Jiji la Arusha limekosa vituo vya daladala, pembeni ya barabara kuu ndio mwisho wa kituo

Jiji la Arusha limekosa vituo vya daladala, pembeni ya barabara kuu ndio mwisho wa kituo

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Hili jiji kwa miundombinu bado kabisa, ni zaidi ya miaka kumi (10) sasa tangu litangazwe jiji, lakini cha kushangaza na kusikitisha hakuna vituo maalumu vya kushusha na kupakia abiria.

Vile vituo vya njiani hakuna alama yoyote inayoonyesha kuwa hapa ni sehemu ya kushusha na kupakia abiria, kwa maana kuwa hakuna kibao wala sehemu ya abiria kumkinga na Mvua wala jua, mteja anasimama popote na anashushwa popote.

La pili kituo /stand ya daladala, hakuna kituo maalumu cha daladala kuingia bali zote hugeuzia barabarani au mwisho wa barabara ambapo hushusha na kupakia abiria hapo hapo, kwa jinsi inavyoonekana sehemu nyingi au mwisho wa vituo vilivyo vingi madereva na Makonda ndio waliopanga uwe mwisho wa kituo na si serikali.

Mfano mzuri daladala za kutoka mjini kwenda Lemara hazina kituo maalumu kilichotengenezwa huko Lemara mwisho bali hugeuzia barabarani.

Daladala za Kwenda Morombo kutoka mjini hadi Morombo pale hawajajengewa kituo maalumu cha kuingilia bali pembeni ya barabara ndo mwisho wao na hugeuzia hapo hapo.

Daladala za kwenda Usa nalo vile vile hawana kituo maalumu huko mwisho.

Daladala za kwenda Engosengiu nao mwisho wao ni barabarani ndipo hugeuzia gari zao hawajajengewa kituo maalumu cha kugeuzia ambapo abiria anaweza kukaa na kusubiri usafiri.

Na sehemu nyingine nyingi tu.

Ni wakati sasa wa jiji kuamka na kuandaa Ramani nzima ya jiji pamoja na kuandaa miundombinu /vituo maalumu vya kujengewa ili kuweka jiji katika hadhi yenye ramani nzuri.
 
Ngoja wahaya waje watunishe vifua "mbere"
 
Sister achana na stand ya daladala kuna mambo mengi hayapo sawa, Arusha haina stand kuu ya mabus yaani ni kila kampuni ya mabus ina stand yake na kushusha abiria na kuwapakiza kila kampuni inaamua sehemu yake kwa mfano BM coach, Dar Express na Kilimanjaro express ushusha abiria pale kwenye jengo la NHC pembeni ya Golden crest sehemu ambayo abiria akishuka inamlazimu kutembea hadi kilombero au klokoni kupata daladala ya route yake vivyo ivyo wanaoshushiwa stand ndogo.

Pia Arusha municipal wanafeli kwenye management ya masoko yao kwa mfano soko la kilombero mvua ikinyesha ni hapatoshi ni kuna tope balaa😂, kitu kingine Arusha waondoe vipanya bhana waweke coasters, waache ushamba coasters sio kwa ajili ya tourists tu.

Kitu nacho ipendea Arusha ina hali ya hewa nzuri, sema udongo wake sasa ni vumbi na tope😂ndo maana boots zinahusika sana,
Kama wakifanyia kazi ivyo vitu na hakika Arusha ni mkoa poa sana sema ndo ivyo imesaulika.
 
Sister achana na stand ya daladala kuna mambo mengi hayapo sawa, Arusha haina stand kuu ya mabus yaani ni kila kampuni ya mabus ina stand yake na kushusha abiria na kuwapakiza kila kampuni inaamua sehemu yake kwa mfano BM coach, Dar Express na Kilimanjaro express ushusha abiria pale kwenye jengo la NHC pembeni ya Golden crest sehemu ambayo abiria akishuka inamlazimu kutembea hadi kilombero au klokoni kupata daladala ya route yake vivyo ivyo wanaoshushiwa stand ndogo.

Pia Arusha municipal wanafeli kwenye management ya masoko yao kwa mfano soko la kilombero mvua ikinyesha ni hapatoshi ni kuna tope balaa😂, kitu kingine Arusha waondoe vipanya bhana waweke coasters, waache ushamba coasters sio kwa ajili ya tourists tu.

Kitu nacho ipendea Arusha ina hali ya hewa nzuri, sema udongo wake sasa ni vumbi na tope😂ndo maana boots zinahusika sana,
Kama wakifanyia kazi ivyo vitu na hakika Arusha ni mkoa poa sana sema ndo ivyo imesaulika.
Kweli Kabisa sijajua ni uongozi au ni ukiritimba, ile stand kubwa ya mabasi ipo pale tokea kabla ya uhuru hadi leo ni ilele, ni kweli kila makampuni mengi yamejianzishia vituo vyao wenyewe ndani ya jiji.

Soko la kilombero ndo mwisho wa matatizo. Halina mpangilio kuanzia mwanzo wa soko hadi mwishowa soko ni vurugu mechi
 
Aah pale soko kuu pananuka mikojo balaa maana makondakta wa Atown ni walevi balaa na muda wote wanalewa uku wanapiga debe
Haaaaa, hapo pembeni ya Soko ambapo ni barabarani ndo madereva wanapakia zao abiria hapo
 
CCM wakija watasema wapinzani walituchelewesha..sasa wako wao arusha nzima utasikia maendeleo ni hatua. Kiukweli huu ni upumbafu. Arusha mnakwama wapi mbona ni mji mkubwa mzuri sana. Kama mpo humu fanyieni kazi hayo maoni ya wa dau yahaupaisha sana mji wa arusha.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata darajani wanashusha na kupakia. Mfano daraja la mto Themi kati ya Sanawari na Mt. Hotel, kati ya Mafao Building na Clock Tower. Traffic wako busy na magari ya private.
 
Kweli Kabisa sijajua ni uongozi au ni ukiritimba, ile stand kubwa ya mabasi ipo pale tokea kabla ya uhuru hadi leo ni ilele, ni kweli kila makampuni mengi yamejianzishia vituo vyao wenyewe ndani ya jiji.
Soko la kilombero ndo mwisho wa matatizo. Halina mpangilio kuanzia mwanzo wa soko hadi mwishowa soko ni vurugu mechi
Arusha unaweza kusafiri ukaa hata miaka kumi ukija kurudi unakuta kwa asilimia kubwa jiji liko vilevile hakuna kilichoboreshwa au kubadilika.
 
Arusha inayosifiwa mitandaoni ni tofauti na Arusha yenyewe ilivyo kiukweli huo mji Bado upoupo tu, kuanzia mpangilio Hadi watu wake wako rafurafu tu, wajifunze Kwa majirani zao Moshi mji unavutia na kupendeza
 
Hata darajani wanashusha na kupakia. Mfano daraja la mto Themi kati ya Sanawari na Mt. Hotel, kati ya Mafao Building na Clock Tower. Traffic wako busy na magari ya private.
Sio kweli. Hapo mto themi kuna kituo kinaitwa Manchester
 
Arusha inayoimbwa ni tofauti na Arusha utakayoiona.
Arusha ni mji mzuri sana when it comes to private sector investments na ni sahihi kabisa kutoa Dar hamna mji mwingine unaoikaribia Arusha hata kidogo but when it comes now kwa public investments Arusha haiwezi hata kuikaribia iringa nahisi siasa hasa kuwa upande wa upinzani maendeleo yalicheleweshwa kanda hii ni aibu Arusha hakuna stendi wala soko la maana. Shame!
 
Back
Top Bottom