Shetani tenaMkuu umeongea point nzito sana.
Mikasa ipo Mikali sana tunaogopa codes..
Matukio ya INSIDER ni ya kawaida kwa Wanaume flani flani hivi...ndio maana tunakufa mapema.
Juzi tu tumeamua case moja matata...mtu unawatoto tisa na wanawake wakali mbaya😀😀😀😀😀😀
Shetani atusamehe...
Tabia za kike, ukitetea basi na wewe utakuwa nazo hizo tabia .Mwanamme kupika sio ushoga rafiki, na utanashati kunukia sio ushoga, yaan ww sijui umekula maharage ya wapi
Huu ni mkasa unaoendelea kwenye maisha yake ya kila siku mbona ngumu kuelewa?kuelewa mkuu akikaa na kukusanya matukio ya mwezi mzima huoni story inakuwa kwenye mtiririko mzuri?
Bro, kwa ushauri tu wa Bure; maliza hii story, just make it final🙏🏼. Inatosha.Kesho tutaendelea na Episode 2. Kesho inaanzia saa 6 lakini. See you soon 🔜
Nitakutumia script zote unisaidie kufinalize. Pia kuna thread nyingi humu JF za kusoma, kama unakesha hapa. Pole sana!Bro, kwa ushauri tu wa Bure; maliza hii story, just make it final🙏🏼. Inatosha.
Umempa dogo jibu la kikatili sana hahahaNitakutumia script zote unisaidie kufinalize. Pia kuna thread nyingi humu JF za kusoma, kama unakesha hapa. Pole sana!
@INSIDER MAN mkuu kuna pm yangu nilikutumia ndg naomba uijibu kama hutajali ndgNitakutumia script zote unisaidie kufinalize. Pia kuna thread nyingi humu JF za kusoma, kama unakesha hapa. Pole sana!
saaa we unacheka nn hapoUmempa dogo jibu la kikatili sana hahaha
Hahahahaha, sio jibu la kikatili😜, nilitaka hii reaction from him. If you want to see a lion, go to it's cage.Umempa dogo jibu la kikatili sana hahaha
Hizo theory ndo zipi hebu mwambie atunuze halafu weka shots hapaNapata mrejesho kutoka kwa wadau😂😂🙌🏿🙌🏿
Na kwa upande mwingine asmah alikua akinipigia sana simu lakini sikutaka kupokeaNikahisi something fishy is going on..
Itaendelea
a moment ago thanks sana boss leo nimekua firstSEASON 02
EPISODE 29
“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”
PREVIOUS:
Saa 12 jioni nilianza safari ya kwenda Dodoma na nilichukua bodaboda wa kunipeleka Magufuli stand. Muda wa jioni mabus huwa yanasumbua hivyo, nilisogea pale darajani kwa Yusuph nikapata private inayokwenda Dodoma.
CONTINUE:
Safari ya kwenda Dodoma ilianza pale na gari ilikuwa ni Harrier. Tulikuwa jumla ya watu sita, pamoja na dereva. Tulikaa wanne nyuma ya seat, tukiwa tumebanana kimtindo—wanaume wawili na wanawake wawili.
Nilipokuwa barabarani, nilikuwa kimya sana, hata sikushirikiana na wenzangu katika mazungumzo. Nilikuwa nikiwaza mipango yangu ya biashara Dodoma na kupanga kumpigia simu dalali kumkumbusha kuhusu jambo letu.
Lengo langu la kwenda Dodoma ni kufungua biashara ya kuuza lubricants za magari na kufanya services. Nia yangu hapo baadae nipanue biashara hii kwa kuuza bidhaa kama vipuri vya magari, urembo, rims, na matairi.
Niliweka lengo kwamba ifikapo Jumatatu ya wiki ijayo, nitakuwa tayari nimeanza biashara yangu. Nilidhamiria kwa dhati kuanzisha biashara. Pia, nilipanga kuwa na nidhamu ya fedha kwa kipindi chote nitakachokuwepo Dodoma.
Saa 7 za usiku, tulipowasili Dodoma, baridi kali lilikuwa limetanda. Nilipata lodge iliyoko karibu na Chuo cha CBE na kwenda kupumzika.
Asubuhi baada ya kuamka jambo la kwanza niliwasiliana na Aggy kumpa taarifa niko Dodoma. Kwa upande wake alishangaa sana kusikia nimekuja bila kumtaarifu mapema na alisema baada ya nusu saa atakuwa around.
Baada ya hapo, nilimpigia simu dalali ili anipe mrejesho pamoja na ratiba zake. Lengo langu lilikuwa kuanza leo hii kutafuta frem za biashara ili mipango yangu iende kama ilivyopangwa. Dalali aliniambia tukutane baadae, na akanihakikishia kwamba bado anaendelea kutafuta frem zingine ili tuwe na chaguo la kutosha wakati wa kuangalia.
Ndani ya nusu saa, Aggy alikuwa tayari amewasili, nami nikatoka kwenda kuonana naye ili tuondoke. Tulipokutana, tulisalimiana kwa furaha na tukakumbatiana kwa upendo, kisha safari yetu ya kuelekea nyumbani kwake ikaanza.
Aggy alionesha kuwa na furaha sana maana mara ya mwisho kuonana ilikuwa ni October kipindi nimeenda na Iryn. Aggy aliulizia kuhusu maendeleo ya nyumbani na hakumsahau Iryn, ndipo mazungumzo yakaanza;
AGGY: “Yule mrembo yupo?”
MIMI: “Yupo mama ila sio Tanzania hii.”
AGGY: “Na kwanini unakuja bila kunipa taarifa na unafikia lodge?”
MIMI: “Nilitaka nikusurprise au hujapenda?”
AGGY: “Tufanye umeshinda.”
MIMI: “Naona unazidi kuwa mrembo nipe siri ya mafanikio au mama anamwaga pesa mingi huko maofisini.”
AGGY: “Hahahahaa hali mbaya Insider bora hata wewe uliejiajiri.”
MIMI: “Hamjawahi kukubali kuhusu hili, sawa bhana.”
Ndani ya muda mfupi tuliwasili nyumbani kwake na alinikaribisha seblen kisha akaniandalia na chai ili ninywe. Aggy alitamani sana kujua sababu iliyonileta Dodoma, nami nilimwambia mipango yangu yote na aliishia kunipongeza. Nilimwambia nitakuwepo Dodoma kwa muda mrefu mpaka pale ambapo nitaona biashara imesimama na haihitaji tena usimamizi wangu.
Aggy aliniaga anarudi ofisini na kutoa ahadi atawahi kurudi, kwa upande wangu nilimpa ratiba zangu za kutoka jioni kwenda kuonana na dalali, na alisema atakuwa karudi tayari, hivyo atanipa kampani ya kwenda.
Saa 10 jioni tulikutana na dalali maeneo ya Sabasaba, kisha tukaanza kuangalia frem zote alizokuwa nazo. Baada ya kuzunguka sana niliipenda frem moja ipo katikati ya mjini ilikuwa location nzuri sana.
Muda ulikuwa umeenda sana, na mhusika wa hii frem alituambia tukutane kesho asubuhi ili kuweka mambo sawa. Baada ya hapo, Aggy alipendekeza tupitie sehemu kwaajili ya kupata chakula cha jioni, tutakapokarudi nyumbani, ni kulala moja kwa moja.
Wakati tulipokuwa tunakula chakula, mazungumzo yaliendelea pale, ambapo Aggy alisema kwamba mwezi ujao anatarajia kusafiri kwenda mkoani kuwasalimia wazazi wake. Nami niliona wazo lake lilikuwa zuri sana, hivyo lilinipa hamasa ya kwenda kumtembelea mama, na tukakubaliana kwamba tutaenda pamoja.
Kama nilivyowahi kusema hapo awali, mimi na Aggy tulisoma katika chuo kimoja, tukichukua course moja. Zaidi ya hilo, tulipitia shule moja ya O-Level, na wazazi wetu pia wanatoka mkoa mmoja.
Baada ya kurudi nyumbani, nilimpigia simu Maggy kumtaarifu kuwa nipo Dodoma, isinge kuwa busara kula buyu ukizingatia ananisaidia sana kuangalia nyumba yangu. Hata hivyo, baada ya kumpigia hakupokea simu zangu, kwa vile muda ulikuwa umekwenda, nilijisemea kwamba akiziona missed call atanipigia.
Aggy alikuwa amepanga nyumba ya vyumba viwili, hivyo alinionesha chumba changu cha kulala, kisha akaniga anakwenda kulala na tutaonana kesho.
Asubuhi baada ya kuamka nilikuwa na ratiba ya kukutana na dalali ili kwenda kufanya malipo kwa fremu iliyokuwa kwenye mipango yetu. Lakini, dalali alinijulisha kuwa kuna fremu nyingine mpya imepatikana na iko kwenye eneo la Sheli, tukakubaliana tuanze kwanza kuiangalia hio frem.
Baada ya kuliona eneo lilikuwa lina mvuto mkubwa, na nikawaza kuwa litakuwa na faida kubwa kama likitumika kama sehemu ya kufanyia service, huku eneo la mjini likiwa kama showroom. Nilionana na mhusika na baada ya maongezi ya muda mrefu akasema wanapangisha kwa 350,000, hivyo nilichukua namba zake za simu na tukaondoka.
Dalali alinishauri kama naweza nichukue eneo la sheli maana nitapata wateja wengi sana wa service, kwani sehemu ni nzuri sana. Tulishauriana sana na nikamwambia anipe muda nijifikirie, na alisema kuhusu fundi yupo dogo anamjua na anacheti cha VETA naweza kufanya naye kazi.
Tulienda straight kuonana na landlord ili tufanye malipo ya frem ya jana na baada ya kukutana na mhusika nilifanya malipo ya 2.4M kwa miezi 6. Sikutaka kupoteza muda nikatafuta fundi wa kuanza kutengeneza shelves ili nianze biashara.
Niliandaa mipango yangu nikaona kuna haja ya kurudi Dar kwaajili ya kuchukua mzigo wa lubricants/vilainishi. Habari njema hii biashara nina uzoefu nayo, hivyo haikuwa shida kwangu kuifanya na kuwatafuta suppliers maana machimbo yote nayajua na nina namba zao.
Niliwaza kutafuta chumba cha kupanga kwa kipindi chote nitakachokuwa Dodoma. Kuendelea kukaa kwa Aggy sikuona jambo la busara ukizingatia mimi ni mtoto wa kiume, nahitaji uhuru.
Mipango yangu ilikuwa kufikia jumatatu niwe nimenza biashara, pia niwe nimeondoka kwa Aggy tayari. Lakini jambo la kwanza nitaanza kwenda Dar, kisha baada ya kurudi nianze mchakato wa kutafuta geto.
Jumamosi frem ilikuwa imekamilika tayari kwa kuingia na kuanza bishara, hivyo nikaona kesho jumapili nirudi Dar, ili jumatatu niwe Kariakoo kuchukua mzigo.
Jioni nilienda kumsalimia Maggy nyumbani kwake maana ilikuwa ni kitambo kimepita bila kuonana. Baaada ya kuwasili pale kwake alinikaribisha, lakini nilianza kwanza kukagua nyumba.
Mazingira ya nyumba yalikuwa mazuri na yakivutia, kwani palikuwa pamepandwa maua maua na miti ndani na nje ya fenzi. Pia nilimsalimia jirani yake ambaye ni mpangaji wangu, baada ya hapo tukaingia ndani kuendelea na maongezi mengine;
MAGGY: “Karibu sana baba mwenye nyumba, sijui nikuletee kinywaji gani?”
MIMI: “Maji yanatosha.”
Alimuagiza dada aniletee maji na story zikaendelea;
MAGGY: “Umekuja lini huku? Halafu kimya kimya.”
MIMI: “Nilitaka nikufumanie una bahati sana.”
MAGGY: “Huhuuu! Yule dada mrembo yupo?”
MIMI: “Yupo masomoni ni muda hatujaonana.”
MAGGY: “Kwa uzuri tu amebarikiwa asee, kuna watu walipendelewa.”
MIMI: “Mbona wewe umependelewa mahips au hujioni?”
MAGGY: “Insider ni mshenzi wewe! Mimi nimefurahi sana kukuona, sijui wifi yangu anaendeleaje na mtoto.”
MIMI: “Wako poa nashukuru Mungu. Bado wewe sijui unasubiri nini.?”
MAGGY: “Wanaume waoaji kama wewe hawapo siku hizi.”
MIMI: “Naamini shemeji yupo ila unamfichaficha.”
MAGGY: “Insider tuachane na haya, nimekumiss sana Dar.”
MIMI: “Karibu sana kwenye mji wetu.”
Tuliongea mambo mengi likiwemo suala langu lililonileta Dodoma, pia kwa upande wake alisema ana mpango wa kutafuta kiwanja aanze ujenzi taratibu. Tulipata dinner ya pamoja na baada ya hapo nilimuaga maana Aggy alikuwa akinipigia sana simu.
Baada ya kuagana na Maggy nilimpigia simu Aggy na alisema ananisubiri ili tukale dinner, nikamwambia nimeshakula tayari, akaomba nimpelekee chips yai na mishikaki.
Baada ya kurudi home nilimtaarifu Aggy kuhusu kurudi Dar siku ya kesho kwaajili ya kuchukua mzigo na nitarudi jumatatu na nikamuaga nikaingia chumbani kulala.
Jumapili asubuhi, niliondoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam na nilifika nyumbani jioni kwenye makazi mapya. Mara baada ya kufika, mazingira yalikuwa tulivu sana kiasi kwamba nilianza kumkumbuka Junior wangu, kwa jinsi nilivyozoea fujo zake ndani, mara agombane na mama yake au dada yake kwa sababu ya utundu wake.
Mazingira ya home yalianza kuniboa mpaka nikatamani kwenda Mbweni kwa Ghati, zile siku mbili nilizolala kwake zilinidatisha sana. Baadae nikaona wacha niende Upepo garden kupoteza muda kwanza nilikuwa jirani na mazingira ya huku.
Nilikwenda nikakaa sehemu ambayo mara ya mwisho nilikuwa na Prisca na nilijukuta namkumbuka tena. Niliagiza bia zangu nikawa nakunywa huku napanga mipango yangu taratibu nikipulizwa na upepo wa bahari.
Jumatatu nilienda Kariakoo nikanunua mzigo wa kutosha, kisha nikauepeleka transporter kwaajili ya kuusafirisha kwenda Dodoma. Gari huwa zinasafiri usiku, hivyo kufikia kesho asubuhi mzigo ungekuwa umefika tayari.
Baada ya kumaliza taratibu zote, nilianza kufanya utafiti kuhusu bei za spares za magari, hasa kwa bei za jumla. Kwa bahati nzuri, Kariakoo nina kaka yangu ambaye anauza spares za magari na yuko mtaa wa MAFIA/SIKUKUU. Amekuwa msaada mkubwa kwangu katika sekta hii, na ana duka lake kubwa sana, anauza kwa jumla, jambo ambalo limenisaidia sana.
Niliwasiliana na Dullah ili tuweze kuonana na lengo nimkabidhi funguo za nyumba incase kama mama J atahitaji kurudi home na tulikutana pale breakpoint Makumbusho japo alifika kwa kuchelewa sana;
DULLAH: “Ndugu yangu nimekuweka sana, nilikuwa naacha maagizo ofisini.”
MIMI: “Naelewa bro! Kama unavyoniona niko busy na mipango yangu hapa.”
DULLAH: “Dadeki kitu Macbook Air hii dukani inakwendaje?”
MIMI: “Mahali uliyolipa kwa Latifah zidisha mara 4.”
DULLAH: “Mseng** wewe unataka kusema ina thamani ya Million 8?”
MIMI: “Ndo maana yake au huamini?.”
DULLAH: “Niambie naona umebadili namba ya simu tayari na ukaondoka bila taarifa, nakutafuta kwa simu sikupati mpaka nikahisi labda dada amekufungia ndani.”
MIMI: “Daah aisee sio poa, halafu unajua ile manzi ina mtoto? Japo anadai baba mtoto alikufa.”
DULLAH: “Mhh! Becareful mzee, umeomba akuoneshe kaburi la baba mtoto?”
MIMI: “Tuachane na haya kaka, mwanamke mwenyewe sina mpango naye ilitokea bahati mbaya wewe ndo uliniforce niende. Unajua nilikuwa Dodoma na nimepata frem tayari?, halafu nimerudi jana kufuata mzigo na kesho mapema naondoka.”
DULLAH: “Hongera sana kaka, itabidi nije Dodoma siku moja maana sijawahi fika kabisa.”
MIMI: “Karibu uje uangalie fursa. Mzee mimi sina story leo, nilichokuitia hapa nilitaka nikupe taarifa ya kuanza biashara na pia nimehama pale home, nimehamia mbezi chini kabisa.”
DULLAH: “Kwanini umehama sehem nzuri kama ile?”
MIMI: “Nimehama kwasababu maalumu, pia naomba nikukabidhi funguo endapo wife akihitaji atawasiliana na wewe.”
DULLAH: “Haina shida bro usiwe na wasiwasi.”
MIMI: “Nashukuru sana, mimi sikai nataka niwahi home nikalale, kesho niwahi kuondoka kwenda Dodoma kupokea mzigo. Baada ya hapo nina safari nyingine tena ya kwenda mkoani kumsalimia mama yangu.”
DULLAH: “Naona unataka ukachukue baraka kwa bimkubwa.”
MIMI: “Muhimu kaka si unajua biashara zina mazingaombwe sana.”
DULLAH: “Naelewa kaka wewe wahi mengine tutaendelea kuwasiliana.”
Baada ya kuachana na Dullah niliondoka straight kuelekea home na baada ya kufika, nilifanya mawasiliano na Aggy anisaidie kumtafuta dada wa kushinda dukani.
Kesho yake nilirudi Dodoma mapema maana nilitumia usafiri wa anga, pia nilikuwa nina safari nyingine ya kwenda mkoani. Baada ya kuwasili nilienda moja kwa moja kufuatilia mzigo wangu na baada ta kuupata nilitafuta usafiri wa kuupeleka dukani.
Baada ya kupeleka mzigo dukani, nilimpigia Aggy simu kumtaarifu kwamba naenda mkoani kumsalimia mama yangu. Aggy alishangaa kwanini haraka sana? Hata sijapata muda wa kupumzika?, nikamwambia ni muhimu sana kwenda, na nikaondoka kwa private.
Niliingia mkoani usiku kwa upande wa pili, mama hakuwa na taarifa za ujio wangu, hivyo nilitaka kumsaprize. Nilipofika home geti lilikuwa tayari limefungwa, ikabidi nigonge, mbwa walikuwa karibu wakaanza kubweka pale, na walikoma mara moja waliponitambua.
Moja ya Mbwa wetu anaitwa Askari, alisogea getini kwa furaha kubwa muda huu. Alianza kutoa kelele za furaha kuniona huku akitikisa mkia wake kwa nguvu na kurukia geti kwa msisimko. Askari ni mbwa ambaye nimemlea tangu akiwa mdogo, na licha ya kwamba naweza kutokuwepo nyumbani kwa muda mrefu, kila ninaporudi, daima ananikumbuka kwa upendo wa kipekee.
Dada alikuja kufungua geti na kunikaribisha ndani na ile kuingia seblen mama alikuwa na wadogo zangu wakiangalia tamthlia na baada ya kuniona aliishia kufurahi na kuja kunikumbatia kwa nguvu.
“Ooh mwanangu nimetoka kukuwazia sio muda mrefu, mbona unakuja bila kutoa taarifa huko umefukuzwa?”
“Sijatokea Dar nilikuwa Dodoma.”
“Kuna nini huko?”
“Kuna biashara nataka kuianza ndiyo imenileta hapa home.”
“Niambie nakusikiliza mwanangu.”
Tulianza maongezi na mama, ambapo nilimshirikisha kuhusu biashara ninayotaka kuanzisha. Mama alifurahi sana na alinipongeza, kisha akasema tutafanya maombezi ya nguvu kabla ya kwenda kulala. Pia, tulizungumza kuhusu mimi kuwa Zambia, na mama alifurahi sana baada ya kupata taarifa kutoka kwa baba.
Baada ya maongezi marefu, nilimkabidhi mama yangu zawadi maalum, simu ya Samsung niliyonunua Dar es Salaam. Mama alifurahi sana kwa zawadi ya simu na bila kuchelewa akaweka line.
Kabla ya kwenda kulala kama familia tulifanya maombi juu ya biashara nayoenda kuianza kwa kufunga Roho za chuma Ulete, tukimwomba Mungu kuondoa maadui watakaojaribu kunikwamisha katika safari yangu ya kibiashara. Tuliiomba pia msaada wa kupata wateja, ili biashara yetu iweze kustawi kwa mafanikio.
Baada ya maombi nilimuaga mama nakwenda kulala na masuala mengine mengi tugaongea kesho panapo majaliwa. Lakini zawadi ya simu ilimgusa sana mama yangu maana alifurahi sana na alizidi kunishukuru.
*****
Jumatano nilirudi Dodoma na niliwasili jioni, nilikuwa nimechoka, lakini nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanza biashara siku inayofuata. Kwa bahati nzuri, Aggy alikuwa tayari amempata dada ambaye angeweza kunisaidia dukani. Huyu dada alikuwa ni mfanyakazi wake wa zamani, kabla Aggy hajafunga biashara yake.
Aggy alinihakikishia kuwa huyu dada ni mchapakazi, mwelewa, na mwenye uaminifu, hivyo atanifaa sana katika biashara yangu. Bila kusita, nilimuomba Aggy amfahamishe ili kesho tukutane kwa ajili ya mazungumzo zaidi na kupanga jinsi ya kuanza kazi pamoja.
Mnamo Alhamisi, tarehe 16/03/2023, nilifungua rasmi biashara yangu. Nilianza kwa kuwajulisha watu wa karibu na kuwaomba waniunge mkono. Nilitembelea garage mbalimbali na kuwaeleza kuhusu biashara yangu, huku nikiwapatia punguzo maalum la bei.
Jumapili, nilimtembelea Mzee Mollel nyumbani kwake ili kumsalimia na kumshirikisha kuhusu biashara mpya niliyofungua. Mzee Mollel ni rafiki wa karibu wa baba yangu, na ninamheshimu sana kama mzazi wangu mwenyewe.
Mzee Mollel alifurahi sana kusikia hizi taarifa na hakuishia hapo akaniashauri nifanye na service kabisa za magari. Alikuwa mulemule kwenye mipango yangu.
“Sasa hivi Dodoma imekua sana na magari yameongezeka kwa wingi. Kama utaweza fanya na service za magari, mteja akija kupata huduma unamuuzia na oil, hivyo mzunguko wa hela utaonekana kwa urahisi. Wewe umetoka Dar es Salaam, basi onyesha utofauti na wafanyabiashara wa hapa. Ukifanya hivyo kwa ufanisi, baada ya mwezi mmoja utaanza kuona mafanikio."
“Ahsante mzee hili la kufanya service lipo kwenye mipango yangu na kuna sehemu nilipata acha nikalifanyie kazi.”
“Wewe ukikamilisha nijulishe wateja nitakuletea wengi sana hili ondoa wasiwasi, cha muhimu kama nilivyokwambia awali onesha utofauti na wengine.”
“Ahsante kwa ushauri wako mzee.”
Mzee alinipongeza sana kwa maamuzi niliyoyachukua na alisema atanisapoti kwa kadri ya uwezo wake. Nilishinda pale kwake mpaka usiku nikapata na dinner, kisha nikaaga na kuondoka kurudi kwa Aggy.
Niliona umuhimu mkubwa wa kulisimamia suala la biashara kwa bidii na umakini wa hali ya juu, kwani kufeli kwangu kutanirudisha katika ajira, jambo ambalo sitaki kabisa. Kwa upande wangu, kuajiriwa ni sawa na kujifunga katika utumwa wa hofu na mashaka ya maisha. Ni kweli, mshahara unaweza kuwa mkubwa, lakini utatosha vipi kulipa uhuru wangu?.
Niliporudi nyumbani, niliwasiliana na dalali na kupanga tukutane kesho na yule kijana ambaye aliniambia angeweza kunifaa kwenye masuala ya service. Pia, tulikubaliana tuwahi kuonana ili tuende kwenye eneo husika, na ikiwezekana, tufanye malipo kabisa
Kesho yake tulikutana na dalali akiwa ameongozana na dogo, nilimfanyia usaili kidogo na niliona yuko vizuri ana uwezo, pia alionesha nia ya kufanya kazi pamoja nami. Baada ya kumalizana na dogo, tulienda kukutana na mhusika mkuu ili kupata muongozo wa namna ya kufanya malipo.
Tulikutana na dada ambaye alionekana kuwa msimamizi wa eneo hilo, na mara ya kwanza, tulikutana na kaka, lakini leo hali ilikuwa tofauti. Dada huyu alikuwa na mvuto wa kipekee maana alikuwa kafungasha vizuri, alitupa muongozo na nikafanya malipo ya miezi sita kwa kiasi cha shilingi 2,100,000.
Baada ya hapo nilikaa chini na dogo ili tupange mipango kuhusu vifaa vya kazi atakavyohitaji maana kama eneo alikuwa keshaliona tayari. Dogo alisema ninunue compressor, mashine kwaajili ya wheel balancing, Automatic tyre changer, stand jack, bila kusahau sare/uniform na buti akiwa kazini na vifaa vingine vingi.
Dogo aliahidi kuwapa taarifa wateja wake wote wa zamani ili waje kwenye ofisi mpya, nami nilimuahidi kumpa bonasi kwa kila mteja mpya atakayeleta. Kuhusu mshahara, tulikubaliana kuwa nitaanza kumlipa 250,000 kwa mwezi, ambapo chakula na nauli zitakuwa juu yangu. Pia, nilimwambia kwamba mambo yakianza kwenda vizuri, atapata bonus kwa kila gari atakaloifanyia service.
Tuliagana kwa makubaliano ya kukutana pindi nitakapokuwa nimekamilisha kununua vifaa vya kazi, na nilimwambia kuwa ndani ya siku mbili vitakuwa tayari, hivyo ajiandae muda wowote nitampigia simu.
Nilipanga hesabu zangu kwa umakini na kugundua kuwa kuna umuhimu wa kurudi Dar es Salaam kwa ajili ya kununua vitendea kazi. Hata hivyo, biashara kule dukani ilikuwa bado ngumu, hasa kwa kuwa duka lilikuwa jipya. Aidha, nilikuwa nikimfundisha dada kuhusu aina za lubricants ili aweze kutoa huduma bora kwa wateja.
Baada ya siku mbili kupita nilirudi tena Dar es Salaam kwaajili ya kununua vifaa na nilienda Posta mtaa wa India. Kuna fundi wangu ndo aliniongoza kwa moja ya supplier ambaye anamjua na amenyooka.
Baada ya kufika dukani niliwaelekeza vifaa navyotaka pamoja na kupewa discount, baada ya kufanya malipo walisema watanitumia na nitapigiwa simu namna ya kupata mzigo wangu.
Nilimaliza mapema sana kisha nikarudi home kupumzika na nilipanga jioni nionane na Hilda kwaajili ya maongezi. Tangu niondoke Dar wiki mbili zilikuwa zimekata tayari, halafu hatukuwa na mawasiliano yoyote
Jioni ilipowadia Hilda alinipigia simu na kuuliza tunakutania wapi? Nami nilimjibu asogee mpaka Mikocheni ‘Triple 7’. Nilianza kujiandaa pale kwa haraka na baada ya nusu saa nilitoka home kuelekea eneo la tukio.
Baada ya kuonana tulianza mazungumzo pale na aliishia kulalamika kwanini sipatikani kwenye simu? Maana amekuwa akinipigia bila mafanikio;
MIMI: “Nilisahau kukupa namba mpya, halafu nilikuwa busy sana kule Dodoma hata hapa unaniona sababu kuna vifaa nimefuata.”
HILDA: “Insider usifanye hivo, uliniahidi utakuwa available pindi nakuhitaji, hata Lucy anakutafuta sana bila mafanikio unatuacha kwenye mataa wenzako.”
MIMI: “Pole mummy ndomana leo nimekutafuta ili tuongee, pia nimekumiss sana ujue.”
HILDA: “Don’t say that, mimi naona ofisi ni chungu, nilishazoea kukuona, kunitania muda wote nakuwa na furaha ofisini, umeniacha mpweke.”
MIMI: “Nollie si yupo?”
HILDA: “Sawa yupo, lakini hatuwezi kuwa na ukaribu kama wako.”
MIMI: “Embu niambie ni nini kiliendelea tangu tuachane kipindi kile ni week 2 tayari.”
HILDA: “Thanks God mzigo tulipata week iliyopita na tumelipa deni tayari, mama alirudi aka clear deni.”
MIMI: “Good news na anasemaje yeye?”
HILDA: “Nothing! Ila alikuulizia nikamwambia bado upo likizo.”
MIMI: “Kuna taarifa yoyote kutoka kwa Iryn?”
HILDA: “Hapana sijasikia ni muda mrefu sana na kila mtu anamuulizia pale ofisini.”
MIMI: “Ahsante kwa mrejesho mzuri bila shaka kwasasa huna stress kila kitu kipo kwenye track huna haja ya kuwa na wasiwasi tena.”
HILDA: “Ripoti zangu si unazipata lakini?”
MIMI: “Niwe mkweli sijawahi hata kuangalia ila tukiachana hapa nikirudi home nitaziangalia.”
HILDA: “Halafu umenikumbusha, Lucy alikuja kwako akaambiwa umehama, hapa ndo amechanganyikiwa anakuwa na wasiwasi sana juu yako.”
MIMI: “Nimehamia jirani hata sio mbali na nilikokuwa naishi zamani.”
HILDA: “Asmah pia anakuulizia sana, anahisi mimi na wewe tuna mawasiano ya siri ila namficha.”
MIMI: “Asmah hana taarifa wala sikumuaga pamoja na Lucy, hivyo hawajui niliko. Kama tulivyokubalina before usimpe mtu namba yangu bila kupata idhini yangu.”
HILDA: “Sawa hili ondoa wasiwasi Insider.”
Tuliendelea na maongezi mengine, lakini nilipata wazo la kwenda kumsalimia Asmah pale kwake kabla sijaondoka kurudi Dodoma kuendelea na mishe zangu.
Nilimdrop Hilda Morocco nami nikaendelea na safari ya kwenda Upanga na nilitumia barabara ya Kawawa ili nikaunge na barabara inayokwenda Makaburini, sikumwambia Hilda kama nakwenda kwa Asmah.
Baada ya kuwasili kwa Asmah nilipark gari usawa wa apartment yake, lakini kwa leo kulikuwa na utofauti maana kuna Crown nyeusi ilikuwa imepark pale.
Baada ya kushuka kutoka kwenye gari, nilipanda hadi ghorofa ya kwanza na kugonga mlango. Sikumpigia simu kwa sababu nilitaka iwe saprize, nilijua kuwa kwa nyakati za usiku, mara nyingi huwa nyumbani. Huu ulikuwa utaratibu wangu wa kawaida, kwenda bila kutoa taarifa.
Asmah alifungua mlango na ile kuniona alishtuka sana na alitoka nje akarudishia mlango;
ASMAH: “Insider what are you doing here?”
MIMI: “What? Mimi ndo wakuniuliza hivo? Hata salamu hakuna.”
ASMAH: “Kwanini unakuja bila taarifa?”
MIMI: “Mara ngapi nakuja hapa kwako bila taarifa?”
ASMAH: “Please naomba uende nitakucheki badae niko na kaka yangu akiona hivi atachukia.”
MIMI: “Ahh! Hayo unaleta wewe mimi nimekuja ili nikusalimie sasa wasiwasi wako ni nini?.”
ASMAH: “Insider please naomba nielewe nitakupigia kwenye simu badae. I’m really sorry.”
MIMI: “Alright no problem! Mimi naondoka.”
Niliamua kuondoka sikutaka kuendelea kupoteza muda, lakini nili smell something fishy kinaendelea. Niliwasha gari yangu ili niondoke, lakini Crown iliyokuwa imepaki pembeni ilinipa mashaka, nikahisi Asmah atakuwa amepata mhuni.
Nilivyofika getini ilibidi nimpige maswali mlinzi kuhusu ile Crown na alisema hii mara ya pili anaiona ikiingia na kutoka. Niliondoka kurudi home ili nikajiandae na safari yangu ya kurudi Dodoma nikaendelee na harakati zangu.
Baada ya kurudi home kutokana na mazingira kuwa ya kimya na upweke nilifikiri nikaona kuna umuhimu wa wife kurudi home. Niliwaza pale nimpigie simu tuongee arudi home, lakini niliona ni heri arudi mwenyewe ili kutunza heshima yangu.
Niliingia Shabiby Online na kukata tiketi yangu ya bus mapema. Pia nilianza kufikiri namna ya kutoka pale kwa Aggy na nikaona pindi nitakapo rudi Dodoma, nianze kutafuta gheto. Nilijiuliza sana, Aggy ni binti na kuna uwezekano kwamba kuna mwanaume anayemlipia kodi, kuendelea kukaa pale kwake ni sawa na kumuumiza. Hata kama tumekuwa marafiki wa muda mrefu, lakini kwa hatua tuliyofikia sasa, kuna baadhi ya mambo yanahitaji kupeana nafasi.
Unajua maana ya mgawanyo wa kazi,au unafikiri kila kitu kinapaswa kufanywa na wote ?Mwanamme kupika sio ushoga rafiki, na utanashati kunukia sio ushoga, yaan ww sijui umekula maharage ya wapi
Baharia🤣DULLAH: “Mhh! Becareful mzee, umeomba akuoneshe kaburi la baba mtoto?”
Inside10 Gily Gru cacutee Watu8SEASON 02
EPISODE 29
“A TRUE STORY BY INSIDER MAN”
PREVIOUS:
Saa 12 jioni nilianza safari ya kwenda Dodoma na nilichukua bodaboda wa kunipeleka Magufuli stand. Muda wa jioni mabus huwa yanasumbua hivyo, nilisogea pale darajani kwa Yusuph nikapata private inayokwenda Dodoma.
CONTINUE:
Safari ya kwenda Dodoma ilianza pale na gari ilikuwa ni Harrier. Tulikuwa jumla ya watu sita, pamoja na dereva. Tulikaa wanne nyuma ya seat, tukiwa tumebanana kimtindo—wanaume wawili na wanawake wawili.
Nilipokuwa barabarani, nilikuwa kimya sana, hata sikushirikiana na wenzangu katika mazungumzo. Nilikuwa nikiwaza mipango yangu ya biashara Dodoma na kupanga kumpigia simu dalali kumkumbusha kuhusu jambo letu.
Lengo langu la kwenda Dodoma ni kufungua biashara ya kuuza lubricants za magari na kufanya services. Nia yangu hapo baadae nipanue biashara hii kwa kuuza bidhaa kama vipuri vya magari, urembo, rims, na matairi.
Niliweka lengo kwamba ifikapo Jumatatu ya wiki ijayo, nitakuwa tayari nimeanza biashara yangu. Nilidhamiria kwa dhati kuanzisha biashara. Pia, nilipanga kuwa na nidhamu ya fedha kwa kipindi chote nitakachokuwepo Dodoma.
Saa 7 za usiku, tulipowasili Dodoma, baridi kali lilikuwa limetanda. Nilipata lodge iliyoko karibu na Chuo cha CBE na kwenda kupumzika.
Asubuhi baada ya kuamka jambo la kwanza niliwasiliana na Aggy kumpa taarifa niko Dodoma. Kwa upande wake alishangaa sana kusikia nimekuja bila kumtaarifu mapema na alisema baada ya nusu saa atakuwa around.
Baada ya hapo, nilimpigia simu dalali ili anipe mrejesho pamoja na ratiba zake. Lengo langu lilikuwa kuanza leo hii kutafuta frem za biashara ili mipango yangu iende kama ilivyopangwa. Dalali aliniambia tukutane baadae, na akanihakikishia kwamba bado anaendelea kutafuta frem zingine ili tuwe na chaguo la kutosha wakati wa kuangalia.
Ndani ya nusu saa, Aggy alikuwa tayari amewasili, nami nikatoka kwenda kuonana naye ili tuondoke. Tulipokutana, tulisalimiana kwa furaha na tukakumbatiana kwa upendo, kisha safari yetu ya kuelekea nyumbani kwake ikaanza.
Aggy alionesha kuwa na furaha sana maana mara ya mwisho kuonana ilikuwa ni October kipindi nimeenda na Iryn. Aggy aliulizia kuhusu maendeleo ya nyumbani na hakumsahau Iryn, ndipo mazungumzo yakaanza;
AGGY: “Yule mrembo yupo?”
MIMI: “Yupo mama ila sio Tanzania hii.”
AGGY: “Na kwanini unakuja bila kunipa taarifa na unafikia lodge?”
MIMI: “Nilitaka nikusurprise au hujapenda?”
AGGY: “Tufanye umeshinda.”
MIMI: “Naona unazidi kuwa mrembo nipe siri ya mafanikio au mama anamwaga pesa mingi huko maofisini.”
AGGY: “Hahahahaa hali mbaya Insider bora hata wewe uliejiajiri.”
MIMI: “Hamjawahi kukubali kuhusu hili, sawa bhana.”
Ndani ya muda mfupi tuliwasili nyumbani kwake na alinikaribisha seblen kisha akaniandalia na chai ili ninywe. Aggy alitamani sana kujua sababu iliyonileta Dodoma, nami nilimwambia mipango yangu yote na aliishia kunipongeza. Nilimwambia nitakuwepo Dodoma kwa muda mrefu mpaka pale ambapo nitaona biashara imesimama na haihitaji tena usimamizi wangu.
Aggy aliniaga anarudi ofisini na kutoa ahadi atawahi kurudi, kwa upande wangu nilimpa ratiba zangu za kutoka jioni kwenda kuonana na dalali, na alisema atakuwa karudi tayari, hivyo atanipa kampani ya kwenda.
Saa 10 jioni tulikutana na dalali maeneo ya Sabasaba, kisha tukaanza kuangalia frem zote alizokuwa nazo. Baada ya kuzunguka sana niliipenda frem moja ipo katikati ya mjini ilikuwa location nzuri sana.
Muda ulikuwa umeenda sana, na mhusika wa hii frem alituambia tukutane kesho asubuhi ili kuweka mambo sawa. Baada ya hapo, Aggy alipendekeza tupitie sehemu kwaajili ya kupata chakula cha jioni, tutakapokarudi nyumbani, ni kulala moja kwa moja.
Wakati tulipokuwa tunakula chakula, mazungumzo yaliendelea pale, ambapo Aggy alisema kwamba mwezi ujao anatarajia kusafiri kwenda mkoani kuwasalimia wazazi wake. Nami niliona wazo lake lilikuwa zuri sana, hivyo lilinipa hamasa ya kwenda kumtembelea mama, na tukakubaliana kwamba tutaenda pamoja.
Kama nilivyowahi kusema hapo awali, mimi na Aggy tulisoma katika chuo kimoja, tukichukua course moja. Zaidi ya hilo, tulipitia shule moja ya O-Level, na wazazi wetu pia wanatoka mkoa mmoja.
Baada ya kurudi nyumbani, nilimpigia simu Maggy kumtaarifu kuwa nipo Dodoma, isinge kuwa busara kula buyu ukizingatia ananisaidia sana kuangalia nyumba yangu. Hata hivyo, baada ya kumpigia hakupokea simu zangu, kwa vile muda ulikuwa umekwenda, nilijisemea kwamba akiziona missed call atanipigia.
Aggy alikuwa amepanga nyumba ya vyumba viwili, hivyo alinionesha chumba changu cha kulala, kisha akaniga anakwenda kulala na tutaonana kesho.
Asubuhi baada ya kuamka nilikuwa na ratiba ya kukutana na dalali ili kwenda kufanya malipo kwa fremu iliyokuwa kwenye mipango yetu. Lakini, dalali alinijulisha kuwa kuna fremu nyingine mpya imepatikana na iko kwenye eneo la Sheli, tukakubaliana tuanze kwanza kuiangalia hio frem.
Baada ya kuliona eneo lilikuwa lina mvuto mkubwa, na nikawaza kuwa litakuwa na faida kubwa kama likitumika kama sehemu ya kufanyia service, huku eneo la mjini likiwa kama showroom. Nilionana na mhusika na baada ya maongezi ya muda mrefu akasema wanapangisha kwa 350,000, hivyo nilichukua namba zake za simu na tukaondoka.
Dalali alinishauri kama naweza nichukue eneo la sheli maana nitapata wateja wengi sana wa service, kwani sehemu ni nzuri sana. Tulishauriana sana na nikamwambia anipe muda nijifikirie, na alisema kuhusu fundi yupo dogo anamjua na anacheti cha VETA naweza kufanya naye kazi.
Tulienda straight kuonana na landlord ili tufanye malipo ya frem ya jana na baada ya kukutana na mhusika nilifanya malipo ya 2.4M kwa miezi 6. Sikutaka kupoteza muda nikatafuta fundi wa kuanza kutengeneza shelves ili nianze biashara.
Niliandaa mipango yangu nikaona kuna haja ya kurudi Dar kwaajili ya kuchukua mzigo wa lubricants/vilainishi. Habari njema hii biashara nina uzoefu nayo, hivyo haikuwa shida kwangu kuifanya na kuwatafuta suppliers maana machimbo yote nayajua na nina namba zao.
Niliwaza kutafuta chumba cha kupanga kwa kipindi chote nitakachokuwa Dodoma. Kuendelea kukaa kwa Aggy sikuona jambo la busara ukizingatia mimi ni mtoto wa kiume, nahitaji uhuru.
Mipango yangu ilikuwa kufikia jumatatu niwe nimenza biashara, pia niwe nimeondoka kwa Aggy tayari. Lakini jambo la kwanza nitaanza kwenda Dar, kisha baada ya kurudi nianze mchakato wa kutafuta geto.
Jumamosi frem ilikuwa imekamilika tayari kwa kuingia na kuanza bishara, hivyo nikaona kesho jumapili nirudi Dar, ili jumatatu niwe Kariakoo kuchukua mzigo.
Jioni nilienda kumsalimia Maggy nyumbani kwake maana ilikuwa ni kitambo kimepita bila kuonana. Baaada ya kuwasili pale kwake alinikaribisha, lakini nilianza kwanza kukagua nyumba.
Mazingira ya nyumba yalikuwa mazuri na yakivutia, kwani palikuwa pamepandwa maua maua na miti ndani na nje ya fenzi. Pia nilimsalimia jirani yake ambaye ni mpangaji wangu, baada ya hapo tukaingia ndani kuendelea na maongezi mengine;
MAGGY: “Karibu sana baba mwenye nyumba, sijui nikuletee kinywaji gani?”
MIMI: “Maji yanatosha.”
Alimuagiza dada aniletee maji na story zikaendelea;
MAGGY: “Umekuja lini huku? Halafu kimya kimya.”
MIMI: “Nilitaka nikufumanie una bahati sana.”
MAGGY: “Huhuuu! Yule dada mrembo yupo?”
MIMI: “Yupo masomoni ni muda hatujaonana.”
MAGGY: “Kwa uzuri tu amebarikiwa asee, kuna watu walipendelewa.”
MIMI: “Mbona wewe umependelewa mahips au hujioni?”
MAGGY: “Insider ni mshenzi wewe! Mimi nimefurahi sana kukuona, sijui wifi yangu anaendeleaje na mtoto.”
MIMI: “Wako poa nashukuru Mungu. Bado wewe sijui unasubiri nini.?”
MAGGY: “Wanaume waoaji kama wewe hawapo siku hizi.”
MIMI: “Naamini shemeji yupo ila unamfichaficha.”
MAGGY: “Insider tuachane na haya, nimekumiss sana Dar.”
MIMI: “Karibu sana kwenye mji wetu.”
Tuliongea mambo mengi likiwemo suala langu lililonileta Dodoma, pia kwa upande wake alisema ana mpango wa kutafuta kiwanja aanze ujenzi taratibu. Tulipata dinner ya pamoja na baada ya hapo nilimuaga maana Aggy alikuwa akinipigia sana simu.
Baada ya kuagana na Maggy nilimpigia simu Aggy na alisema ananisubiri ili tukale dinner, nikamwambia nimeshakula tayari, akaomba nimpelekee chips yai na mishikaki.
Baada ya kurudi home nilimtaarifu Aggy kuhusu kurudi Dar siku ya kesho kwaajili ya kuchukua mzigo na nitarudi jumatatu na nikamuaga nikaingia chumbani kulala.
Jumapili asubuhi, niliondoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam na nilifika nyumbani jioni kwenye makazi mapya. Mara baada ya kufika, mazingira yalikuwa tulivu sana kiasi kwamba nilianza kumkumbuka Junior wangu, kwa jinsi nilivyozoea fujo zake ndani, mara agombane na mama yake au dada yake kwa sababu ya utundu wake.
Mazingira ya home yalianza kuniboa mpaka nikatamani kwenda Mbweni kwa Ghati, zile siku mbili nilizolala kwake zilinidatisha sana. Baadae nikaona wacha niende Upepo garden kupoteza muda kwanza nilikuwa jirani na mazingira ya huku.
Nilikwenda nikakaa sehemu ambayo mara ya mwisho nilikuwa na Prisca na nilijukuta namkumbuka tena. Niliagiza bia zangu nikawa nakunywa huku napanga mipango yangu taratibu nikipulizwa na upepo wa bahari.
Jumatatu nilienda Kariakoo nikanunua mzigo wa kutosha, kisha nikauepeleka transporter kwaajili ya kuusafirisha kwenda Dodoma. Gari huwa zinasafiri usiku, hivyo kufikia kesho asubuhi mzigo ungekuwa umefika tayari.
Baada ya kumaliza taratibu zote, nilianza kufanya utafiti kuhusu bei za spares za magari, hasa kwa bei za jumla. Kwa bahati nzuri, Kariakoo nina kaka yangu ambaye anauza spares za magari na yuko mtaa wa MAFIA/SIKUKUU. Amekuwa msaada mkubwa kwangu katika sekta hii, na ana duka lake kubwa sana, anauza kwa jumla, jambo ambalo limenisaidia sana.
Niliwasiliana na Dullah ili tuweze kuonana na lengo nimkabidhi funguo za nyumba incase kama mama J atahitaji kurudi home na tulikutana pale breakpoint Makumbusho japo alifika kwa kuchelewa sana;
DULLAH: “Ndugu yangu nimekuweka sana, nilikuwa naacha maagizo ofisini.”
MIMI: “Naelewa bro! Kama unavyoniona niko busy na mipango yangu hapa.”
DULLAH: “Dadeki kitu Macbook Air hii dukani inakwendaje?”
MIMI: “Mahali uliyolipa kwa Latifah zidisha mara 4.”
DULLAH: “Mseng** wewe unataka kusema ina thamani ya Million 8?”
MIMI: “Ndo maana yake au huamini?.”
DULLAH: “Niambie naona umebadili namba ya simu tayari na ukaondoka bila taarifa, nakutafuta kwa simu sikupati mpaka nikahisi labda dada amekufungia ndani.”
MIMI: “Daah aisee sio poa, halafu unajua ile manzi ina mtoto? Japo anadai baba mtoto alikufa.”
DULLAH: “Mhh! Becareful mzee, umeomba akuoneshe kaburi la baba mtoto?”
MIMI: “Tuachane na haya kaka, mwanamke mwenyewe sina mpango naye ilitokea bahati mbaya wewe ndo uliniforce niende. Unajua nilikuwa Dodoma na nimepata frem tayari?, halafu nimerudi jana kufuata mzigo na kesho mapema naondoka.”
DULLAH: “Hongera sana kaka, itabidi nije Dodoma siku moja maana sijawahi fika kabisa.”
MIMI: “Karibu uje uangalie fursa. Mzee mimi sina story leo, nilichokuitia hapa nilitaka nikupe taarifa ya kuanza biashara na pia nimehama pale home, nimehamia mbezi chini kabisa.”
DULLAH: “Kwanini umehama sehem nzuri kama ile?”
MIMI: “Nimehama kwasababu maalumu, pia naomba nikukabidhi funguo endapo wife akihitaji atawasiliana na wewe.”
DULLAH: “Haina shida bro usiwe na wasiwasi.”
MIMI: “Nashukuru sana, mimi sikai nataka niwahi home nikalale, kesho niwahi kuondoka kwenda Dodoma kupokea mzigo. Baada ya hapo nina safari nyingine tena ya kwenda mkoani kumsalimia mama yangu.”
DULLAH: “Naona unataka ukachukue baraka kwa bimkubwa.”
MIMI: “Muhimu kaka si unajua biashara zina mazingaombwe sana.”
DULLAH: “Naelewa kaka wewe wahi mengine tutaendelea kuwasiliana.”
Baada ya kuachana na Dullah niliondoka straight kuelekea home na baada ya kufika, nilifanya mawasiliano na Aggy anisaidie kumtafuta dada wa kushinda dukani.
Kesho yake nilirudi Dodoma mapema maana nilitumia usafiri wa anga, pia nilikuwa nina safari nyingine ya kwenda mkoani. Baada ya kuwasili nilienda moja kwa moja kufuatilia mzigo wangu na baada ta kuupata nilitafuta usafiri wa kuupeleka dukani.
Baada ya kupeleka mzigo dukani, nilimpigia Aggy simu kumtaarifu kwamba naenda mkoani kumsalimia mama yangu. Aggy alishangaa kwanini haraka sana? Hata sijapata muda wa kupumzika?, nikamwambia ni muhimu sana kwenda, na nikaondoka kwa private.
Niliingia mkoani usiku kwa upande wa pili, mama hakuwa na taarifa za ujio wangu, hivyo nilitaka kumsaprize. Nilipofika home geti lilikuwa tayari limefungwa, ikabidi nigonge, mbwa walikuwa karibu wakaanza kubweka pale, na walikoma mara moja waliponitambua.
Moja ya Mbwa wetu anaitwa Askari, alisogea getini kwa furaha kubwa muda huu. Alianza kutoa kelele za furaha kuniona huku akitikisa mkia wake kwa nguvu na kurukia geti kwa msisimko. Askari ni mbwa ambaye nimemlea tangu akiwa mdogo, na licha ya kwamba naweza kutokuwepo nyumbani kwa muda mrefu, kila ninaporudi, daima ananikumbuka kwa upendo wa kipekee.
Dada alikuja kufungua geti na kunikaribisha ndani na ile kuingia seblen mama alikuwa na wadogo zangu wakiangalia tamthlia na baada ya kuniona aliishia kufurahi na kuja kunikumbatia kwa nguvu.
“Ooh mwanangu nimetoka kukuwazia sio muda mrefu, mbona unakuja bila kutoa taarifa huko umefukuzwa?”
“Sijatokea Dar nilikuwa Dodoma.”
“Kuna nini huko?”
“Kuna biashara nataka kuianza ndiyo imenileta hapa home.”
“Niambie nakusikiliza mwanangu.”
Tulianza maongezi na mama, ambapo nilimshirikisha kuhusu biashara ninayotaka kuanzisha. Mama alifurahi sana na alinipongeza, kisha akasema tutafanya maombezi ya nguvu kabla ya kwenda kulala. Pia, tulizungumza kuhusu mimi kuwa Zambia, na mama alifurahi sana baada ya kupata taarifa kutoka kwa baba.
Baada ya maongezi marefu, nilimkabidhi mama yangu zawadi maalum, simu ya Samsung niliyonunua Dar es Salaam. Mama alifurahi sana kwa zawadi ya simu na bila kuchelewa akaweka line.
Kabla ya kwenda kulala kama familia tulifanya maombi juu ya biashara nayoenda kuianza kwa kufunga Roho za chuma Ulete, tukimwomba Mungu kuondoa maadui watakaojaribu kunikwamisha katika safari yangu ya kibiashara. Tuliiomba pia msaada wa kupata wateja, ili biashara yetu iweze kustawi kwa mafanikio.
Baada ya maombi nilimuaga mama nakwenda kulala na masuala mengine mengi tugaongea kesho panapo majaliwa. Lakini zawadi ya simu ilimgusa sana mama yangu maana alifurahi sana na alizidi kunishukuru.
*****
Jumatano nilirudi Dodoma na niliwasili jioni, nilikuwa nimechoka, lakini nilikuwa na matumaini makubwa ya kuanza biashara siku inayofuata. Kwa bahati nzuri, Aggy alikuwa tayari amempata dada ambaye angeweza kunisaidia dukani. Huyu dada alikuwa ni mfanyakazi wake wa zamani, kabla Aggy hajafunga biashara yake.
Aggy alinihakikishia kuwa huyu dada ni mchapakazi, mwelewa, na mwenye uaminifu, hivyo atanifaa sana katika biashara yangu. Bila kusita, nilimuomba Aggy amfahamishe ili kesho tukutane kwa ajili ya mazungumzo zaidi na kupanga jinsi ya kuanza kazi pamoja.
Mnamo Alhamisi, tarehe 16/03/2023, nilifungua rasmi biashara yangu. Nilianza kwa kuwajulisha watu wa karibu na kuwaomba waniunge mkono. Nilitembelea garage mbalimbali na kuwaeleza kuhusu biashara yangu, huku nikiwapatia punguzo maalum la bei.
Jumapili, nilimtembelea Mzee Mollel nyumbani kwake ili kumsalimia na kumshirikisha kuhusu biashara mpya niliyofungua. Mzee Mollel ni rafiki wa karibu wa baba yangu, na ninamheshimu sana kama mzazi wangu mwenyewe.
Mzee Mollel alifurahi sana kusikia hizi taarifa na hakuishia hapo akaniashauri nifanye na service kabisa za magari. Alikuwa mulemule kwenye mipango yangu.
“Sasa hivi Dodoma imekua sana na magari yameongezeka kwa wingi. Kama utaweza fanya na service za magari, mteja akija kupata huduma unamuuzia na oil, hivyo mzunguko wa hela utaonekana kwa urahisi. Wewe umetoka Dar es Salaam, basi onyesha utofauti na wafanyabiashara wa hapa. Ukifanya hivyo kwa ufanisi, baada ya mwezi mmoja utaanza kuona mafanikio."
“Ahsante mzee hili la kufanya service lipo kwenye mipango yangu na kuna sehemu nilipata acha nikalifanyie kazi.”
“Wewe ukikamilisha nijulishe wateja nitakuletea wengi sana hili ondoa wasiwasi, cha muhimu kama nilivyokwambia awali onesha utofauti na wengine.”
“Ahsante kwa ushauri wako mzee.”
Mzee alinipongeza sana kwa maamuzi niliyoyachukua na alisema atanisapoti kwa kadri ya uwezo wake. Nilishinda pale kwake mpaka usiku nikapata na dinner, kisha nikaaga na kuondoka kurudi kwa Aggy.
Niliona umuhimu mkubwa wa kulisimamia suala la biashara kwa bidii na umakini wa hali ya juu, kwani kufeli kwangu kutanirudisha katika ajira, jambo ambalo sitaki kabisa. Kwa upande wangu, kuajiriwa ni sawa na kujifunga katika utumwa wa hofu na mashaka ya maisha. Ni kweli, mshahara unaweza kuwa mkubwa, lakini utatosha vipi kulipa uhuru wangu?.
Niliporudi nyumbani, niliwasiliana na dalali na kupanga tukutane kesho na yule kijana ambaye aliniambia angeweza kunifaa kwenye masuala ya service. Pia, tulikubaliana tuwahi kuonana ili tuende kwenye eneo husika, na ikiwezekana, tufanye malipo kabisa
Kesho yake tulikutana na dalali akiwa ameongozana na dogo, nilimfanyia usaili kidogo na niliona yuko vizuri ana uwezo, pia alionesha nia ya kufanya kazi pamoja nami. Baada ya kumalizana na dogo, tulienda kukutana na mhusika mkuu ili kupata muongozo wa namna ya kufanya malipo.
Tulikutana na dada ambaye alionekana kuwa msimamizi wa eneo hilo, na mara ya kwanza, tulikutana na kaka, lakini leo hali ilikuwa tofauti. Dada huyu alikuwa na mvuto wa kipekee maana alikuwa kafungasha vizuri, alitupa muongozo na nikafanya malipo ya miezi sita kwa kiasi cha shilingi 2,100,000.
Baada ya hapo nilikaa chini na dogo ili tupange mipango kuhusu vifaa vya kazi atakavyohitaji maana kama eneo alikuwa keshaliona tayari. Dogo alisema ninunue compressor, mashine kwaajili ya wheel balancing, Automatic tyre changer, stand jack, bila kusahau sare/uniform na buti akiwa kazini na vifaa vingine vingi.
Dogo aliahidi kuwapa taarifa wateja wake wote wa zamani ili waje kwenye ofisi mpya, nami nilimuahidi kumpa bonasi kwa kila mteja mpya atakayeleta. Kuhusu mshahara, tulikubaliana kuwa nitaanza kumlipa 250,000 kwa mwezi, ambapo chakula na nauli zitakuwa juu yangu. Pia, nilimwambia kwamba mambo yakianza kwenda vizuri, atapata bonus kwa kila gari atakaloifanyia service.
Tuliagana kwa makubaliano ya kukutana pindi nitakapokuwa nimekamilisha kununua vifaa vya kazi, na nilimwambia kuwa ndani ya siku mbili vitakuwa tayari, hivyo ajiandae muda wowote nitampigia simu.
Nilipanga hesabu zangu kwa umakini na kugundua kuwa kuna umuhimu wa kurudi Dar es Salaam kwa ajili ya kununua vitendea kazi. Hata hivyo, biashara kule dukani ilikuwa bado ngumu, hasa kwa kuwa duka lilikuwa jipya. Aidha, nilikuwa nikimfundisha dada kuhusu aina za lubricants ili aweze kutoa huduma bora kwa wateja.
Baada ya siku mbili kupita nilirudi tena Dar es Salaam kwaajili ya kununua vifaa na nilienda Posta mtaa wa India. Kuna fundi wangu ndo aliniongoza kwa moja ya supplier ambaye anamjua na amenyooka.
Baada ya kufika dukani niliwaelekeza vifaa navyotaka pamoja na kupewa discount, baada ya kufanya malipo walisema watanitumia na nitapigiwa simu namna ya kupata mzigo wangu.
Nilimaliza mapema sana kisha nikarudi home kupumzika na nilipanga jioni nionane na Hilda kwaajili ya maongezi. Tangu niondoke Dar wiki mbili zilikuwa zimekata tayari, halafu hatukuwa na mawasiliano yoyote
Jioni ilipowadia Hilda alinipigia simu na kuuliza tunakutania wapi? Nami nilimjibu asogee mpaka Mikocheni ‘Triple 7’. Nilianza kujiandaa pale kwa haraka na baada ya nusu saa nilitoka home kuelekea eneo la tukio.
Baada ya kuonana tulianza mazungumzo pale na aliishia kulalamika kwanini sipatikani kwenye simu? Maana amekuwa akinipigia bila mafanikio;
MIMI: “Nilisahau kukupa namba mpya, halafu nilikuwa busy sana kule Dodoma hata hapa unaniona sababu kuna vifaa nimefuata.”
HILDA: “Insider usifanye hivo, uliniahidi utakuwa available pindi nakuhitaji, hata Lucy anakutafuta sana bila mafanikio unatuacha kwenye mataa wenzako.”
MIMI: “Pole mummy ndomana leo nimekutafuta ili tuongee, pia nimekumiss sana ujue.”
HILDA: “Don’t say that, mimi naona ofisi ni chungu, nilishazoea kukuona, kunitania muda wote nakuwa na furaha ofisini, umeniacha mpweke.”
MIMI: “Nollie si yupo?”
HILDA: “Sawa yupo, lakini hatuwezi kuwa na ukaribu kama wako.”
MIMI: “Embu niambie ni nini kiliendelea tangu tuachane kipindi kile ni week 2 tayari.”
HILDA: “Thanks God mzigo tulipata week iliyopita na tumelipa deni tayari, mama alirudi aka clear deni.”
MIMI: “Good news na anasemaje yeye?”
HILDA: “Nothing! Ila alikuulizia nikamwambia bado upo likizo.”
MIMI: “Kuna taarifa yoyote kutoka kwa Iryn?”
HILDA: “Hapana sijasikia ni muda mrefu sana na kila mtu anamuulizia pale ofisini.”
MIMI: “Ahsante kwa mrejesho mzuri bila shaka kwasasa huna stress kila kitu kipo kwenye track huna haja ya kuwa na wasiwasi tena.”
HILDA: “Ripoti zangu si unazipata lakini?”
MIMI: “Niwe mkweli sijawahi hata kuangalia ila tukiachana hapa nikirudi home nitaziangalia.”
HILDA: “Halafu umenikumbusha, Lucy alikuja kwako akaambiwa umehama, hapa ndo amechanganyikiwa anakuwa na wasiwasi sana juu yako.”
MIMI: “Nimehamia jirani hata sio mbali na nilikokuwa naishi zamani.”
HILDA: “Asmah pia anakuulizia sana, anahisi mimi na wewe tuna mawasiano ya siri ila namficha.”
MIMI: “Asmah hana taarifa wala sikumuaga pamoja na Lucy, hivyo hawajui niliko. Kama tulivyokubalina before usimpe mtu namba yangu bila kupata idhini yangu.”
HILDA: “Sawa hili ondoa wasiwasi Insider.”
Tuliendelea na maongezi mengine, lakini nilipata wazo la kwenda kumsalimia Asmah pale kwake kabla sijaondoka kurudi Dodoma kuendelea na mishe zangu.
Nilimdrop Hilda Morocco nami nikaendelea na safari ya kwenda Upanga na nilitumia barabara ya Kawawa ili nikaunge na barabara inayokwenda Makaburini, sikumwambia Hilda kama nakwenda kwa Asmah.
Baada ya kuwasili kwa Asmah nilipark gari usawa wa apartment yake, lakini kwa leo kulikuwa na utofauti maana kuna Crown nyeusi ilikuwa imepark pale.
Baada ya kushuka kutoka kwenye gari, nilipanda hadi ghorofa ya kwanza na kugonga mlango. Sikumpigia simu kwa sababu nilitaka iwe saprize, nilijua kuwa kwa nyakati za usiku, mara nyingi huwa nyumbani. Huu ulikuwa utaratibu wangu wa kawaida, kwenda bila kutoa taarifa.
Asmah alifungua mlango na ile kuniona alishtuka sana na alitoka nje akarudishia mlango;
ASMAH: “Insider what are you doing here?”
MIMI: “What? Mimi ndo wakuniuliza hivo? Hata salamu hakuna.”
ASMAH: “Kwanini unakuja bila taarifa?”
MIMI: “Mara ngapi nakuja hapa kwako bila taarifa?”
ASMAH: “Please naomba uende nitakucheki badae niko na kaka yangu akiona hivi atachukia.”
MIMI: “Ahh! Hayo unaleta wewe mimi nimekuja ili nikusalimie sasa wasiwasi wako ni nini?.”
ASMAH: “Insider please naomba nielewe nitakupigia kwenye simu badae. I’m really sorry.”
MIMI: “Alright no problem! Mimi naondoka.”
Niliamua kuondoka sikutaka kuendelea kupoteza muda, lakini nili smell something fishy kinaendelea. Niliwasha gari yangu ili niondoke, lakini Crown iliyokuwa imepaki pembeni ilinipa mashaka, nikahisi Asmah atakuwa amepata mhuni.
Nilivyofika getini ilibidi nimpige maswali mlinzi kuhusu ile Crown na alisema hii mara ya pili anaiona ikiingia na kutoka. Niliondoka kurudi home ili nikajiandae na safari yangu ya kurudi Dodoma nikaendelee na harakati zangu.
Baada ya kurudi home kutokana na mazingira kuwa ya kimya na upweke nilifikiri nikaona kuna umuhimu wa wife kurudi home. Niliwaza pale nimpigie simu tuongee arudi home, lakini niliona ni heri arudi mwenyewe ili kutunza heshima yangu.
Niliingia Shabiby Online na kukata tiketi yangu ya bus mapema. Pia nilianza kufikiri namna ya kutoka pale kwa Aggy na nikaona pindi nitakapo rudi Dodoma, nianze kutafuta gheto. Nilijiuliza sana, Aggy ni binti na kuna uwezekano kwamba kuna mwanaume anayemlipia kodi, kuendelea kukaa pale kwake ni sawa na kumuumiza. Hata kama tumekuwa marafiki wa muda mrefu, lakini kwa hatua tuliyofikia sasa, kuna baadhi ya mambo yanahitaji kupeana nafasi.