Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir

Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir

Swali la kujiuliza ni iweje hii leo baada ya miaka 57 kupita Sheikh Suleiman Takadir anarejeshwa upya katika historia ya kupigani uhuru wa Tanganyika? Hiki ni kitendawili kinachongoja kuteguliwa.


Nani anamrejesha? hivi harakati za kudai uhuru,miaka hiyo zingefanyika mkoa wa kilimanjaro au mbeya,hilo baraza la wazee wa TANU,wajumbe wake wangekuwa wa imani ipi? wakati harakati za kudai uhuru zinaendelea DSM,je wakazi wa mikoa mingine walikuwa wamelala wakisubili wa islam wa DAR wawaletee uhuru?
anachoeleza mwandishi ni historia, na ndio ukweli, kukubali au kukataa ni uhuru wa kila mtu, haifuti historia yenyewe.
 
Hamna shida kaka binaadamu tunakosea. Nipo nasoma andiko ulilonirejesha nitakuja kuchangia baada ya kulisoma
 
anachoeleza mwandishi ni historia, na ndio ukweli, kukubali au kukataa ni uhuru wa kila mtu, haifuti historia yenyewe.

Myoyambend,
Juan Manuel
hajasome kitabu changu ndiyo sababu anajisemea tu kuhusu
Kilimanjaro.

Wakati wa ukoloni pakijulikana kama Jimbo la Kaskazini jimbo likiunganisha
sehemu za Arusha na Moshi.

Hebu tumpe Juan Manuel historia kidogo ya pale Moshi mjini na ikiwa hakutosheka
In Sha Allah nitampandisha Mgombani na haya ninayoweka hapa ni kutoka kitabu
cha Abdul Sykes:

"Inasemekana miongoni mwa matawi yote ya TANU nchini Tanganyika, tawi pekee lililoungwa mkono na wanawake na wao kuwa ndiyo nguvu kuu ya chama, lilikuwa tawi la TANU la Moshi mjini. Nguvu kuu ya TANU ilikuwa wanawake waliokuwa wakiuza mbege, pombe maarufu ya kienyeji huko Kilimanjaro. Uuzaji wa pombe huko Kilimanjaro ilikuwa ni kazi ya wanawake tu, wanaume hawakujishughulisha nayo. Mkuu wa kilabu cha pombe alikuwa mwanamke mmoja wa Kimasai, Mama Binti Maalim. Ingawa mume wa Binti Maalim, Jumbe Mohamed, alikuwa mtumishi wa serikali, na kwa hiyo alijitenga na siasa, hili halikumzuia mke wake, Binti Maalim kuwa mwanachama na mwanaharakati wa TANU. Binti Maalim alihakikisha kwamba kila mwanamke aliyekuwa akifanya biashara mahali pale alikuwa mwanachama wa TANU na alikuwa akitoa sehemu katika kipato chake kusaidia harakati za kudai uhuru. Wanachama wa mwanzo kujiunga na TANU walikuwa wale akina mama wauza pombe waliohamasishwa kujiunga na chama na Mama Binti Maalim.

Nafasi ya wanawake katika harakati mjini Moshi inaweza kuonekana katika katika safari yake ya pili ya Nyerere Kilimanjaro. Katika safari hiyo Nyerere alifikia nyumbani kwa Bibi Halima Selengia aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya tawi la TANU Moshi. Safari yake ya kwanza Nyerere alifkia KNCU Hotel (Hoteli ya Kilimanjaro Native Cooperative Union). Wakati huo TANU ilikuwa haijaota mizizi. Lakini katika safari yake ya pili wanachama walidai kwamba lazima Nyerere atayarishiwe malazi yake na TANU."
 
Pamoja na yote haya nini kifanyike ili kuondoa mivutano ya kidini na chuki za wazi zinazoanza kujitokeza kati yetui? Ningeshauri ili mjadala huu uwe na manufaa tujitahidi kwenda zaidi katika kutafuta suluhisho. Historia kama historia ni somo zuri na lina mambo mengi. Ukweli na relevancy ya historia inategemea mambo mengi. Ni nani alifanya utafiti na kuandika matukio ya kihistroria? Nini mtizamo wake binafsi wa kifalsafa na ni nini kilichomsukuma kufanya huo utafiti? Jambo ambalo muandishi "A" anaweza kuliona mhimu kuandikwa katika historia ya Tanzania ya leo, muandishi "B" anaweza, kutokana na mtizamo wake wa kifalsafa, akaliona sio mhimu. Historia ni kila kilichotokea jana na juzi. Hata haya tunayojadiliana sio ajabu mwanahistoria yeyote akayaona mhimu kuyaweka katika kumbukumbu za baadae. Kwa hiyo tusibishane sana katika usahihi wa alichokiandika kaka Mohammed bali tuangalie kama kinaweza kutusaidia katika kujenga Tanzania ya leo na kesho ya watu wanaoishi kwa upendo, umoja, amani na ushirikiano. Kuikosoa Tanzania ya jana kutakuwa na maana kama kutatupelekea kujenga Tanzania bora kuliko ya jana na sio kinyume chake. Kama kuikosoa Tanzania ya juzi kutapelekea tuishi katika maisha ya chuki na mgawanyiko kuliko juzi, kukosoa huko kutakuwa hakuna manufaa hata kidogo.
 
George Jinasa,
Msimamo wa serikali ni kuwa hakuna tatizo nchini petu.

Kama hakuna tatizo na kila kitu ni shwari hapawezi kuwa na utashi
wa kurekebisha chochote.

Nchi imeshikamana katika umoja.
 
Kwa maoni yangu, bila kujali nini msimamo wa Serikali, sisi kama watanzania, wenye nchi, tunahaki na wajibu wa kutafakari juu ya mstakbari wa kesho ya nchi yetu. Mijadala inayofanyika katika mtandao huu na mitandao mingine ya kijamii inaonesha pasna shaka kwamba kuna majibizano yanayoashiria chuki za kidini miongoni mwetu. Kama hali hii ikiachwa iendelee huku tukishuhudia madhara yake hayatakuwa sana kwa Serikali bali kwetu na vizazi vyetu.
 
Myoyambend,
Juan Manuel
hajasome kitabu changu ndiyo sababu anajisemea tu kuhusu
Kilimanjaro.

Wakati wa ukoloni pakijulikana kama Jimbo la Kaskazini jimbo likiunganisha
sehemu za Arusha na Moshi.

Hebu tumpe Juan Manuel historia kidogo ya pale Moshi mjini na ikiwa hakutosheka
In Sha Allah nitampandisha Mgombani na haya ninayoweka hapa ni kutoka kitabu
cha Abdul Sykes:

"Inasemekana miongoni mwa matawi yote ya TANU nchini Tanganyika, tawi pekee lililoungwa mkono na wanawake na wao kuwa ndiyo nguvu kuu ya chama, lilikuwa tawi la TANU la Moshi mjini. Nguvu kuu ya TANU ilikuwa wanawake waliokuwa wakiuza mbege, pombe maarufu ya kienyeji huko Kilimanjaro. Uuzaji wa pombe huko Kilimanjaro ilikuwa ni kazi ya wanawake tu, wanaume hawakujishughulisha nayo. Mkuu wa kilabu cha pombe alikuwa mwanamke mmoja wa Kimasai, Mama Binti Maalim. Ingawa mume wa Binti Maalim, Jumbe Mohamed, alikuwa mtumishi wa serikali, na kwa hiyo alijitenga na siasa, hili halikumzuia mke wake, Binti Maalim kuwa mwanachama na mwanaharakati wa TANU. Binti Maalim alihakikisha kwamba kila mwanamke aliyekuwa akifanya biashara mahali pale alikuwa mwanachama wa TANU na alikuwa akitoa sehemu katika kipato chake kusaidia harakati za kudai uhuru. Wanachama wa mwanzo kujiunga na TANU walikuwa wale akina mama wauza pombe waliohamasishwa kujiunga na chama na Mama Binti Maalim.

Nafasi ya wanawake katika harakati mjini Moshi inaweza kuonekana katika katika safari yake ya pili ya Nyerere Kilimanjaro. Katika safari hiyo Nyerere alifikia nyumbani kwa Bibi Halima Selengia aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya tawi la TANU Moshi. Safari yake ya kwanza Nyerere alifkia KNCU Hotel (Hoteli ya Kilimanjaro Native Cooperative Union). Wakati huo TANU ilikuwa haijaota mizizi. Lakini katika safari yake ya pili wanachama walidai kwamba lazima Nyerere atayarishiwe malazi yake na TANU."

Mkuu historia yako naikubali maana inazungumzia mambo madogomadogo ambayo ki ukweli historia za nchi huwa hazi ya accomodate, nakumbuka wakqti nipo high school pake Benjamin nilisoma HGL na kwa huu mchepuo ulinifanya kusoma vitabu vingi hasa vya riwaya na tamthiria na kuba kitabu kinoja kiliitea A letter from who reads" mwandishi simkumbiki ila nachotaka kusema hapa ni kwamba kunashairi moja lililokuwa likielezea difa alizopewa mfalme.mmoja wa china aliyeujenga ukuta mkubwa wa nchi ile lakin mwandishi baadae anauliza hivi huyu nfalme alikuwa pekeyake?, anaendelea kuuliza waapi watu waliochanganya udongo wakati wa ujenzi?, wako waapi walioveba kokoto za zege?, je hakuna hata aliyempikia mfalme wakati wa ujenzi?, yan mwandishi anaukiza maswali ambayo majibu take kuyapata ni ndoto.....

hicho ndicho ninachokuona wewe unajaribu jukifnya na mimi kila siku nimejuwa nikivutiwa sana na haya majina unayoyaeleza kama akina abdulsyjes na ally sykes, mzee tambaza mimi hata bado ntafuta kumjua baba yake mzazi wa raisi wetu mzee mrisho kikwete kwenye harakati za uhuru maaana naamini hata kama wewe hujamtaja lakini mimi naamin pia anamchango na uhuru wa hii tanzania yetu.......

mimi nisichokubaliana na wewe ni kwamba wewe unatumia dini kama sababu ya wao kutotajwa kitu ambacho mimi sikikubali.......

huu ni mfumo tu wa ulimwengu kama tunavyo msikia sana marehem Patrice Lumumba Kongo ila kuna watu wliomsaidia mpaka yeye kufika pale ila hatutakuja kuwajua kamwe....leo hii utasikia museven alimtoa Obote madarakani na kushika nchi unadhani alikuwa pekeyake?, mandela huyo hapo anamasifa kibao watu hawajui hata kama kuna mtu anaitwa Otambo kwa maana ya Oliver Tambo ambaye ndiye aliyekuwa mpambanaji mkuu muda woote mandela akiwa jela........

na hawa watu inatokea tu nyota inawawakia kuwa maarufu kuliko wenzao kitu ambacho binafsi sikipendi ila ndivyo inavyoonekana kuwa kila mahali.......na nataman tuachane na mfumo huu kama ikiwezekana

ninachomaanisha ni kwamba kutotajwa kwa ndugu woote waliopigania uhuru au kutoa mchango kwenye hayo mapambano yapaswa kukumbukwa tena kila mkoa na si tu dar........ila kusema kwamba waislam hawatamkwi sababu ya dini yao hilo nalikataa jwa nguvu zangu zote kwani kama ingekuwa ni mkakati hakuna mtu anayewezabkushindana na watu wenye imani...

sasahivi kuna matishio mengi ya ugaidi na bahsti mbayabnikikufauatisha mtindo wa kutumia majina unaoutumia wewe utakuta wengi kama si wote watuhumiwa wa ugaidi huwa na majina ya kiislam na ulishawahi kusikia kiongozi yeyote akisema waislam ni magaidi?, hakuna watasema tu kuwa kuna magaidi wamekutwa na siraha kwenye nyumba ya ibada........

hapa sababu ni ile ile hakuna mtu aliyewahi kupigana kujaribu kuiua imani flani akafanikiwa kwani imani ni kitu kingine..........

nilifurahi kwente mahojiano yako na yule mtu wa studio pale alipokuuliza kwa jazba kuwa TANU ilifika mahala ikamezwa na dini zingine njebya waisam na wakaamua hata kukataza "asalam aleykum"(mniwie radhi kama nimeikosea) kama salaam na wewe ukamjibu jibu zuri sana kuwa waislam wenyewe kwa kuyasoma mazingira hawakutaka tanu kuonekana kama chama cha kiislam......

na ndio waliokuwa hata hatwaitikii wakisalimiwa swali ni je kama watu wenyewe walikataa udini kwenye chama unadhan kwenye serikali si itakuwa zaidi...

kikubwa hapa ni kwamba kwakweli watu walishachoka na ukoloni na walijuwa hawajali ni nani atakaye watoa kwenye hayo makucha bila kujali dini rangi walankabila, yan wao walikuwa hawawazi kabisa huu udiniudini na ndiyo maana nadhan walishinda.....

siyo kwamba wadini hawakuwepo walikuwepo ila walishindwa na baada ya na mambo yana wawia magum wakaamua kujiunga tanu ila mimi siiamini hiyo nia yao kwa dhat kwan naamin walitua zile slogan za "if you cant fight him join him" na kwa staili hii malalamiko hayatakoma na ndito maana tunataka mtu yeyote mwenye mapenzi mema na nchi yetu asilete story za uchochezi kama hizi za kwako....

mi ninaamini kwa story kama hizi za kwako kuna mtu mahala alikosa kazi kihalali kabisa ila akisha kukudoma hapa na sababu jinalake ni la kiislam ataanza kuchukia viongozi na watanzania woote wanaopenda amani na mtu huyo itakuwa tahisi hata kwa yeye kujiua huku akiondoka na wengine kitu ambacho si hatari tuu bali ni kibaya.............

kwani duniani kote pepetrous woote wa majanga ama mauaji ya kimbali wao wenyewe huwa hawafi ila wanawasababishia wengine kuangamia kwa ajili ya ambition zao na ndiyo maana sintaacha usemi wangu wa "MCHEZO WAO MAUTI YETU"

hebu acha mr Mohammed.
 
Myoyambend,
Tumekwenda vyema ila kwa hilo neno "acha."
Sikulipenda kwani ni karipio.

TANU haikupata kumezwa na yoyote.

Waasisi wake na waliokuwa mstari wa mbele ukiwatoa wachache
kama Zuberi Mtemvu na Said Chamwenyewe hapo New Street
walikuwapo hadi 1963 walipofukuzwa katika mkutano uliofanyika
Arnautoglo Hall.

Ningependa unifahamishe kama umesoma kitabu cha Abdul Sykes
maana inaelekea kutoka katika hoja zako huijui historia ya TANU.

Ili tuwe na mjadala wa maana ni lazima wewe ulijue somo lenyewe
kwanza.

Nifahamishe kama umesoma kitabu changu.
 
Myoyambend,
Tumekwenda vyema ila kwa hilo neno "acha." Sikulipenda kwani ni karipio. TANU haikupata kumezwa na yoyote. Waasisi wake na waliokuwa mstari wa mbele ukiwatoa wachache kama Zuberi Mtemvu na Said Chamwenyewe hapo New Street walikuwapo hadi 1963 walipofukuzwa katika mkutano uliofanyika Arnautoglo Hall. Ningependa unifahamishe kama umesoma kitabu cha Abdul Sykes maana inaelekea kutoka katika hoja zako huijui historia ya TANU. Ili tuwe na mjadala wa maana ni lazima wewe ulijue somo lenyewe kwanza. Nifahamishe kama umesoma kitabu changu.

Naomba nikutake radhi mkuu kwa hilo neno "acha" kama ulivyo lifasiri ila sikumanaanisha kukaripia bali kuonyesha hatari ya uchochezi.

Pia sijapat kukisoma kitabu chochote bali kuperuz vitu ninavyoitaka kwa kuputia google tuu, so utanisaidia kama nikikipata mkuu..
 
Jembepori,
Uchochezi uko wapi katika kazi zangu?
Ndipo nimekuuliza umesoma kitabu changu?

Bahati mbaya hukunipa jibu.

Nilichofanya mimi ni kuiweka sawa historia ya kupigania uhuru wa
Tanganyika ambayo nina ushahidi kulikuwa na njama ya kuifuta na
sababu kubwa ni kuwa kwa kiasi kikubwa sana historia hii ni historia
ya Waislam wa Tanganyika.

Sasa ikiwa unataka ushahidi wa haya nikuelezayo nifahamishe nitoe
darsa kwa ajili yako na kwa faida ya Majlis.

Hakuna uchochezi katika kusema kuwa Wakikuyu ndiyo kabila pekee
Kenya lililonyanyua silaha kupambana na ukoloni.

Huo ndiyo ukweli wa historia ya Kenya hata kama Wajaluo wataingia unyonge.
 
Jembepori,
Uchochezi uko wapi katika kazi zangu? Ndipo nimekuuliza umesoma kitabu changu? Bahati mbaya hukunipa jibu. Nilichofanya mimi ni kuiweka sawa historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika ambayo nina ushahidi kulikuwa na njama ya kuifuta na sababu kubwa ni kuwa kwa kiasi kikubwa sana historia hii ni historia ya Waislam wa Tanganyika. Sasa ikiwa unataka ushahidi wa haya nikuelezayo nifahamishe nitoe darsa kwa ajili yako na kwa faida ya Majlis. Hakuna uchochezi katika kusema kuwa Wakikuyu ndiyo kabila pekee Kenya lililonyanyua silaha kupambana na ukoloni. Huo ndiyo ukweli wa historia ya Kenya hata kama Wajaluo wataingia unyonge.

Hapo ndipo unaponichanganya mkuu, kusema kuwa waislam ndiyo waliopigania uhuru si kweli, sema kulingana na makoloni yaliyotutawala pwani ilikuwa na waislam wengi, na hatubishi kuwa kwa namna moja ama nyingine watu mbalimbali walijitahidi kupigania uhuru kwa nyakati tofauti..............

sitaki kusema kwamba yan watu walikuwa wanauchekelea tu ukoloni mpaka nyerere alipokuja, hapana........

jitihada zilikuwepo tangu vita vya majimaji na akina isike tabora, mirambo kiyungi, mkwawa yana watu walikuwa wanajitahid kupingana na ukoloni kwa uwezo waliojuwa nao, kikabila, kimkoa na vinginevyo.....

hata mwl nyerere alipokuwa anafundisha st mary pale tabora alikuwa katibu wa TAA mkoa wa tabora na alikuwa anakuja mara kwa mara dar es salaambkwenye vikao, so uongozi wa TAA taifa ulijuwepo na yeye by then alikuwa bwana mdogo tuu...........

ninachotaka kueleza hapa ni kuwa nyerere naye anamchango wake kama ukipenda basi tuite kwa niaba ya wasio waislam na mimi naamini kwa sababu yeye alifanikiwa ndiyo maana anatajwa sana kuliko waliomtangulia, hii ni kawaida tu maana hata darasana mtu anayefauru ndiye anayepongezwa sasa huku kufanikiwa kwake ama ilikuwa bahati yake ama ilikuwa uwezo wake binafsi wa kuwafanya watu wamkubali na kumwamini mpaka kumtuma UNO ilihali waislam walikuwa wengi siwezi kulionhelea hilo........

ninachosema ni kwamba unaweza kusema wakikuyu ndiyo kabila pekee waliopigania uhuru wa kenya ila huwezi kusema waislam ndiyo watu wa pekee wakioupiganua uhuru wa tanganyika.......

eti mwisho wakamtuma tu mkristo aende UNO yan hiyo si tu utani pia itakuwa ni ajabu kwani mahala kama UNO huwez tu kwenda kwa kujisikia ama kutimwa tu na watu bilakichwachako kuwa kamili.....

ulipata kuletakisa cha mtu mmojq kutoka moshialiyeenda UNO hata kabla ya nyerere ila ulihitimisha vizuri kwa kusema kuwa hakufanikiwa ingawa alisindikizwa..........

kazima ukubali kuwa ingawa ji lazima kuwataja na wazee wetu wengine waliomsaidia mwl kupigania uhuru, pia nyerere kama mtu anamchqngo wake na yeye anapaswa kukumbukwa na kuenziwa pia,...........

sioni ni waapi historia inapotoshwa ilihali aliyeenda UNO ni nyerere, aliyesain mabadilishano ya hati za uhuru karimjee alikuwa nyerere, aliyeenda kukagua gwaride la malikia akiwa na gavana alikuwa nyerere, aliyepokea hata hati uhuru alikuwa ni yeye, sasakama tunataka kuwakumbuka na watu walio muazima suti, ama wale waliomwandikia speech, ama hata waliompikia tuwakumbuke tu kwani ni haki yao..............

sasa kama hawatajwi na hakuna shaka kuwa nyerere ndiye aliyeenda kudai uhuru ama mengineyo nikiyoyataja hapo juu, kama kuna moja ambalo si kweli utuambie lakin kama ni hizi story za watu kusahaulika nadhan nimeshalisemea vya kutosha...............
 
Hapo ndipo unaponichanganya mkuu, kusema kuwa waislam ndiyo waliopigania uhuru si kweli, sema kulingana na makoloni yaliyotutawala pwani ilikuwa na waislam wengi, na hatubishi kuwa kwa namna moja ama nyingine watu mbalimbali walijitahidi kupigania uhuru kwa nyakati tofauti..............

sitaki kusema kwamba yan watu walikuwa wanauchekelea tu ukoloni mpaka nyerere alipokuja, hapana........

jitihada zilikuwepo tangu vita vya majimaji na akina isike tabora, mirambo kiyungi, mkwawa yana watu walikuwa wanajitahid kupingana na ukoloni kwa uwezo waliojuwa nao, kikabila, kimkoa na vinginevyo.....

hata mwl nyerere alipokuwa anafundisha st mary pale tabora alikuwa katibu wa TAA mkoa wa tabora na alikuwa anakuja mara kwa mara dar es salaambkwenye vikao, so uongozi wa TAA taifa ulijuwepo na yeye by then alikuwa bwana mdogo tuu...........

ninachotaka kueleza hapa ni kuwa nyerere naye anamchango wake kama ukipenda basi tuite kwa niaba ya wasio waislam na mimi naamini kwa sababu yeye alifanikiwa ndiyo maana anatajwa sana kuliko waliomtangulia, hii ni kawaida tu maana hata darasana mtu anayefauru ndiye anayepongezwa sasa huku kufanikiwa kwake ama ilikuwa bahati yake ama ilikuwa uwezo wake binafsi wa kuwafanya watu wamkubali na kumwamini mpaka kumtuma UNO ilihali waislam walikuwa wengi siwezi kulionhelea hilo........

ninachosema ni kwamba unaweza kusema wakikuyu ndiyo kabila pekee waliopigania uhuru wa kenya ila huwezi kusema waislam ndiyo watu wa pekee wakioupiganua uhuru wa tanganyika.......

eti mwisho wakamtuma tu mkristo aende UNO yan hiyo si tu utani pia itakuwa ni ajabu kwani mahala kama UNO huwez tu kwenda kwa kujisikia ama kutimwa tu na watu bilakichwachako kuwa kamili.....

ulipata kuletakisa cha mtu mmojq kutoka moshialiyeenda UNO hata kabla ya nyerere ila ulihitimisha vizuri kwa kusema kuwa hakufanikiwa ingawa alisindikizwa..........

kazima ukubali kuwa ingawa ji lazima kuwataja na wazee wetu wengine waliomsaidia mwl kupigania uhuru, pia nyerere kama mtu anamchqngo wake na yeye anapaswa kukumbukwa na kuenziwa pia,...........

sioni ni waapi historia inapotoshwa ilihali aliyeenda UNO ni nyerere, aliyesain mabadilishano ya hati za uhuru karimjee alikuwa nyerere, aliyeenda kukagua gwaride la malikia akiwa na gavana alikuwa nyerere, aliyepokea hata hati uhuru alikuwa ni yeye, sasakama tunataka kuwakumbuka na watu walio muazima suti, ama wale waliomwandikia speech, ama hata waliompikia tuwakumbuke tu kwani ni haki yao..............

sasa kama hawatajwi na hakuna shaka kuwa nyerere ndiye aliyeenda kudai uhuru ama mengineyo nikiyoyataja hapo juu, kama kuna moja ambalo si kweli utuambie lakin kama ni hizi story za watu kusahaulika nadhan nimeshalisemea vya kutosha...............

We'll said.. Bravo..
 
Jembepori,
Nakuuliza tena umesoma kitabu cha Abdul Sykes?

Kisha nikakuuliza nikupe ushahidi wa kufuta historia ya Waislam katika
TANU na harakati za kupigania uhuru?

Ukinipa majibu ya maswali haya tutakwenda kwa mstari kufahamishana
iweje historia ya TANU imekuja kuandikwa upya na Mohamed Said
na sasa mwaka wa 18 unaingia hajajitokeza profesa yoyote nchini kwetu
kukipinga kitabu hiki?
 
Jembepori,
Nakuuliza tena umesoma kitabu cha Abdul Sykes? Kisha nikakuuliza nikupe ushahidi wa kufuta historia ya Waislam katika TANU na harakati za kupigania uhuru? Ukinipa majibu ya maswali haya tutakwenda kwa mstari kufahamishana iweje historia ya TANU imekuja kuandikwa upya na Mohamed Said na sasa mwaka wa 18 unaingia hajajitokeza profesa yoyote nchini kwetu kukipinga kitabu hiki?

Mi sijawahi kuvisoma info zangu huwa nazipata google
 
2013,
Huna moja ulijualo katika.Vita ya Maji Maji.

Ushawasikia Sheikh Sultan Hassan bin Massaninga au Sheikh
Sultan bin Abdulrauf
au Selemani Mamba?

Unajua jina la Mkwawa kuwa ni Abdallah unajua alikuwa na
nduguye katika majemadari wake anaitwa Yusuf?

Unajua Mkwawa alikuwa na rafiki yake Muhammad bin Khalfan
maarufu kwa jina la Rumaliza?

Ushapatapo kuisikia historia hii popote?
Hayo ya suti usiyalete unapozungumza na mimi.

Mimi siko hapa Majlis kufanya upuuzi.
Niko hapa kufanya mjadala wa heshima.
 
Jembepori,
Kisome kitabu cha Abdul Sykes uone ni mwaka gani alichukua
uongozi wa African Association kutoka kwa baba yake ni kipi
alifanya kuipa TAA sura ya chama cha siasa na ilikuwa mwaka
gani.

Soma ukutane na Chief Kidaha Makwaia 1950/51 uone mkakati
wa kuunda TANU na nini kilitokea.

Google haiwezi kukupa haya yote.

Soma ushangae iweje historia ya TANU iandikwe na wazalendo
hawa wote wasitajwe?

Hivi unajua kuwa mpaka leo baadhi ya mafaili ya TANU yako
katika nyaraka za marehemu Ally Sykes mdogo wake Abdul?

Hili limewezekana vipi?

460%3E_632240.jpg


Wanamajlis,
Ingia hapa usome pitio la kitabu hiki:
https://www.jamiiforums.com/jamii-i...-nyakati-za-abdulwahid-sykes-1924-1968-a.html
 
2013,
Huna moja ulijualo katika.Vita ya Maji Maji. Ushawasikia Sheikh Sultan Hassan bin Massaninga au Sheikh Sultan bin Abdulrauf au Selemani Mamba? Unajua jina la Mkwawa kuwa ni Abdallah unajua alikuwa na nduguye katika majemadari wake anaitwa Yusuf? Unajua Mkwawa alikuwa na rafiki yake Muhammad bin Khalfan maarufu kwa jina la Rumaliza? Ushapatapo kuisikia historia hii popote? Hayo ya suti usiyalete unapozungumza na mimi. Mimi siko hapa Majlis kufanya upuuzi. Niko hapa kufanya mjadala wa heshima.

Kwanza kabisa ningerudi kwenye habari za Shekh Takadir.

Ingekuaje TANU kuongozwa na wasiosoma kama alivyokuwa akitaka shekh Takadir kwakuwa tu ni waislamu?
Umoja ni nguvu na kidole kimoja hakivunji chawa..lakini Takadir wanataka akili ndogo iongoze akili kubwa. Why is that?!

Kama waislamu ni wengi kwanini basi walimpinga shekh Takadir?

waislamu wa TANU, waliona kosa gani la Takadir.ambalo Leo hii wewe mwandishi wa kitabu hujaliona?

Nani alaumiwe nyerere au waislamu waliomkataa shekh Takadir?

Jambo jingine.. Shekh Takadir amefutwa katika historia kwasababu ya kupalilia UDiNi. Na hakuwa na malengo sawa na wapigania Uhuru wa nchi na wanaharakati wengineo. Yeye alikuwa mdini. Hakuna haja ya kumweka kwenye historia kwasababu hakushiriki Bali alikuwa na malengo yake ya udininaizeshen. Aliichukulia TANU kama Chombo cha kimaslahi kwa dini yake zaidi. Aliwakataa wasomi kwasababu ya dini zao na sio uzalendo wao.

Takadir Hakuwa mzalendo. Sioni sababu zenye mashiko za kumrudisha kwenye historia na wala kulitaja jina lake popote.

Je upo umuhimu wa kuwataja mashujaa wa usaliti katika historia ya nchi yetu
I don't think so...

Pia historia yako inaonyesha wazi kuwa wakristo ndio walikuwa wamesoma kabla ya Uhuru.
Na waislamu hawajasoma. Nyerere aliikuta hii hali japo aliendelea na harakati za kupigania uhuru wa nchi. Nyerere alimtaja 'Ujinga" kama adui wa maendeleo. Watanzania waliafikiana na fikra zake. Na alijitahidi kubadilisha hali ili waislamu wapate Elimu ili kuleta uwiano sawa.
Nguvu ya nyerere inatokana na kupata sapoti ya waislamu na wakristo. Historian imelenga kuwakumbuka watanzania waliokuwa mstari wa mbele kuleta umoja na mshikamano. Ili tujivunie nchi yetu.

Haikua kazi rahisi lakini aliweza, kutaifisha shule nyingi sana za kanisa zenye utamaduni wa kikristo na kuzifanya za watanzania. Nyerere anaweza kuwa na mapungufu ya hapa na pale lakini alikuwa na dhamira njema.alifanya makosa kwa dhamira njema. Mfano kuunda vijiji vya ujamaa, kuingana na Zanzibar n.k.

Mpaka hapa naamini kabisa vitabu vyako havipendezi na vinaweza kutumika kufarakanisha watanzania kwa misingi ya dini zao kama alivyotaka shekh Takadir mpaka waislamu wakamkataa.

Pia Nina imani tukitumia assumption' ya akili ya shekh Takadir, ni kwamba hata kama tungepata Uhuru. Wakristo wasingekubali kuwa kutawaliwa na waislamu. Na pengine wangedai Uhuru wao. Kama kule sudani. Na Zanzibar ingeendelea kutawaliwa na sultani Mwarabu.

Kuhusu hoja yako hapo juu. Ni kama unataka kusema Mkwawa alipigana Jihadi dhidi ya wakoloni wa kijerumani. Hii ina maana mkwawa alikuwa Jihadists. I can't chew that either...
 
Hiyo kuhusu Moshi mjini Bw.Mohammed uko sahihi kabisa hakuna mushkel.Naomba pia utupe mchango wa Mzee Yussuf Ngozi baba yake msanii Mzee Chilo
 
Oldonyosambu,
Soma kitabu cha Abdul Sykes utakuta habari za Yusuf Ngozi.
 
Back
Top Bottom