Jinsi biashara ya Uber ilivyonikutanisha na dada huyu mrembo wa ajabu

SEASON : 02
CHAPTER 8
“A TRUE STORY BY INSIDERMAN”

PREVIOUS
Baada ya game kuisha hatukukaa sana tukaondoka kurudi home na wife ndo alikuwa wakwanza kushuka kwa gari. Muda huu niliikumbuka ile voice ambayo nilikuwa nimerecord kule hotelini, hivyo niliona ndo muda sahihi wa kuisikiliza.

CONTINUE

Niliangalia tena kama kuna usalama na nili-lock gari nikaanza kuisikiliza ile voice na ukweli nilikuwa nahamu sana ya kujua mazungumzo yao. Nilifanikiwa kuiplay na haya ndo yalikuwa maongezi yao na zaidi ya 90% yalikuwa kwa kiingereza,

CLAIRE: “Baby vipi kuhusu mimba yako, so unakwenda kuwa mama? You said you don’t trust him.”

IRYN: “Huyu mtoto nimempa zawadi Insider, kama atafanya ujinga ni juu yake.”

CLAIRE: “Ulikuwa unalalamika Insider ana mahusiano ya siri na moja ya wafanyakazi wako, mimi naona Insider atakusumbua tu best yangu. Hio mimba bado ni changa sana you can abort before it’s too late, Insider loves you because you are a rich and nothing more, listen to me."

IRYN: “No Claire Insider hana habari na Pesa zangu hakuna hata siku alishaomba pesa kutoka kwangu na juzi tu hapa amenambia hataki tumlipe mshahara maana ni dharau kwake. Kuhusu kunipenda hili naweza ku-agree Kuwa Insider huenda hana mapenzi kwangu lakini ana mapenzi kwa huyu mtoto tumboni.”

CLAIRE: “Mwanaume kama hana mapenzi kwa mama how come awe na mapenzi kwa mtoto? Acha kujidanganya, haimake sense kabisa na ukizingatia Insider ni mme wa mtu tayari, fanya maamuzi magumu kabla ya mambo kuharibika. Usipokuwa makini utaweza poteza familia yako pamoja na ndugu zote na bado Insider akakupiga na kitu kizito, ukajikuta unarudi ulikotoka na majuto juu.”

IRYN: “Remember, Insider is the only one who cared about me during that bad time, and now you're talking shit about him?"

CLAIRE: “I know you love him lakini kubali kupokea ushauri na kumbuka sisi ni marafiki tangu utotoni, sitapenda kuona best yangu unapata shida hapo baadae. Una miezi 9 ya kulea tumboni bado una miaka 3 ya kulea mtoto afu aje akufanyie ujinga unafikiri mimi nitajiskiaje?”

Iryn alinyamaza kimya kwa sekunde kadhaa na aliendelea kuongea,

IRYN: “Claire kama Insider atabadilika huyu mtoto atabaki kuwa furaha kwangu na siwezi ku abort kwahili sikuungi mkono dear. Pia nikwambie kama kuna lolote litatokea lawama zije kwangu maana mimi ndo niliyeamua kubeba hii mimba bila kumshirikisha.”

CLAIRE: “Anyway, umejipangaje huko Ethiopia? Nakumbuka uliniambia ndo jambo linalokupa stress kwasasa na hatukamaliza maongezi yetu.”

IRYN: “I don’t know maana nitakapotoa taarifa watataka kumjua Insider then lazima waseme suala la ndoa na hapa ndo utata utakuja maana Insider ana mke tayari.”

CLAIRE: “You told me bado hajafunga ndoa, hapo inaweza kuwa 50-50 anything can happen. Mimi cha kukushauri get him to marry you first.”

IRYN: “I don’t think it will work, he’s always smart and he knows what he is doing."

CLAIRE: “Nafikiri bado hujaamua na umekubali kuwa mchepuko, lakini kama utakubali ushauri wangu hakuna kisichowezekana.”

IRYN: “Claire we can stop here, he’s coming tutaongea haya.”

Baada ya kuisikiliza voice hapa ndo nilikuwa na uhakika wa 100% kuwa Claire ni snitch kwangu na niliona kama ana wivu wala sio kingine. Kwa upande mwingine nilijilaumu sana kuwahi kurudi maana maongezi yao yaliishia pazuri sana na Claire alikuwa ametema sumu kali sana.

Niliwaza kuhusu suala la kwenda Ethiopia na niliona kama nilifanya maamuzi ya haraka sana kumkubalia Iryn. Kwenda Ethiopia ni kama kutembea na kitanzi shingoni, niliwaza na kuona sina sababu ya kwenda huko.

“Nimeshampa ahadi ya kwenda huko tena kukaa week nzima, daah huu ni msala. Week ni kubwa sana kukaa kule lolote linaweza tokea, ikitokea Iryn akanitambulisha kwa familia yake kuwa mimi ndo mpenzi wake? Na wakija kujua mimi na mke tayari itakuaje?.”

Niliona naumiza kichwa kwa matatizo yaliyosababishwa na Iryn mwenyewe, tatizo langu mimi lilikuwa kwenye mtoto tu maana niliona lolote linaweza tokea, ukizingatia ile mimba bado ni ndogo. Niliona Claire bado ananguvu sana ya ushawishi kwa Iryn na lolote linaweza kutokea.

Niliona kuna umuhimu wa kutafuta wazee wa busara wa kunipa ushauri juu ya hili suala na kuna mzee wangu wangu tulikuwa tunapatana sana kipindi niko taasisi X, hivyo niliona kuna haja ya kwenda kuongea naye kuhusu hii ishu.

Suala la kuwaambia wazazi na ndugu zangu wa karibu niliona bado ni mapema sana na sitakiwi kuwa na haraka sana atleast mimba ifike miezi 6 kidogo naweza kuwa na ujasiri wa kumwambia hata dada yangu. Mimba ya mama J nilikaa miezi 6 ndo nilitoa taarifa kwa dada then nikampa taarifa mama, sikuona umuhimu wa kushirikisha familia yangu kwasasa.

Niliwaza mama anakuja jumamosi na atakaa na sisi mwezi mzima hapohapo nina safari ya kwenda Ethiopia na Iryn. Niliwaza hili jambo mbona linakuwa gumu sana? Na roho yangu kwenda Ethiopia ilikuwa inasitasita kwakweli. Kwa mbali nilimuona mama J katoka nje na amesimama kibarazani na akiangalia usawa wangu ni kama alikuwa anajiuliza mbona huyu mwanaume hatoki shida ni nini?.

Baada ya kuingia ndani nilikaa seblen nikicheza na Junior maana tulikuwa wawili tu pale sebleni na muda huu nilichukua simu yangu kuangalia kama Iryn amefika au laah. Hakukuwa na text yoyote kutoka kwake na mimi nilimtumia ujumbe kumuuliza kama amefika salama.

Nilianza kuview status za whatsapp maana na niliview status za Prisca nikaona kam-wish mama yake happy birthday. Nilireply kwa ujumbe uliosomeka “Happy birthday to our beautiful mama” na haikuchua muda Prisca alireply na tukaanza kuchati pale. Tuliendelea kuchat pale na kubwa alitaka nimpe majibu ya ile text yake ya mwisho kunitumia ya kuwa friends with benefits na mimi nilimwambia hilo halina shida kama karidhia.

Nilifikiri nikaona kuna haja ya kuendelea kuwa na Prsica kama mchepuko wangu ukizingatia tuna historia tayari. Niliona kama kaanza kujielewa hivi, hivyo hatonisumbua kama zamani na itakuwa rahisi sana kumcontroll.
******
Siku ya jumamosi mama yangu mzazi alikuja Dar es Salaam na alisema ataendelea kukaa na sisi mpaka Christmass ndio ataondoka kurudi mkoani. Asubuhi tulikuwa na usafi wa jumla pale home, kwa upande mwingine kila jumamosi ya mwisho wa mwezi huwa tunafanya usafi wa pamoja kwa wapangaji wote. Hii ni ratiba iliyowekwa na sisi tuliukuta huu utaratibu baada ya kuhamia.

Saa 10 jioni niliondoka na wife kwenda Magufuli bus terminal kwaajili ya kumpokea mama na aliwasili mida ya saa 11 jioni. Baada ya mama kuwasili tulikumbatiana na alimgeukia wife wakakumbatiana pia, ndo kuondoka kurudi home. Barabarani zilikuwa ni story za huko nyumbani na wife ndo alikuwa busy na mama mkwe wake, huku mimi nikiwa busy na usukani.

Baada ya kurudi home mama ombi lake la kwanza lilikuwa ni kumuona mjukuu wake na bahati nzuri Junior alikuwa pale seblen na furaha ya mama ilitimia baada ya kumuona. Mara ya mwisho mama kuja Dar ilikuwa ni baada ya wife kujifungua na kipindi hicho Junior alikuwa na miezi 2 tu. Kwa upande mwingine mama alifurahi sana kumuona dada bado tuko naye ukizingatia tumeishi naye toka Junior ni mdogo na kipindi kile mama anakuja Elena alikuwepo.

Baada ya kupata chakula cha usiku tulifanya ibada ya pamoja pale seblen na baada ya hapo mimi niliaga nakwenda kulala na niliwaacha wakiongea.

Jumapili asubuhi niliamka mapema kwenda kazini maana nilikuwa nina kazi ya kuanza kuandaa bonus za mwaka kwaajili ya wafanyakazi. Ni utaratibu wa kampuni kwa kila mwisho wa mwaka kutoa bonus na mshahara double, hivyo nilitaka nikamilishe hesabu mapema ili mishahara iwahi kutoka kwaajili ya sikukuu za Chtristmas na mwaka mpya.

Asubuhi wakati naondoka mama alikuwa bado kalala hivyo nilimuaga wife na kuondoka kwenda Masaki. Ilikuwa ni mida ya saa 2 asubuhi wakati nawasili pale ofisini kwa upande mwingine nilikuta wafanyakazi wako busy sana. Kwa siku za weekend kunakuwa na wateja wengi sana, hasa kuanzia ile asubuhi mpaka usiku.

Mimi niliendelea na majukumu yangu na baada ya nusu saa Hilda alikuwa kawasili na alikuja ofisini kunisalimia, tukapiga story mbili tatu akaondoka kwenda kuendelea na majukumu yake. Kwa upande mwingine stock ilikuwa umekata na tulikuwa na odda nyingi sana, hivyo niliona niwasiliane na Iryn maana toka tuongee kabla hajaondoka hakunipa ripoti.

Iryn yeye ndo huwa anaagiza mzigo pamoja na kulipia baada ya hapo ndo ananiachia mimi kwenye masuala ya kodi na clearing. Baada ya kumpigia simu alipokea na tukaanza mazungumzo na habari mbaya alisema anaumwa,

MIMI: “Mummy unasumbuliwa na nini?”

IRYN: “Nahisi mabadiliko ya mimba natapika sana.”

MIMI: “Pole mke wangu, nilitaka kukuliza kuhusu mzigo umefikia wapi? Tuna odda nyingi na stock hakuna kitu, mzigo wa mwisho uliagiza mdogo.”

IRYN: “Kuna mzigo uko njiani unakuja ni week tayari nilikuwa busy na wewe sikufuatilia mails, soon nakutumia details. Kuna mwingine nimefanya payment tayari lakini shida ni Meli niliyopata gharama za usafirishaji ziko juu sana kwa contena, supplier anaendelea kucheki meli nyingine.”

MIMI: “Ok sawa haina shida baby, mimi naomba nikuache maana nina kazi kibao hapa.”

IRYN: “Wait, ushaanza kufuatilia Passport?.”

Ukweli sikuwa nimenza process zozote na sikutaka kumdanganya hivyo nilimwambia ukweli,

MIMI: “Bado baby but kesho jumatatu nitaanza usiwe na wasiwasi.”

IRYN: “Why you’re not serious?. Tarehe 16 tutaondoka kwenda Ethiopia.”

MIMI: “Baby muda bado upo mwingi sana hili lisikupe mawazo.”

Baada ya kuachana na Iryn pale niliona tayari nishajiingiza kwenye kitanzi maana waswahili wanasema ahadi ni deni. Niliwaza hivi kama nitaghairi hii safari Iryn atachukua hatua gani? yani nilikuwa sina imani kabisa ya kwenda huko Ethiopia.

Muda huu Asmah aliingia ofisini amependeza sana na alikuwa ndo anafika na mimi kama kawaida yangi nilimpa sifa pale na nilimzingua kwanini kachelewa?”

MIMI: “HR unaingia saa 4 asubuhi serious?”

ASMAH: “Jana nimechelewa kulala na ulivyonambia utakuja ofisini mapema bhasi nikawa na amani. Insider stock haina kitu zimebaki wigi chache sana kwaajili ya wateja na unajua december hii customer ni wengi.”

MIMI: “Ni kweli, hizo pisi msitoe nje zibaki kwaajili ya sisi lakini kuna mzigo unakuja na soon utakuwa umewasili tayari.”

ASMAH: “Umeongea na Iryn mwenyewe?”

MIMI: “Yeah ameconfirm na mwingine bado anahangaika na meli analalamika gharama zimekuwa kubwa za usafirishaji.”

Baada ya mazungumza na Asmah, alitoka kwenda kuweka utaratibu na mimi muda huu nilianza kuyambuka yale mazungumzo ya Iryn na Claire na nilijisemea I have to do something.

Saa 9 za mchana niliondoka ofisini na lengo kubwa niende Mbweni kumsalimia Jane maana ilikuwa ni wiki imeisha bila kukanyaga pale kwake. Kipindi niko njiani nilimkumbuka yule dada ambaye tulibadilishana namba pale car wash lakini alikuwa hajanicheki, niliona dada ana dharau sana.

Baada ya kuwasili kwa Jane nilimkuta mama Pama pale seblen akiwa na wageni, nilimsalimia tukaendelea na maongezi na baadae Jane alitoka na alifurahi sana kuniona.

Pale kwa Jane ukweli ni wananiheshimu sana tena sana ilifika stage mpaka baadhi ya marafiki zake Jane walidhani mimi ni ndugu damu wa Pama. Jane alinipa ishara na mimi nilijua tu anataka tutoke nje tuongee na mimi ndo nilikuwa wa kwanza kutoka na yeye alifuata.

Tulikaa garden tukizungumza na kubwa ilikuwa ni suala la Mary maana Jane alitaka tuyamalize haya mambo haraka sana. Jane alionekana kuwa serious sana kwenye maongezi yake,

“Shem unajua wewe na Mary ndo watu wangu muhimu sana na nina waheshimu, sipendi jinsi mnavyoishi kwasasa kwanini msikae chini mkamaliza tofauti zenu?”

“Shem unajua fika Mary anahisia za kimapenzi kwangu na zile ni hasira ila atakaa sawa tu trust me. Mary namuheshimu sana ndomana sijataka kufanya ujinga wowote kwake maana najua italeta shida huko mbeleni, ni vizuri anichukie lakini kwa faida ya maisha yake kwasasa hawezi kuelewa.”

“I really appreciate naomba nikuulize jambo lakini kuwa honesty na mimi, yule dada (Iryn) ni nani kwako?.”

Niliona Jane anauliza maswali sensitive sana na niliona hata nikimwambia ukweli hakuna faida atakayopata, zaidi mahusiano yangu na Iryn yabaki kuwa ni siri,

“Shem yule ni bossy wangu kama nilivyokutambulisha na nina muheshimu sana, hatuna mahusiano zaidi ya hapa.”

“Sawa Insider mpaka nimekuuliza ujue ile siku kwenye lile sakata la Mary pale seblen niliona mabadiliko yake, na nikahisi mpo kwenye mahusiano”.

“Hiyo sio sababu lile suala alilofanya Mary ni la kitoto na alinikera sana, naamini Mary ndo anakupa hizi taarifa za uongo.”

“Insider naomba mkae na Mary myamalize na umwambie ukweli, sidhani Mary anakuchukia kwa hili kuna vitu unamfanyia ndomana.”

“Sawa shem haina shida nitakaa nae chini usiwe na wasiwasi.”

“Tuachane na haya ila Insider unabalaa sana shem wangu, yule dada alimtetemesha sana Mary afu she is very confident.”

Tulianza kucheka pale na Jane maana hata yeye alimkubali Iryn kuwa ni mrembo makini na kamkubali. Pia, Jane alinipa taarifa kuhusu 40 ya mtoto na alisema baada ya hapo ndo nitamkabidhi rasmi gari yake. Kwa upande mwingine alinipa taarifa ya kupewa zawadi ya gari kutoka kwa Umoja wa kikundi cha Pama na alisema hajui ni gari gani na itakuwa surprise siku hiyo ya 40 ya mtoto.

Saa 12 za jioni niliondoka kurudi nyumbani maana wife alikuwa kashaanza kupiga simu nonstop. Baada ya kuwasili home nilimkuta mama yuko seblen anacheza na mjukuu wake na tulisamiana pale nikakaaa kwenye coach.
Baadae tuliamua kutoka nje kukaa kibarazani kuendelea na maongezi maana niliona mama anakosa uhuru wa kuongea pale seblen,

MAMA: “Mpaka jumapili unakwenda kazini mwanangu?”

MIMI: “Hapana ila mara chache kama kuna jambo huwa nakwenda si unajua mimi ndo kila kitu?”

MAMA: “Bossy wako anaonekana ni mkarimu sana ile siku alinambia mama natamani sana nikujue siku maana Insider ni mchapakazi mzuri.”

MIMI: “Amesafiri mara moja kama atarudi bado upo atakuja kukusalimia na atafurahi sana kukufahamu.”

MAMA: “Yule binti mimba iliyoharibika anaendeleaje?

Nikajisemea mama kaanza kufukua makaburi kumbe hajasahau tu,

MIMI: “Yuko salama mama ila hatuna mawasiliano kwasasa niliamua kukaa naye mbali yale makosa yasijirudie tena.”

MAMA: “Vizuri lakini Roho inanambia bado anakupenda, naomba kuwa makini sana kwa hili mwanangu.”

Ilibidi nibadili mada niliona mama anakoenda siko kabisa,

MIMI: “Nambie harusi ni ya nani kwanza? Maana hatukuongea hili kabisa.”

MAMA: “Ni binti wa mama TUSI , si unamkumbuka yule bint yake wa kwanza?.”

MIMI: “Simkumbuki kabisa, bhasi tutakwenda wote na vipi kuhusu michango?

MAMA: “Tutakwenda na mama J, muwe mnahudhuria harusi za wenzenu ili mpate hamasa ya kuoana mapema. Na suala la harusi yenu mmefikia wapi? Haya ni maamuzi na mipango yenu, lakini siku zinakwenda.”

MIMI: “Harusi tutafunga mama ngoja amalize chuo kwanza nabado najipanga kiuchumi.”

MAMA: “Mwanangu unataka mjipangaje? Unajua kadri mnavyochelewa ndo mnampa nafasi shetani?”

MIMI: “Ndomana mama yangu upo najua unatuombea ili shetani asilete majanga.”

MAMA: “Biblia inasema mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Mimi nawaombea sana sana, lakini mnatakiwa na nyinyi mkumbuke kujiombea sawa mwanangu?”

Mama akishaanza masuala ya vifungu vya bible huwa nakuwa mpole sana, na muda huu wife alitoka na juice akatupa pamoja na mama. Tulikuwa na maongezi mengi sana na mama lakini cha ajabu lile jambo ambalo alisema kama ameoneshwa namficha hakuliongelea kabisa na mimi wasiwasi wangu ndo ulikuwa pale.

Mama aliniaga anakwenda kumsaidia wife kupika na mimi nilibaki pale kibarazani nikiwaza mambo mbalimbali ambayo yakinichanganya akili, likiwepo suala la Iryn la kwenda huko Ethiopia.

Jumatatu nilikuwa nina ratiba mbili muhimu ya kwanza ni kwenda kuonana na mzee wangu pale taasisi “X” na ratiba ya pili ni kwenda Uhamiaji kufuatilia suala la Passport.

Saa 3 za asubuhi nilikuwa nimewasili taasisi “X”, lakini nilikuta kuna mabadiliko makubwa sana pale, kwani asilimia kubwa ya watu nao fahamiana nao walikuwa hawapo, wamehamishwa. Kwa upande mwingine baadhi walikuwepo tunaofahamiana lakini sura nyingi zilikuwa ngeni. Idara niliyokuwa nafanyia kazi kulikuwa na watu wapya lakini ni watu wawili tu walikuwa wamebakishwa ambao ni kaka na dada yangu, ambao walipelekwa department zingine.

Baada ya kuelekezwa idara walizohamishiwa nilikwenda kwanza kuonana na dada yangu na tulipiga sana story na alinipa taarifa kuwa mzee wangu alikutana na panga kapelekwa mkoani, hivyo sikuwa na jinsi maana plan yangu ikawa imefeli. Namba yake nilikuwa nayo lakini kwa masuala kama haya niliona halina nguvu kuongea kwa simu na niliwaza nitafute plan B maana plan A ishafeli.

Baada ya kuachana na sister nilikwenda onana na brother angu na tulipiga story kadhaa kisha nikaenda msalimia manager wa ile taasisi. Manager baada ya kuniona alifurahi sana na tuliishia kupiga story nyingi sana za maisha maana toka tuachane hatuwahi onana wala hatukuwa na mawasiliano, licha ya kufanya kazi zake nyingi sana.

Habari kubwa manager alisema walikuwa na kikao na majina yetu yalipendekezwa kwaajili ya kupewa ajira maana tuna experience na tulichapa sana kazi kipindi kile. Manager alisisitiza sana hili suala kuwa ni serious na soon tutaanza pigiwa simu kwaajili ya kupewa mikataba. Mimi niliishia kumuitikia lakini nilijisemea hata kama nikweli siwezi kuikubali hio offer ya serikali ya kunilipa mshahara wa 1.5M, afu niache kazi yenye maslahi kwangu ambayo nalipwa mara 3 zaidi.

Kumkosa mzee wangu pale ofisini nilinyong’onyea sana na ukweli sikuwa na option kabisa na mzee aliyekuwa amebakia ni mmoja tu ambaye alinisaidia wakati natoa mahali ya mama J. Niliona kumshirikisha hili jambo italeta matatizo na nilijisemea sitakiwi kutumia nguvu sana kwenye hili suala, mambo yatakaa sawa tu.

Niliondoka kuelekea Kurasini pale Uhamiaji kwaajili ya kufuatilia Passport na nilikuwa tayari nimefanya mawasiliano na jamaa yangu ambaye anafanyia kazi pale na tulisoma Advance pamoja. Baada ya kuwasili pale tulionana na tuliongea kuhusu hili suala na alinihakikishia itatoka haraka nisiwe na wasiwasi kwa hili.

Niliondoka kuelekea Mikocheni na lengo langu nikaonane na Lucy maana toka Iryn aondoke hatukonana na niliwaza huenda ana jambo lolote la kunambia. Mchana nilikuwa nimewasili pale ofisini na nilimkuta anajisomea, baada ya kuniona alinambia anataka kwenda kula lunch, ikabidi na mimi niliunge.

Muda ambao tulikuwa tunapata lunch Lucy alinambia Iryn kamfungukia kuwa anamimba yangu na ananipenda sana. Lucy aliendelea kunisisitiza kwamba kwasasa nisimpe stress zisizo na msingi wala kumkera na nifocus na maendeleo ya kampuni. Kwa upande mwingine tuliendelea na mipango ya kiofisi na kubwa nilimwambia anisaidie kuandaa performance report ya kila mfanyakazi wa pale Mikocheni kwa mwaka mzima ili niweze kuandaa bonus zao zitoke mapema na mishahara.

Baada ya maongezi ya kiofisi tulianza maongezi mengine na nilishangaa kuona Lucy akiniulizia taarifa za Bob na mimi nikawaza huenda Bob kashamtongoza tayari. Japo Lucy hakutaka kuongea lolote nilihisi kuna kitu hakipo sawa na nilijisemea nitamcheki Bob anipe mkanda mzima wa kinachoendelea.

Saa 11 jioni niliamua kurudi home mapema maana niliona kurudi late na mama yupo pale home haiwezi leta picha nzuri ukizingatia mama anaonekana kuwa na maongezi mengi sana na mimi.

Baada ya kurudi home nilimkuta mama yuko nje na Junior akimwendesha kwa gari yake na nilimsalimia na tukaendelea na mazungumzo. Mama alishangaa sana kuona nina gari tatu pale home na mimi nilimwambia yakwangu ni moja tu ambayo ni ile Ist mpya na zingine sio zangu.

Tulianza kupanga mipango ya harusi na alisema harusi itafanyika Tabata na siku ya ijumaa itabidi twende Kariakoo kwaajili ya kununua zawadi za harusi. Mama alisema kama kikundi chao huko mkoani wamechanga kwaajili ya sherehe na yeye ndo mhasibu wa kikundi chao. Kwa upande wangu nilimwambia nitamfanyia shopping na nitampeleka saloon akang’arishwe na aliishia kufurahi.

Kwa upande mwingine mama alinisisitiza sana nitulie na kama nina wanawake wa nje bhasi niachane nao kwani Mungu amenipa mke bora na nimuheshimu sana mama J. Si unajua tena mambo ya wazazi, mama alinipa sana lectures na alikuwa hakosei sehemu za kupiga point.

Wakati nikiendelea kuongea na mama, Iryn alianza kupiga simu na mimi sikutaka kupokea simu zake muda huu maana nilikuwa na mazungumzo na mama. Baada ya kuona akiendelea kupiga simu kwa fujo nilimuaga mama mara moja nakwenda ndani kuoga then narudi.

Baada ya kupokea simu yake kama kawaida alianza kulalamika kwanini sipokei simu zake na ilibidi nimdanganye kuwa nilikuwa nadrive na simu ilikuwa silent. Sikutaka kumwambia Iryn kuwa mama yuko home maana nilijua angenisumbua sana kutaka kuongea naye na ingeleta tatizo.

Mimi na Iryn huwa tunakuwa na maongezi marefu sana, unakuta tunaweza ongea hata lisaa na bado hakuna dalili za kumaliza maongezi. Kwa upande mwingine aliuliza kuhusu progress za ufuatiliaji wa Passport na nilimwambia tayari nimeanza mchakato na soon nitakuwa nayo. Tangu Iryn arudi Dar na kuondoka niliona wivu kwangu umeongezeka sana na alikuwa akipiga sana simu mpaka kero na hapo anataka tuwe tunaongea tu ndo furaha yake.

*****
Ijumaa tulikwenda Kariakoo kununua hizo zawadi kwaajili ya harusi na tulianza kwanza kufanya shopping maduka ya Sinza, then tukamalizia Kariakoo. Zawadi ambazo mama alikuwa anataka kununua ni pamoja na fridge, Jiko na mazaga mengine. Kwa Kariakoo nina wadau wengi sana pale, hivyo haikuwa shida kwangu na tulipata fridge nzuri na bei kitonga.

Baada ya kumaliza shopping ilibidi twende Tabata kuzipeleka zawadi ili ziwe karibu na eneo la tukio. Break yetu ilikuwa Kinyerezi kwa mama TUSI na alikuwa kafikia kwa binti yake ambaye anaolewa na nilimsalimia pale na alifanya kunitambulisha binti yake maana tulikuwa hatujuani.

Jumamosi asubuhi mama alinipa ratiba kwamba tunatakiwa kuwahi kwenda ukumbini hivyo itabidi wawahi kwenda saloon ili kufikia saa 12 jioni tuwe amefika eneo la tukio. Saa 9 mchana wife na mama waliondoka kwenda Mikocheni na nilikuwa nishampanga tayari Lucy kuwa mama yangu anakuja hivyo asizingue.

Saa 12 jioni niliwapitia pale ofisini na nilikuta wamependeza sana kwakweli yaani ungemuona mama J wangu ungedata. Kwa upande mwingine Lucy aliniita pembeni na alianza umbeya wake na kubwa alifurahi sana kumuona mama yangu na aliishia kunimwagia sifa kuwa tumefanana sana.

Saa 1 usiku na madakika tulikuwa tumewasili Baracuda Highland hall na niliweza kuonana na mama zangu wa mkoani. Niliwasilimia pale na wao walifurahi sana kuniona na kama kawaida ya wamama waliishia kunichamba kwanini nakaa na mtoto wa watu bila kufunga ndoa?. Niliishia kujitetea pale na niliwapa ahadi kuwa soon na mimi nafunga ndoa, waliishia kumfurahia mama J na tukazama ndani eneo la tukio.

Tulikaa upande wa ndugu za Bibi-harusi na Kwenye meza yetu tulikuwa 10, mama alikuwa amekaa kati yangu na wife na muda huu tulikuwa tunapiga story wote watatu. Mama aliendelea kusisitiza tufunge ndoa mapema kwani muda unakwenda na sio lazima tufunge ndoa ya gharama, lawama zote zilikuwa zinakuja kwangu. Wakati story zimenoga kwa upande mwingine Iryn alianza kupiga simu na mimi nilikuwa nazimute maana sikuona sababu ya kuongea naye muda huu, na alipiga mara tatu.

Harusi ilikuwa nzuri sana kwakweli mpaka nikapata ka wivu na mimi nifunge harusi na mama J, lakini nikikumbuka suala la Iryn nikawa nakosa nguvu. Harusi iliisha saa 6 za usiku na tuliendelea kumsubiri mama maana alikuwa ana kikao na wamama wenzake na walitumia kama lisaa ndo tukarudi home kulala.

Jumapili nilichelewa sana kuamka na nilikutana na missed call nyingi tu, missed call 2 ilikuwa ni namba mpya, lakini nilipotezea na nilikwenda seblen kuangalia kama mama kaamka salama. Nilimkuta mama akicheza na mjukuu wake na nikamwambia jioni tutatoka wote kwenda kutembea na kupata dinna.

Nilitoka nje ili niweze kuongea na Iryn maana alikuwa kapiga sana simu pamoja na texts juu, nilimpigia simu na haikuchukua muda akapokea ila alionekana kuchukia sana,

IRYN: “Baby kwanini hupokei simu zangu toka jana?”

MIMI: “Sorry, sikuwa sehem nzuri ndomana.”

IRYN: “Unamaanisha nini kusema hukuwa sehemu nzuri? Na kwanini hujanambia kama mama amekuja Dar?”

Nikajisemea Lucy kashampa taarifa Iryn na nilisahau kumwambia asiseme hivyo sikuona sababu ya kum-mind Lucy,

MIMI: “Ningekwambia mummy kaja juzi na masuala ya harusi ndo yamemleta na ndo nilikuwa naye jana huko kwenye harusi.”

IRYN: “Sijapenda Kutonipa taarifa, four days remain before our trip to Ethiopia na nitakuja Dar ili tuondoke wote. Naomba nikija nimuone mama by any means, this is not for me, it's for your child."

MIMI: “Sawa no problem I’ll do my best”

Sikutaka kumkatalia maana ningeanzisha matatizo mengine hivyo nilikubali lakini nikijua hili jambo haliwezi tokea kwasasa. Muda wa kwenda Ethiopia ulikuwa unakuja kwa spidi sana na niliwaza pale nitatumia gia gani ya kuondokea pale home kwenda huko?. Niliwaza nimuache mama yangu mzazi home then niende na Iryn? Niliona kama haiwezekani.

Wakati nikiendelea kuwaza simu ya Prisca iliingia na baada ya kufanya nae maongezi alinipa taarifa kuwa kwasasa yuko Changanyikeni hivyo niwe nakwenda kumsalimia. Baada ya kuongea na Prisca nilifanya kumpigia simu dogo ripota wangu na nikamwambia aache kumfuatilia Prisca, amuache na maisha yake. Kwa upande wake dogo alishangaa sana na aliuliza kwanini nimeamua hivyo? Nilimwambia kwasasa hatuko kwa mahusiano, hivyo sioni sababu ya kumfuatilia .

Jioni tuliondoka familia nzima kwenda Karambezi cafe kwaajili ya kupata dinna ya pamoja na lengo langu kubwa mama afurahie kuja Dar. Baada ya kuwasili pale tuliagiza chakula lakini kwa mama ilikuwa shida kidogo kwani zile menu zilikuwa zinamshinda na nilifanya kumchagulia chips na beef.

Tuliendelea kupiga story pale na mama alionekana kulipenda sana eneo hili na muda huu simu yangu ilianza kuita na ilikuwa ni namba ambayo ilinitafuta asubuhi. Nilitoka na nikaenda kupokea simu,

ANONYMOUS: “Hello Insider za kwako?”

MIMI: “Salama habari yako pia.”
Wakati nataka kuuliza who’s this kwa haraka alijitambulisha,

ANONYMOUS: “Unaongea na Ghati tulikutana Carwash Mbweni.”

Hapa ndo kumkumbuka yule dada na ile siku tunakutana hakunambia jina lake,

MIMI: “Now nimekufaham mrembo, niliwaza umeamua kunipotezea maana kimya sana mpaka nimesahau.”

ANONYMOUS: “Sorry, nilipata emergence ya haraka, so nilikuwa bush kuna mradi nilienda simamia. Nimerudi sio muda na kitu cha kwanza nimeenda kwenye gari kutafuta business card yako ndo nimekupigia.”

MIMI: “Ooh thank you na pole na safari.”

ANONYMOUS: “Asante, upo pande zipi?”

MIMI: “Seems unataka tuonane.”

ANONYMOUS: “Yeah If possible maana niko tu, na sina pakwenda.”

MIMI: “Kwa leo ratiba ipo taiti mummy nitakucheki next week.”

ANONYMOUS: “No problem basi ngoja mimi nilale byee.”

Baada ya kuachana na dada nilisave namba yake na nikarudi mezani kujumuika na kina mama. Nakumbuka tulikaa pale mpaka saa 4 za usiku ndo kurudi home kulala na hii siku mama alisema atakuwa na kikao na sisi, kwani ana mazungumzo muhimu sana ya kuzungumza nasi.

*****
Tulikuwa tumeanza wiki mpya na zilikuwa zimebaki siku 3 tu za kwenda Ethiopia na ile asubuhi nilikwenda Kurasini kuchukua Passport yangu ilikuwa tayari imetoka. Baada ya kutoka pale Kurasini nilikwenda moja kwa moja mpaka Masaki lakini wakati niko njiani niliwaza nitafute sehemu nitulie kwanza.

Niliamua kwenda Cocobeach kutulia kwanza na kulifikiria hili jambo kwa makini sana before sijafanya mistake yoyote. Pale Coco nilitumia muda mwingi sana kulifiri hili suala na majibu niliyowaza nisiende huko Ethiopia na nilianza kuwaza nitatoa sababu gani?.

“Ok! Iryn anajua mama yuko Dar naweza mwambia tutakuwa na kikao cha familia ambacho ni muhimu niwepo, hivyo sitoweza kwenda Ethiopia. Sasa, Insider kama Iryn umempa ahadi ya kwenda ina maana hukujua mama anakuja? Kumbuka ana mimba yako tayari, kumpeleka Ethiopia kuna shida gani?”

Ni Roho mbili ambazo zilikuwa zinashindana ndani yangu, lakini hii ya kutokwenda ilikuwa na nguvu na nikajisemea potelea mbali kama atanichukia kwa hili, i’ts okay bado nitabaki kuwa baba mtoto ila kwenda huko sitathubutu Roho yangu imekataa.

Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana na nikaona kuna haja ya kwenda home kuongea na mama kuhusu hili suala la mimba ya Iryn. Niliona kwa stage niliyofikia ni ngumu sana kuwa na maamuzi sahihi, hivyo nahitaji msaada hata kwa mama yangu mzazi before mambo hayajaharibika.

Niliona sometimes kama mwanaume inatakiwa kuwa na maamuzi magumu, nibora mama ajue mapema kinachoendelea before it’s too late na maamuzi yafanyike mapema. Kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na kucheki ni Iryn alikuwa anapiga na nikajisemea leo namchana ukweli siendi Ethiopia.

CHAPTER 9




 
Natamani kujua kifo cha mama iryn ilikuaje isije kuwa huyo mama iryn anamuita mama kahusika,maana kama rafik wa damu kiasi hicho halaf kabeba mume wa rafik yake huyo ana roho ya kichawi kabisa anaonyesha upendo kqa iryn ila ana roho ngumu sana inabidi silense investigation ifanyike kujiridhisha ba kifo cha mama iryn i feel lyk something somewhere na ni kama iryn ameanza shtuka kitu.
 
SEASON 02
CHAPTER 09

“BY INSIDER MAN”

PREVIOUS:
Niliona sometimes kama mwanaume inatakiwa kuwa na maamuzi magumu, nibora mama ajue mapema kinachoendelea before it’s too late na maamuzi yafanyike mapema. Kwa upande mwingine simu yangu ilianza kuita na kucheki ni Iryn alikuwa anapiga na nikajisemea leo namchana ukweli siendi Ethiopia.

CONTINUE:
Niliamua kuipotezea simu yake kwanza na nilichukua maamuzi ya kuondoka maeneo haya. Wakati nimeingia kwenye gari nilikuwa nikitafakari namna ya kuongea naye ili aweze kunielewa. Unajua niliwaza Iryn ni kama mke tayari, pia yale maongezi yake na Claire alionesha kuwa side yangu, hivyo mpaka akaomba twende Ethiopia ni kweli anahitaji kampani yangu, sasa mimi nafanyaje?.

Kumpa jibu kuwa siendi niliona sio jibu zuri, hivyo inabidi nitafute namna ya kuongea naye na anielewe ili amani iendelee kuwepo. Baada ya kufikiri sana niliona nimpe conditions zangu na kama atakubaliana nazo bhasi nitaenda huko Ethiopia na kama atagoma bhasi kwangu itakuwa sherehe.

Muda ulikuwa umekwenda sana maana nilikuwa niko kwa zaidi ya masaa 3 pale Coco beach. Niliondoka mitaa ile kwenda ofisini kuangalia maendeleo na sikukaa sana nikaondoka kwenda kuonana na Sumaiya maana alikuwa anahitaji sana kuonana na mimi.

Baada ya kufika pale ofisini kwake tulipanda juu kabisa ghorofani ili tufanye mazungumzo yetu na taarifa kubwa alizonipa ni kuhusu kununua gari na alisema ataanza na hiyo Toyota Ist. Nilimpeleka Morocco ili tukaangalie gari zilizopo na kama kuna gari ataipenda, bhasi aweke booking mapema maana alisema kufikia ijumaa atakuwa amekamilisha.

Tulikwenda palepale kwa jamaa niliye fahamiana naye kupitia mzee Pama na baada ya kuwasili pale alituonesha Ist tano (5) na zote zilikuwa ni kali, lakini Sumaiya aliipenda moja yenye rangi ya dark blue. MBaada ya mazungumzo ya muda mrefu Jamaa alitupunguzia mpaka kufikia 14.5M, ukweli ilikuwa ni Ist ya moto sana.

Bila kuchelewa Sumaiya alifanya malipo ya 12M kwa kutransfer na balance inayobaki alisema atamalizia Ijumaa, then akabidhiwe na gari yake. Niliagana na Sumaiya pale na nikarudi home kupumzika, wakati niko njiani nilikuwa nafikiri namna ya kudeal na suala la Iryn.

Ndani ya muda mfupi nilikuwa niko home na Elena aliniambia mama amelala, hivyo nili kwenda kukaa nje kibarazani maana kichwa changu kilikuwa na vitu vingi sana. Ulishawaza mpaka kichwa kinauma na bado hupati majibu? Bhasi ndo hali niliyokuwa nayo mimi Insider maana nilikuwa dilemma na sijui nifanye maamuzi gani.

Baada ya nusu saa mama alitoka pale nje kibarazani na baada ya kusalimiana tulianza maongezi,

MAMA: “Mwanangu upo sawa kweli? Nimekuona muda mrefu upo kwenye mawazo shida ni nini?”

MIMI: “Mama hata usijali niko sawa ni mambo ya kazini yananiumiza kichwa.”

MAMA: “Kweli mwanangu? Nakujua vizuri sana na kama unanidanganya mimi mama yako naelewa.”

Niliwaza pale sijui nimwambie tu ukweli wa kinachoendelea? Lakini nikaona hapana nitakuwa nimefanya maamuzi ya haraka sana,

MIMI: “Kuna shot imetokea huko ofisin ndo inanipa mawazo hapa kuwa imeenda wapi?maana hesabu zote ziko sawa ila balance ndo inagoma.”

MAMA: “Pole sana inabidi utulize akili hapo na ikitokea hujui inakuaje?”

MIMI: “Nakatwa mshahara maana mimi ndo top natakiwa kufuatilia kila mauzo ya siku, nilifanya kauzembe.”

MAMA: “Na pale Salon ndo ofisi yako iliko?”

MIMI: “Ile ni branch yetu ila ofisi kuu ipo Masaki, ni karibu na tulikokwenda jana usiku ndo ipo kule.”

Muda huu Junior alisikika akilia na mama alikwenda kuangalia shida ni nini? na aliniacha pale kibarazani.

Baada ya dakika 20 hivi, Iryn alipiga simu tena na mimi nilipokea kwa haraka sana na tukaanza mazungumzo,

MIMI: “Hey mummy za wewe?”

IRYN: “Safi darling, pole na kazi.”

Kwanza nilishangaa kuona Iryn kawa mpole maana angeanza na kulalamika why sijapokea simu zake?,

MIMI: “Mimi niko poa just tired, what’s new?”

IRYN: “Ijumaa tunatakiwa kwenda Ethiopia na sikuelewi elewi baby.”

MIMI: “Mummy naomba nikupe conditions zangu za kwenda huko Ethiopia.”

IRYN: “Go ahead, nakusikiliza.”

MIMI: “Moja sitalala kwenu naomba nitafutie hotel, naomba usije kuja kulala hotelini mpaka tunaondoka na utalala home. Pili, naomba usifanye utambulisho wowote kwenu wala kuonesha signs zozote za mimi na wewe tuko kwenye mahusiano. Mwisho, sitakaa wiki na wewe nafikiri siku 3 zinatosha mama yuko home na biashara inategemea usimamizi wangu.”

IRYN: “Done.”

MIMI: “What?”

IRYN: “I said done, Ijumaa nitakuja Dar then tutaondoka wote kwenda huko.”

MIMI: “Sawa mummy no problem.”

Baada ya kuachana na Iryn nilishangaa sana kuona akikubali matakwa yangu bila kusumbuana na muda huu nilianza kuwaza gia ya kutokea pale home.
***
Asubuhi nilipigiwa simu na namba ngeni na alijitambulisha vizuri, akanambia niende Ubalozi wa Ethiopia nikiwa na passport yangu. Sikutaka kuuliza maswali kabisa maana nilijua yatakuwa ni maagizo kutoka kwa Iryn na mimi nilijiandaa nikaondoka kuelekea Masaki.

Nilimpigia simu Iryn na kumpa taarifa juu ya kupigiwa simu na yeye alisema huyo mtu amempa maagizo hivyo nimpe ushirikiano maana muda umekwenda tayari. Break yangu ya kwanza ilikuwa ni pale ubalozini na baada ya kuonana na huyo mtu kuna documents nilizijaza chap. Nilijaza nakwenda Ethiopia kwaajili ya utalii na baada ya kumaliza kuzijaza, akanambia atanipigia simu na mimi ndo kuondoka.

Niliondoka kuelekea ofisini na nilimkuta Asmah amelala kwenye coach, ile kalalia tumbo makalio yako juu na mimi nilimuwasha na kibao cha kalio “PAAH” na alianza kulalamika pale,

“Insider mbona unatabia mbaya hivi?”

“Wewe unalalaje hivyo ofisini? Au unataka kunipa stim!?”

“Ulitaka nilalaje sasa?”

“Ningekuja kukuonesha sema umelala kimitego sana.”

“Insider una matatizo ya akili wewe.”

Tuliendelea kufanya kazi huku tunapiga story za hapa napale na utani mwingi. Mida ya mchana Hilda alikuja kutushtua tukapate lunch.

Hii siku nilishinda ofisini maana nilikuwa ninaandaa maripoti ya hesabu za mwaka afu nilikuwa napunguza makazi hata nikiondoka mambo yaende. Sikuona sababu ya kumficha Asmah na nilimpa taarifa kuwa nitasafiri mara moja kwenda Ethiopia na nitamuachia ofisi iwe chini ya usimamizi wake.

Mida ya jioni Allen alinipigia simu na akanambia tuoanane Samakisamaki ili tucheki na game kabisa. Hii siku kulikuwa na match ya nusu fainali kati ya Argentina na Croatia na mimi sikuona sababu ya kwenda home mapema hivyo tulikubalina tutaonana pale. Wakati naongea na Allen kwa upande mwingine Asmah alikuwa makini sana kusikiliza maongezi yetu na yeye alisema tutaenda wote kuangalia mpira.

Mida ya saa 2 usiku tulitoka kuelekea maeneo kwa upande mwingine Allen alikuwa amefika muda mrefu na alikuwa kashanipa taarifa amefika tayari. Baada ya kuwasili tulijumuika naye na yeye hakutegemea kama ningeenda na Asmah na nilifanya utambulisho na story zingine zikaendelea.

Game iliisha kwa Argentina kushinda 3 bila na nilikuwa na furaha sana hii siku kwakweli maana tulifuzu kwenda fainali. Baada ya game nilimpa Asmah kampani ya usafiri mpaka kwake Upanga na baada ya kuwasili kwake nilipark gari pembeni. Muda huu tulikuwa tukiendelea na mazungumzo yetu na kubwa nilitaka kujua yeye na Iryn walikuwa na mazungumzo gani?

MIMI: “Asmah embu niambie Iryn amekwambia nini alivyorudi Dar?”

ASMAH: “Hakuna chochote alichoongea zaidi ya story za kawaida.”

MIMI: “Mbona ulikuwa unaonekana kumwogopa sana? Au unanificha?”

Asmah alikosa majibu ya hili swali langu alinyamaza kimya, nilivyoona yuko kimya nilipitisha mkono wangu wa kushoto nyuma yake na nikanza kukipapasa kiuno chake,

ASMAH: “Insider stop! please!”

MIMI: “Kipindi kile unaumwa mguu ulikuwa unanifunulia mwenyewe sahivi unanipa masharti sindio?”

ASMAH: “No! sijamaanisha hivyo but sija-do muda mrefu sana utanipa majaribu bure na sitaki chochote kitokee baina yetu.”

MIMI: “Kwahiyo kukushika kiuno nakupa majaribu? Bhasi una matatizo jitathmini.”

Na muda huu nilifungua kifungo cha skin jeans yake kwa haraka sana taah! Na ile nataka kutalii kwenye bustani alinishika mkono, na akaendelea kulalama,

ASMAH: “Insider stop this please, wewe umesha lewa na hizi sio akili zako.”

MIMI: “Asmah niachie mkono wangu ndo utafanya nikukamie kweli.”

Asmah ilikuwa mpole maana nguvu ya kunikazia alikuwa anaitolea wapi kwanza? Na aliniachia nifanye nachotaka. Ile kuingiza mkono daah! Bustani yake ilikuwa imeshamwagiliwa vizuri.

MIMI: “Kidogo tu uko hoi stage uliyofikia ni mbaya sana.”

ASMAH: “I told you before hukutaka kunielewa.”

MIMI: “Mara ya mwisho ku-do ni lini?”

ASMAH: “Nikikwambia hutanielewa tatizo, utasema nakudanganya.”

MIMI: “Nitakuamini maana ukweli nimeushuhudia kwa macho yangu.”

ASMAH: “Sijakutana na mtu mwingine zaidi yako kipindi kile.”

MIMI: “Nenda kalale kesho saa 4 asubuhi tutakwenda Posta wote.”

Asmah aliniangalia na akaondoka na mimi sikutaka kupoteza muda nikaondoka kurudi home maana wife alikuwa kashaanza kupiga simu kwa fujo. Kipindi niko njiani nilikuwa nawaza kuhusu Asmah na niliona kuna haja ya kumuhudumia maana stage aliyofika ni mbaya sana. Hata mimi kwa upande wangu nilikuwa naingiwa na tamaa ya kutamani kumla kwa mara ya pili.

Baada ya kurudi home ile kuingia ndani nakutana na mama yuko seblen pamoja na wife na aliishia kunipiga jicho kali sana, mimi sikujali na niliwasalimia nikapitiliza kwenda chumbani kuoga.

Mawazo yangu makubwa yalikuwa ni namna ya kutoka pale home na kwenda huko Ethiopia na niliwaza nitumie mbinu gani? Ambayo itamake sense na isilete maswali. Niliwaza nikiwaambia nakwenda Zanzibar kufuata mzigo mwisho wa siku nitapigiwa simu afu sipatikani italeta shida, ni bora nidanganye nakwenda Kenya hata nisipopatikana ni freshy.

“Sasa niwaage ijumaa nakwenda Kenya kuna mzigo umefikia kule hivyo inabidi nikaufuate pamoja na kufanya clearing mapema, hii sababu ita make sense.”

Asubuhi nilitoka mapema kwenda ofisini maana nilikuwa na ratiba ya kwenda Posta na Asmah. Niliendelea kuandaa documents ambazo Iryn alikuwa kanitumia za mzigo na nikaendelea kumsubiri Asmah. Haikuchukua muda Asmah naye aliwasili pale ofisini na alionekana kuwa na aibu kidogo, nilijua ni ile ishu ya jana usiku.

Tulisalimiana then tukaondoka kuelekea Posta na ile baada ya kuingia kwa gari nilianza kumzingua tena,

“Naona unanionea aibu mummy.”

“Insider ulichofanya jana sio heshima, umenikwaza.”

“Sawa mummy sitakukwaza tena usijali.”

Nilikuwa nakwenda na Asmah Posta ili aendelee kupata uzoefu taratibu hata kama sipo awe anajua pakuanzia na kutokea, si mnajua mambo ya custom yalivyo na complications?, na ukisema umuachie kila kitu agent utakuwa unapigwa.

Kipindi niko njiani nilifanya kuwasiliana na dada wa clearing ili tuonane na tufanye malipo yote kwa pamoja. Kwa kila stage tunayoanza na kupita nilikuwa namuelekeza Asmah na yeye alionesha kuwa makini na kuelewa.

Kwenye mida ya saa 7 mchana tulikuwa tumekamilisha kila kitu na tulikwenda kupumzika moja ya mgahawa pale Posta tukipata lunch. Baada ya lunch tuliondoka na nilipitia ofisini kwa mama wa2 maana alikuwa ameniomba kama nitapita Alli Hassan road nipitie tuonane.

Baada ya kuwasili pale ofisini kwake tulikwenda moja kwa moja mpaka reception kumsubiri na nilikuwa nimempa taarifa tayari. Baada ya dakika 10 mama wa2 alitoka kuja pale reception tukaendelea na maongezi.

MIMI: “Mama mkwe leo umewaka sana.”

MAMA WA2: “Ooh jamani! Nimefurahi kukuona japo unakesi za kujibu.”

MIMI: “Kesi gani hizo mama mkwe.”

MAMA WA2: “Wake zako kule home wanakuulizia sana, ulisema utakuja mchukua Rachel mpaka leo kimya.”

MIMI: “Hao nitakuja kuwasilimia haina shida, afu sijakwambia mama yangu yuko home.”

MAMA WA2: “Mbona hujanambia nije kumwona mama mke mwenza, jumapili nitakuja na kina Rachel.”

MIMI: “Bad news ijumaa na safari nakwenda Kenya one time ila sitokaa, nikirudi tu nitakupa taarifa uje.”

MAMA WA2: “Insider kwa mishemishe sikuwezi na huyu dada ni nani? Hujanitambulisha bado.”

MIMI: “Huyu anaitwa Asmah ni HR wa kampuni.”

Na mama wa2 alifanya kusolimiana na Asmah maana walikuwa bado hawajasalimiana na aliomba tukae pembeni ili tuongee. Kuna mchongo mama wa2 alikuwa ananipa ambao na mimi ningepata commission na baada ya maongezi ya muda mrefu tulifikia makubaliano na niliukubali mchongo. Tuliagana pale na mama wa2 na tukaondoka na Asmah maeneo yale kurudi ofisini, lakini wakati tuko njiani Asmah alikuwa ananipiga sana maswali,

ASMAH: “Insider huyu mama ni nani?”

MIMI: “Unataka kusema ni lishangazi langu sindio?, huyu ni mtu wangu wa karibu kama wewe.”

Asmah alicheka na akaendelea kuongea,

ASMAH: “Hapana sijamaanisha hivyo, last time nilikuuliza umefahamianaje na Iryn lakini hukunipaga majibu ya kueleweka.”

MIMI: “Nilikujibu sema umesahau.”

ASMAH: “Ulinijibu kimkato sana, kama uliweza kufahamiana na Iryn na akakuzoea na bado amekuwa mpenzi wako, una nyota.”

MIMI: “Mbona wewe hujisifii sasa? Kwahiyo mimi kufahamiana na wewe sio nyota?”

ASMAH: “Insider mimi kwa Iryn sio kitu, kujifananisha na yeye namkosea heshima.”

MIMI: “Asmah tatizo lako ni moja tu hujikubali, lakini wewe ni moja ya wanawake warembo hapa duniani.”

ASMAH: “Napata wapi ujasiri wa kujilinganisha na Iryn? kwanza kanizidi kipato, kanizidi uzuri bado kaniajiri.”

Ilibidi nicheke maana Asmah alikuwa kaongea ukweli mtupu na muda huu tulikuwa tumeshawasili ofisini na maongezi yaliishia hapo.

Niliendelea kukaa pale ofisini na nilipata wazo la kwenda kwa Jane kumpa taarifa kwamba sitokuwepo kwenye arobaini ya mtoto. Niliwaza ni busara nikaenda Mbweni kuonana na Jane ana kwa ana kuliko kupiga simu na kutoa taarifa.

Saa 12 jioni nilikuwa nimewasili pale kwa Jane na Vicky ndo aliyenifungulia gate na baada ya kupark gari niliendelea kupiga story na Vicky pale nje then nikaingia ndani. Kwa upande mwingine pale seblen palikuwa na mama Jane na pindi anaponiona huwa anafurahi sana na nilimsalimia tukawa tunaongea.

Jane alitoka ndani na kama kawaida yake alinipa ishara na tulikwenda kukaa garden kwaajili ya mazungumzo,

MIMI: “Shem maandalizi yanakwendaje ya 40 ya mtoto?”

JANE: “Unafikiri kuna maandalizi bhasi? Bado hata tulichoanza.”

MIMI: “Mary bado anakuja hapa home?”

JANE: “Toka uje weekend hajaja tena ila aliniambia atakuja ijumaa hii.”

MIMI: “Shem mimi nimekuja kukupa taarifa sitokuwepo hio jumamosi maana nimepata emergence na ninaondoka ijumaa hii kwenda Kenya.”

JANE: “Jamani! Mbona hivyo shem? Kuna shida gani imetokea ifanye usiwepo?”

MIMI: “Ni masuala ya kiofisi tu ndomana na sina mtu wa kusema aende zaidi yangu, natamani sana ningekuwepo ila naamini hakuna kitacho haribika.”

JANE: “Insider ulipaswa uwepo shem, kuna zawadi nilikuwa nimekuandalia nikukabidhi hio siku kama mchango wako kwangu kwa kipindi chote, sasa nitafanyaje?”

MIMI: “Naelewa shem na naomba samahani kwa hili maana ni suala ambalo limekuja haraka na sina jinsi. Kuhusu zawadi unaweza mpa hata Mary ili nirahisishe mazingira ya kuonana naye na tuyamalize.”

JANE: “Uwasiliane naye na umpe taarifa.”

Niliagana na Jane kuondoka kurudi home na kipindi niko njiani nilijisikia vibaya sana kuondoka na kuikosa arobaini ya mtoto, ukizingatia uwepo wangu ungekuwa ni muhimu sana. Kwa upande mwingine Jane alionekana kutozipokea vizuri taarifa zangu ni kama nilikuwa nimemkatili na hakutegemea.

Nilitoa simu nikampigia Mary lakini ilikuwa inatumika na nilipiga kama mara 3 bado namba inatumika. Baada ya dakika 10 nilipiga tena lakini bado niliambiwa inatumika na nikapark gari pembeni ili nimtumie ujumbe kwenye whatsapp. Baada ya kufungua whatsapp nilibaini ameniblock na hapa ndo nilishangaa sana nikajisemea kweli Mary yuko serious hataki mazoea na mimi this time.

*****
Ijumaa ilikuwa ndo safari ya kwenda Ethiopia na maamuzi niliyoyachukua niliona ni ya busara ukizingatia Iryn ni kama mke wangu. Niliona sometimes ni bora ujifanye mjinga ili mambo yaende maana Iryn amenipa heshima kubwa sana. Zawadi kubwa ya kumpa sina hata kumpeleka Ethiopia iwe mtihani? Niliona mambo kama haya ndo yatafanya mapenzi yake kwangu yaendelee kuongezeka.

Kuhusu home niliwapanga kuwa nimepata emergence ya kwenda Kenya kuna mzigo nakwenda kuufata na umefikia bandari ya Mombasa. Home hawakuwa na shida kabisa maana waliona ni suala la kazi, hivyo sinabudi kwenda huko. Yule mtu wa Iryn pale ubalozini alikuwa kanicheki jumatano na alinipa visa yangu kwaajili ya safari.

Nilinunua zawadi ya ua kwaajili ya kumpa Iryn na nilikwenda JNIA maana yeye alikuwa anatarajia kuingia saa 9 za mchana. Saa 10 jioni aliwasili na baada ya kuonana alikuja akanikumbatia na alikuwa amependeza sana. Kwa upande wetu sisi tulikuwa tunatarajia kuondoka na ndege ya saa 12 jioni na tulikaa pale Bao cafe tukipiga story.

Kwa upande wake alionekana kuwa sawa tu maana wasiwasi wangu ulikuwa kwenye tumbo lake, na lilikuwa la kawaida tu. Nilitoa zawadi ya ua nikamkabidhi pale na alifurahi sana, na yeye alitoa zawadi ya simu akanipa ilikuwa ni iphone 14 pro.

IRYN: “Darling leo tutalala wote hotelini then kesho tutakwenda home.”

MIMI: “Mhh! si watakushtukia umelala hotelini?”

IRYN: “Hapana nimewambia naingia kesho so it won’t be a problem.”

MIMI: “Na tunakwenda lini kwenye kaburi la mama?”

IRYN: “Jumapili ndo kumbukizi ya mazishi yake.”

MIMI: “Na vipi kuhusu mimba unaonaje haiwezi kuleta shida? Na wasiwasi watajua hali yako.”

IRYN: “Mara nyingi usiku ndo inanisumbua ila haitakuwa tatizo niko makini I promise. Mama mkwe wangu hajambo? Na wish sana nimuone hata kwa mbali tu.”

MIMI: “Usijali utamwona kuwa na subira baby.”

IRYN: “Lini hiyo? Maana chance ndo sasa au utanipeleka mkoani?”

MIMI: “Wewe usijali nipe muda niendelee kuandaa mazingira sawa mummy?”

IRYN: “Sawa darling no problem.”

Tulicheck-in na safari ya kwenda Ethiopia ikaanza, kimbembe tuko kwenye ndege mahaba yalikuwa motomoto hata hatukujali kama watu. Nilianza kumuuliza maswali Iryn kuhusu mila zao maana nilitamani sana kuzijua ili nisizingue huko Ethiopia.

IRYN: “Mama yangu ana mixer ya Mursi na Oromo tribe maana babu ni Mmursi na bibi ni Oromo. Babu alikufa mama akiwa mdogo sana na kupelekea kulelewa na bibi miaka yote na hii ikapelekea sisi kubase kwenye Oromo tribe. Bibi yangu yupo home utamwona na kama unavyoniona mimi tumefafana kila kitu wewe utaona nitakutambulisha.”

MIMI: “Sawa haina shida nifundishe na namna ya kusalimia watu ili nisizingue huko.”

IRYN: “Nitakufundisha baadhi ya maneno muhimu ya kuongea just in case”

Na alianza kunifundisha pale taratibu na mimi nilikuwa makini sana kumsikiliza maana sikutaka kuzingua huko,

How are you?- Isin attam?

I’m fine-Nagaa

What is your name?- maqaan ke eenyu?

And you?- ati ho?

Where are you from?- Biyyi ke eessa?

I’m from Tanzania-Biyyo ko Tanzania.

How old are you? -umuriin ke waggaa meeqa?

I'm good -Fayyaadha

Do you speak english?- Afaan Ingiliizi beekta?

Thank you- Galatoomi

“Baby nafikiri haya ndo muhimu endelea kuyapitia uyajue yatakusaidia kwa kiasi chake. Baby ondoa wasiwasi ukoo wetu ni wakarimu sana hata watu wote kwa ujumla ni wakarimu hawana shida kabisa. Utauona ukoo wetu wote kesho na naomba uwe na amani hata usiwe na wasiwasi I know you’re confident.”

MIMI: “Naona unanipa matumaini lakini kwa mwanaume kuja ukweni kwa mara ya kwanza tena bila washenga ni kipengele. Nimekuja sababu ya mama na sio wewe, naomba usioneshe sign zozote zitakazo onesha tuko kwa mahusiano.”

Saa 4 za usiku tuliwasili Addis Ababa lakini hatukushuka maana safari yetu ilikuwa kwenda Bahir Dar. Huu ni mji ambao upo kaskazini mwa Addis Ababa na ndo Lake Tana liliko, na umbali wa kutoka Addis mpaka Bahir ni kama 600km hivi haina utofauti sana wa Dar na Dodoma.

Tulikaa kama nusu saa pale Addis na tukaondoka kuelekea Bahir na tulitumia nusu saa tukawa tumewasili. Muda ambao tuna land mji ulionekana kuwa mzuri sana kwakweli na baada ya kushuka kwa ndege tuliondoka kwenda hotelini.

Muda huu mimi nilikuwa kimya hata yeye alikuwa kimya mpaka tunawasili hotel ya Blue nile na ipo karibu na lake Tana. Wakati tumefika hotelini huku njiani nilikuwa napishana na warembo visu balaa, nilijikuta naanza kushangaa aisee ni hatari.

Nilisikia Iryn akisema,

IRYN: “Baby, keep walking. Wha the f*ck are you looking at?”

Nilinyamaza kimya maana nilikuwa nimezingua na nimesahau uwepo wa Iryn na aliendelea kuongea,

“You said mimi ni mwanamke mrembo hapa duniani umeona warembo sasa? Nafikiri mpaka tunaondoka huku utakuwa umeona hali halisi kuwa mimi ni wa kawaida tu.”

Kauli aliyosema Iryn ilikuwa ina ka ukweli ndani yake maana pisi niliyokuwa nimepishana nayo ilikuwa ni hatari tupu.

MIMI: “Mummy wewe ni mwanamke mrembo bado sijaona wa kukuzidi.”

Na nilisikia akini fyonza,

IRYN: “Fyoooooh! umepagawa na dada wa watu mpaka ukageuka, hii ni hotel ya kitalii na most ya watalii wanafikia hapa, utakutana na warembo wengi sana. Sijui kwanini nilikuleta hii hotel utaweza kuvumilia kweli?”

MIMI: “Sasa baby kwanini umenileta hapa kama unajua haya yatatokea? Anyway mimi najitambua siwezi fanya ujinga unaouwaza.”

IRYN: “Insider wewe ni mtu mzima tayari fanya lolote ambalo unaona litakupa furaha, huenda naongea na mtu ambaye bado hajataka kujua majukumu yake.”

MIMI: “Baby kwanini unasema maneno hayo? Ni nini maana ya kuja huku?”

Muda huu tulikuwa tuko room yetu tayari na nilikuwa nafikiri kwanini Iryn anaongea maneno kama haya? Na toka aje Dar niliona mabadiliko yake, nikahisi kuna jambo haliko sawa. Nikawaza acha leo nimuoneshe ukichaa wangu maana haujui, mazoea yanazidi sasa ngoja nimuoneshe. Yeye alikuwa amekaa kitandani, haraka nilimkamata nikambana kitandani ile tunaangaliana na alikuwa hawezi kufurukuta, maana nilimbana kisawasawa,

“Leo utanambia siri zote zinazoendelea kati yako na Claire, lasivyo nitakuharibu hapa na uzuri niko kwenu tuone utanifanya nini.?”

Nilikuwa nimembadilikia na alianza kuogopa,

IRYN: “Insider, stop this. You’re disrespecting me.”

MIMI: “Ndo uongee sasa nadhani hunijui vizuri, unaniletea dharau zako za kiseng*seng* leo nakuonesha mimi ni kichaa, afu tuone kama utanipeleka police.”

IRYN: “What's wrong with you? You forgot I'm pregnant?”

Na aliendelea kufurukuta ili ajinasue lakini wapi nilikuwa nimemdhibiti vizuri,

MIMI: “Naelewa ila naomba uniheshimu na sio kunipangia nini cha kufanya hili sio ombi ni lazima, shenzi zako. Na umwambie Claire aache usnitch wake kabla sijamfanya mbaya I know what is really going on na mimi sio mtoto, kwanza nimekuzidi miaka pumbavu.”

Na nikamwachia pale,

IRYN: “Don’t dare ever touch me like that again.”

Na mimi nilianza kucheka kwa dharau pale na yeye aliishia kununa akalala bila kuoga na kula akasahau.

Asubuhi baada ya kuamka alikuwa kanuna sana, nilimpa salamu lakini hakuijibu na baada ya kujiandaa tulikwenda kupata breakfast. Wakati tunapata breakfast yeye alikuwa busy na simu yake na mimi nilikuwa busy na simu yangu. Mida ya saa 5 asubuhi tuliondoka pale hotelini kwenda kwao na tulitumia muda mchache sana kuwasili kwa makadirio ya haraka kutoka pale hotelini mpaka kwao ni kama 10km.

Baada ya kushuka kwa Tax mbele yangu ilikuwa inaonekana nyumba kubwa nyeupe nzuri na Iryn alisema hapa ndo home na haikuchukua muda tulifunguliwa gate tukaingia ndani. Kwa upande mwingine niliona mama mtu mzima akija na dada watatu kwa spidi sana usawa wetu na wakamkumbatia Iryn. Yule mama mtu mzima nilimgundua ni mama yake mkubwa maana nilikuwa namuona kwa picha tu.

Baada ya kuingia ndani Iryn alifanya utambulisho pale na alianza kunitambulisha mama yake mkubwa na alisema wale ni wadogo zake kasoro mmoja ndo alikuwa ni dada yake. Kwa upande wangu Iryn alinitambulisha kwa ndugu zake mimi ndo manager wake ambaye nasimamia kampuni zote alizoacha mama yake. Wenyeji walionesha kunifurahia na haikuchukua muda bibi yake alitoka ndani na alifurahi sana kumuona Iryn, na kweli walikuwa wamefanana sana.

Asilimia kubwa ya maongezi yaliyokuwa yanatumika hapa ni lugha yao, mimi nilikuwa kimya maana sikuwa naelewa chochote. Seblen nilikuwa mpole sana maana nilikuwa kama nimetengwa hivi na Iryn alionekana kuwa busy sana na ndugu zake.

Baada ya nusu saa Jimmy aliingia na alifurahi sana kuniona na hapa kidogo nikawa na amani maana alikaa pembeni yangu tukawa tunapiga story. Baadae tulitoka nje kukaa na tukaendelea na story zetu na kubwa nilishangaa akiniambia anajua kila kitu kinachoendelea kati yangu na Iryn na alinitoa wasiwasi. (Kuhusu Jimmy ref Season1 Epsode 56)

Mida ya saa 1 jioni mimi niliamua kuondoka na nilimwomba Jimmy anipe kampani, lakini kabla ya kuondoka nilimwomba aniitie Iryn ili niweze kumuaga mke wangu. Baada ya dakika 10 alitoka na tulizungumza kidogo sana maana alikuwa bado kaninunia na nikajisema kumbe alichukulia serious, wakati mimi nilifanya kwa utani tu na sisi tukaondoka.

Hotelini nilikuwa peke yangu maana sikuwa na kampani yoyote, hivyo nikapata wazo la kwenda kupoteza muda kwenye bar ya pale hotelin. Wakati natoka Tanzania nilitembea na $2,000 kama amergence na nilitoa noti 3 za dollar 100 nikaweka mfukoni, huyo nikasogea eneo la tukio.

Ethiopia wana sarafu yao wanaita birr sasa baada ya kufika pale bar nilimuuliza mhudumu kama naweza kulipa kwa dollar? Akanambia naweza kulipia, Japo nikosa kisheria maana nilitakiwa kufanya exchange. Nilimwambia nitampa dolla 10 ya usumbufu yeye atanisaidia kufanya exchange kwa muda wake, kwanza mhudumu mwenyewe ni pini balaa.

Niliagiza wine yangu na nikaanza kuinywa taratibu kwa upande mwingine nilikuwa nazi-zoom pisi za kihabeshi oyaa ni hatari sio poa mpaka nikaanza kudata. Nikakumbuka ule msemo unaosema “tembea uone” pisi ambazo zilikuwa zinaranda randa ni balaa. Kama pisi ikaja bongo ukafanikiwa kuimiliki unaweza kuhonga mpaka bandari na ukaipa Kigamboni kama kifungashio.

Nilimuuliza mhudumu kama nataka pisi ya kulala nayo iliyonyooka niandae kiasi gani? alinambia inategemea na quality ila kwa pisi kali wastani ni $100 tu. Aliuliza kama nahitaji nimtajie room namba yangu then mrembo atakuja naye mtaka kutokana na offa yangu. Sikutaka kuingia tamaa za kijinga na nilirudi room kulala maana niliona kuendelea kubaki pale ningeshawishika tu!, warembo niliokuwa nawaona ni balaa.

Baada ya kurudi room nilianza kuchati na Asmah maana alikuwa kanicheki na kuuliza kama nimefika salama. Tulichati sana huu usiku ni kama alihisi sina kampani na kwa mara ya kwanza Asmah alinifungukia kuwa ananipenda toka muda mrefu na alikuwa anategema labda kuna siku nitakuja mfungukia.

Asmah aliendelea kufunguka kuwa kwasasa hataki matatizo na Iryn maana amemuwahi na anabariki mahusiano yetu. Kwa upande mwingine aliendelea kukazia kuwa hajapenda Kitendo nilichomfanyia ile siku usiku na nisirudie tena.
***
Asubuhi Jimmy alikuja kunichukua pale hotelini hatukwenda home bali tulikwenda moja kwa moja makaburini. Tulitumia kama dakika 40 kuwasili makaburini na hapo tulikuwa spidi balaa ni sawa na mwendo wa kutoka Mwenge hadi Bagamoyo.

Tuliwakuta baadhi ya watu wamewasili pale na baada ya dakika 20 hivi akina Iryn waliingia na jumla ya watu ilikuwa kama 50 hivi. Ilifanyika ibada pale makaburini na baadae watu walianza kuweka mashada na maua kama kumbukizi na nilimuona Iryn akilia kwenye kaburi la mama yake.

Daah! Nilijisikia vibaya na niliumia sana kuona Iryn akilia vile, katika siku zote ambazo nimeishi na Iryn sikuwahi kumuona akilia namna ile. Nilitamani sana kwenda kumpoza lakini niliona mazingira sio rafiki na niliishia kuumia ndani kwa ndani. Niliwaza pale kama Iryn analia vile kwaajili ya mama yake bhasi kuna haja kubwa sana ya kuwapenda wazazi wetu wakiwa hai.

Saa 8 za mchana tulirudi home kwaajili ya kuendelea na ratiba zingine na baada ya kuwasili pale home tulipata chakula cha pamoja. Jimmy alitoka ndani na alikuja kunipa kampani pale nje maana tulikuwa garden tumetengenezewa hema na viti kwaajili ya wageni.

Nilitumia nafasi hii kumuuliza maendeleo ya Iryn na akanambia yuko sawa kwa sasa na ametulia. Japo nilitamani sana ningepata hata nafasi ya kuongea naye lakini niliona itakuwa ngumu kutokana na yale mazingira. Jimmy alikuwa ananipa historia ya Iryn na mama yake na alinambia kwamba walipendana sana enzi za uhai wake na kumuona Iryn akilia vile ni kawaida. Jimmy aliendelea kuongea na alinambia nimefanya kazi kubwa sana kumuweka Iryn sawa maana alikuwa ni mtu wa mawazo sana tangu afiwe na mama yake.

Kwa upande mwingine pale home palionekana kuwa na wageni wengi sana na asilimia kubwa walikuwa wakinishangaa maana waliona mimi ni kama mzamiaji. Mida ya saa 11 jioni tuliondoka na Jimmy pale home na kwenda moja ya bar/lounge kwaajili ya kuangalia fainal ya kombe la Dunia.

Mimi na Jimmy wote tulikuwa mashabiki wa Argentina na baada ya kuwasili pale lounge, tulitafuta angle nzuri tukakaa na game ilianza saa 12 jioni kamili kama bongo tu. Katika fainali ambayo nilikuwa naangalia kwa presha ni pamoja na hii maana zilirudi goli 2 dakika za mwisho. Bado tukaenda extra time tukapata goli la tatu, bado likarudi tena aisee ilikuwa ni bonge la fainali.

Muda wa penalty mimi nilisema siangalii maana nilijua tumeshakosa ubingwa tayari lakini Mungu alisaidia tukashinda kombe. Nilikuwa na furaha sana hii siku kwakweli na Jimmy aliagiza moet tukaendelea kuinywa maana ilikuwa ni shangwe na furaha kwa mashabiki wa Argentina.

Baadae kuna pisi yake kali sana ilikuja kutupa kampani pale na Jimmy alinitambulisha kuwa yule ni mpenzi wake. Nje na kelele za furaha, lakini eneo hili lilionekana kuwa na warembo sana, pia wazungu walikuwa wengi ni kama unavyoona vile Samaki samaki.

Kwenye mida ya saa 5 za usiku Jimmy alinipa taarifa kuwa Iryn ananiulizia maana amekuja hotelini hajanikuta na amemwambia tuliko. Ndani ya dakika 15 Iryn aliwasili pale na alimpiga Jimmy jicho kali sana bila hata kumsemesha na akaniomba tutoke nje ili tuongee,

MIMI: “Mummy unaendeleaje kwasasa?”

IRYN: “Niko poa, nimekuja hotelini sijakukuta kumbe umetoka na Jimmy.”

MIMI: “Yeah! Shem wangu kanitoa maana niko peke yangu tu hana kampani sina.”

IRYN: “Sitaki kukuona unatoka na Jimmy.”

MIMI: “Kwanini tena? Ni shem wangu shida iko wapi?”

IRYN: “Sizipendi tabia zake za kupenda wanawake ni hajatulia, angekuwa anakuheshimu hata asingeleta mwanamke pale.”

MIMI: “Amenitambulisha ni mpenzi wake sasa shida iko wapi?”

IRYN: “Mwanamke wake yuko pale home na mtoto wake, kamuacha kaja huku kuonana na malaya zake, naomba tuondoke twende hotelini please!.”

MIMI: “Sisi tumekuja kuangalia match bhana, ngoja nikamuage tuondoke.”

Ile nataka kwenda kumuaga alinivuta kunikataza na tukaondoka pale kurudi hotelini. Baada ya kurudi hotelini kwa upande wangu nilikuwa nina mizuka yangu, sasa ile kumshika si akani push kuonesha hataki dudu na nilishangaa sana.

“Sasa mummy unenitoa kwa Jimmy kisa wivu wako, unanirudisha hotelini hata kunipa utamu ni shida si ungeniacha tu kule mimi niendelee kupoteza muda?”

Iryn aliniangalia na hakujibu kitu aliishia kunyamaza kimya, na mimi niliendelea kuongea,

“Hii safari sijui why nimekuja huku maana Roho yangu ilikuwa haitaki, haya ndo matokeo ya kuforce. Anyway kesho mimi naondoka maana sioni faida ya kuendelea kubaki huku kama unaninunia.”

Mimi nilikwenda kuoga na baada ya kutoka washroom nilikuta Iryn hayupo na mimi nilijua ameondoka kurudi kwao, ni wivu wake ulikuwa una msumbua. Pale kitandani kulikuwa na karatasi nyeupe ameiandika na niliichukua ili nisome alichoniandikia.

CHAPTER 10
 
Umetisha mno....Usichelewe next
 
Daah kumbe hii story inaendelea.. basi utakua umeniacha mbali sana maana niliishia pale IRYN keshazira kuongea na wewe na anaenda SA
 
Daah kumbe hii story inaendelea.. basi utakua umeniacha mbali sana maana niliishia pale IRYN keshazira kuongea na wewe na anaenda SA
Mimi niliikuta inaendelea
.

Baada ya irylin kubeba damu ya jamaa demu kaona amgande jamaa.

Story ndio inaendelea kwa hapo.

Ila nilichogundua. Mwanamke kabla hajaliwa. Alitoa ukamla na akawa hataki kuliwa na mwanaume mwingine kwa maana sio malaya baasi ndio kipindi anachoptia INSIDER MAN

Iryln sio malaya hivyo diudu ya INSIDER MAN ndio pekee sasa naona dem anazidi kuchanganukiwa. Swali je Mama J anajua dem ni mke mwenza??
 
tat
Hii movie ilibamba sana 1st season sahv imepoa sana.
zo n msmuliaj stor isngepoa tatzo huyo jamaaa yan mpak ajskie kutuma so imepelekea stor kupoa koz hamu ya kupata kitu inaishia pnd kitu knapochelewa kupatkana so stor bado kupoa sema msmuliaj.kapelekea kukosekana radha iliotegemewa ktk vchwa vya weng
HAYO N MAWAZO YANG SIO LAZMA KUYAPOKEA WALA KUYAJIBU
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…