Jiji la Arusha lamkana Mfanyabiashara Chambulo wadai 'amepotosha'

Jiji la Arusha lamkana Mfanyabiashara Chambulo wadai 'amepotosha'

Mkurugenzi wa Jiji mwizi huyo, hiyo ni dili kapiga na mfanya biashara alisema wazi wazi alilipa mil 24 ila wao walimpa risiti ya mil 3 anatakiwa kulipa, huo ni mchezo wa ofisi ya jiji, huyo Mkurugenzi mwizi sana anajulikana. Mkurugenzi ana mapete makubwa mikono yote kuliko msanii Daimond hapo kuna mtumishi wa umma kweli?

Alafu RC Makonda kasema anaunda kamati inayojumuisha wataalam wote kuchunguza sakata zima, iweje huyo Mkurugenzi wa Jiji la Arusha akimbilie kwenye vyombo vya habari na kuwaita kuongea nao, huyu anaanza kujihami kwani ni mwizi na anajulikana tabia ya wizi wake tokea Serengeti aliko kuwa mwanzani kabla ya kuhamia Arusha, tatizo ni huyo Mkurugenzi, mwizi kabisa huyo, na RC Makonda anza na huyo Mkurugenzi, anajifanya kuzunguka zunguka hiyo issue ndogo sana ni wizi wa wazi na mhusika ni huyo Mkurugenzi..
 
Kama wanadai Kodi mil.200 how comes watoe demand note ya mil.3?

Warudishe mil.21 walizopiga hakuna mjinga hapa
Hivi unadhani issue ni Mil 21 tu? huyo ni mtu mmoja kaamua kusema tu mara hii lakini hapo piga watu zaidi ya mia wanapiga hivyo kwa maana ni mabilioni ya pesa mapato ya serikali yanapotea, namaanisha mabilioni ni vile serikali tu ni kama hawako serious. Kama wako serious ungesikia wizara husika wameweka camp kufanya uhakiki na kuchukuwa hatua.
 
Mkurugenzi wa Jiji mwizi huyo, hiyo ni dili kapiga na mfanya biashara alisema wazi wazi alilipa mil 24 ila wao walimpa risiti ya mil 3 anatakiwa kulipa, huo ni mchezo wa ofisi ya jiji, huyo Mkurugenzi mwizi sana anajulikana. Mkurugenzi ana mapete makubwa mikono yote kuliko msanii Daimond hapo kuna mtumishi wa umma kweli?

Alafu RC Makonda kasema anaunda kamati inayojumuisha wataalam wote kuchunguza sakata zima, iweje huyo Mkurugenzi wa Jiji la Arusha akimbilie kwenye vyombo vya habari na kuwaita kuongea nao, huyu anaanza kujihami kwani ni mwizi na anajulikana tabia ya wizi wake tokea Serengeti aliko kuwa mwanzani kabla ya kuhamia Arusha, tatizo ni huyo Mkurugenzi, mwizi kabisa huyo, na RC Makonda anza na huyo Mkurugenzi, anajifanya kuzunguka zunguka hiyo issue ndogo sana ni wizi wa wazi na mhusika ni huyo Mkurugenzi..
Mapete kapewa ajilinde sasa naona kama yanaanza kuzidiwa hivi 😛
 
Kwa huu mtido wa kuanika taarifa za mteja ni udhaifu wa halmashauri ya jiji la Arusha ktk ukusanyaji wa mapato na wameonesha kukosa umakini kwa kiwangi kikubwa na kibaya kabisa TAMISEMI wana makubaliano ya kubadilishana taarifa na taarifa za mlipa kodi ni siri lakini hawa jiji wamemuanika mfanyabiashara taarifa zake za kikodi kitu ambacho ni kosa. Wao wanatakiwa kumalizana kisheria mahakamani na siyo kuleta kwenye social media. Hakika ningekuwa Samia ningemfuta kazi Mkurugenzi. Na uliyeleta uzi hapa kama unampenda Mkurugenzi wako futa hii thread
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa chama cha mawakala wa utalii Tanzania (TATO) Wilbard Chambulo kuituhumu Halmashauri ya jiji la Arusha kudai kuwa ameilipa Halmashauri hiyo milioni 24 kwenye kodi aliyokuwa akidaiwa lakini akashangazwa kuona taarifa za malipo alizopatiwa zinaonesha kuwa amelipa milioni tatu (3) pekee hivyo kuibua hisia hasi na madai ya uhujumu wa fedha za umma kwa baadhi ya maafisa wa Halmashauri ya jiji hilo leo, Jumatatu Aprili 15.2024 Halmashauri hiyo imekanusha vikali madai hayo

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Mhandisi Juma Hamsini amesema madai ya Chambulo ambaye ni mfanyabiashara na mdau wa masuala ya utalii wa muda mrefu si ya kweli, kwa kuwa baada ya kuibua tuhuma hizo Halmashauri ya jiji la Arusha na ofisi ya Katibu Tawala mkoa wa Arusha ilifanya ufuatiliiaji wa taarifa za mifumo ya kikodi za Chambulo (kwa kuwa hakuna fedha inayopokelewa mkononi), na baada ya ufuatiliaji huo wamejiridhisha masuala kadha wa kadha yanayoleta utata wa ushiri wake kwenye ulipaji wa kodi za serikali hususani zile anazopaswa kulipa kwenye Halmashauri hiyo

Mhandisi Hamsini amesema inadaiwa kuwa Chambulo anamiliki kampuni mbili tofauti ambazo ni 'The Tanganyika Wilderness Camps Limited' na 'Tanganyika Wilderness Camps Limited' ambazo kampuni zote hizo licha ya kwamba zinafanya shughuli zake kwenye maeneo mbalimbali lakini usajili wake umefanyika Arusha, lakini namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) inayotumika ni moja jambo ambalo linaleta majawabu kuwa mmiliki wa kampuni hizo ni mtu mmoja ambaye ni Wilbard Chambulo

Hata hivyo Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa kwenye kumbukumbu za kikodi inaonesha kuwa mauzo ya mfanyabiashara huyo Kwa mwaka yanafikia bilioni 90 ambapo katika fedha hiyo kodi anayopaswa kulipa Halmashauri ni milioni 200 na ushee ambayo kimsingi anadaiwa kwa kuwa licha ya kwamba anaeleza kulipa milioni 24 lakini 'demand note' aliyotumiwa na Halmashauri ni milioni tatu (3) pekee

Ameendelea kufafanua kuwa kampuni ya 'Tanganyika Wilderness Camps Limited' ililipa shilingi 3,347,002.75 kama 'service levy' na kampuni ya 'The Tanganyika Wilderness Camps Limited' ililipa 'service levy' ya shilingi 19,273,028.51 ambayo kiuhalisia inakaribia milioni 20, hata hivyo itambulike kuwa kampuni inayoonekana kwenye mfumo ni ile ya 'Tanganyika Wilderness Camps Limited' iliyolipa shilingi milioni tatu (3) na ushee, na ile kampuni ya pili ambayo ni 'The Tanganyika Wilderness Camps Limited' taarifa zake hazisomi kwenye mfumo husika

Suala la kampuni ya 'The Tanganyika Wilderness Camps Limited' kutoonekana kwenye mfumo linaleta ukakasi kuhusu taarifa sahihi za kodi za mfanyabiashara husika kwa kuwa kampuni hiyo inadaiwa fedha nyingi, hivyo alichokisema mfanyabiashara huyo hakina uhalisia kwa sababu amedai kulipa kodi ya milioni 24 kwa kuwa amejumlisha milioni tatu na ushee aliyolipa kwenye kampuni ya kwanza na milioni 19 na ushee aliyolipa kwenye kampuni ya pili, jambo ambalo halikubaliki kwa kuwa kila kampuni inajitegemea na inapaswa kulipa kodi yake kwa makadirio yake

Amesema inawezekana hiyo ni sehemu ya janjajanja inayotumiwa na mfanyabiashara huyo kwa kuamua kufungua kampuni nyingine kwa kuwa ameona kampuni ya awali ina deni kubwa, na ndio maana kampuni yenye deni kubwa la zaidi ya milioni 200 ndio ambayo haionekani kwenye mfumo

Aidha, Mhandisi Hamsini amedai kuwa amekuwa akimfahamu mfanyabiashara huyo kwa muda mrefu tangu wakati yeye (Mkurugenzi) akihudumu Halmashauri ya wilaya ya Serengeti, ambapo amekuwa akisumbua kwenye ulipaji wa kodi za serikali, na kuongeza kuwa licha ya sintofahamu yote hiyo lakini mfanyabiashara huyo hajawahi kufika kwenye ofisi za Halmashauri ya jiji la Arusha kueleza hoja zake badala yake amekuwa akiwakimbiakimbia maafisa wa Halmashauri pale wanapotaka kutimiza majukumu yao.....

(inaendelea)
 
Hii mbungi ni kali sana. Hilo neno BILIONI 90 litaamsha siafu wengi sana. Hadi sasa bado mechi iko droo.
Hiyo hela b90 huyo jamaa hajawahi kuimiliki lakini ukisikia mauzo ya hela hiyo maana yake
Mfano wewe una duka na kwa siku una wastani wa mauzo ya laki nne tu basi kwa mwaka utakuwa na mauzo ya zaidi ya milioni 100 hela ambayo hujawahi kumiliki kwa pamoja



Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Siku chache baada ya Mwenyekiti wa chama cha mawakala wa utalii Tanzania (TATO) Wilbard Chambulo kuituhumu Halmashauri ya jiji la Arusha kudai kuwa ameilipa Halmashauri hiyo milioni 24 kwenye kodi aliyokuwa akidaiwa lakini akashangazwa kuona taarifa za malipo alizopatiwa zinaonesha kuwa amelipa milioni tatu (3) pekee hivyo kuibua hisia hasi na madai ya uhujumu wa fedha za umma kwa baadhi ya maafisa wa Halmashauri ya jiji hilo leo, Jumatatu Aprili 15.2024 Halmashauri hiyo imekanusha vikali madai hayo

Akizungumza na wanahabari ofisini kwake Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Mhandisi Juma Hamsini amesema madai ya Chambulo ambaye ni mfanyabiashara na mdau wa masuala ya utalii wa muda mrefu si ya kweli, kwa kuwa baada ya kuibua tuhuma hizo Halmashauri ya jiji la Arusha na ofisi ya Katibu Tawala mkoa wa Arusha ilifanya ufuatiliiaji wa taarifa za mifumo ya kikodi za Chambulo (kwa kuwa hakuna fedha inayopokelewa mkononi), na baada ya ufuatiliaji huo wamejiridhisha masuala kadha wa kadha yanayoleta utata wa ushiri wake kwenye ulipaji wa kodi za serikali hususani zile anazopaswa kulipa kwenye Halmashauri hiyo

Mhandisi Hamsini amesema inadaiwa kuwa Chambulo anamiliki kampuni mbili tofauti ambazo ni 'The Tanganyika Wilderness Camps Limited' na 'Tanganyika Wilderness Camps Limited' ambazo kampuni zote hizo licha ya kwamba zinafanya shughuli zake kwenye maeneo mbalimbali lakini usajili wake umefanyika Arusha, lakini namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) inayotumika ni moja jambo ambalo linaleta majawabu kuwa mmiliki wa kampuni hizo ni mtu mmoja ambaye ni Wilbard Chambulo

Hata hivyo Mkurugenzi huyo ameeleza kuwa kwenye kumbukumbu za kikodi inaonesha kuwa mauzo ya mfanyabiashara huyo Kwa mwaka yanafikia bilioni 90 ambapo katika fedha hiyo kodi anayopaswa kulipa Halmashauri ni milioni 200 na ushee ambayo kimsingi anadaiwa kwa kuwa licha ya kwamba anaeleza kulipa milioni 24 lakini 'demand note' aliyotumiwa na Halmashauri ni milioni tatu (3) pekee...

MWisho

View attachment 2964450View attachment 2964451View attachment 2964452
Nilijua baada ya ile speech kwa Gavana wa BOT, CCM walichukizwa sana kwa sababu ameibua hoja ya kukatwa mrija muhimu kwa madon wa chama.

Sasa kinachoendelea ni umafia na soon atapewa jina baya. Speech ya hivi karibuni ya Hangaya ilikuwa inahusika sana sana.

Artificial Intelligent
 
"hakuna kulipa cash" halafu statement inaonesha malipo ni "cash".

Mkurugenzi wa jiji jitayarishe kuondoka, ni mwizi tu, hakuna zaidi.

Mtajuwa kwanini huyo ni mzungu.
Chambulo ni Maasai ...kuhusu tuhuma mwache mkurugenzi atoe ushahidi kuhusu hizo kampuni mbili..japo nazo hazijui vizuri ( TWC na KIBO)..
 
Inaonekana mfanyabiashara alikuwa akisaidiwa kutokulipa kodi sahihi huku na yeye akiwasaidia maafisa kuishi mjini; hiyo kujichanganya kwake kutapelekea kuangalia miaka yake yote kama alikuwa akilipa kodi sahihi, vinginevyo atalipa madeni ya miaka yake yote na penati.​
 
Inaonekana mfanyabiashara alikuwa akisaidiwa kutokulipa kodi sahihi huku na yeye akiwasaidia maafisa kuishi mjini; hiyo kujichanganya kwake kutapelekea kuangalia miaka yake yote kama alikuwa akilipa kodi sahihi, vinginevyo atalipa madeni ya miaka yake yote na penati.​
Watu wanachangia kimhemko ila technically tajiri kajichanganya mno. Watamnyoosha
 
Hiyo hela b90 huyo jamaa hajawahi kuimiliki lakini ukisikia mauzo ya hela hiyo maana yake
Mfano wewe una duka na kwa siku una wastani wa mauzo ya laki nne tu basi kwa mwaka utakuwa na mauzo ya zaidi ya milioni 100 hela ambayo hujawahi kumiliki kwa pamoja



Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Acha kunifundisha vitu ninavyovifanya kila siku. Kwa kiingereza tunaita TURNOVER
 
Mmh sidhani isee..
Mtu unaingiza billion 90 unaenda kujianika kwa sababu ya kodi ya 24 million.
Hii mbona kama haingii akilini sawasawa
Hiyo ni mzunguko wake tu na sio kwamba anazo hizo hela. Turnover yake kwa mwaka itakuwa inafika kabisa hiyo. Jamaa ana magari ya kitalii mengi mno na kila siku yako barabarani. Isitoshe ana hotel nyingi za kitalii. Chambulo ni tajiri mkubwa kwenye utalii ila uropokaji utamponza
 
Huyo jamaa ni bilionea ila mbona analipa kodi kiduchu.Kuna kitu hakipo sawa.
Kodi yaani tax inalipwa TRA tuu hiyo inayolipwa Halmashauri sio tax ni service levy.

Hii Service levy halmaushi wanatakuwa kulipwa si zaidi ya 0.3 asilimia ya mauzo.

Kwa upande wa tax kampuni inatakiwa kulipa asilimia 30 ya faida kama kodi kwenda TRA na kodi nyingine za zuio kama PAYE na kodi ya zuio za rent.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ni mzunguko wake tu na sio kwamba anazo hizo hela. Turnover yake kwa mwaka itakuwa inafika kabisa hiyo. Jamaa ana magari ya kitalii mengi mno na kila siku yako barabarani. Isitoshe ana hotel nyingi za kitalii. Chambulo ni tajiri mkubwa kwenye utalii ila uropokaji utamponza
Chamburo Ile bange yake inampeleka pabaya... Kwenye hili HAYUPO sahihi
 
Back
Top Bottom