtu mwisho wa cku anakuumiza.

WATU WENGI WAAMINIFU NDIYO HUWA WANAUMIZWA KWA KUWA HUHISI WATU WOTE NI WAAMINIFU KAMA WALIVYO WAO, KUNDI HILI HUUMIZWA ZAIDI ZAIDI.

Binafsi suala la kuamini watu nimeachana na kupunguza kwa asilimia 85%.

Suala la kukopesha pesa mtu nimeacha mwisho nitakupa 30k hata ukinizurumu basi siyo issue.

Nasisitiza tena acha kuamini watu kupita kiasi, mtu unaweza kufanya naye biashara miaka 4 ila mwisho wa cku ukampa 30M asionekane tena.
mtu akikuomba umkopeshe kiasi chochote cha pesa we mpe 1/4 kwa kumsaidia tu mwambie hali c nzuri pokea hii ila siyo kumkopesha epuka lawama na kuumizwa nafsi kwa kila hali
 
usemalo ni kweli , siku hizi imani ilikufa kabisa , hata watoto wangu huwa nawaangalia kwa mbali kwa ishu za pesa
Dah mkuu ata watoto wa kuwazaa huwaamini ! Hhhhhhhh hii dunia inaelekea mwisho sasa
 
Mwaka 2016 nilimuamini rafiki yangu nikasajili line yangu kwakutumia kitambulisho chake ,niliweka 250,000 kwenye tigo pesa huku na yeye akijuwa hilo.

Kilichofuata jamaa aka lock line ya simu akaenda li new mpya akatoa pesa yote halafu akaitupa ile line nilivyo fatilia tigo headquarter wakaniambia kuwa mimi mwenyewe nilipiga simu ku block line yangu.


Aaaaaaa binadamu [emoji114]
 
😂😂 tanzania ye2 tu hii , ila yule ni vile tulikuwa kama mandugu , tumebebana since chuo ,alifanikiwa mbele yangu kimaisha kwa muda nilikaa kwake , tukajuana muda , sema alivoniosha mpaka leo siamini
🙌 aisee,kuna watu mnaishi
 
Back
Top Bottom