Jinamizi la Udini Tanzania: Utabiri wa Sheikh Suleiman Takadir

Ukweli wanaujua laikini wanajitoa ufahamu hongera sana mzee wetu Mohamed Said kwakuweka wazi kila kitu mbele ya hadhara na hakika umefanikiwa kututoa upofu sisi ambao tulikuwa hatujui kilichofanywa na kinachofanywa na hawa madhali dhidi ya dini ya kweli
 
Last edited by a moderator:
Wakatoliki wampe tu JKN Utakatifu maana chuki mliyo nayo juu yake ni kubwa mno.

Usilolijua ni kama usiku wa kiza kinene.

Kwa JKN kuwa mtakatifu mmh.

Ni rahisi kwa ngamia kupenya katika tundu ya sindano kuliko JKN ...

Kwa alichofanya na kuwafanyia wananchi wake KIUCHUMI na hata kijamii ndio athari zake zinaonekana sasa hivi. na yote hayo ni matunda ya uongozi wake uliokuwa wa mabavu na vitisho na unafiki kibaaaaao.

Poleni
 
Hakika wewe ni Great Thinker ulietawaliwa na busara tofauti na Mazoko aliejikita ktk majivuno na jazba
Mazoko,
Sijui kwa nini hii makala ya Sheikh Suleiman Takadir imekukasirisha.

Hapa tulipofika panatosha.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mazoko hili kashaambiwa sana sijui kwanini hataki kutoka kwenye kichaka cha udini.

 
Last edited by a moderator:
Udini mnauhubiri nakuueneza nyie na sio mzee Mohamed Said kwakuwa nyie ndo mmekewa mstari wambele kuudhoofisha uislam ktk nyanja zote nia yenu ikiwa ni kutaka kuisambaratisha dini ya kiislam kitu ambacho hamtokiweza.
Mzee Mohamed ametoa na ushahid juu ya wanaoeneza chuki za udin kuwa ninyie haohao mkitumia njia mbalimbali ikiwa ni pa1 na baraza la mitihani ili mtimize malengo yenu.
 
Last edited by a moderator:
Tunahitaji hitimisho, sio kutoa history. Tunataka tujue waislaam wanataka nini ili waridhike maana haya malaamiko bila kujua tunafika vip tamati ili wenzetu waridhike maana Tanzania ni ya wote

Hitimisho la hili ni KUTENDA HAKI KWA JAMII YOTE KAMA WANANCHI NA KUHAKIKISHA WANANCHI WOTE WANAKUWA KATIKA DARAJA MOJA KUSIWE NA MATABAKA kama ilivyo sasa TGk kwa dini moja kujiona ndio waliosoma saaaana na wana haki zaidi ya dini nyengine.

Haki ikisimama basi kutakuwa hakuna shida. Ikumbukwe kuwa HISTORIA ni kama PEMBE LA NG'OMBE huwezi kulificha.

Sasa ndio mnaona Historia inavyojirudia.

Msipoziba ufa mtajenga ukuta.


Muitishe mjada wa kitaifa kulijadili hili la udini bila kificho wala soni na baadae mtafute ufumbuzi wake.
 
Nyie ndo mmejificha kwenye kichaka cha udini huku mkijifanya mnahubiri amani,nia yenu mnatka muachwe mfanye upuuzi wenu dhidi ya wenzenu,hebu fuatilia humuhumu jukwaani wala usiende mbali,kati ya waislam na wakristo ambao ni chanzo cha mada zakichokozi zinazoambatana na maneno ya kejeli dhidi ya wenzao?Naamini kama hutojitoa ufahamu utagundua nani mwanzilishi wa chokochoko za kidin.
Mkuu Mazoko hili kashaambiwa sana sijui kwanini hataki kutoka kwenye kichaka cha udini.
 
Last edited by a moderator:

imani ya ukweli haisambaratishwi na mwanadamu .na.Mungu wa kweli hapiganiwi wala kutetewa kwa mapanga , au aina yoyote ya silaha...ukiona imani yoyote inapiganiwa na wanadamu kwa kutumia nguvu basi kuna haja ya kuichunguza imani hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo ni kwamujibu wa imani yako,si kila imani,ukiitaka pepo nilazima uipiganie kwa hali na mali ili kuiweka sawa njia inayokupeleka peponi ili uonyeshe nia thabit yakuitaka pepo.Mungu ameshaahidi kuwa atailinda na kamwe hakuna atakaeweza kusambaraTisha dini yake.So njia yakuilinda nikupitia sisi wanaadam ambao tumepewa nguvu na akili zakutuwezesha kuipigania kwakufuata mafundisho ndani ya kitabu kitukufu.
imani ya ukweli haisambaratishwi na mwanadamu .na.Mungu wa kweli hapiganiwi wala kutetewa kwa mapanga , au aina yoyote ya silaha...ukiona imani yoyote inapiganiwa na wanadamu kwa kutumia nguvu basi kuna haja ya kuichunguza imani hiyo.
 

basi hiyo imani inawafaa sana wababe kama Hittler, Musollini, Panya Road, Al -Shabaab, Al Qaeda, Boko Haram...wauaji wa vikongwe huko shinyanga na wasiojali utu wa mwanadamu kama wauaji wa albino
 
Mkuu Mazoko hili kashaambiwa sana sijui kwanini hataki kutoka kwenye kichaka cha udini.

Ngongo,
Unatumia lugha kali kuwa "nishaambiwa sana."

Hiyo "sana" nadhani una maana watu wengi na mara nyingi.
Mimi hayo yote siyakubali kwa kuwa si kweli.

Hilo la kwanza.
Pili ni kuwa mimi siandiki hicho unachokiita wewe "udini."

Unasema "kichaka cha udini."

Nami nishakuambia sana kuwa maandishi yangu yamekuwa katika
"catalogue" ya Islam/Politics/History.

Mara kadhaa nimekueleza hili na nikakuelekeza kama utapenda
kujua zaidi angalia Library of Congress maandishi yangu yako
katika "catalogue" ipi.

Sijaishia hapo nimekupa hadi paper ambazo nimewasilisha katika
vyuo mbalimbali na vitabu nilivyoandika na vikachapwa na wachapaji
wakubwa wa dunia - Oxford University Press, Nairobi na New York.

Itawezekana vipi hawa wakachapa "udini?"

Sasa nakuongoza kitu kingine.

Haya ninayokuandikieni hapa takriban yote yanatoka katika kitabu
changu, "The Life and Times of Abduliwahid Sykes..." (1998).

Kitabu hiki kimefanyiwa "review" na John Iliffe (University of Cambridge)
Jonathon Glassman(Northwestern University), James Brenan (London
School of Oriental and African Studies).

Baadhi ya hawa waliofanya "review" ya kitabu changu nimeshafanyanao
mijadala ya wazi kwenye vyuo vyao huko kwao.

Hakuna yoyote kati ya hao kasema kuwa ninaandika "udini.''

Nadhani umenielewa na sitegemei tena kama utakuja kunihoji tena
kuhusu hicho unachokiita, "udini."

Lakini baada ya kukupa maelezo haya ikiwa utakuja tena kwangu na
hoja hii nitajua hakika lipo tatizo upande wako.
 

Mazoko,
Naam natafakhar kuwa nimeandika na Oxford University Press.

Hao si mchezo bwana.
Wakichapa kazi yako jua wewe una kitu cha ziada.

Uliza utaambiwa.
 

mimi binafsi pamoja na Ukristo wangu wote (pia ninao ndugu kadhaa Waislamu) naheshimu sana maandiko ya huyu mzee Mohamed. sana tu.

ninaweza nisiwe nakubaliana naye kwa content ya material yake lakini ninapenda jinsi anavyokwepa kutumia maneno makali kama uliyotumia wewe ndugu.

na hapa ndipo ninarudi kwa mzee wangu Mohamed. inawezekana pengine nia yako ni njema unapoleta haya maandiko humu kwenye mitandao, lakini kumbuka kuwa yanapokuwa yanaonekana kuegemea upande mmoja wa imani lazima sentiments zinazokinzana zitaibuka na kufanya watu waanze kuonyeshana chuki zao dhahiri.

hizi chuki zinazozalishwa kwenye mitandao kutokana na mada za aina hii zina tendency ya kuwa na trickle-down effect kwenye jamii pana.....vijana wana-conceive doctrine ya "ufia dini" na kupelekea kufanya yale ambayo sisi sote hatutaki yatokee kwani hatima ya madhara (athari) yake haitachagua imani ya mtu!

narudia tena, nia yako inaweza kuwa njema sana lakini inaonekana dhahiri kuwa-polarise wasomaji wako na kuzaa chuki kubwa baina yao (mimi si mmoja wa hao, lakini kinachonipata ni hofu zaidi).

naomba nitumie mfano wa "bank robber" for argument sake only. kuna "bank robber" mmoja alipokamatwa baada ya kuua walinzi 2 wa usiku wa benki moja alikiri kuwa alishiriki kwenye tukio lile la ujambazi kwa vile alikuwa na shida kubwa kifedha - alikuwa anasomesha watoto wa ukoo wake mzima. ilikuja kuwa verified baadae kuwa alikuwa anasema ukweli na hivyo "aliua na kupora benki kwa nia njema". sad.

kwa hiyo, mzee wangu sheikh Mohamed, naomba utuepushe na janga linalotukodolea macho mbeleni. najua unayo hekima na utaitumia na kujaribu kusikiliza kilio cha sisi wenye hofu.

wabillahi tawfiq!

 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said , mdini aliyekubuhu na anayehangaika sana kuona tunatenganishwa na dini

Hatare sana
 
Last edited by a moderator:
Nimesoma hii makala kwenye gazeti la Raia mwema nilichojifunza nikuwa mzee Takadir alikuwa na maono ya mbali.

Ukiangalia kiundani utagundua kuwa waislam walikuwa mstari wa mbele katka harakati za kuleta uhuru ila tatzo wengi hawakuwa na elimu na ndio chanzo cha bifu la nyerere na Takadir,sasa nafikiri kuna haja kwa muslimu kuwekeza katka elimu maana ndo chanzo cha Tanu kuingiza watu wengine toka nje.Kwa imani yangu nikuwa kama waislam watawekeza katka elimu lugha ya kuonewa itaisha.
 

Bukoba Vijijini,
Ahsante kwa hayo ulioandika.

Waislam baada ya uhuru 1961 waliitisha Muslim Congress mwaka 1962 na
1963 na wakaweka mipango ya elimu chini ya East African Muslim Welfare
Society (EAMWS) chini ya uongozi wa Tewa Said Tewa.

In Sha Allah iko siku nitaweka hapa nini kilitokea baada ya kujulikana kuwa
Waislam sasa watapiga hatua katika elimu.

Hii ni mada ya kujitegemea.

EAMWS ikapigwa marufuku kuwa si chama halali hakitakiwi Tanzania na Mufti
Sheikh Hassan bin Amir
aliyekuwa akihimiza elimu kwa Waislam akafukuzwa
nchini.

Serikali ikawaundia Waislam BAKWATA.
 

M Mbabe,
Usiwe na hofu yoyote ndugu yangu.

Mimi nimekuja hapa kuandika historia ya kweli ili tujue tulikotoka na kwa kujua
huko tutajisahihisha.
 
M Mbabe,
Usiwe na hofu yoyote ndugu yangu.

Mimi nimekuja hapa kuandika historia ya kweli ili tujue tulikotoka na kwa kujua
huko tutajisahihisha.

sheikh Mohamed, nina imani hekima yako ni zaidi ya hilo jawabu lako japo juu.

tafadhali sana soma katikati ya mistari nilichokiandika. ninaweza nisiwe mweledi sana kukuzidi, lakini ninaamnini sauti yangu ya unyonge inaweza kuwa imebeba wito maalumu unaostahili kusikizwa nawe.

tafadhali sana sheikh..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…