Mad Max
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 26,961
- 77,890
Wakuu, kuna siku tulidiscuss kuhusu mashindano ya magari ya Formula One.
Madereva wa Formula 1, ni "Marubani" wa Jet za ardhini
Leo tungejaribu kugusia kidogo kuhusu mashindano ya pikipiki, MotoGP.
Utangulizi
MotoGP ni mashindano ya pikipiki yanayosimamiwa na kuratibiwa na Fédération Internationale de Motocyclisme (FIM).
Wanashindania nini?
Tofauti na mashindano mengine mengi, MotoGP kuna aina tatu za mashindano vinaenda kwa pamoja.
Kwanza ni Driver Championship, Pili ni Constructor Championship na Tatu ni Team Championship.
Kwa mfano, msimu wa mwaka 2022 na 2023 Francesco Bagnaia (bwana mdogo hapo juu) ndio alikua Rider Word Champion, akiwa na Ducati Lenovo Team ambao nao wamechukua makombe karibia misimu minne yote iliopita kombe la Team Championship (nembo yao hii hapa)
Na chini, Ducati GP8 ndio ilioshinda Constructors Championship.
Hii ni tofauti na tulivyoona kwenye Formula 1, kwenyewe kuna Driver na Team (Team na Constructor kule wameungana) Championship.
Team & Constructor
Kama tulivyogusia hapo, kwenye MotoGP mbali na madereva kushindana, basi kuna Team na Constructors pia wanashindana.
Team wanapokea pikipiki kutoka kwa constructor walieingia nae mkataba.
Wakishaipokea wanaruhusiwa kufanya tunning ndogo ndogo na kutoa support kwa dereva wao.
Wakati wa racing, dereva anakua anawasiliana na team yake muda wote kwaajili ya updates mbalimbali za race, track na pikipiki.
Team zipo za aina mbili, kuna factory teams na satelite teams.
Hawa factory teams wanakua wameungana moja wa moja na constructors wao wanaowapa pikipiki, kwa mfano: Yamaha Factory Racing, Ducati Lenovo Team au Honda Repsol Team.
Satellite team wao hawahusiani na constructor moja kwa moja, na unaweza ukakuta huu msimu wanatumia pikipiki ya Honda msimu ujao wakatumia Yamaha. Mfano: Gresini Racing (wanatumia Ducati), LCR Honda (wanatumia Honda).
Msimu huu teams zipo 11 sometimes zinakuaga 12, na kila team ina madereva wawili.
Constructors ndio makampuni yanayotengeneza izo pikipiki. Hapo wanaoneshana ubabe wa technology na best machine.
Pikipiki zinazotengenezwa na kila constructor zinakua zinafuata masharti yaliyowekwa na FIM.
Constructor mmoja anaweza kuprovide pikipiki kwa team ata zaidi ya moja.
Kwa msimu huu constructors wapo sita tu, Ducati, Yamaha, Honda, KTM, Apria na GasHas (huyu ni mgeni, ni kama tawi la KTM).
Pikipiki
Pikipiki zinazotumika kwenye MotoGP zimetengenezwa maalum tu kwaajili ya racing, sio za kutumiwa wala kuuzwa kwa watumiaji wa kawaida.
Engine zake zinakua na displacement kubwa kama 1000 cc na zinatengeneza power kubwa hadi 250 hp.
Kutokana na kua na displacement kubwa na power kubwa, zinakua na acceleration kubwa sana na speed hadi ya 400 km/h, na hadi leo top speech iliowahi kuonekana kwenye race ni 366 km/h.
Hizi bikes zina accerelate kufika top speed quicker kuliko F1 cars kwenye same track.
Pamoja na ivyo, hivi pikipiki ni nyepesi sana, thanks to carbon fiber material, na zina body kits maalum kwaajili ya kusaidia iwe stable ata ikiwa katika speed kali.
Pikipiki zote zinatumia matairi kutoka kwa supplier mmoja, Michellin.
Hii pikipiki haiuzwi, ila kama ingekua inauzwa ingecost wastani wa $3 Million.
Madereva
Hawa madereva ni professional na wana leseni maalumu ya kushiriki aya mashindano.
Madereva wanakua physically fit na higher endurance.
Kwahiyo wakati wanaendesha wanakua na umakini wa hali ya juu kwaajili ya kucontrol iyo pikipiki na huku unakua makini kuzuia collision na madereva wenzio, na huku unapambana na effect za G-Forces wakati wa braking, acceleration na kona.
Wakati unaangalia MotoGP utaona madereva kwenye kona wanalala hivi, inayowasaidia kukata kali saaana wakiwa katika speed kali, sometimes utaona magoti yanagusa chini.
Msimu huu tuna madereva 22 kutoka kwenye team 11, wanaotumia pikipiki kutoka constructors 6.
Viwanja (circuit)
MotoGP inafanyika kwenye viwanja mbalimbali katika msimu mzima, kama F1 tu.
Mfano hapo juu kiwanja cha Mugello Circuit, kilichopo Italia kinatumika kwenye F1 na MotoGP. Na hiki chini ni cha Qatar.
Viwanja vinatofautiana, vingine unakuta vina challenges nyingi kuliko vingine kama vile kona nyingi wakati vingine straights nyingi. Ila viwanja vyote vina sehemu za highspeed na sehemu za kona kali, hapa ndio ushindani unapotokea.
Racing zinafanyika sehemu mbalimbali za Dunia katika viwanja kama unavyoona kwenye ramani hapo juu. Hizo green ni nchi ambazo michuano mwaka huu inafanyika na red iliwahi kufanyika miaka ya nyuma.
Mashindano
Mashindano ya MotoGP yanafanyika weekend kwa muda wa siku tatu, kuanzia Ijumaa hadi Jumapili.
Day 1 (Ijumaa): Free Practice.
Ijumaa kunakua na sessions mbili za free practice ambapo madereva na team zao wanajiweka familiar na circuit na kutest pikipiki zao. Kunakua na practice nyingine ya tatu jumamosi.
Lakini Free Practice sessions sio tu za mazoezi na kutest pikipiki, ila kila dereva tutachukua fastest lap yake ya kila practice (FP1, FP2 na FP3) na zitadetermine ni qualifying session gani kesho ataingia.
Yaani hivi, madereva 10 wenye marks nyingi za FP1, FP2 na FP3 wanaenda moja kwa moja kwenye Qualifying 2 (Q2) na wale waliobakia kuanzia 11 hadi 222 inabidi waanze kupambana Q1 (utanielewa hapa chini siku ya Qualifying).
Day 2 (Jumamosi): Qualifying (au tuseme Grid Formation).
Jumamosi kunakua na free practice moja kama tulivyosema, na kunakua na qualifying sessions mbili, tunaziita Q1 na Q2.
Qualifying sessions ndio itakayoamua nani kesho jumapili kwenye race awe namba moja tunavyoanza, nani awe mbili na nani awe wa mwisho (grid).
Qualifying imegawanyika katika sessions mbili, Q1 na Q2.
Qualifying 1 (Q1)
Tukianza na Q1, tunawachukua wale madereva waliokua nje ya top 10 ya marks za FP1, FP2 na FP3 na kuwashindanisha. Wawili watakaokua na speed kali kabisa wataenda Q2 kujumuika na wale 10 wenzie.
Waliobakia 10 wenyewe hawataenda Q2, wao watasubiria siku ya race wataanzia iyo nafasi waliyomaliza Q1.
Yaani yule wa tatu atakua namba 13, wa nne atakua namba 14, ivo ivo hadi 22.
Qualifying 2 (Q2)
Sasa tunakuja kwenye Q2 ambaoo tunagombaniana sasa nani kesho kwenye race atakaa namba 1 hadi namba 12?
Kwahiyo dereva atakaeset fastest lap kwenye Q2 ndio atakaekua pole (yaani nafasi ya kwanza/au tuseme atakaa mbele) kesho wakati wa race.
Ikumbukwe, Q1 na Q2 haushindani na dereva mwenzio, it’s race against time. Mnapewa dakika 15 tu, kwahiyo katika izo dakika 15 utafanya lap ngapi, na tunachukua lap ambayo umetumia muda mdogo kabisa (fastest lap) ndio tunaitumia kukujudge.
Day 3 (Jumapili): Race Day
Wakati wa race yenyewe, kutegemea urefu na aina ya circut, madereva wanatakiwa washindane kukamilisha idadi fulani ya laps. Mostly, race ni dakika 40 hadi 45, kwahiyo katika huo muda dereva unatakiwa umaintain speed, balance kuchakaa kwa tyre na jitahidi sana kuepuka crashes.
Kwa kuanza, jumapili asubuhi kunakuaga na warm-up session, inschukua kama dk 15 hadi 20 ambapo ni kama nafasi ya mwisho kuwapa madereva na team kujua vizuri chombo na circuit. Hii mara nyingi uwa haioneshwi labda uifatilie kwenye MotoGP TV yao officially.
Ikifika jioni nusu saa kabla ya race madereva na pikipiki wanajipanga kwenye grid kama inavyotakiwa kisha wanaanza race.
Race inaanza kwa formation lap ambayo ni lap moja hutakiwi kumuovertake wa mbele yako, lengo ni kupasha moto tyres na brakes.
Baada ya formation lap kila mtu anarudi kwenye grid, mnasubiria green lights then mnaanza race.
Tofauti na F1, kwenye MotoGP hakuna pit stop sijui kubadirisha tyre wala kufanya nini, mkianza mmeanza.
Labda ikitokea mabadiriko makubwa sana ya hali ya hewa ndio kunakua flag to flag race, yaani mnaruhusiwa kubadirisha pikipiki katikati ya race lengo kubadirisha tyres labda from dry kwenda tyres.
Points
Kama Formula 1, dereva anapata point ya kila race kutegemea na nafasi aliyomaliza.
Dereva wa kwanza anapata point 25, wa pili 20, wa tatu 16 na kuendelea hadi wa 15 anapata 1 waliobakia zero.
Kwahiyo unakua unakusanya point kila race katika msimu mzima, na mwisho wa msimu dereva mwenye point nyingi ndio Word Champion.
Teams pia zinakusanya point kutoka kwenye madereva wake iliowatoa. Nazi zinajumlishwa mwisho wa msimu tunapata kombe la team.
Constructor nae hivo hivo, lakini ikitokea mfano Ducati ametoa mshindi namba 1, 2, na 3 tunachukua point kubwa tu ya 1. Constructors hawana accumulated points kama teams (katika race). Ila nao tutajumlisha na tutapata mshindi wa kombe la constructors.
Sheria & Kanuni
Kama ilivyomichezo mingine, MitoGP pia ina kanuni, sheria na taratibu ili kufanya mchezo uwe safe, fair na exciting.
Kanuni zipo kwaajili ya madereva na team, pikipiki, race yenyewe nk.
Mfano kwa pikipiki, baadhi ya sheria za msimu huu ni:
Kuna mengi sana ya kujifunza kwenye MotoGP lakini nimeandikwa kwa ufupi, wengine watasaidia au nitajaribu edit.
MotoGP ni more exciting kuangalia sana sometimes naonaga kuliko F1 sema marketing yake haifikii F1.
Madereva wa Formula 1, ni "Marubani" wa Jet za ardhini
Leo tungejaribu kugusia kidogo kuhusu mashindano ya pikipiki, MotoGP.
Utangulizi
MotoGP ni mashindano ya pikipiki yanayosimamiwa na kuratibiwa na Fédération Internationale de Motocyclisme (FIM).
Wanashindania nini?
Tofauti na mashindano mengine mengi, MotoGP kuna aina tatu za mashindano vinaenda kwa pamoja.
Kwanza ni Driver Championship, Pili ni Constructor Championship na Tatu ni Team Championship.
Kwa mfano, msimu wa mwaka 2022 na 2023 Francesco Bagnaia (bwana mdogo hapo juu) ndio alikua Rider Word Champion, akiwa na Ducati Lenovo Team ambao nao wamechukua makombe karibia misimu minne yote iliopita kombe la Team Championship (nembo yao hii hapa)
Na chini, Ducati GP8 ndio ilioshinda Constructors Championship.
Hii ni tofauti na tulivyoona kwenye Formula 1, kwenyewe kuna Driver na Team (Team na Constructor kule wameungana) Championship.
Team & Constructor
Kama tulivyogusia hapo, kwenye MotoGP mbali na madereva kushindana, basi kuna Team na Constructors pia wanashindana.
Team wanapokea pikipiki kutoka kwa constructor walieingia nae mkataba.
Wakishaipokea wanaruhusiwa kufanya tunning ndogo ndogo na kutoa support kwa dereva wao.
Wakati wa racing, dereva anakua anawasiliana na team yake muda wote kwaajili ya updates mbalimbali za race, track na pikipiki.
Team zipo za aina mbili, kuna factory teams na satelite teams.
Hawa factory teams wanakua wameungana moja wa moja na constructors wao wanaowapa pikipiki, kwa mfano: Yamaha Factory Racing, Ducati Lenovo Team au Honda Repsol Team.
Satellite team wao hawahusiani na constructor moja kwa moja, na unaweza ukakuta huu msimu wanatumia pikipiki ya Honda msimu ujao wakatumia Yamaha. Mfano: Gresini Racing (wanatumia Ducati), LCR Honda (wanatumia Honda).
Msimu huu teams zipo 11 sometimes zinakuaga 12, na kila team ina madereva wawili.
Constructors ndio makampuni yanayotengeneza izo pikipiki. Hapo wanaoneshana ubabe wa technology na best machine.
Pikipiki zinazotengenezwa na kila constructor zinakua zinafuata masharti yaliyowekwa na FIM.
Constructor mmoja anaweza kuprovide pikipiki kwa team ata zaidi ya moja.
Kwa msimu huu constructors wapo sita tu, Ducati, Yamaha, Honda, KTM, Apria na GasHas (huyu ni mgeni, ni kama tawi la KTM).
Pikipiki
Pikipiki zinazotumika kwenye MotoGP zimetengenezwa maalum tu kwaajili ya racing, sio za kutumiwa wala kuuzwa kwa watumiaji wa kawaida.
Engine zake zinakua na displacement kubwa kama 1000 cc na zinatengeneza power kubwa hadi 250 hp.
Kutokana na kua na displacement kubwa na power kubwa, zinakua na acceleration kubwa sana na speed hadi ya 400 km/h, na hadi leo top speech iliowahi kuonekana kwenye race ni 366 km/h.
Hizi bikes zina accerelate kufika top speed quicker kuliko F1 cars kwenye same track.
Pamoja na ivyo, hivi pikipiki ni nyepesi sana, thanks to carbon fiber material, na zina body kits maalum kwaajili ya kusaidia iwe stable ata ikiwa katika speed kali.
Pikipiki zote zinatumia matairi kutoka kwa supplier mmoja, Michellin.
Hii pikipiki haiuzwi, ila kama ingekua inauzwa ingecost wastani wa $3 Million.
Madereva
Hawa madereva ni professional na wana leseni maalumu ya kushiriki aya mashindano.
Madereva wanakua physically fit na higher endurance.
Kwahiyo wakati wanaendesha wanakua na umakini wa hali ya juu kwaajili ya kucontrol iyo pikipiki na huku unakua makini kuzuia collision na madereva wenzio, na huku unapambana na effect za G-Forces wakati wa braking, acceleration na kona.
Wakati unaangalia MotoGP utaona madereva kwenye kona wanalala hivi, inayowasaidia kukata kali saaana wakiwa katika speed kali, sometimes utaona magoti yanagusa chini.
Msimu huu tuna madereva 22 kutoka kwenye team 11, wanaotumia pikipiki kutoka constructors 6.
Viwanja (circuit)
MotoGP inafanyika kwenye viwanja mbalimbali katika msimu mzima, kama F1 tu.
Viwanja vinatofautiana, vingine unakuta vina challenges nyingi kuliko vingine kama vile kona nyingi wakati vingine straights nyingi. Ila viwanja vyote vina sehemu za highspeed na sehemu za kona kali, hapa ndio ushindani unapotokea.
Racing zinafanyika sehemu mbalimbali za Dunia katika viwanja kama unavyoona kwenye ramani hapo juu. Hizo green ni nchi ambazo michuano mwaka huu inafanyika na red iliwahi kufanyika miaka ya nyuma.
Mashindano
Mashindano ya MotoGP yanafanyika weekend kwa muda wa siku tatu, kuanzia Ijumaa hadi Jumapili.
Day 1 (Ijumaa): Free Practice.
Ijumaa kunakua na sessions mbili za free practice ambapo madereva na team zao wanajiweka familiar na circuit na kutest pikipiki zao. Kunakua na practice nyingine ya tatu jumamosi.
Lakini Free Practice sessions sio tu za mazoezi na kutest pikipiki, ila kila dereva tutachukua fastest lap yake ya kila practice (FP1, FP2 na FP3) na zitadetermine ni qualifying session gani kesho ataingia.
Yaani hivi, madereva 10 wenye marks nyingi za FP1, FP2 na FP3 wanaenda moja kwa moja kwenye Qualifying 2 (Q2) na wale waliobakia kuanzia 11 hadi 222 inabidi waanze kupambana Q1 (utanielewa hapa chini siku ya Qualifying).
Day 2 (Jumamosi): Qualifying (au tuseme Grid Formation).
Jumamosi kunakua na free practice moja kama tulivyosema, na kunakua na qualifying sessions mbili, tunaziita Q1 na Q2.
Qualifying sessions ndio itakayoamua nani kesho jumapili kwenye race awe namba moja tunavyoanza, nani awe mbili na nani awe wa mwisho (grid).
Qualifying imegawanyika katika sessions mbili, Q1 na Q2.
Qualifying 1 (Q1)
Tukianza na Q1, tunawachukua wale madereva waliokua nje ya top 10 ya marks za FP1, FP2 na FP3 na kuwashindanisha. Wawili watakaokua na speed kali kabisa wataenda Q2 kujumuika na wale 10 wenzie.
Waliobakia 10 wenyewe hawataenda Q2, wao watasubiria siku ya race wataanzia iyo nafasi waliyomaliza Q1.
Yaani yule wa tatu atakua namba 13, wa nne atakua namba 14, ivo ivo hadi 22.
Qualifying 2 (Q2)
Sasa tunakuja kwenye Q2 ambaoo tunagombaniana sasa nani kesho kwenye race atakaa namba 1 hadi namba 12?
Kwahiyo dereva atakaeset fastest lap kwenye Q2 ndio atakaekua pole (yaani nafasi ya kwanza/au tuseme atakaa mbele) kesho wakati wa race.
Ikumbukwe, Q1 na Q2 haushindani na dereva mwenzio, it’s race against time. Mnapewa dakika 15 tu, kwahiyo katika izo dakika 15 utafanya lap ngapi, na tunachukua lap ambayo umetumia muda mdogo kabisa (fastest lap) ndio tunaitumia kukujudge.
Day 3 (Jumapili): Race Day
Wakati wa race yenyewe, kutegemea urefu na aina ya circut, madereva wanatakiwa washindane kukamilisha idadi fulani ya laps. Mostly, race ni dakika 40 hadi 45, kwahiyo katika huo muda dereva unatakiwa umaintain speed, balance kuchakaa kwa tyre na jitahidi sana kuepuka crashes.
Kwa kuanza, jumapili asubuhi kunakuaga na warm-up session, inschukua kama dk 15 hadi 20 ambapo ni kama nafasi ya mwisho kuwapa madereva na team kujua vizuri chombo na circuit. Hii mara nyingi uwa haioneshwi labda uifatilie kwenye MotoGP TV yao officially.
Ikifika jioni nusu saa kabla ya race madereva na pikipiki wanajipanga kwenye grid kama inavyotakiwa kisha wanaanza race.
Race inaanza kwa formation lap ambayo ni lap moja hutakiwi kumuovertake wa mbele yako, lengo ni kupasha moto tyres na brakes.
Baada ya formation lap kila mtu anarudi kwenye grid, mnasubiria green lights then mnaanza race.
Tofauti na F1, kwenye MotoGP hakuna pit stop sijui kubadirisha tyre wala kufanya nini, mkianza mmeanza.
Labda ikitokea mabadiriko makubwa sana ya hali ya hewa ndio kunakua flag to flag race, yaani mnaruhusiwa kubadirisha pikipiki katikati ya race lengo kubadirisha tyres labda from dry kwenda tyres.
Points
Kama Formula 1, dereva anapata point ya kila race kutegemea na nafasi aliyomaliza.
Dereva wa kwanza anapata point 25, wa pili 20, wa tatu 16 na kuendelea hadi wa 15 anapata 1 waliobakia zero.
Kwahiyo unakua unakusanya point kila race katika msimu mzima, na mwisho wa msimu dereva mwenye point nyingi ndio Word Champion.
Teams pia zinakusanya point kutoka kwenye madereva wake iliowatoa. Nazi zinajumlishwa mwisho wa msimu tunapata kombe la team.
Constructor nae hivo hivo, lakini ikitokea mfano Ducati ametoa mshindi namba 1, 2, na 3 tunachukua point kubwa tu ya 1. Constructors hawana accumulated points kama teams (katika race). Ila nao tutajumlisha na tutapata mshindi wa kombe la constructors.
Sheria & Kanuni
Kama ilivyomichezo mingine, MitoGP pia ina kanuni, sheria na taratibu ili kufanya mchezo uwe safe, fair na exciting.
Kanuni zipo kwaajili ya madereva na team, pikipiki, race yenyewe nk.
Mfano kwa pikipiki, baadhi ya sheria za msimu huu ni:
- Engine iwe na cc 1000 tu, iwe four stroke, bila turbo wala supercharging.
- Power ni 240 hp tu.
- Maximum speed 340 km/h.
- Uzito iwe 158 kg tu, kwa kucompare Boxer BM-150 ina kilo 125.
- Mafuta tank lita 22 tu.
- Gear 6 tu.
- Nyingine ni technical sana kwetu mfano aerodynamics, aina ya suspensions na brakes.
Kuna mengi sana ya kujifunza kwenye MotoGP lakini nimeandikwa kwa ufupi, wengine watasaidia au nitajaribu edit.
MotoGP ni more exciting kuangalia sana sometimes naonaga kuliko F1 sema marketing yake haifikii F1.