Uchaguzi 2020 Jiji la Mwanza lasimama usiku kwa ujio wa Tundu Lissu - Septemba 25

Mkuu hii kauli aliitoa lini?
Ahahaha,dah
 
Watanzania wasisahau kabisa kaprinciple tulikokubaliana kuwa wakileta vya kula watu wale kama kawaida, wakileta sebene na wasanii wa Fiesta, watu wacheze na kuserebuka.. Ila KURA zote kwa Lissu na wabunge wa Chadema. Lazma Jiwe arudi kwao mwaka huu. Hawezi kutupelekesha hivi!
 
Hawana jinsi kwa mahaba haya makubwa ambayo Watanzania tumemuonyesha Lissu the GREATEST.

Nikiangalia hizi kampeni za Lissu na nikikumbuka ile fateful day September 7th, 2017 naona kama vile naangalia Hollywood movie but in REAL LIFE.

Mpaka kufika 28 Oktoba 2020, naamini akina Sirro na Mabeyo watakuwa wamekwishaunga mkono juhudi za Lissu!
 
Kuna clip Afande kafurahi yupo pamoja na watu anampungia mkono Lissu.

Ni kwasababu Lissu anatetea Maslahi yao ya kuongezewa mishahara.
Ni kama Lissu kamaliza ngome zote za CCM.

Sehemu atakayochuana kura na magu ni Dodoma.

Wagogo mnisamehe kwanini mpo nyuma hivi?
Wagogo wako nyuma kwa sababu ni Wagogo kama Ndugai dhaifu fundi wa kutumia rungu hata kushinda Ubunge halafu bado wanampitisha bila kupingwa. Mpinzani wake Lissu amejichimbia Dodoma badala ya Dar es Salaam kuandaa mbinu za kutangazwa mshindi maana NEC watatangaza matokeo ya Uchaguzi toka Makao Makuu. CCM pia wapo hapo na leo Katibu Mwenezi amejaribu kujibu hoja zilitolewa kwenye kampeni kwa taarifa ya yaliyojiri Bungeni lililofungwa miezi mitatu iliyopita.
 
Siyo Lisu , kumbuka bado Majaliwa yupo analala Mwanza Siku ya 3 au 4 anavisit visiwani tu.
 
Kuanzisha kitu haimaani umri mkubwa
Sikiliza bwana mdogo, tupo tulioikataa TANU mfumo wa vyama vingi ulipofutwa mwaka 1965. Tuliikataa CCM ilipoasisiwa mwaka 1977 kwa vyama viwili TANU ya Tanzania bara na ASP ya Tanzania Visiwani kuungana. Mimi nimekuwa mpinzani kwa miaka hiyo yote hata kabla ya vyama vingi na hata sasa hivi si Chadema wala ACT ila ni mpinzani wa CCM.

Naamini chama kikikaa madarakani kwa muda mrefu kinalewa madaraka na kujifikiria kina hati milki ya taifa letu. Nafikiri umenielewa hadi hapo. Mambo ya ujinga ujinga sitaki, kwaheri...Tanzania yawezekana bila hiki chama ambacho eti kikisimamisha hata kichaa, anasukumiziwa uongozi.
 
haya maandamano ya usiku jiwe hatapata usingizi maana anawaza siku Lissu akikataa matokeo ya uongo itakuwaje.
mi namshauri auze ndege moja awarudishie machinga hela zao kabla ya uchaguzi itasaidia kupunguza hasira za wapiga kura.
Sio machinga tu, hata walio fukuzwa kazi na hawajalipwa stahiki zao, ambao hawajaajiriwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watasema hawana haja ya kufanya kampeni tena maana wameshashinda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakika huyu ni mkombozi aliyetabiriwa kuikomboa nchi kutoka kwenye makucha ya wakoloni weusi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…